< Job 6 >
1 Forsothe Joob answeride, and seide,
Kisha Ayubu akajibu:
2 Y wolde, that my synnes, bi whiche Y `desseruede ire, and the wretchidnesse which Y suffre, weren peisid in a balaunce.
“Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
3 As the grauel of the see, this wretchidnesse schulde appere greuousere; wherfor and my wordis ben ful of sorewe.
Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 For the arowis of the Lord ben in me, the indignacioun of whiche drynkith vp my spirit; and the dredis of the Lord fiyten ayens me.
Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
5 Whether a feeld asse schal rore, whanne he hath gras? Ethir whether an oxe schal lowe, whanne he stondith byfor a `ful cratche?
Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
6 Ether whethir a thing vnsauery may be etun, which is not maad sauery bi salt? Ether whether ony man may taaste a thing, which tastid bryngith deeth?
Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
7 For whi to an hungri soule, yhe, bittir thingis semen to be swete; tho thingis whiche my soule nolde touche bifore, ben now my meetis for angwisch.
Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
8 Who yyueth, that myn axyng come; and that God yyue to me that, that Y abide?
“Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
9 And he that bigan, al to-breke me; releesse he his hond, and kitte me doun?
kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
10 And `this be coumfort to me, that he turmente me with sorewe, and spare not, and that Y ayenseie not the wordis of the hooli.
Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
11 For whi, what is my strengthe, that Y suffre? ethir which is myn ende, that Y do pacientli?
“Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
12 Nethir my strengthe is the strengthe of stoonus, nether my fleisch is of bras.
Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
13 Lo! noon help is to me in me; also my meyneal frendis `yeden awey fro me.
Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
14 He that takith awei merci fro his frend, forsakith the drede of the Lord.
“Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
15 My britheren passiden me, as a stronde doith, that passith ruschyngli in grete valeis.
Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
16 Snow schal come on hem, that dreden frost.
wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
17 In the tyme wherynne thei ben scaterid, thei schulen perische; and as thei ben hoote, thei schulen be vnknyt fro her place.
lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
18 The pathis of her steppis ben wlappid; thei schulen go in veyn, and schulen perische.
Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
19 Biholde ye the pathis of Theman, and the weies of Saba; and abide ye a litil.
Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
20 Thei ben schent, for Y hopide; and thei camen `til to me, and thei ben hilid with schame.
Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
21 Now ye ben comun, and now ye seen my wounde, and dreden.
Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
22 Whether Y seide, Brynge ye to me, and yiue ye of youre catel to me? ethir,
Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
23 Delyuere ye me fro the hond of enemy, and rauysche ye me fro the hond of stronge men?
au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
24 Teche ye me, and Y schal be stille; and if in hap Y vnknew ony thing, teche ye me.
“Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
25 Whi han ye depraued the wordis of trewthe? sithen noon is of you, that may repreue me.
Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
26 Ye maken redi spechis oneli for to blame, and ye bryngen forth wordis in to wynde.
Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
27 Ye fallen in on a fadirles child, and enforsen to peruerte youre frend.
Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
28 Netheles fille ye that, that ye han bigunne; yyue ye the eere, and se ye, whether Y lie.
“Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
29 Y biseche, answere ye with out strijf, and speke ye, and deme ye that, that is iust.
Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
30 And ye schulen not fynde wickidnesse in my tunge, nethir foli schal sowne in my chekis.
Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?