< Job 31 >
1 I made couenaunt with myn iyen, that Y schulde not thenke of a virgyn.
“Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
2 For what part schulde God aboue haue in me, and eritage Almyyti God of hiye thingis?
Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
3 Whether perdicioun is not to a wickid man, and alienacioun of God is to men worchynge wickidnesse?
Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
4 Whether he biholdith not my weies, and noumbrith alle my goyngis?
Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
5 If Y yede in vanyte, and my foot hastide in gile,
“Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
6 God weie me in a iust balaunce, and knowe my symplenesse.
Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
7 If my step bowide fro the weie; if myn iye suede myn herte, and a spotte cleuede to myn hondis;
kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
8 sowe Y, and another ete, and my generacioun be drawun out bi the root.
basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
9 If myn herte was disseyued on a womman, and if Y settide aspies at the dore of my frend; my wijf be the hoore of anothir man,
“Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
10 and othir men be bowid doun on hir.
basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
11 For this is vnleueful, and the moost wickidnesse.
Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
12 Fier is deourynge `til to wastyng, and drawynge vp bi the roote alle generaciouns.
Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
13 If Y dispiside to take doom with my seruaunt and myn hand mayde, whanne thei stryueden ayens me.
“Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
14 What sotheli schal Y do, whanne God schal rise to deme? and whanne he schal axe, what schal Y answere to hym?
nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
15 Whether he, that wrouyte also hym, made not me in the wombe, and o God formede me in the wombe?
Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
16 If Y denyede to pore men that, that thei wolden, and if Y made the iyen of a wydewe to abide;
“Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
17 if Y aloone eet my mussel, and a faderles child eet not therof;
kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
18 for merciful doyng encreesside with me fro my yong childhed, and yede out of my modris wombe with me;
lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
19 if Y dispiside a man passynge forth, for he hadde not a cloth, and a pore man with out hilyng;
kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
20 if hise sidis blessiden not me, and was not maad hoot of the fleeces of my scheep;
ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
21 if Y reiside myn hond on a fadirles child, yhe, whanne Y siy me the hiyere in the yate;
na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
22 my schuldre falle fro his ioynt, and myn arm with hise boonys be al to-brokun.
basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
23 For euere Y dredde God, as wawis wexynge gret on me; and `Y myyte not bere his birthun.
Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
24 If Y gesside gold my strengthe, and if Y seide to purid gold, Thou art my trist;
“Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
25 if Y was glad on my many ritchessis, and for myn hond foond ful many thingis;
kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
26 if Y siy the sunne, whanne it schynede, and the moone goynge clereli;
kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
27 and if myn herte was glad in priuyte, and if Y kisside myn hond with my mouth;
hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
28 which is the moost wickidnesse, and deniyng ayens hiyeste God;
basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
29 if Y hadde ioye at the fallyng of hym, that hatide me, and if Y ioide fulli, that yuel hadde founde hym;
“Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
30 for Y yaf not my throte to do synne, that Y schulde asaile and curse his soule;
lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
31 if the men of my tabernacle seiden not, Who yyueth, that we be fillid of hise fleischis? a pilgryme dwellide not with outforth;
kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
32 my dore was opyn to a weiegoere;
Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
33 if Y as man hidde my synne, and helide my wickidnesse in my bosum;
kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
34 if Y dredde at ful greet multitude, and if dispisyng of neyyboris made me aferd; and not more Y was stille, and yede not out of the dore;
kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
35 who yyueth an helpere to me, that Almyyti God here my desire? that he that demeth,
(“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
36 write a book, that Y bere it in my schuldre, and cumpasse it as a coroun to me?
Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
37 Bi alle my degrees Y schal pronounce it, and Y schal as offre it to the prynce.
Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
38 If my lond crieth ayens me, and hise forewis wepen with it;
“Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
39 if Y eet fruytis therof with out money, and Y turmentide the soule of erthetileris of it;
kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
40 a brere growe to me for wheete, and a thorn for barli.
basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.