< John 11 >

1 And ther was a sijk man, Lazarus of Bethanye, of the castel of Marie and Martha, hise sistris.
Mtu mmoja aitwaye Lazaro, mwenyeji wa Bethania, alikuwa mgonjwa. (Kijiji cha Bethania kilikuwa mahali walipokaa Maria na Martha, dada yake.
2 And it was Marye, which anoyntide the Lord with oynement, and wipte hise feet with hir heeris, whos brother Lazarus was sijk.
Maria ndiye yule aliyempaka Bwana marashi na kumpangusa kwa nywele zake. Lazaro, kaka yake, ndiye aliyekuwa mgonjwa.)
3 Therfor hise sistris senten to hym, and seide, Lord, lo! he whom thou louest, is sijk.
Basi, hao dada wakatuma ujumbe huu kwa Yesu: “Bwana, rafiki yako ni mgonjwa!”
4 And Jhesus herde, and seide to hem, This syknesse is not to the deth, but for the glorie of God, that mannus sone be glorified bi hym.
Yesu aliposikia hivyo akasema, “Ugonjwa huo hautaleta kifo, ila ni kwa ajili ya kumtukuza Mungu; ameugua ili kwa njia hiyo Mwana wa Mungu atukuzwe.”
5 And Jhesus louyde Martha, and hir sistir Marie, and Lazarus.
Yesu aliwapenda Martha, dada yake na Lazaro.
6 Therfor whanne Jhesus herde, that he was sijk, thanne he dwellide in the same place twei daies.
Alipopata habari kwamba Lazaro ni mgonjwa, Yesu aliendelea kukaa mahali hapo alipokuwa kwa siku mbili zaidi.
7 And after these thingis he seide to hise disciplis, Go we eft in to Judee.
Kisha akawaambia wanafunzi wake, “Twendeni tena Yudea!”
8 The disciplis seien to hym, Maister, now the Jewis souyten for to stoone thee, and eft goist thou thidir?
Wanafunzi wakamwambia, “Mwalimu! Muda mfupi tu umepita tangu Wayahudi walipotaka kukuua kwa mawe, nawe unataka kwenda huko tena?”
9 Jhesus answerde, Whether ther ben not twelue ouris of the dai? If ony man wandre in the dai, he hirtith not, for he seeth the liyt of this world.
Yesu akajibu, “Je, saa za mchana si kumi na mbili? Basi, mtu akitembea mchana hawezi kujikwaa kwa kuwa anauona mwanga wa ulimwengu huu.
10 But if he wandre in the niyt, he stomblith, for liyt is not in him.
Lakini mtu akitembea usiku atajikwaa kwa maana mwanga haumo ndani yake.”
11 He seith these thingis, and aftir these thingis he seith to hem, Lazarus, oure freend, slepith, but Y go to reise hym fro sleep.
Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini mimi nitakwenda kumwamsha.”
12 Therfor hise disciplis seiden, Lord, if he slepith, he schal be saaf.
Wanafunzi wake wakamwambia, “Bwana, ikiwa amelala, basi atapona.”
13 But Jhesus hadde seid of his deth; but thei gessiden, that he seide of slepyng of sleep.
Wao walidhani kwamba alikuwa amesema juu ya kulala usingizi, kumbe alikuwa amesema juu ya kifo cha Lazaro.
14 Thanne therfor Jhesus seide to hem opynli, Lazarus is deed;
Basi, Yesu akawaambia waziwazi, “Lazaro amekufa;
15 and Y haue ioye for you, that ye bileue, for Y was not there; but go we to hym.
Lakini nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini. Haya, twendeni kwake.”
16 Therfor Thomas, that is seid Didymus, seide to euen disciplis, Go we also, that we dien with hym.
Thoma (aitwaye Pacha) akawaambia wanafunzi wenzake, “Twendeni nasi tukafe pamoja naye!”
17 And so Jhesus cam, and foond hym hauynge thanne foure daies in the graue.
Yesu alipofika huko alikuta Lazaro amekwisha kaa kaburini kwa siku nne.
18 And Bethany was bisidis Jerusalem, as it were fiftene furlongis.
Kijiji cha Bethania kilikuwa karibu na Yerusalemu umbali upatao kilomita tatu.
19 And many of the Jewis camen to Mary and Martha, to coumforte hem of her brothir.
Wayahudi wengi walikuwa wamefika kwa Martha na Maria kuwafariji kwa kifo cha kaka yao.
20 Therfor as Martha herde, that Jhesu cam, sche ran to hym; but Mary sat at home.
Basi, Martha aliposikia kwamba Yesu alikuwa anakuja, akaenda kumlaki; lakini Maria alibaki nyumbani.
21 Therfor Martha seide to Jhesu, Lord, if thou haddist be here, my brother hadde not be deed.
Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!
22 But now Y woot, that what euere thingis thou schalt axe of God, God schal yyue to thee.
Lakini najua kwamba hata sasa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”
23 Jhesus seith to hir, Thi brother schal rise ayen.
Yesu akamwambia, “Kaka yako atafufuka.”
24 Martha seith to hym, Y woot, that he schal rise ayen in the ayen risyng in the laste dai.
Martha akamjibu, “Najua kwamba atafufuka wakati wa ufufuo, siku ya mwisho.”
25 Jhesus seith to hir, Y am ayen risyng and lijf; he that bileueth in me, yhe, thouy he be deed, he schal lyue;
Yesu akamwambia, “Mimi ndimi ufufuo na uzima. Anayeniamini mimi hata kama anakufa, ataishi:
26 and ech that lyueth, and bileueth in me, schal not die with outen ende. Bileuest thou this thing? (aiōn g165)
na kila anayeishi na kuniamini, hatakufa kamwe. Je, waamini hayo?” (aiōn g165)
27 Sche seith to hym, Yhe, Lord, Y haue bileued, that thou art Crist, the sone of the lyuynge God, that hast come in to this world.
Martha akamwambia, “Ndiyo Bwana! Naamini kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni.”
28 And whanne sche hadde seid this thing, sche wente, and clepide Marie, hir sistir, in silence, and seide, The maister cometh, and clepith thee.
Baada ya kusema hayo, Martha alikwenda kumwita Maria, dada yake, akamwabia faraghani, “Mwalimu yuko hapa, anakuita.”
29 Sche, as sche herd, aroos anoon, and cam to hym.
Naye aliposikia hivyo, akainuka mara, akamwendea Yesu.
30 And Jhesus cam not yit `in to the castel, but he was yit in that place, where Martha hadde comun ayens hym.
Yesu alikuwa hajaingia kijijini, ila alikuwa bado mahali palepale Martha alipomlaki.
31 Therfor the Jewis that weren with hir in the hous, and coumfortiden hir, whanne thei sayn Marie, that sche roos swithe, and wente out, thei sueden hir, and seiden, For sche goith to the graue, to wepe there.
Basi, Wayahudi waliokuwa nyumbani pamoja na Maria wakimfariji walipomwona ameinuka na kutoka nje ghafla, walimfuata. Walidhani alikuwa anakwenda kaburini kuomboleza.
32 But whanne Marie was comun where Jhesus was, sche seynge hym felde doun to his feet, and seide to hym, Lord, if thou haddist be here, my brother hadde not be deed.
Basi, Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa na kumwona, alipiga magoti, akamwabia, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!”
33 And therfor whanne Jhesu saiy hir wepyng, and the Jewis wepynge that weren with hir, he `made noise in spirit, and troblide hym silf,
Yesu alipomwona analia, na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye wanalia pia, alijawa na huzuni na kufadhaika moyoni.
34 and seide, Where han ye leid hym? Thei seien to hym, Lord, come, and se.
Kisha akawauliza, “Mlimweka wapi?” Wakamwambia, “Bwana, njoo uone.”
35 And Jhesus wepte. Therfor the Jewis seiden,
Yesu akalia machozi.
36 Lo! hou he louede hym.
Basi, Wayahudi wakasema, “Tazameni jinsi alivyompenda!”
37 And summe of hem seiden, Whethir this man that openyde the iyen of the borun blynde man, myyte not make that this schulde not die?
Lakini baadhi yao wakasema, “Je, huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya Lazaro asife?”
38 Therfor Jhesus eft makynge noise in hym silf, cam to the graue. And there was a denne, and a stoon was leid theronne.
Basi, Yesu akiwa amehuzunika tena moyoni, akafika kaburini. Kaburi lenyewe lilikuwa pango, na lilikuwa limefunikwa kwa jiwe.
39 And Jhesus seith, Take ye awey the stoon. Martha, the sistir of hym that was deed, seith to hym, Lord, he stynkith now, for he hath leye foure daies.
Yesu akasema, “Ondoeni hilo jiwe!” Martha, dada yake huyo aliyekufa, akamwambia, “Bwana, amekwishaanza kunuka; amekaa kaburini siku nne!”
40 Jhesus seith to hir, Haue Y not seid to thee, that if thou bileuest, thou schalt se the glorie of God?
Yesu akamwambia, “Je, sikukwambia kwamba ukiamini utaona utukufu wa Mungu?”
41 Therfor thei token awei the stoon. And Jhesus lifte vp hise iyen, and seide, Fadir, Y do thankyngis to thee, for thou hast herd me; and Y wiste,
Basi, wakaliondoa lile jiwe. Yesu akatazama juu mbinguni, akasema, “Nakushukuru Baba kwa kuwa wewe wanisikiliza.
42 that thou euermore herist me, but for the puple that stondith aboute, Y seide, that thei bileue, that thou hast sent me.
Najua kwamba unanisikiliza daima. Lakini nimesema hayo kwa ajili ya watu hawa waliopo hapa ili wapate kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.”
43 Whanne he hadde seid these thingis, he criede with a greet vois, Lazarus, come thou forth.
Alipokwisha sema hayo, akaita kwa sauti kubwa: “Lazaro! Toka nje!”
44 And anoon he that was deed, cam out, boundun the hondis and feet with boondis, and his face boundun with a sudarie. And Jhesus seith to hem, Vnbynde ye hym, and suffre ye hym to go forth.
Huyo aliyekuwa amekufa akatoka nje, huku amefungwa sanda miguu na mikono, na uso wake umefunikwa. Yesu akawaambia, “Mfungueni, mkamwache aende zake.”
45 Therfor many of the Jewis that camen to Marie and Martha, and seyn what thingis Jhesus dide, bileueden in hym.
Basi, Wayahudi wengi waliokuwa wamefika kwa Maria walipoona kitendo hicho alichokifanya Yesu wakamwamini.
46 But summe of hem wente to the Farisees, and seiden to hem, what thingis Jhesus `hadde don.
Lakini baadhi yao walikwenda kwa Mafarisayo wakatoa taarifa ya jambo hilo alilofanya Yesu.
47 Therfor the bischopis and the Farisees gadriden a counsel ayens Jhesu, and seiden, What do we? for this man doith many myraclis.
kwa hiyo makuhani wakuu na Mafarisayo wakafanya kikao cha Baraza kuu, wakasema, “Tufanye nini? Mtu huyu anafanya ishara nyingi mno.
48 If we leeue hym thus, alle men schulen bileue in hym; and Romayns schulen come, and schulen take our place and oure folk.
Tukimwacha tu watu wote watamwamini, nao Waroma watakuja kuliharibu Hekalu letu na taifa letu!”
49 But oon of hem, Cayfas bi name, whanne he was bischop of that yeer, seide to hem,
Hapo, mmoja wao aitwaye Kayafa, ambaye alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, akawaambia, “Ninyi hamjui kitu!
50 Ye witen nothing, ne thenken, that it spedith to you, that o man die for the puple, and that al the folc perische not.
Je, hamwoni kwamba ni afadhali kwenu mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa zima liangamizwe?”
51 But he seide not this thing of hym silf, but whanne he was bischop of that yeer, he prophesiede, that Jhesu was to die for the folc,
Yeye hakusema hivyo kwa hiari yake mwenyewe, bali kwa vile alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, alibashiri kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa lao;
52 and not oneli for the folc, but that he schulde gadere in to oon the sones of God that weren scaterid.
na wala si kwa ajili yao tu, bali pia apate kuwaleta pamoja watoto wa Mungu waliotawanyika.
53 Therfor fro that day thei souyten for to sle hym.
Basi, tangu siku hiyo viongozi wa Wayahudi walifanya mipango ya kumwua Yesu.
54 Therfor Jhesus walkide not thanne opynli among the Jewis; but he wente in to a cuntre bisidis desert, in to a citee, that is seid Effren, and there he dwellide with hise disciplis.
Kwa hiyo, Yesu hakutembea tena hadharani kati ya Wayahudi, bali alitoka hapo, akaenda mahali karibu na jangwa, katika mji uitwao Efraimu. Akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.
55 And the pask of the Jewis was niy, and many of the cuntrey wenten vp to Jerusalem bifor the pask, to halewe hem silf.
Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa karibu, na watu wengi walikwenda Yerusalemu ili wajitakase kabla ya sikukuu hiyo.
56 Therfor thei souyten Jhesu, and spaken togidere, stondynge in the temple, What gessen ye, for he cometh not to the feeste day?
Basi, wakawa wanamtafuta Yesu; nao walipokusanyika pamoja Hekaluni wakaulizana, “Mwaonaje? Yaonekana kwamba haji kabisa kwenye sikukuu, au sivyo?”
57 For the bischopis and Farisees hadden youun a maundement, that if ony man knowe where he is, that he schewe, that thei take hym.
Makuhani wakuu na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba mtu akijua mahali aliko Yesu awaarifu kusudi wamtie nguvuni.

< John 11 >