< Job 30 >

1 But now yongere men in tyme scornen me, whos fadris Y deynede not to sette with the doggis of my flok.
“Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
2 Of whiche men the vertu of hondis was for nouyt to me, and thei weren gessid vnworthi to that lijf.
Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
3 Thei weren bareyn for nedynesse and hungur; that gnawiden in wildirnesse, and weren pale for pouert and wretchidnesse;
Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
4 and eeten eerbis, aud the ryndis of trees; and the roote of iunyperis was her mete.
Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
5 Whiche men rauyschiden these thingis fro grete valeis; and whanne thei hadden foundun ony of alle, thei runnen with cry to tho.
Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
6 Thei dwelliden in deseertis of strondis, and in caues of erthe, ethir on grauel, `ethir on cley.
Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
7 Whiche weren glad among siche thingis, and arettiden delices to be vndur buschis.
Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
8 The sones of foolis and of vnnoble men, and outirli apperynge not in erthe.
Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
9 But now Y am turned in to the song of hem, and Y am maad a prouerbe to hem.
“Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
10 Thei holden me abhomynable, and fleen fer fro me, and dreden not to spete on my face.
Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
11 For God hath openyd his arowe caas, and hath turmentid me, and hath set a bridil in to my mouth.
Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
12 At the riytside of the eest my wretchidnessis risiden anoon; thei turneden vpsedoun my feet, and oppressiden with her pathis as with floodis.
Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
13 Thei destrieden my weies; thei settiden tresoun to me, and hadden the maistri; and `noon was that helpide.
Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
14 Thei felden in on me as bi a brokun wal, and bi yate openyd, and weren stretchid forth to my wretchidnessis.
Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
15 Y am dryuun in to nouyt; he took awei my desir as wynd, and myn helpe passide awei as a cloude.
Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
16 But now my soule fadith in my silf, and daies of turment holden me stidfastly.
“Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
17 In nyyt my boon is persid with sorewis; and thei, that eten me, slepen not.
Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
18 In the multitude of tho my cloth is wastid, and thei han gird me as with coler of a coote.
Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
19 Y am comparisound to cley, and Y am maad lijk to a deed sparcle and aisch.
Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
20 Y schal cry to thee, and thou schalt not here me; Y stonde, and thou biholdist not me.
“Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
21 Thou art chaungid in to cruel to me, and in the hardnesse of thin hond thou art aduersarie to me.
Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
22 Thou hast reisid me, and hast set as on wynd; and hast hurtlid me doun strongli.
Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
23 Y woot, that thow schalt bitake me to deeth, where an hows is ordeyned to ech lyuynge man.
Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
24 Netheles thou sendist not out thin hond to the wastyng of hem; and if thei fallen doun, thou schalt saue.
“Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
25 Y wepte sum tyme on him, that was turmentid, and my soule hadde compassioun on a pore man.
Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
26 Y abood goodis, and yuelis ben comun to me; Y abood liyt, and derknessis braken out.
Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
27 Myn ynnere thingis buyliden out with outen my reste; daies of turment camen bifor me.
Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
28 Y yede morenynge, and Y roos with out woodnesse in the cumpenye, and criede.
Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
29 Y was the brother of dragouns, and the felow of ostrigis.
Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
30 My skyn was maad blak on me, and my boonys drieden for heete.
Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
31 Myn harpe is turned in to morenyng, and myn orgun in to the vois of weperis.
Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.

< Job 30 >