< John 8 >

1 But Jhesus wente in to the mount of Olyuete.
Lakini Yesu akaenda katika Mlima wa Mizeituni.
2 And eerli eft he cam in to the temple; and al the puple cam to hym; and he sat, and tauyte hem.
Alfajiri na mapema Yesu akaja tena Hekaluni, watu wote wakakusanyika, akakaa akaanza kuwafundisha.
3 And scribis and Fariseis bryngen a womman takun in auoutrye, and thei settiden hir in the myddil,
Walimu wa sheria na Mafarisayo wakamleta mwanamke mmoja aliyefumaniwa akizini. Wakamsimamisha katikati ya umati wa watu wote.
4 and seiden to hym, Maystir, this womman is now takun in auoutrie.
Wakamwambia Yesu, “Mwalimu, huyu mwanamke amekutwa akizini.
5 And in the lawe Moises comaundide vs to stoone suche; therfor what seist thou?
Katika sheria, Mose alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake wa namna hii, mpaka wafe. Sasa wewe wasemaje?”
6 And thei seiden this thing temptynge hym, that thei myyten accuse hym. And Jhesus bowide hym silf doun, and wroot with his fyngur in the erthe.
Walimuuliza swali hili kama mtego ili wapate sababu ya kumshtaki. Lakini Yesu akainama akaanza kuandika ardhini kwa kidole chake.
7 And whanne thei abiden axynge hym, he reiside hym silf, and seide to hem, He of you that is without synne, first caste a stoon in to hir.
Walipoendelea kumuulizauliza akainuka, akawaambia, “Kama kuna mtu yeyote miongoni mwenu ambaye hana dhambi na awe wa kwanza kumtupia jiwe.”
8 And eft he bowide hym silf, and wroot in the erthe.
Akainama tena na kuandika ardhini.
9 And thei herynge these thingis, wenten awei oon aftir anothir, and thei bigunnen fro the eldre men; and Jhesus dwelte aloone, and the womman stondynge in the myddil.
Waliposikia haya, wakaanza kuondoka mmoja mmoja, wakianzia wazee, hadi Yesu akabaki peke yake na yule mwanamke akiwa amesimama mbele yake.
10 And Jhesus reiside hym silf, and seide to hir, Womman, where ben thei that accusiden thee? no man hath dampned thee.
Yesu akainuka na kumwambia, “Wako wapi wale waliokuwa wanakuhukumu kuwa mwenye hatia?”
11 Sche seide, No man, Lord. Jhesus seide `to hir, Nethir Y schal dampne thee; go thou, and now aftirward nyle thou synne more.
Yule mwanamke akajibu, “Hakuna hata mmoja Bwana.” Yesu akamwambia, “Hata mimi sikuhukumu. Nenda zako, kuanzia sasa usitende dhambi tena.”]
12 Therfor eft Jhesus spak to hem, and seide, Y am the liyt of the world; he that sueth me, walkith not in derknessis, but schal haue the liyt of lijf.
Kisha Yesu akasema nao tena akawaambia, “Mimi ni nuru ya ulimwengu. Mtu yeyote akinifuata hatatembea gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.”
13 Therfor the Fariseis seiden, Thou berist witnessyng of thi silf; thi witnessyng is not trewe.
Mafarisayo wakamwambia, “Ushuhuda wako haukubaliki kwa kuwa unajishuhudia mwenyewe.”
14 Jhesus answerde, and seide to hem, And if Y bere witnessyng of my silf, my witnessyng is trewe; for Y woot fro whennus Y cam, and whidur Y go.
Yesu akawajibu, “Hata kama najishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ni kweli kwa sababu najua nilikotoka na ninakokwenda. Lakini ninyi hamjui nilikotoka wala ninakokwenda.
15 But ye witen not fro whennus Y cam, ne whidur Y go. For ye demen aftir the fleisch, but Y deme no man;
Ninyi mnahukumu kwa kufuata vipimo vya kibinadamu, mimi simhukumu mtu yeyote.
16 and if Y deme, my doom is trewe, for Y am not aloone, but Y and the fadir that sente me.
Lakini hata kama nikihukumu, uamuzi wangu ni sahihi kwa sababu sitoi hukumu yangu peke yangu, bali niko pamoja na Baba, aliyenituma.
17 And in youre lawe it is writun, that the witnessyng of twei men is trewe.
Imeandikwa katika Sheria yenu kwamba, ushahidi wa watu wawili ni thabiti.
18 Y am, that bere witnessyng of my silf, and the fadir that sente me, berith witnessyng of me.
Mimi najishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenituma hunishuhudia.”
19 Therfor thei seiden to hym, Where is thi fadir? Jhesus answeride, Nether ye knowen me, nethir ye knowen my fadir; if ye knewen me, perauenture ye schulden knowe also my fadir.
Ndipo wakamuuliza, “Huyo Baba yako yuko wapi?” Yesu akawajibu, “Ninyi hamnifahamu mimi ni nani, wala hammfahamu Baba yangu. Kama mngenifahamu mimi, mngemfahamu na Baba yangu.”
20 Jhesus spak these wordis in the tresorie, techynge in the temple; and no man took hym, for his our cam not yit.
Yesu alisema maneno haya alipokuwa akifundisha katika chumba cha hazina Hekaluni. Lakini hakuna mtu aliyemkamata kwa kuwa saa yake ilikuwa haijawadia.
21 Therfor eft Jhesus seide to hem, Lo! Y go, and ye schulen seke me, and ye schulen die in youre synne; whidur Y go, ye moun not come.
Yesu akawaambia tena, “Ninaenda zangu, nanyi mtanitafuta, lakini mtakufa katika dhambi zenu. Niendako mimi ninyi hamwezi kuja.”
22 Therfor the Jewis seiden, Whether he schal sle hym silf, for he seith, Whidur Y go, ye moun not come?
Ndipo wale Wayahudi wakasema, “Je, atajiua? Je, hii ndiyo sababu amesema, ‘Niendako mimi ninyi hamwezi kuja’?”
23 And he seide to hem, Ye ben of bynethe, Y am of aboue; ye ben of this world, Y am not of this world.
Akawaambia, “Ninyi mmetoka chini, mimi nimetoka juu. Ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.
24 Therfor Y seide to you, that ye schulen die in youre synnes; for if ye bileuen not that Y am, ye schulen die in youre synne.
Niliwaambia kuwa mtakufa katika dhambi zenu, kwa maana msipoamini ya kwamba ‘Mimi Ndiye,’ mtakufa katika dhambi zenu.”
25 Therfor thei seiden to hym, Who art thou? Jhesus seide to hem, The bigynnyng, which also speke to you.
Wakamuuliza, “Wewe ni nani?” Naye Yesu akawajibu, “Mimi ndiye yule ambaye nimekuwa nikiwaambia tangu mwanzo.
26 Y haue many thingis to speke, and deme of you, but he that sente me is sothefast; and Y speke in the world these thingis, that Y herde of hym.
Nina mambo mengi ya kusema juu yenu na mengi ya kuwahukumu. Lakini yeye aliyenituma ni wa kweli, nami nanena na ulimwengu niliyoyasikia kutoka kwake.”
27 And thei knewen not, that he clepide his fadir God.
Hawakuelewa kuwa alikuwa akiwaambia juu ya Baba yake wa Mbinguni.
28 Therfor Jhesus seith to hem, Whanne ye han areisid mannus sone, thanne ye schulen knowe, that Y am, and of my silf Y do no thing; but as my fadir tauyte me, Y speke these thingis.
Kisha Yesu akawaambia, “Mtakapokwisha kumwinua juu Mwana wa Adamu, ndipo mtakapojua kuwa, ‘Mimi ndiye yule niliyesema na kwamba mimi sitendi jambo lolote peke yangu bali ninasema yale tu ambayo Baba yangu amenifundisha.
29 And he that sente me is with me, and lefte me not aloone; for Y do euermore tho thingis, that ben plesynge to hym.
Yeye aliyenituma yu pamoja nami, hajaniacha, kwa kuwa siku zote nafanya mapenzi yake.’”
30 Whanne he spak these thingis, manye bileueden in hym.
Wengi waliomsikia Yesu akisema maneno haya wakamwamini.
31 Therfor Jhesus seide to the Jewis, that bileueden in hym, If ye dwellen in my word, verili ye schulen be my disciplis;
Kisha Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, “Kama mkidumu katika maneno yangu, mtakuwa wanafunzi wangu kweli kweli.
32 and ye schulen knowe the treuthe, and the treuthe schal make you fre.
Ndipo mtaijua kweli nayo kweli itawaweka huru.”
33 Therfor the Jewis answeriden to hym, We ben the seed of Abraham, and we serueden neuere to man; hou seist thou, That ye schulen be fre?
Wao wakamjibu, “Sisi tu wazao wa Abrahamu, nasi hatujawa watumwa wa mtu yeyote. Wawezaje kusema kwamba tutawekwa huru?”
34 Jhesus answeride to hem, Treuli, treuli, Y seie to you, ech man that doith synne, is seruaunt of synne.
Yesu akajibu, “Amin, amin nawaambia, kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi.
35 And the seruaunt dwellith not in the hows with outen ende, but the sone dwellith with outen ende. (aiōn g165)
Mtumwa hakai nyumbani anakotumika siku zote, lakini mwana hukaa nyumbani daima. (aiōn g165)
36 Therfor if the sone make you fre, verili ye schulen be fre.
Hivyo Mwana akiwaweka huru mtakuwa huru kweli kweli.
37 Y woot that ye ben Abrahams sones, but ye seken to sle me, for my word takith not in you.
Ninajua ya kuwa ninyi ni wazao wa Abrahamu, lakini mnatafuta wasaa wa kuniua kwa sababu ndani yenu hamna nafasi ya neno langu.
38 Y speke tho thingis, that Y say at my fadir; and ye doen tho thingis, that ye sayn at youre fadir.
Ninasema yale niliyoyaona mbele za Baba yangu, nanyi inawapa kufanya yale mliyosikia kutoka kwa baba yenu.”
39 Thei answerden, and seiden to hym, Abraham is oure fadir. Jhesus seith to hem, If ye ben the sones of Abraham, do ye the werkis of Abraham.
Wakajibu, “Baba yetu ni Abrahamu.” Yesu akawaambia, “Kama mngekuwa wazao wa Abrahamu mngefanya mambo yale aliyofanya Abrahamu.
40 But now ye seken to sle `me, a man that haue spoken to you treuthe, that Y herde of God; Abraham dide not this thing.
Lakini sasa ninyi mnatafuta kuniua, mtu ambaye nimewaambia kweli ile niliyosikia kutoka kwa Mungu, Abrahamu hakufanya jambo la namna hii.
41 Ye doen the werkis of youre fadir. Therfor thei seiden to hym, We ben not borun of fornycacioun; we han o fadir, God.
Ninyi mnafanya mambo afanyayo baba yenu.” Wakamjibu, “Sisi hatukuzaliwa kwa uzinzi. Tunaye Baba mmoja, Mungu pekee.”
42 But Jhesus seith to hem, If God were youre fadir, sotheli ye schulden loue me; for Y passide forth of God, and cam; for nether Y cam of my silf, but he sente me.
Yesu akawaambia, “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mngenipenda, kwa maana nilitoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikuja kwa ajili yangu mwenyewe, ila yeye alinituma.
43 Whi knowen ye not my speche? for ye moun not here my word.
Kwa nini hamwelewi ninayowaambia? Ni kwa sababu hamwezi kusikia nisemacho.
44 Ye ben of the fadir, the deuel, and ye wolen do the desyris of youre fadir. He was a mansleere fro the bigynnyng, and he stood not in treuthe; for treuthe is not in hym. Whanne he spekith lesyng, he spekith of his owne; for he is a liere, and fadir of it.
Ninyi ni watoto wa baba yenu ibilisi, nanyi mnataka kutimiza matakwa ya baba yenu. Yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo, wala hakushikana na kweli maana hamna kweli ndani yake. Asemapo uongo husema yaliyo yake mwenyewe kwa maana yeye ni mwongo na baba wa huo uongo.
45 But for Y seie treuthe, ye bileuen not to me.
Lakini kwa sababu nimewaambia kweli hamkuniamini!
46 Who of you schal repreue me of synne? if Y sey treuthe, whi bileuen ye not to me?
Je, kuna yeyote miongoni mwenu awezaye kunithibitisha kuwa mwenye dhambi? Kama nawaambia yaliyo kweli, mbona hamniamini?
47 He that is of God, herith the wordis of God; therfor ye heren not, for ye ben not of God.
Yeye atokaye kwa Mungu husikia kile Mungu asemacho. Sababu ya ninyi kutosikia ni kwa kuwa hamtokani na Mungu.”
48 Therfor the Jewis answeriden, and seiden, Whether we seien not wel, that thou art a Samaritan, and hast a deuel?
Wayahudi wakamjibu Yesu, “Je, hatuko sahihi tunaposema ya kwamba wewe ni Msamaria na ya kwamba una pepo mchafu?”
49 Jhesus answerde, and seide, Y haue not a deuel, but Y onoure my fadir, and ye han vnhonourid me.
Yesu akawajibu, “Mimi sina pepo mchafu, bali ninamheshimu Baba yangu, nanyi mnanidharau.
50 For Y seke not my glorye; there is he, that sekith, and demeth.
Lakini mimi sitafuti utukufu wangu mwenyewe, bali yuko anayetaka kunitukuza, naye ndiye mwamuzi.
51 Treuli, treuli, Y seie to you, if ony man kepe my word, he schal not taste deth with outen ende. (aiōn g165)
Amin, amin nawaambia, mtu yeyote akilitii neno langu hataona mauti milele.” (aiōn g165)
52 Therfor the Jewis seiden, Now we han knowun, that thou hast a deuel. Abraham is deed, and the prophetis, and thou seist, If ony man kepe my word, he schal not taste deth withouten ende. (aiōn g165)
Ndipo Wayahudi wakamwambia, “Sasa tumejua kwamba una pepo mchafu. Ikiwa Abrahamu alikufa na vivyo hivyo manabii, nawe unasema ‘Mtu akitii neno langu hatakufa milele.’ (aiōn g165)
53 Whether thou art grettere than oure fader Abraham, that is deed, and the prophetis ben deed; whom makist thou thi silf?
Je, wewe ni mkuu kuliko baba yetu Abrahamu ambaye alikufa na manabii ambao nao pia walikufa? Hivi wewe unajifanya kuwa nani?”
54 Jhesus answeride, If Y glorifie my silf, my glorie is nouyt; my fadir, is that glorifieth me, whom ye seien, that he is youre God.
Yesu akawajibu, “Kama nikijitukuza utukufu wangu hauna maana. Baba yangu, huyo ambaye ninyi mnadai kuwa ni Mungu wenu, ndiye anitukuzaye mimi.
55 And ye han not knowun hym, but Y haue knowun hym; and if Y seie that Y knowe hym not, Y schal be a liere lich to you; but Y knowe hym, and Y kepe his word.
Ingawa hamkumjua, mimi ninamjua. Kama ningesema simjui, ningekuwa mwongo kama ninyi, lakini mimi ninamjua na ninalitii neno lake.
56 Abraham, youre fadir, gladide to se my dai; and he saiy, and ioyede.
Baba yenu Abrahamu alishangilia kwamba angaliiona siku yangu, naye akaiona na akafurahi.”
57 Thanne the Jewis seiden to hym, Thou hast not yit fifti yeer, and hast thou seien Abraham?
Wayahudi wakamwambia, “Wewe hujatimiza hata miaka hamsini, wewe wasema umemwona Abrahamu?”
58 Therfor Jhesus seide to hem, Treuli, treuli, Y seie to you, bifor that Abraham schulde be, Y am.
Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, kabla Abrahamu hajakuwako, ‘Mimi niko.’”
59 Therfor thei token stonys, to caste to hym; but Jhesus hidde hym, and wente out of the temple.
Ndipo wakaokota mawe ili kumpiga, lakini Yesu akajificha, naye akatoka Hekaluni.

< John 8 >