< John 3 >

1 And there was a man of the Farisees, Nychodeme bi name, a prince of the Jewis.
Basi palikuwa na mtu mmoja Farisayo, jina lake Nikodemo, mmoja wa Baraza la Wayahudi lililotawala.
2 And he cam to Jhesu bi niyt, and seide to hym, Rabi, we witen, that thou art comun fro God maister; for no man may do these signes, that thou doist, but God be with hym.
Huyu alimjia Yesu usiku akamwambia, “Rabi, tunajua kuwa wewe ni mwalimu uliyetumwa na Mungu, kwa maana hakuna mtu awezaye kufanya miujiza hii uifanyayo wewe, kama Mungu hayuko pamoja naye.”
3 Jhesus answerde, and seide to hym, Treuli, treuli, Y seie to thee, but a man be borun ayen, he may not se the kyngdom of God.
Yesu akamjibu, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu anayeweza kuuona Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa mara ya pili.”
4 Nychodeme seide to hym, Hou may a man be borun, whanne he is eeld? whether he may entre ayen in to his modris wombe, and be borun ayen?
Nikodemo akauliza, “Awezaje mtu kuzaliwa wakati akiwa mzee? Hakika hawezi kuingia mara ya pili kwenye tumbo la mama yake ili azaliwe!”
5 Jhesus answeride, Treuli, treuli, Y seie to thee, but a man be borun ayen of watir, and of the Hooli Goost, he may not entre in to the kyngdom of God.
Yesu akamwambia, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu yeyote anayeweza kuingia Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa kwa maji na kwa Roho.
6 `That that is borun of the fleisch, is fleisch; and `that that is borun of spirit, is spirit.
Mwili huzaa mwili, lakini Roho huzaa roho.
7 Wondre thou not, for Y seide to thee, It bihoueth you to be borun ayen.
Kwa hiyo usishangae ninapokuambia huna budi ‘kuzaliwa mara ya pili.’
8 The spirit brethith where he wole, and thou herist his vois, but thou wost not, fro whennus he cometh, ne whidir he goith; so is ech man that is borun of the spirit.
Upepo huvuma popote upendapo. Mvumo wake unausikia lakini huwezi ukafahamu utokako wala uendako. Ndivyo ilivyo kwa kila mtu aliyezaliwa na Roho.”
9 Nychodeme answeride, and seide to hym, Hou moun these thingis be don?
Nikodemo akamuuliza, “Mambo haya yanawezekanaje?”
10 Jhesus answeride, and seide to hym, Thou art a maister in Israel, and knowist not these thingis?
Yesu akamwambia, “Wewe ni mwalimu mashuhuri wa Waisraeli, nawe huelewi mambo haya?
11 Treuli, treuli, Y seie to thee, for we speken that that we witen, and we witnessen that that we han seyn, and ye taken not oure witnessyng.
Amin, amin ninakuambia, sisi tunazungumza lile tunalolijua na tunashuhudia lile tuliloliona. Lakini ninyi watu hamkubali ushuhuda wetu.
12 If Y haue seid to you ertheli thingis, and ye bileuen not, hou if Y seie to you heueneli thingis, schulen ye bileue?
Nimewaambia mambo ya duniani, nanyi hamkuniamini, mtaniaminije basi nitakapowaambia mambo ya mbinguni?
13 And no man stieth in to heuene, but he that cam doun fro heuene, mannys sone that is in heuene.
Hakuna mtu yeyote aliyekwenda mbinguni isipokuwa yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu.
14 And as Moises areride a serpent in desert, so it bihoueth mannys sone to be reisid,
Kama vile Mose alivyomwinua yule nyoka kule jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu.
15 that ech man that bileueth in hym, perische not, but haue euerlastynge lijf. (aiōnios g166)
Ili kila mtu amwaminiye awe na uzima wa milele. (aiōnios g166)
16 For God louede so the world, that he yaf his `oon bigetun sone, that ech man that bileueth in him perische not, but haue euerlastynge lijf. (aiōnios g166)
“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. (aiōnios g166)
17 For God sente not his sone in to the world, that he iuge the world, but that the world be saued bi him.
Kwa maana Mungu hakumtuma Mwanawe kuuhukumu ulimwengu, bali kupitia kwake ulimwengu upate kuokolewa.
18 He that bileueth in hym, is not demed; but he that bileueth not, is now demed, for he bileueth not in the name of the `oon bigetun sone of God.
Yeyote amwaminiye hahukumiwi, lakini asiyeamini amekwisha kuhukumiwa, kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.
19 And this is the dom, for liyt cam in to the world, and men loueden more derknessis than liyt; for her werkes weren yuele.
Hii ndiyo hukumu kwamba: Nuru imekuja ulimwenguni, nao watu wakapenda giza kuliko nuru kwa sababu matendo yao ni maovu.
20 For ech man that doith yuele, hatith the liyt; and he cometh not to the liyt, that hise werkis be not repreued.
Kwa kuwa kila atendaye maovu huchukia nuru, wala haji kwenye nuru ili matendo yake maovu yasifichuliwe.
21 But he that doith treuthe, cometh to the liyt, that hise werkis be schewid, that thei ben don in God.
Lakini yule aishiye kwa ukweli huja kwenye nuru, ili ionekane wazi kwamba matendo yake yametendeka katika Mungu.”
22 Aftir these thingis Jhesus cam, and hise disciplis, in to the loond of Judee, and there he dwellide with hem, and baptiside.
Baada ya haya, Yesu na wanafunzi wake walikwenda katika nchi ya Uyahudi, nao wakakaa huko kwa muda na kubatiza.
23 And Joon was baptisinge in Ennon, bisidis Salym, for many watris weren there; and thei camen, and weren baptisid.
Yohana naye alikuwa akibatiza huko Ainoni karibu na Salimu kwa sababu huko kulikuwa na maji tele. Watu wazima wakamjia huko ili kubatizwa.
24 And Joon was not yit sent in to prisoun.
(Hii ilikuwa kabla Yohana hajatiwa gerezani).
25 Therfor a questioun was maad of Jonys disciplis with the Jewis, of the purificacioun.
Mashindano yakazuka kati ya baadhi ya wanafunzi wa Yohana na Myahudi mmoja kuhusu suala la desturi ya kunawa kwa utakaso.
26 And thei camen to Joon, and seiden `to hym, Maister, he that was with thee biyonde Jordan, to whom thou hast borun witnessyng, lo! he baptisith, and alle men comen to hym.
Wakamwendea Yohana wakamwambia, “Rabi, yule mtu aliyekuwa pamoja nawe ngʼambo ya Mto Yordani, yule uliyeshuhudia habari zake, sasa anabatiza na kila mtu anamwendea!”
27 Joon answerde, and seide, A man may not take ony thing, but it be youun to hym fro heuene.
Yohana akawajibu, “Hakuna mtu yeyote awezaye kupata kitu chochote isipokuwa kile tu alichopewa kutoka mbinguni.
28 Ye you silf beren witnessyng to me, that Y seide, Y am not Crist, but that Y am sent bifore hym.
Ninyi wenyewe ni mashahidi wangu kwamba nilisema, ‘Mimi si Kristo, ila nimetumwa nimtangulie.’
29 He that hath a wijf, is the hosebonde; but the freend of the spouse that stondith, and herith hym, ioieth with ioye, for the vois of the spouse. Therfor in this thing my ioye is fulfillid.
Bibi arusi ni wa bwana arusi. Lakini rafiki yake bwana arusi anayesimama karibu naye na kusikiliza kutoka kwake, hufurahi sana aisikiapo sauti ya bwana arusi. Kwa sababu hii furaha yangu imekamilika.
30 It bihoueth hym to wexe, but me to be maad lesse.
Yeye hana budi kuwa mkuu zaidi na mimi nizidi kuwa mdogo.”
31 He that cam from aboue, is aboue alle; he that is of the erthe, spekith of the erthe; he that cometh from heuene, is aboue alle.
“Yeye ajaye kutoka juu yu juu ya yote, yeye aliye wa duniani ni wa dunia, naye huzungumza mambo ya duniani. Yeye aliyekuja kutoka mbinguni, yu juu ya yote.
32 And he witnessith that thing that he hath seie, and herde, and no man takith his witnessing.
Yeye hushuhudia yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna yeyote anayekubali ushuhuda wake.
33 But he that takith his witnessyng, hath confermyd that God is sothefast.
Lakini yeyote anayekubali huo ushuhuda anathibitisha kwamba, Mungu ni kweli.
34 But he whom God hath sent, spekith the wordis of God; for not to mesure God yyueth the spirit.
Yeye aliyetumwa na Mungu husema maneno ya Mungu, kwa kuwa Mungu humtoa Roho pasipo kipimo.
35 The fadir loueth the sone, and he hath youun alle thingis in his hoond.
Baba anampenda Mwana, naye ametia vitu vyote mikononi mwake.
36 He that bileueth in the sone, hath euerlastynge lijf; but he that is vnbileueful to the sone, schal not se euerlastynge lijf, but the wraththe of God dwellith on hym. (aiōnios g166)
Yeyote anayemwamini Mwana ana uzima wa milele, lakini yeye asiyemwamini Mwana hatauona uzima, bali ghadhabu ya Mungu itakuwa juu yake.” (aiōnios g166)

< John 3 >