< John 20 >
1 And in o dai of the wouke Marie Maudeleyn cam eerli to the graue, whanne it was yit derk. And sche say the stoon moued awei fro the graue.
Alfajiri na mapema siku ya kwanza ya juma, kulipokuwa kungali giza bado, Maria Magdalene alikwenda kaburini na kukuta lile jiwe limeondolewa penye ingilio.
2 Therfor sche ran, and cam to Symount Petre, and to another disciple, whom Jhesus louede, and seith to hem, Thei han takun the Lord fro the graue, and we witen not, where thei han leid hym.
Hivyo akaja akikimbia kwa Simoni Petro pamoja na yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, na kusema, “Wamemwondoa Bwana kaburini, na hatujui walikomweka!”
3 Therfor Petre wente out, and thilke other disciple, and thei camen to the graue.
Petro na yule mwanafunzi mwingine wakaondoka mara kuelekea kaburini.
4 And thei tweyne runnen togidre, and thilke othere disciple ran bifor Petre, and cam first to the graue.
Wote wawili walikuwa wanakimbia, lakini yule mwanafunzi mwingine akakimbia mbio zaidi kuliko Petro, akatangulia kufika kaburini.
5 And whanne he stoupide, he sai the schetis liynge, netheles he entride not.
Alipofika, akainama na kuchungulia mle kaburini, akaona vile vitambaa vya kitani mle ndani, lakini hakuingia.
6 Therfor Symount Petre cam suynge hym, and he entride in to the graue, and he say the schetis leid,
Ndipo Simoni Petro akaja, akimfuata nyuma akaenda moja kwa moja hadi ndani ya kaburi. Naye akaona vile vitambaa vya ile sanda vikiwa pale chini
7 and the sudarie that was on his heed, not leid with the schetis, but bi it silf wlappid in to a place.
na kile kitambaa kilichokuwa kichwani mwa Yesu. Kitambaa hicho kilikuwa kimekunjwa mahali pa peke yake, mbali na vile vitambaa vya kitani vya ile sanda.
8 Therfor thanne thilke disciple that cam first to the graue, entride, and sai, and bileuede.
Kisha yule mwanafunzi aliyetangulia kufika kaburini naye akaingia ndani, akaona, akaamini,
9 For thei knewen not yit the scripture, that it behofte him to rise ayen fro deth.
(kwa kuwa mpaka wakati huo walikuwa bado hawajaelewa kutoka Maandiko kwamba ilikuwa lazima Yesu afufuke kutoka kwa wafu).
10 Therfor the disciplis wenten eftsoone to hem silf.
Kisha hao wanafunzi wakaondoka wakarudi nyumbani kwao.
11 But Marie stood at the graue with outforth wepynge. And the while sche wepte, sche bowide hir, and bihelde forth in to the graue.
Lakini Maria Magdalene akasimama nje ya kaburi akilia. Alipokuwa akilia, akainama, kuchungulia mle kaburini,
12 And sche sai twei aungels sittinge in white, oon at the heed and oon at the feet, where the bodi of Jhesu was leid.
naye akaona malaika wawili wamevaa mavazi meupe, wameketi pale mwili wa Yesu ulipokuwa umelazwa, mmoja upande wa kichwani na mwingine upande wa miguuni.
13 And thei seien to hir, Womman, what wepist thou? Sche seide to hem, For thei han take awei my lord, and Y woot not, where thei han leid him.
Wakamuuliza Maria, “Mwanamke, mbona unalia?” Akawaambia, “Nalia kwa kuwa wamemchukua Bwana wangu na sijui walikomweka.”
14 Whanne sche hadde seid these thingis, sche turnede bacward, and sai Jhesu stondinge, and wiste not that it was Jhesu.
Baada ya kusema hayo, akageuka, akamwona Yesu amesimama, lakini hakumtambua.
15 Jhesus seith to hir, Womman, what wepist thou? whom sekist thou? She gessynge that he was a gardynere, seith to him, Sire, if thou hast takun him vp, seie to me, where thou hast leid him, and Y schal take hym awei.
Yesu akamwambia, “Mwanamke, mbona unalia? Unamtafuta nani?” Maria akidhani ya kuwa aliyekuwa anaongea naye ni mtunza bustani, kwa hiyo akamwambia, “Bwana, kama ni wewe umemchukua, tafadhali nionyeshe ulikomweka, nami nitamchukua.”
16 Jhesus seith to hir, Marie. Sche `turnede, and seith to hym, Rabony, that is to seie, Maister.
Yesu akamwita, “Maria!” Ndipo Maria akamgeukia Yesu na kusema naye kwa Kiebrania, “Rabboni!” (maana yake Mwalimu).
17 Jhesus seith to hir, Nyle thou touche me, for Y haue not yit stied to my fadir; but go to my britheren, and seie to hem, Y stie to my fadir and to youre fadir, to my God and to youre God.
Yesu akamwambia, “Usinishike, kwa maana sijapaa kwenda kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu ukawaambie, ‘Ninapaa kwenda kwa Baba yangu ambaye ni Baba yenu, kwa Mungu wangu ambaye ni Mungu wenu.’”
18 Marie Maudeleyne cam, tellinge to the disciplis, That Y sai the Lord, and these thingis he seide to me.
Kwa hiyo Maria Magdalene akaenda kuwatangazia wanafunzi wa Yesu, akisema, “Nimemwona Bwana!” Naye akawaambia kwamba Yesu alikuwa amemweleza mambo hayo yote.
19 Therfor whanne it was eue in that dai, oon of the sabatis, and the yatis weren schit, where the disciplis weren gaderid, for drede of the Jewis, Jhesus cam, and stood in the myddil of the disciplis, and he seith to hem, Pees to you.
Ikawa jioni ya ile siku ya kwanza ya juma, wanafunzi wake walikuwa pamoja, milango ikiwa imefungwa kwa kuwaogopa Wayahudi. Naye Yesu aliwatokea, akasimama katikati yao, akasema, “Amani iwe nanyi!”
20 And whanne he hadde seid this, he schewide to hem hondis and side; therfor the disciplis ioieden, for the Lord was seyn.
Baada ya kusema haya, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Wanafunzi wake wakafurahi sana walipomwona Bwana.
21 And he seith to hem eft, Pees to you; as the fadir sente me, Y sende you.
Yesu akawaambia tena, “Amani iwe nanyi! Kama vile Baba alivyonituma mimi, mimi nami nawatuma ninyi.”
22 Whanne he had seid this, he blewe on hem, and seide, Take ye the Hooli Goost;
Naye alipokwisha kusema haya, akawavuvia, akawaambia, “Pokeeni Roho Mtakatifu.
23 whos synnes ye foryyuen, tho ben foryouun to hem; and whos ye withholden, tho ben withholdun.
Mkimwondolea mtu yeyote dhambi zake, zitaondolewa, na yeyote msiyemwondolea dhambi zake, hazitaondolewa.”
24 But Thomas, oon of the twelue, that is seid Didimus, was not with hem, whanne Jhesus cam.
Lakini Tomaso, aliyeitwa Didimasi, yaani Pacha, mmoja wa wale kumi na wawili, hakuwa pamoja nao Yesu alipokuja.
25 Therfor the othere disciplis seiden, We han seyn the Lord. And he seide to hem, But Y se in hise hondis the fitchinge of the nailis, and putte my fyngur in to the places of the nailis, and putte myn hond in to his side, Y schal not bileue.
Hivyo wale wanafunzi wengine wakamwambia, “Tumemwona Bwana.” Lakini yeye akawaambia, “Nisipoona zile alama za misumari mikononi mwake, na kuweka kidole changu kwenye hizo alama za misumari na mkono wangu ubavuni mwake, sitaamini.”
26 And after eiyte daies eftsoone hise disciplis weren with ynne, and Thomas with hem. Jhesus cam, while the yatis weren schit, and stood in the myddil, and seide, Pees to you.
Baada ya siku nane, wanafunzi wake walikuwa tena pamoja ndani ya nyumba, naye Tomaso alikuwa pamoja nao. Ndipo Yesu akaja milango ikiwa imefungwa na kusimama katikati yao akasema, “Amani iwe nanyi.”
27 Afterward he seith to Thomas, Putte in here thi fyngur, and se myn hondis, and putte hidur thin hond, and putte in to my side, and nyle thou be vnbileueful, but feithful.
Kisha akamwambia Tomaso, “Weka kidole chako hapa na uone mikono yangu, nyoosha mkono wako uguse ubavuni mwangu. Usiwe na shaka, bali uamini tu.”
28 Thomas answeride, and seide to him, My Lord and my God.
Tomaso akamwambia, “Bwana wangu na Mungu wangu!”
29 Jhesus seith to him, Thomas, for thou hast seyn me, thou bileuedist; blessid ben thei, that seyn not, and han bileued.
Yesu akamwambia, “Umeamini kwa kuwa umeniona? Wamebarikiwa wale ambao hawajaona lakini wameamini.”
30 And Jhesus dide many othere signes in the siyt of hise disciplis, whiche ben not writun in this book.
Yesu alifanya miujiza mingine mingi mbele za wanafunzi wake, ambayo haikuandikwa katika kitabu hiki.
31 But these ben writun, that ye bileue, that Jhesus `is Crist, the sone of God, and that ye bileuynge haue lijf in his name.
Lakini haya yameandikwa ili mweze kuamini ya kuwa Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu, na kwa kumwamini mpate uzima katika jina lake.