< John 21 >
1 Afterward Jhesus eftsoone schewide hym to hise disciplis, at the see of Tiberias.
Baada ya mambo hayo Yesu alijidhihirisha tena kwa wanafunzi katika Bahari ya Tiberia; hivi ndivyo alivyojidhihirisha mwenyewe:
2 And he schewide him thus. There weren togidere Symount Petre, and Thomas, that is seid Didimus, and Nathanael, that was of the Cane of Galilee, and the sones of Zebedee, and tweyne othere of hise disciplis.
Simon Petro alikuwa pamoja na Thomaso aitwaye Didimas, Nathanaeli wa kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo na wanafunzi wengine wawili wa Yesu.
3 Symount Petre seith to hem, Y go to fische. Thei seyn to hym, And we comen with thee. And `thei wenten out, `and wenten in to a boot. And in that niyt thei token no thing.
Simon Petro akawaambia, “Mimi naenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia, “Sisi, pia tutaenda nawe.” Wakaenda wakaingia kwenye mashua, lakini usiku huo wote hawakupata chochote.
4 But whanne the morewe was comun, Jhesus stood in the brenke; netheles the disciplis knewen not, that it was Jhesus.
Na asubuhi kulipokucha, Yesu alisimama ufukweni, nao wanafunzi hawakutambua kuwa alikuwa Yesu.
5 Therfor Jhesus seith to hem, Children, whethir ye han ony souping thing? Thei answeriden to hym, Nay. He seide to hem,
Kisha Yesu akawambia, “Vijana, mna chochote cha kula?” Nao wakamjibu, “Hapana.”
6 Putte ye the nett in to the riyt half of the rowing, and ye schulen fynde. And thei puttiden the nett; and thanne thei miyten not drawe it for multitude of fischis.
Akawambia, “Shusheni wavu upande wa kuume wa mashua, nanyi mtapata kiasi.” Kwa hiyo wakashusha wavu nao hawakuweza kulivuta tena kwa sababu ya wingi wa cha samaki.
7 Therfor thilke disciple, whom Jhesus louede, seide to Petre, It is the Lord. Symount Petre, whanne he hadde herd that it is the Lord, girte hym with a coote, for he was nakid, and wente in to the see.
Basi yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda akamwambia Petro, “Ni Bwana.” Naye Simon Petro aliposikia kuwa ni Bwana, akajifunga vazi lake (maana hakuwa amelivaa vizuri), kisha akajitupa baharini.
8 But the othere disciplis camen bi boot, for thei weren not fer fro the lond, but as a two hundrid cubitis, drawinge the nett of fischis.
Wale wanafunzi wengine wakaja kwenye mashua (kwani hawakuwa mbali na pwani, yapata mita mia moja kutoka ufukweni), nao walikuwa wakivuta zile nyavu zilizokuwa zimejaa samaki.
9 And as thei camen doun in to the lond, thei sayn coolis liynge, and a fisch leid on, and breed.
Walipofika ufukweni, waliona moto wa mkaa pale na juu yake kulikuwa na samaki pamoja na mkate.
10 Jhesus seith to hem, Bringe ye of the fyschis, whiche ye han takun now.
Yesu akawambia, “Leteni baadhi ya samaki mliovua sasa hivi.”
11 Symount Petre wente vp, and drowy the nett in to the lond, ful of grete fischis, an hundrid fifti and thre; and whanne thei weren so manye, the nett was not brokun.
Basi Simon Petro akapanda na kuukokota ule wavu uliokuwa umejaa samaki wakubwa, kiasi cha samaki 153; japo walikuwa wengi, ule wavu haukuchanika.
12 Jhesus seith to hem, Come ye, ete ye. And no man of hem that saten at the mete, durste axe hym, Who art thou, witinge that it is the Lord.
Yesu akawaambia, “Njoni mpate kifungua kinywa.” Hakuna hata mmoja wa wanfunzi aliyethubutu kumwuliza, “Wewe ni nani?” Walijua kuwa alikuwa ni Bwana.
13 And Jhesus cam, and took breed, an yaf to hem, and fisch also.
Yesu akaja, akachukua ule mkate, kisha akawapa, akafanya vivyo hivyo na kwa wale samaki.
14 Now this thridde tyme Jhesus was schewid to hise disciplis, whanne he hadde risun ayen fro deth.
Hii ilikuwa mara ya tatu kwa Yesu kujidhihirisha kwa wanafunzi wake baada ya kufufuka toka wafu.
15 And whanne thei hadde etun, Jhesus seith to Simount Petre, Symount of Joon, louest thou me more than these? He seith to him, Yhe, Lord, thou woost that Y loue thee. Jhesus seith to hym, Fede thou my lambren.
Baada ya kuwa wamefungua kinywa, Yesu akamwambia Simon Petro, “Simon mwana wa Yohana je, wanipenda mimi kuliko hawa?” Petro akajibu, “Ndiyo, Bwana; “Wewe wajua kuwa mimi nakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha wanakondoo wangu.”
16 Eft he seith to hym, Symount of Joon, louest thou me? He seith to him, Yhe, Lord, thou woost that Y loue thee. He seith to him, Fede thou my lambren.
Akamwambia mara ya pili, “Simon mwana wa Yona, je, wanipenda?” Petro akamwambia, “Ndiyo, Bwana; wewe wajua kuwa nakupenda. “Yesu akamwambia, “Chunga kondoo wangu.”
17 He seith to him the thridde tyme, Simount of Joon, louest thou me? Petre was heuy, for he seith to hym the thridde tyme, Louest thou me, and he seith to him, Lord, thou knowist alle thingis; thou woost that Y loue thee. Jhesus seith to hym, Fede my scheep.
Akamwambia tena mara ya tatu, “Simon, mwana wa Yohana, Je wanipenda?” Naye Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, “Je Wewe wanipenda?” Naye akamwambia, “Bwana, unajua yote; unajua kuwa nakupenda.” Yesu akamwambia, Lisha kondoo wangu.
18 Treuli, treuli, Y seie to thee, whanne thou were yongere, thou girdidist thee, and wandridist where thou woldist; but whanne thou schalt waxe eldere, thou schalt holde forth thin hondis, and another schal girde thee, and schal lede thee whidur thou wolt not.
Amini, amini, nakuambia, ulipokuwa kijana ulizoea kuvaa nguo mwenyewe na kwenda kokote ulikotaka; lakini utakapokuwa mzee, utanyosha mikono yako, na mwingine atakuvalisha nguo na kukupeleka usikotaka kwenda.”
19 He seide this thing, signifynge bi what deth he schulde glorifie God. And whanne he hadde seid these thingis, he seith to hym, Sue thou me.
Yesu alisema haya ili kuonesha ni aina gani ya kifo ambacho Petro angemtukuza Mungu. Baada ya kuwa amesema haya, akamwambia Petro, “Nifuate.”
20 Petre turnede, and say thilke disciple suynge, whom Jhesus louede, which also restid in the soper on his brest, and he seide to hym, Lord, who is it, that schal bitraie thee?
Petro aligeuka na kumwona yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda akawafuata- Huyu ndiye aliyekuwa amajiegemeza kwenye kifua cha Yesu wakati wa chakula cha jioni na kumwuliza, “Bwana, ni nani atakayekusaliti?”
21 Therfor whanne Petre hadde seyn this, he seith to Jhesu, Lord, but what this?
Petro alimwona na kisha akamwuliza Yesu, “Bwana, Huyu mtu atafanya nini?”
22 Jhesus seith to him, So I wole that he dwelle til that Y come, what to thee? sue thou me.
Yesu akamjibu, “Kama nataka abaki mpaka nitakapokuja, hilo linakuhusu nini?” Nifuate.”
23 Therfor this word wente out among the britheren, that thilke disciple dieth not. And Jhesus seide not to hym, that he dieth not, but, So Y wole that he dwelle til Y come, what to thee?
Kwa hiyo habari hii ikaenea miongoni mwa wale ndugu, kwamba mwanafunzi huyo hatakufa. Lakini Yesu hakumwambia Petro kuwa, mwanafunzi huyo hafi, “Kama nataka yeye abaki mpaka nitakapokuja yakuhusu nini?”
24 This is thilke disciple, that berith witnessyng of these thingis, and wroot hem; and we witen, that his witnessyng is trewe.
Huyu ndiye mwanafunzi atoaye ushuhuda wa mambo haya, na ndiye aliye andika mambo haya, na tunajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli.
25 And ther ben also manye othere thingis that Jhesus dide, whiche if thei ben writun bi ech bi hym silf, Y deme that the world hym silf schal not take tho bookis, that ben to be writun.
Kuna mambo mengine mengi ambayo Yesu aliyafanya. Kama kila moja lingeandikwa, nadhani kwamba ulimwengu wenyewe usingetosha kuviweka vitabu ambavyo vingeandikwa.