< John 16 >

1 These thingis Y haue spokun to you, that ye be not sclaundrid.
“Nimewaambia mambo haya yote ili msije mkaiacha imani.
2 Thei schulen make you with outen the synagogis, but the our cometh, that ech man that sleeth you, deme that he doith seruyce to God.
Watawatenga na masinagogi. Naam, saa yaja ambayo mtu yeyote atakayewaua atadhani kwa kufanya hivyo anamtumikia Mungu.
3 And thei schulen do to you these thingis, for thei han not knowun the fadir, nether me.
Nao watawatenda haya kwa sababu hawamjui Baba wala mimi.
4 But these thingis Y spak to you, that whanne the our `of hem schal come, ye haue mynde, that Y seide to you.
Lakini nimewaambia ninyi mambo haya, ili saa hiyo ikiwadia mpate kukumbuka ya kuwa nilikuwa nimewaambia. Sikuwaambia mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
5 Y seide not to you these thingis fro the bigynnyng, for Y was with you. And now Y go to hym that sente me, and no man of you axith me, Whidur `thou goist?
“Sasa mimi ninakwenda kwake yeye aliyenituma, lakini hakuna hata aniulizaye, ‘Unakwenda wapi?’
6 but for Y haue spokun to you these thingis, heuynesse hath fulfillid youre herte.
Kwa sababu nimewaambia mambo haya, mioyo yenu imejawa na huzuni.
7 But Y seie to you treuthe, it spedith to you, that Y go; for if Y go not forth, the coumfortour schal not come to you; but if Y go forth, Y schal sende hym to you.
Lakini nawaambia kweli, yafaa mimi niondoke, kwa kuwa nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu, lakini nikienda nitamtuma kwenu.
8 And whanne he cometh, he schal repreue the world of synne, and of riytwisnesse, and of doom.
Naye atakapokuja, atauthibitishia ulimwengu kuhusu dhambi, haki na hukumu.
9 Of synne, for thei han not bileued in me;
Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi,
10 and of riytwisnesse, for Y go to the fadir, and now ye schulen not se me;
kwa habari ya haki, kwa sababu ninakwenda kwa Baba, nanyi hamtaniona tena,
11 but of doom, for the prince of this world is now demed.
kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa.
12 Yit Y haue many thingis for to seie to you, but ye moun not bere hem now.
“Bado ninayo mambo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili sasa.
13 But whanne thilke spirit of treuthe cometh, he schal teche you al trewthe; for he schal not speke of hym silf, but what euer thinges he schal here, he schal speke; and he schal telle to you tho thingis that ben to come.
Atakapokuja huyo Roho wa kweli atawaongoza awatie katika kweli yote. Yeye hatanena kwa ajili yake mwenyewe, bali atanena yale yote atakayosikia, naye atawaonyesha mambo yajayo.
14 He schal clarifie me, for of myne he schal take, and schal telle to you.
Atanitukuza mimi, kwa maana atayachukua yaliyo yangu na kuwajulisha ninyi.
15 Alle thingis `whiche euer the fadir hath, ben myne; therfor Y seide to you, for of myne he schal take, and schal telle to you.
Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu. Ndiyo maana nimesema Roho atachukua yaliyo yangu na kuwajulisha ninyi.
16 A litil, and thanne ye schulen not se me; and eftsoone a litil, and ye schulen se me, for Y go to the fadir.
“Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona.”
17 Therfor summe of hise disciplis seiden togidere, What is this thing that he seith to vs, A litil, and ye schulen not se me; and eftsoone a litil, and ye schulen se me, for Y go to the fadir?
Baadhi ya wanafunzi wakaulizana, “Ana maana gani asemapo, ‘Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona’? Naye ana maana gani asemapo, ‘Kwa sababu ninakwenda kwa Baba’?”
18 Therfor thei seiden, What is this that he seith to vs, A litil? we witen not what he spekith.
Wakaendelea kuulizana, “Ana maana gani asemapo, ‘Kitambo kidogo’? Hatuelewi hilo analosema.”
19 And Jhesus knew, that thei wolden axe hym, and he seide to hem, Of this thing ye seken among you, for Y seide, A litil, and ye schulen not se me; and eftsoone a litil, and ye schulen se me.
Yesu akatambua kuwa walitaka kumuuliza juu ya hilo, hivyo akawaambia, “Je, mnaulizana nina maana gani niliposema, ‘Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona’?
20 Treuli, treuli, Y seie to you, that ye schulen mourne and wepe, but the world schal haue ioye; and ye schulen be soreuful, but youre sorewe schal turne in to ioye.
Amin, amin nawaambia, ninyi mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utafurahi. Ninyi mtahuzunika, lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.
21 A womman whanne sche berith child, hath heuynesse, for hir tyme is comun; but whanne sche hath borun a sone, now sche thenkith not on the peyne, for ioye, for a man is borun in to the world.
Mwanamke anapokuwa na utungu wa kuzaa huwa na maumivu kwa sababu saa yake imewadia. Lakini mtoto akiisha kuzaliwa, yule mwanamke husahau maumivu hayo kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa mtoto ulimwenguni.
22 And therfor ye han now sorew, but eftsoone Y schal se you, and youre herte schal haue ioie, and no man schal take fro you youre ioie.
Hivyo ninyi mna maumivu sasa, lakini nitawaona tena, nayo mioyo yenu itafurahi na furaha yenu hakuna awaondoleaye.
23 And in that day ye schulen not axe me ony thing; treuli, treuli, `Y seie to you, if ye axen the fadir ony thing in my name, he schal yyue to you.
Katika siku hiyo hamtaniuliza neno lolote. Amin, amin nawaambia, kama mkimwomba Baba jambo lolote kwa jina langu, yeye atawapa.
24 `Til now ye axiden no thing in my name; `axe ye, `and ye schulen take, that youre ioie be ful.
Mpaka sasa hamjaomba jambo lolote kwa Jina langu. Ombeni nanyi mtapewa, ili furaha yenu ipate kuwa kamili.
25 Y haue spokun to you these thingis in prouerbis; the our cometh, whanne now Y schal not speke to you in prouerbis, but opynli of my fadir Y schal telle to you.
“Nimewaambia mambo haya kwa mafumbo. Saa yaja ambapo sitazungumza nanyi tena kwa mafumbo bali nitawaeleza waziwazi kuhusu Baba.
26 In that dai ye schulen axe in my name; and Y seie not to you, that Y schal preye the fadir of you;
Siku hiyo mtaomba kwa Jina langu. Wala sitawaambia kwamba nitamwomba Baba kwa ajili yenu,
27 for the fadir hym silf loueth you, for ye han loued me, and han bileued, that Y wente out fro God.
kwa maana Baba mwenyewe anawapenda, kwa sababu mmenipenda mimi na mmeamini kwamba nimetoka kwa Mungu.
28 Y wente out fro the fadir, and Y cam in to the world; eftsoone Y leeue the world, and Y go to the fadir.
Nilitoka kwa Baba na kuja ulimwenguni, sasa naondoka ulimwenguni na kurudi kwa Baba.”
29 Hise disciplis seiden to hym, Lo! now thou spekist opynli, and thou seist no prouerbe.
Ndipo wanafunzi wake wakasema, “Sasa unazungumza waziwazi, wala si kwa mafumbo.
30 Now we witen, that thou wost alle thingis; and it is not nede to thee, that ony man axe thee. In this thing we bileuen, that thou wentist out fro God.
Sasa tumejua kwamba wewe unajua mambo yote, wala hakuna haja ya mtu kukuuliza maswali. Kwa jambo hili tunaamini kwamba ulitoka kwa Mungu.”
31 Jhesus answeride to hem, Now ye bileuen.
Yesu akawajibu, “Je, sasa mnaamini?
32 Lo! the our cometh, and now it cometh, that ye be disparplid, ech in to hise owne thingis, and that ye leeue me aloone; and Y am not aloone, for the fadir is with me.
Saa inakuja, naam, imekwisha kuwadia, mtakapotawanyika kila mmoja kwenda nyumbani kwake na kuniacha peke yangu. Lakini mimi siko peke yangu kwa sababu Baba yu pamoja nami.
33 These thingis Y haue spokun to you, that ye haue pees in me; in the world ye schulen haue disese, but trust ye, Y haue ouercomun the world.
Nimewaambia mambo haya, ili mpate kuwa na amani mkiwa ndani yangu. Ulimwenguni mtapata dhiki. Lakini jipeni moyo, kwa maana mimi nimeushinda ulimwengu.”

< John 16 >