< John 6 >
1 Aftir these thingis Jhesus wente ouere the see of Galilee, that is Tiberias.
Baada ya haya, Yesu alikwenda ngʼambo ya Bahari ya Galilaya, ambayo pia huitwa Bahari ya Tiberia.
2 And a greet multitude suede hym; for thei sayn the tokenes, that he dide on hem that weren sijke.
Umati mkubwa wa watu uliendelea kumfuata, kwa sababu waliona ishara nyingi za miujiza alizofanya kwa wagonjwa.
3 Therfor Jhesus wente in to an hil, and sat there with hise disciplis.
Kisha Yesu akapanda mlimani akaketi huko pamoja na wanafunzi wake.
4 And the paske was ful niy, a feeste dai of the Jewis.
Pasaka ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
5 Therfor whanne Jhesus hadde lift vp hise iyen, and hadde seyn, that a greet multitude cam to hym, he seith to Filip, Wherof schulen we bie looues, that these men ete?
Yesu alipotazama na kuuona ule umati mkubwa wa watu ukimjia, akamwambia Filipo, “Tutanunua wapi mikate ili watu hawa wale?”
6 But he seide this thing, temptynge hym; for he wiste what he was to do.
Aliuliza swali hili kumpima, kwa maana alishajua la kufanya.
7 Filip answerde to hym, The looues of tweyn hundrid pans sufficen not to hem, that ech man take a litil what.
Filipo akamjibu, “Hata fedha kiasi cha dinari mia mbili, hazitoshi kununua mikate ya kuwapa watu hawa ili kila mtu apate kidogo.”
8 Oon of hise disciplis, Andrew, the brothir of Symount Petre,
Mmoja wa wanafunzi wake aitwaye Andrea, ndugu yake Simoni Petro, akamwambia,
9 seith to him, A child is here, that hath fyue barli looues and twei fischis; but what ben these among so manye?
“Hapa kuna mvulana mmoja mwenye mikate mitano ya shayiri na samaki wawili wadogo. Lakini hivi vitatosha nini kwa umati huu wote?”
10 Therfor Jhesus seith, Make ye hem sitte to the mete. And there was myche hey in the place. And so men saten to the mete, as `fyue thousynde in noumbre.
Yesu akasema, “Waketisheni watu chini.” Palikuwa na majani mengi katika eneo lile, nao watu wakaketi. Palikuwa na wanaume wapatao 5,000.
11 And Jhesus took fyue looues, and whanne he hadde do thankyngis, he departide to men that saten to the mete, and also of the fischis, as myche as thei wolden.
Ndipo Yesu akachukua ile mikate, akamshukuru Mungu na kuwagawia wale watu waliokuwa wameketi. Akafanya vivyo hivyo na wale samaki. Kila mtu akapata kadiri alivyotaka.
12 And whanne thei weren fillid, he seide to hise disciplis, Gadir ye the relifs that ben left, that thei perischen not.
Watu wote walipokwisha kula na kushiba, akawaambia wanafunzi wake, “Kusanyeni vipande vilivyobaki vya ile mikate, kisipotee chochote.”
13 And so thei gadriden, and filliden twelue cofyns of relif of the fyue barli looues and twei fischis, that lefte to hem that hadden etun.
Hivyo wakavikusanya, wakajaza vikapu kumi na viwili kwa vipande vya ile mikate mitano ya shayiri na samaki wale wawili wadogo vilivyobakishwa na waliokula.
14 Therfor tho men, whanne thei hadden seyn the signe that he hadde don, seiden, For this is verili the profete, that is to come in to the world.
Baada ya watu kuona muujiza ule Yesu aliofanya, walianza kusema, “Hakika huyu ndiye Nabii ajaye ulimwenguni!”
15 And whanne Jhesus hadde knowun, that thei weren to come to take hym, and make hym kyng, he fleiy `aloone eft in to an hille.
Yesu akijua kwamba walitaka kuja kumfanya awe mfalme wao, kwa nguvu, akajitenga nao akaenda milimani peke yake.
16 And whanne euentid was comun, his disciplis wenten doun to the see.
Ilipofika jioni, wanafunzi wake waliteremka kwenda baharini.
17 And thei wenten vp in to a boot, and thei camen ouer the see in to Cafarnaum. And derknessis weren maad thanne, and Jhesus was not come to hem.
Wakaingia kwenye mashua, wakaanza kuvuka bahari kwenda Kapernaumu. Wakati huu kulikuwa tayari giza na Yesu alikuwa hajajumuika nao.
18 And for a greet wynde blew, the see roos vp.
Bahari ikachafuka kwa sababu upepo mkali ulikuwa unavuma.
19 Therfor whanne thei hadden rowid as fyue and twenti furlongis or thretti, thei seen Jhesus walkynge on the see, and to be neiy the boot; and thei dredden.
Wanafunzi walipokuwa wamekwenda mwendo wa karibu maili tatu au nne, walimwona Yesu akitembea juu ya maji akikaribia mashua, nao wakaogopa sana.
20 And he seide to hem, Y am; nyle ye drede.
Lakini Yesu akawaambia, “Ni mimi. Msiogope.”
21 Therfor thei wolden take hym in to the boot, and anoon the boot was at the loond, to which thei wenten.
Ndipo wakamkaribisha kwa furaha ndani ya mashua, na mara wakafika ufuoni walikokuwa wakienda.
22 On `the tother dai the puple, that stood ouer the see, say, that ther was noon other boot there but oon, and that Jhesu entride not with hise disciplis in to the boot, but hise disciplis aloone wenten.
Siku iliyofuata, wale watu waliokuwa wamebaki ngʼambo waliona kwamba palikuwepo na mashua moja tu na kwamba Yesu hakuwa ameondoka pamoja na wanafunzi wake, ila walikuwa wameondoka peke yao.
23 But othere bootis camen fro Tiberias bisidis the place, where thei hadden eetun breed, and diden thankyngis to God.
Lakini zikaja mashua nyingine kutoka Tiberia zikafika karibu na mahali pale walipokula mikate baada ya Bwana kumshukuru Mungu.
24 Therfor whanne the puple hadde seyn, that Jhesu was not there, nether hise disciplis, thei wenten vp in to bootis, and camen to Cafarnaum, sekynge Jhesu.
Mara wale watu wakatambua kwamba Yesu hakuwepo hapo, wala wanafunzi wake. Wakaingia kwenye mashua hizo, wakaenda Kapernaumu ili kumtafuta Yesu.
25 And whanne thei hadden foundun hym ouer the see, thei seiden to hym, Rabi, hou come thou hidur?
Walipomkuta Yesu ngʼambo ya bahari wakamuuliza, “Rabi, umefika lini huku?”
26 Jhesus answerde to hem, and seide, Treuli, treuli, Y seie to you, ye seken me, not for ye sayn the myraclis, but for ye eten of looues, and weren fillid.
Yesu akawajibu, “Amin, amin nawaambia, ninyi hamnitafuti kwa kuwa mliona ishara na miujiza, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba.
27 Worche ye not mete that perischith, but that dwellith in to euerlastynge lijf, which mete mannys sone schal yyue to you; for God the fadir hath markid hym. (aiōnios )
Msishughulikie chakula kiharibikacho, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele, ambacho Mwana wa Adamu atawapa. Yeye ndiye ambaye Mungu Baba amemtia muhuri.” (aiōnios )
28 Therfor thei seiden to hym, What schulen we do, that we worche the werkis of God?
Ndipo wakamuuliza, “Tufanye nini ili tupate kuitenda kazi ya Mungu?”
29 Jhesus answerde, and seide to hem, This is the werk of God, that ye bileue to hym, whom he sente.
Yesu akawajibu, “Kazi ya Mungu ndiyo hii: Mwaminini yeye aliyetumwa naye.”
30 Therfor thei seiden to hym, What tokene thanne doist thou, that we seen, and bileue to thee? what worchist thou?
Hivyo wakamuuliza, “Utafanya ishara gani ya muujiza, ili tuione tukuamini? Utafanya jambo gani?
31 Oure fadris eeten manna in desert, as it is writun, He yaf to hem breed fro heuene to ete.
Baba zetu walikula mana jangwani, kama ilivyoandikwa, ‘Aliwapa mikate kutoka mbinguni ili wale.’”
32 Therfor Jhesus seith to hem, Treuli, treuli, Y seie to you, Moyses yaf you not breed fro heuene, but my fadir yyueth you veri breed fro heuene;
Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, si Mose aliyewapa mikate kutoka mbinguni, bali Baba yangu ndiye anawapa mkate wa kweli kutoka mbinguni.
33 for it is very breed that cometh doun fro heuene, and yyueth lijf to the world.
Kwa maana mkate wa Mungu ni yule ashukaye kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.”
34 Therfor thei seiden to hym, Lord, euere yyue vs this breed.
Wakamwambia, “Bwana, kuanzia sasa tupatie huo mkate siku zote.”
35 And Jhesus seide to hem, Y am breed of lijf; he that cometh to me, schal not hungur; he that bileueth in me, schal neuere thirste.
Yesu akawaambia, “Mimi ndimi mkate wa uzima. Yeye ajaye kwangu, hataona njaa kamwe na yeye aniaminiye, hataona kiu kamwe.
36 But Y seid to you, that ye han seyn me, and ye bileueden not.
Lakini kama nilivyowaambia, mmeniona lakini bado hamwamini.
37 Al thing, that the fadir yyueth to me, schal come to me; and Y schal not caste hym out, that cometh to me.
Wale wote anipao Baba watakuja kwangu na yeyote ajaye kwangu, sitamfukuzia nje kamwe.
38 For Y cam doun fro heuene, not that Y do my wille, but the wille of hym that sente me.
Kwa kuwa nimeshuka kutoka mbinguni si ili kufanya mapenzi yangu, bali mapenzi yake yeye aliyenituma.
39 And this is the wille of the fadir that sente me, that al thing that the fadir yaf me, Y leese not of it, but ayen reise it in the laste dai.
Haya ndiyo mapenzi yake yeye aliyenituma, kwamba, nisimpoteze hata mmoja wa wale alionipa, bali niwafufue siku ya mwisho.
40 And this is the wille of my fadir that sente me, that ech man that seeth the sone, and bileueth in hym, haue euerlastynge lijf; and Y schal ayen reyse hym in the laste dai. (aiōnios )
Kwa maana mapenzi ya Baba yangu ni kwamba kila mmoja amtazamaye, Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele, nami nitawafufua siku ya mwisho.” (aiōnios )
41 Therfor Jewis grutchiden of hym, for he hadde seid, Y am breed that cam doun fro heuene.
Wayahudi wakaanza kunungʼunika kwa kuwa alisema, “Mimi ndimi mkate ulioshuka kutoka mbinguni.”
42 And thei seiden, Whether this is not Jhesus, the sone of Joseph, whos fadir and modir we han knowun. Hou thanne seith this, That Y cam doun fro heuene?
Wakasema, “Huyu si Yesu, mwana wa Yosefu, ambaye baba yake na mama yake tunawajua? Anawezaje basi sasa kusema, ‘Nimeshuka kutoka mbinguni’?”
43 Therfor Jhesus answerde, and seide to hem, Nyle ye grutche togidere.
Hivyo Yesu akawaambia, “Acheni kunungʼunikiana ninyi kwa ninyi.
44 No man may come to me, but if the fadir that sente me, drawe hym; and Y schal ayen reise hym in the laste dai. It is writun in prophetis,
Hakuna mtu awezaye kuja kwangu kama asipovutwa na Baba aliyenituma, nami nitamfufua siku ya mwisho.
45 And alle men schulen be able for to be tauyt `of God. Ech man that herde of the fadir, and hath lerned, cometh to me.
Imeandikwa katika Manabii, ‘Wote watafundishwa na Mungu.’ Yeyote amsikilizaye Baba na kujifunza kutoka kwake, huyo huja kwangu.
46 Not for ony man hath sey the fadir, but this that is of God, hath sey the fadir.
Hakuna mtu yeyote aliyemwona Baba isipokuwa yeye atokaye kwa Mungu, yeye ndiye peke yake aliyemwona Baba.
47 Sotheli, sotheli, Y seie to you, he that bileueth in me, hath euerlastynge lijf. (aiōnios )
Amin, amin nawaambia, yeye anayeamini anao uzima wa milele. (aiōnios )
49 Youre fadris eeten manna in desert, and ben deed.
Baba zenu walikula mana jangwani, lakini wakafa.
50 This is breed comynge doun fro heuene, that if ony man ete therof, he die not.
Lakini hapa kuna mkate utokao mbinguni, ambao mtu yeyote akiula, hatakufa.
51 Y am lyuynge breed, that cam doun fro heuene. If ony man ete of this breed, he schal lyue withouten ende. And the breed that Y schal yyue, is my fleisch for the lijf of the world. (aiōn )
Mimi ni mkate wa uzima ule uliotoka mbinguni. Mtu yeyote akiula mkate huu, ataishi milele. Mkate huu ni mwili wangu, ambao nitautoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.” (aiōn )
52 Therfor the Jewis chidden togidere, and seiden, Hou may this yyue to vs his fleisch to ete?
Ndipo Wayahudi wakaanza kuhojiana vikali wao kwa wao wakisema, “Mtu huyu awezaje kutupatia mwili wake tuule?”
53 Therfor Jhesus seith to hem, Treuli, treuli, Y seie to you, but ye eten the fleisch of mannus sone, and drenken his blood, ye schulen not haue lijf in you.
Hivyo Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, msipoula mwili wa Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu.
54 He that etith my fleisch, and drynkith my blood, hath euerlastynge lijf, and Y schal ayen reise hym in the laste dai. (aiōnios )
Mtu yeyote aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, anao uzima wa milele. Nami nitamfufua siku ya mwisho. (aiōnios )
55 For my fleisch is veri mete, and my blood is very drynk.
Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli.
56 He that etith my fleisch, and drynkith my blood, dwellith in me, and Y in hym.
Yeyote alaye mwili wangu na kunywa damu yangu, atakaa ndani yangu nami nitakaa ndani yake.
57 As my fadir lyuynge sente me, and Y lyue for the fadir, and he that etith me, he schal lyue for me.
Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, na kama nami ninavyoishi kwa sababu ya Baba, hivyo anilaye mimi ataishi kwa sababu yangu.
58 This is breed, that cam doun fro heuene. Not as youre fadris eten manna, and ben deed; he that etith this breed, schal lyue withouten ende. (aiōn )
Huu ndio mkate ushukao kutoka mbinguni, si kama ule mkate baba zenu waliokula nao wakafa. Lakini yeye aulaye mkate huu ataishi milele.” (aiōn )
59 He seide these thingis in the synagoge, techynge in Cafarnaum.
Yesu alisema maneno haya alipokuwa akifundisha katika sinagogi huko Kapernaumu.
60 Therfor many of hise disciplis herynge, seiden, This word is hard, who may here it?
Wengi wa wafuasi wake waliposikia jambo hili wakasema, “Mafundisho haya ni magumu. Ni nani awezaye kuyapokea?”
61 But Jhesus witynge at hym silf, that hise disciplis grutchiden of this thing, seide to hem, This thing sclaundrith you?
Yesu alipojua kwamba wafuasi wake wananungʼunika kuhusu mafundisho yake, akawaambia, “Je, jambo hili limewaudhi?
62 Therfor if ye seen mannus sone stiynge, where he was bifor?
Ingekuwaje basi kama mngemwona Mwana wa Adamu akipaa kwenda zake huko alipokuwa kwanza?
63 It is the spirit that quykeneth, the fleisch profitith no thing; the wordis that Y haue spokun to you, ben spirit and lijf.
Roho ndiye atiaye uzima, mwili haufai kitu. Maneno haya niliyowaambia ni Roho tena ni uzima.
64 But ther ben summe of you that bileuen not. For Jhesus wiste fro the bigynnynge, which weren bileuynge, and who was to bitraye hym.
Lakini baadhi yenu hamwamini.” Kwa maana Yesu alifahamu tangu mwanzo wale ambao hawangemwamini miongoni mwao na yule ambaye angemsaliti.
65 And he seide, Therfor Y seide to you, that no man may come to me, but it were youun to hym of my fadir.
Akaendelea kusema, “Hii ndiyo sababu niliwaambia kwamba hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.”
66 Fro this tyme many of hise disciplis wenten abak, and wenten not now with hym.
Tangu wakati huo wafuasi wake wengi wakarejea nyuma wakaacha kumfuata.
67 Therfor Jhesus seide to the twelue, Whether ye wolen also go awei?
Hivyo Yesu akawauliza wale wanafunzi wake kumi na wawili, “Je, ninyi pia mnataka kuondoka?”
68 And Symount Petre answeride to hym, Lord, to whom schulen we gon? Thou hast wordis of euerlastynge lijf; (aiōnios )
Simoni Petro akamjibu, “Bwana, tuondoke twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele. (aiōnios )
69 and we bileuen, and han knowun, that thou art Crist, the sone of God.
Tunaamini na kujua kuwa wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu.”
70 Therfor Jhesus answerde to hem, Whether Y chees not you twelue, and oon of you is a feend?
Ndipo Yesu akajibu, “Je, sikuwachagua ninyi kumi na wawili? Lakini mmoja wenu ni ibilisi.”
71 And he seide this of Judas of Symount Scarioth, for this was to bitraye hym, whanne he was oon of the twelue.
(Hapa alikuwa anasema juu ya Yuda, mwana wa Simoni Iskariote. Ingawa alikuwa mmoja wa wale kumi na wawili, ndiye ambaye baadaye angemsaliti Yesu.)