< Joshua 21 >
1 And the princes of meynees of Leuy neiyiden to Eleazar, preest, and to Josue, sone of Nun, and to the duykis of kynredis, bi alle the lynagis of the sones of Israel;
Kisha wakuu wa koo za Walawi walimwendea Eliazari kuhani, na kwa Yoshua mwana wa Nuni, na kwa viongozi wa familia za mababu zao miongoni mwa watu wa Israeli.
2 and the Leuytis spaken to hem in Sylo, of the lond of Canaan, and seiden, The Lord comaundide bi the honde of Moises, that citees schulden be youun to vs to dwelle ynne, and the subarbis of tho to werk beestis to be fed.
Waliwaambia, “Yahweh aliwaagizeni ninyi kwa mkono wa Musa kwamba mtupatieni miji ya kuishi yenye maeneo kwa ajili ya kuchungia ya mifugo.” waliyasema haya huko Shilo katika nchi ya Kanaani.
3 And the sones of Israel yauen `of her possessiouns, bi comaundement of the Lord, citees and the subarbis of tho.
Hivyo, kwa agizo la Yahweh, watu wa Israeli waliwapa Walawi kutoka katika urithi wa wao miji ifuatayo pamoja na maeneo yao ya kuchungia.
4 And the lot yede out in to the meynee of Caath, of the sones of Aaron, preest, of the lynages of Juda, and of Symeon, and of Beniamyn, threttene citees;
Upigaji wa kura kwa ajili ya koo za Wakohathi ulileta matokeo haya: makuhani ambao ni wazawa wa Haruni ambao walitokana na Walawi, walipokea miji kumi na mitatu waliopewa kutoka kwa kabila la Yuda, kutoka kabila la Simoni, na kutoka kabila la Benyamini.
5 and to the othere of the sones of Caath, that is, to dekenes that weren left, of the lynagis of Effraym, and of Dan, and of the half lynage of Manasse, ten citees.
Koo zilizobaki za Wakohathi walipokea kwa kupiga kura kwa miji kumi kutoka katika kabila za Efraimu, Dani, na kutoka kwa nusu ya kabila la Manase.
6 Sotheli lot yede out to the sones of Gerson, that thei schulden take of the lynagis of Isachar, and of Aser, and of Neptalym, and of the half lynage of Manasses `in Basan, threttene citees in noumbre;
Na watu wazawa wa Gershoni walipewa miji kumi na mitatu kwa kupigiwa kura kutoka kwa koo za kabila la Isakari, Asheri, Nafutali, na nusu ya kabila la Manase katika Bashani.
7 and to the sones of Merari, bi her meynees, of the lynagis of Ruben, and of Gad, and of Zabulon, twelue citees.
Watu waliokuwa wazawa wa Merari walipokea miji kumi na miwili kutoka katika makabila ya Rubeni, Gadi na Zabuloni.
8 And the sones of Israel yauen to dekenes cytees, and the subarbis `of tho, as the Lord comaundide bi the hond of Moises; and alle yauen bi lot.
Basi, watu wa Israeli waliwapa Walawi miji hii pamoja na maeneo yao ya kuchungia, kwa kupiga kura, kama vile Yahweh alivyokuwa ameagiza kwa mkono wa Musa.
9 Of the lynagis of the sones of Juda, and of Symeon, Josue yaf citees;
Kutoka kwa makabila la Yuda na Simoni, waliwapa nchi katika miji ifuatayo iliyoorodheshwa kwa majina.
10 to the sones of Aaron, bi the meynees of Caath, of the kyn of Leuy, of whiche citees these ben the names; for the firste lot yede out to hem;
Miji hii walipewa wazawa wa Haruni, ambao walikuwa miongoni mwa koo za Wakohathi, ambao walitoka katika kabila la Lawi. Kwa kuwa upigaji wa kura ya kwanza uliwaangukiwa wao.
11 Cariatharbe, of the fadir of Enach, which is clepid Ebron, in the hil of Juda, and the subarbis therof bi cumpas;
Waisraeli waliwapatia Kiriathi Arba ( Arba alikuwa ni baba wa Anaki), eneo hilo liliitwa pia Hebroni, katika nchi ya milima ya Yuda, pamoja na maeneo ya kulishia mifugo yaliyouzunguka mji.
12 sotheli he hadde youe the feeldis and townes therof to Caleph, sone of Jephone, to haue in possessioun.
Lakini mashamba ya mji na vijiji vyake vilikuwa tayari ameshapewa Kalebu mwana Yefune, kama mali yake.
13 Therfor Josue yaf to the sones of Aaron, preest, Ebron, a citee of refuyt, and the subarbis `of it, and Lebnam with hise subarbis,
Na kwa wana wa Haruni kuhani, waliwapa Hebroni pamoja na eneo lake la kulishia mifugo ambao ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu bila kukusudia na Libna pamoja na maeneo ya kulishia mifugo.
14 and Jether, and Yschymon,
Na Yatiri pamoaja na maeno yake ya kuchungia, na Eshitemoa pamoja na maeneo yake ya malisho.
15 and Elon, and Dabir, and Ayn, and Lethan,
Lakini pia waliwapa Holoni pamoja na maeneo yake ya malisho, Debiri pamoja na maeneo yake ya malisho,
16 and Bethsames, with her subarbis; nyne citees, of twei lynagis, as it is seid.
Aini pampoja na maeneo yake ya malisho, na Bethi Shemeshi pamoja na maeneo yake ya malisho. Ilikuwa ni miji kumi na tisa ambayo walipewa kutoka katika makabila haya mawilil.
17 Sotheli of the lynage of the sones of Beniamyn, he yaf Gabaon, and Gabee, and Anatoth, and Almon, with her subarbis;
Kutoka katika kabilala Benyamini walipewa Gibea pamoja na maeneo yake ya malisho, na Geba pamoja na maeneo yake ya malisho,
na Anathothi pamoja na maeneo yake ya malisho, na amoni pamoja na vitongoji vyake vinne.
19 Alle the citees togidere of the sones of Aaron, preest, weren threttene, with her subarbis.
Miji waliyopewa makuhani, wana wa Haruni, ilikuwa ni miji kumi na mitatu kwa ujumla, kujumlisha na maeneo yake ya malisho.
20 Forsothe to `the othere, bi the meynees of the sones of Caath, of the kyn of Leuy, this possessioun was youun;
Na kwa ajili ya sehemu ya familia ya Kohathi iliyosalia, wale Walawi walio wa familia ya Kohathi, walipewa miji kutoka katika kabila la Efraimu kwa kupiga kura.
21 of the lynage of Effraym, the citee of refuyt, Sichen, with hise subarbis, in the hil of Effraym, and Gazer,
Walipewa Shekemu pamoja na maeneo yake ya malisho katika nchi ya milima ya Efraimu - mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu bila kukusudia, na Gezeri pamoja na maeneo yake ya malisho,
22 and Sebsam, and Bethoron, with her subarbis;
na Kibzaimu pamoja na maeneo yake ya malisho, na Bethi Horoni pamoja na maeneo yake ya malisho, ilikuwa miji minne kwa ujumla wake.
23 `foure citees; also of the lynage of Dan, Helthece, and Gebethon, and Haialon,
Kutoka katika kabila la Dani, ukoo wa Kohathi ulipewa Elteke pamoja na maeneo yake ya malisho, na Gibethoni pamoja na maeneo yake ya malisho, na
24 and Gethremmon, with her subarbis;
Aijaloni pamoja na maeneo yake ya malisho, na Gathrimoni pamoja na maeneo yake ya malisho, ilikuwa ni miji minne kwa ujumla wake.
25 `foure citees; sotheli of the half lynage of Manasses, Thanach, and Gethremon, with her subarbis; `twei citees.
Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, ukoo wa Kohathi walipewa miji miwili - Taanaki pamoja na maeneo yake ya malisho na Gathirimoni pamoja na maeneo yake ya malisho.
26 Alle the citees ten, and the subarbis `of tho weren youun to the sones of Caath, of the lowere degree.
Kulikuwa na miji kumi kwa ujumla wake kwa ajili ya koo zilizosalia za Wakohathi, pamoja na maeneo yao ya malisho.
27 Also to the sones of Gerson, of the kyn of Leuy, Josue yaf of the half lynage of Manasses, citees of refuyt, Gaulon in Basan, and Bosra, with her subarbis, `twei citees.
Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, jamaa za Gershoni, ambazo hizi zilikuwa ni koo zingine za Walawi, zilipewa Golani katika Bashani pamoja na maeneo yao ya malisho, ni mji wa makimbilio kwa ajili ya mtu yeyote aliyeua mtu bila kukusudia, sambamba na Beeshitera pamoja na maeneo yake ya malisho - ilikuwa miji miwili kwa ujumla.
28 Forsothe of the lynage of Isachar, he yaf Cesion, and Daberath,
Koo za Gershoni zilipewa pia miji minne kutoka kwa kabila la Isakari - Kishoni sambamba na maeneo yake ya malisho, Daberathi pamoja na maeneo yake ya malisho,
29 and Jerimoth, and Engannym, with her subarbis; `foure citees.
Yarmuthi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Engnimu pamoja na maeneo yake ya malisho.
30 Of the lynage of Aser, he yaf Masal, and Abdon,
Kutoka katika kabila la Asheri, walipewa miji minne kwa ujumla - Mishali pamoja na maeneo yake ya malisho, Abdoni pamoja na maeneo yake ya malisho,
31 and Elecath, and Roob, with her subarbis; `foure citees.
Helikathi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Rehobu pamoja na maeneo yake ya malisho.
32 Also of the lynage of Neptalym, `he yaf the citee of refuyt, Cedes in Galile, and Amodor, and Carthan, with her subarbis; `thre citees.
Kutoka kwa kabila la Nafutali, nasaba za Gershoni walipewa miji mitatu kwa ujumla - Kedeshi katika Galilaya pamoja na maeneo yake ya malisho, ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu yeyote aliyeua mtu bila kukusudia; na Hamothidori pamoja na maeneo yake ya malisho, na Kartani pamoja na maeneo yake ya malisho.
33 Alle the citees of the meynees of Gerson weren threttene, with her subarbis.
Kulikuwa na miji kumi na mitatu kwa ujumla, kujumuisha na maeneo yake ya malisho, kwa ajili ya koo za Gershoni.
34 Sotheli to the sones of Merary, dekenes of the lowere degree, bi her meynees, was youun Getheran, of the linage of Zabulon, and Charcha, and Demna, and Nalol;
Na kwa Walawi waliosalia, koo za Merari waliokuwa wamepewa kutoka katika kabila la Zabuloni: Yokneamu pamoa na maeneo yake ya marisho, Karta pamoja na maeneo yake ya malisho,
35 `foure citees, with her subarbis.
Dimna pamoja na maeneo yake ya malisho, na Nahalali pamoja na maeneo yake ya malisho- ilikuwa ni miji minne kwa ujumla.
36 And of the lynage of Gad, he yaf the citee of refuyt, Ramoth in Galaad, and Manaym, and Esebon, and Jaser; `foure citees, with her subarbis.
Kwa mbari za Merari walipewa miji minne kutoka katika kabila la Rubeni: Bezeri pamoja na maeneo yake ya malisho, Yahazi pamoja na maene yake ya malisho,
37 And of the lynage of Ruben, biyende Jordan, ayens Jerico, he yaf `the citee of refuyt, Bosor in the wildirnesse of Mysor, and Jazer, and Jecson, and Maspha; `foure citees, with her subarbis.
na Kedemothi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Mefaathi pamoja na maeneo yake ya malisho.
Kutoka katika kabila la Gadi walipewa miji ya Ramothi katika Gileadi pamoja na sehemu zake za malisho - huu ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu mwenzake bila kukusudia - na Mahanaimu pamoja na sehemu zake za malisho.
Koo za Merari zilipewa pia Heshiboni pamoja na maeneo yake ya malisho, na Yazeri pamoja na malisho yake.
40 Alle the citees of Merary, bi her meynees and kynredis, weren twelue.
Hii ilikuwa ni miji minne kwa ujumla wake. Hii yote ilikuwa ni miji ya koo kadhaa za Merari, ambao walitoka katika kabila la Lawi, miji kumi na miwili walipewa wao kwa kupiga kura.
41 And so alle the citees of Leuytis, in the myddis of possessioun of the sones of Israel, weren eiyte and fourti, with her subarbis;
Miji waliyopewa Walawi kutoka katikati ya nchi iliyomilikiwa na watu wa Israeli ilikuwa miji arobaini na nane, kujumuisha na sehemu za malisho yao.
42 and alle citees weren departid by meynees.
Miji hii kila mmoja ulikuwa na maeneo yake ya malisho kwa kuuzunguka mji. Miji hii yote ilikuwa hivyo.
43 And the Lord yaf to Israel al the lond which he swoor hym silf to yyue to the fadris `of hem, and thei hadden it in possessioun, and dwelliden therynne.
Basi Yahweh aliwapa Israeli nchi yote ambayo aliwaapia baba zao kuwa atawapa. Waisraeli waliimiliki nchi na wakakaa humo.
44 And pees was youun of hym in to alle naciouns `by cumpas; and noon of enemyes was hardi to withstonde hem, but alle weren dryuen in to the lordschip `of hem.
Kisha Yahweh akawapa pumziko kwa kila upande, kama tu alivyowaahidia baba zao. Hakuna hata adui mmoja atakayeweza kuwashinda. Yawhew aliwatia maadui wao wote mikononi mwao.
45 Forsothe nether o word, which he bihiyte him silf to yyue to hem, was voide, but alle wordis weren fillid in werkis.
Hakuna hata kitu kimoja miongoni kwa ahadi nzuri ambazo Yahweh alizisema kwa nyumba ya Israeli ambazo hazikutimia. Ahadi zote zilitimia.