< Job 12 >

1 Sotheli Joob answeride, and seide,
Ndipo Ayubu akajibu:
2 Therfor ben ye men aloone, that wisdom dwelle with you?
“Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
3 And to me is an herte, as and to you, and Y am not lowere than ye; for who knowith not these thingis, whiche ye knowen?
Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
4 He that is scorned of his frend, as Y am, schal inwardli clepe God, and God schal here hym; for the symplenesse of a iust man is scorned.
“Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
5 A laumpe is dispisid at the thouytis of riche men, and the laumpe is maad redi to a tyme ordeyned.
Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
6 The tabernaclis of robberis ben plenteuouse, `ether ful of goodis; and boldli thei terren God to wraththe, whanne he hath youe alle thingis in to her hondis.
Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
7 No wondur, ax thou beestis, and tho schulen teche thee; and axe thou volatilis of the eir, and tho schulen schewe to thee.
“Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
8 Speke thou to the erthe, and it schal answere thee; and the fischis of the see schulen telle tho thingis.
au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
9 Who knowith not that the hond of the Lord made alle these thingis?
Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
10 In whos hond the soule is of ech lyuynge thing, and the spirit, `that is, resonable soule, of ech fleisch of man.
Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
11 Whether the eere demeth not wordis, and the chekis of the etere demen sauour?
Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
12 Wisdom is in elde men, and prudence is in myche tyme.
Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
13 Wisdom and strengthe is at God; he hath counsel and vndurstondyng.
“Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
14 If he distrieth, no man is that bildith; if he schittith in a man, `noon is that openith.
Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
15 If he holdith togidere watris, alle thingis schulen be maad drie; if he sendith out tho watris, tho schulen distrie the erthe.
Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
16 Strengthe and wisdom is at God; he knowith bothe hym that disseyueth and hym that is disseyued.
Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
17 And he bryngith conselours in to a fonned eende, and iugis in to wondryng, ethir astonying.
Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
18 He vnbindith the girdil of kyngis, and girdith her reynes with a coorde.
Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
19 He ledith her prestis with out glorie, and he disseyueth the principal men, `ethir counselours;
Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
20 and he chaungith the lippis of sothefast men, and takith awei the doctrine of elde men.
Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
21 He schedith out dispisyng on princes, and releeueth hem, that weren oppressid.
Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
22 Which schewith depe thingis fro derknessis; and bryngith forth in to liyt the schadewe of deeth.
Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
23 Which multiplieth folkis, and leesith hem, and restorith hem destried in to the hool.
Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
24 Which chaungith the herte of princes of the puple of erthe; and disseyueth hem, that thei go in veyn out of the weie.
Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
25 Thei schulen grope, as in derknessis, and not in liyt; and he schal make hem to erre as drunken men.
Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.

< Job 12 >