< Jeremiah 36 >

1 And it was don, in the fourthe yeer of Joachym, sone of Josie, kyng of Juda, this word was maad of the Lord to Jeremye, and seide,
Katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilimjia nabii Yeremia kutoka kwa Bwana, kusema:
2 Take thou the volym of a book, and thou schalt write therynne alle the wordis, whiche Y spake to thee ayens Israel and Juda, and ayens alle folkis, fro the dai in whiche Y spak to thee, fro the daies of Josie `til to this dai.
“Chukua kitabu uandike ndani yake maneno yote niliyonena nawe kuhusu Israeli, Yuda na mataifa mengine yote, tangu nilipoanza kunena nawe wakati wa utawala wa Yosia hadi sasa.
3 If perauenture whanne the hous of Juda herith alle the yuels whiche Y thenke to do to hem, ech man turne ayen fro his worste weye, and Y schal be merciful to the wickidnesse and synne of hem.
Labda watu wa Yuda watakaposikia juu ya kila maafa ninayokusudia kuwapiga nayo, kila mmoja wao atageuka kutoka njia zake mbaya, kisha nitasamehe uovu wao na dhambi yao.”
4 Therfor Jeremye clepide Baruk, the sone of Nerye; and Baruk wroot of the mouth of Jeremye in the volym of a book alle the wordis of the Lord, whiche he spak to hym.
Hivyo Yeremia akamwita Baruku mwana wa Neria, naye Yeremia alipokuwa akiyakariri maneno yote aliyoyasema Bwana, Baruku akayaandika katika kitabu.
5 And Jeremye comaundide to Baruk, and seide, Y am closid, and Y may not entre in to the hous of the Lord.
Kisha Yeremia akamwambia Baruku, “Nimezuiliwa, mimi siwezi kuingia katika Hekalu la Bwana.
6 Therfor entre thou, and rede of the book, in which thou hast write of my mouth the wordis of the Lord, in hering of the puple, in the hous of the Lord, in the dai of fastyng; ferthermore and in heryng of al Juda, that comen fro her citees, thou schalt rede to hem;
Basi wewe nenda katika nyumba ya Bwana siku ya kufunga, uwasomee watu maneno ya Bwana kutoka kitabu hiki yale uliyoyaandika kutoka kinywani mwangu. Wasomee watu wote wa Yuda waliofika kutoka miji yao.
7 if perauenture the preier of hem falle in the siyt of the Lord, and eche man turne ayen fro his worste weie; for whi the strong veniaunce and indignacioun is greet, which the Lord spak ayens this puple.
Labda wataomba na kusihi mbele za Bwana na kila mmoja akageuka kutoka njia zake mbaya, kwa sababu hasira na ghadhabu zilizotamkwa dhidi ya watu hawa na Bwana ni kubwa.”
8 And Baruk, the sone of Nerie, dide aftir alle thingis, which Jeremye, the prophete, comaundide to hym; and he redde of the book the wordis of the Lord, in the hous of the Lord.
Baruku mwana wa Neria akafanya kila kitu nabii Yeremia alichomwambia kufanya. Alisoma maneno ya Bwana katika Hekalu la Bwana kutoka kile kitabu.
9 Forsothe it was doon, in the fyueth yeer of Joachym, sone of Josie, kyng of Juda, in the nynthe monethe, thei prechiden fastynge in the siyt of the Lord, to al the puple in Jerusalem, and to al the multitude, that cam togidere fro the citees of Juda in to Jerusalem.
Katika mwezi wa tisa, mnamo mwaka wa tano wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, wakati wa kufunga mbele za Bwana, ilitangazwa kwa watu wote walioko Yerusalemu, na wale wote waliokuwa wamekuja kutoka miji ya Yuda.
10 And Baruc redde of the volym the wordis of Jeremye, in the hous of the Lord, in the treserie of Gamarie, sone of Saphan, scryuen, in the hiyere porche, in the entring of the newe yate of the hous of the Lord, in audience of al the puple.
Kutoka chumba cha Gemaria mwana wa Shafani mwandishi, kilichokuwa katika ua wa juu kwenye ingilio la Lango Jipya la Hekalu, Baruku akawasomea watu wote waliokuwa katika Hekalu la Bwana maneno ya Yeremia kutoka kwenye kile kitabu.
11 And whanne Mychie, the sone of Gamarie, sone of Saphan, hadde herd alle the wordis of the Lord,
Basi Mikaya mwana wa Gemaria, mwana wa Shafani, aliposikia maneno yote ya Bwana kutoka kwenye kile kitabu,
12 of the book, he yede doun in to the hous of the kyng, to the treserye of the scryuen. And lo! alle the princes saten there, Elisama, the scryuen, and Dalaie, the sone of Semeye, and Elnathan, the sone of Achabor, and Gamarie, the sone of Saphan, and Sedechie, the sone of Ananye, and alle princes.
alishuka hadi kwenye chumba cha mwandishi kwenye jumba la kifalme, mahali walipokuwa wameketi maafisa wote: yaani Elishama mwandishi, Delaya mwana wa Shemaya, Elnathani mwana wa Akbori, Gemaria mwana wa Shafani, Sedekia mwana wa Hanania, na maafisa wengine wote.
13 And Mychee telde to hem alle the wordis, whiche he herde Baruc redynge of the book, in the eeris of the puple.
Baada ya Mikaya kuwaambia kila kitu ambacho alikuwa amesikia Baruku akiwasomea watu kutoka kwenye kile kitabu,
14 Therfor alle the princes senten to Baruc Judi, the sone of Nathathie, sone of Selemye, sone of Chusi, and seiden, Take in thin hond the book, of which thou reddist in audience of the puple, and come thou. Therfor Baruc, the sone of Nereie, took the book in his hoond, and cam to hem.
maafisa wote wakamtuma Yehudi mwana wa Nethania, mwana wa Shelemia, mwana wa Kushi, kumwambia Baruku, “Leta hicho kitabu ambacho umewasomea watu, nawe mwenyewe uje.” Ndipo Baruku mwana wa Neria akawaendea akiwa na hicho kitabu mkononi mwake.
15 And thei seiden to hym, Sitte thou, and rede these thingis in oure eeris; and Baruc redde in the eeris of hem.
Wakamwambia, “Tafadhali, keti na utusomee hicho kitabu.” Ndipo Baruku akawasomea kile kitabu.
16 Therfor whanne thei hadden herd alle the wordis, thei wondriden ech man to his neiybore, and thei seiden to Baruc, Owen we to telle to the kyng alle these wordis?
Walipoyasikia maneno hayo yote, wakatazamana wao kwa wao kwa woga na kumwambia Baruku, “Lazima tutoe taarifa ya maneno haya yote kwa mfalme.”
17 And thei axiden hym, and seiden, Schewe thou to vs, hou thou hast write alle these wordis of his mouth.
Kisha wakamuuliza Baruku, “Tuambie, uliandikaje haya yote? Je, yalitoka kinywani mwa Yeremia?”
18 Forsothe Baruc seide to hem, Of his mouth he spak, as redynge to me, alle these wordis; and Y wroot in a book with enke.
Baruku akajibu, “Ndiyo, maneno haya yote yalitoka kinywani mwa Yeremia, nami nikayaandika kwa wino katika hiki kitabu.”
19 And alle the princes seiden to Baruc, Go, be thou hid, thou and Jeremye; and no man wite where ye ben.
Ndipo wale maafisa wakamwambia Baruku, “Wewe na Yeremia nendeni mkajifiche. Mtu yeyote asijue mahali mlipo.”
20 And thei entriden to the kyng, in to the halle; forsothe thei bitoken the book to be kept in to the treserie of Elisame, the scryuen. And thei telden alle the wordis, in audience of the kyng.
Baada ya kuhifadhi kile kitabu ndani ya chumba cha Elishama mwandishi, wakamwendea mfalme katika ua wa nje na kumwarifu kila kitu.
21 Therfor the kyng sente Judi, that he schulde take the book. Which took the book fro the treserie of Elysame, the scryuen, and redde in audience of the kyng, and of alle the princes, that stoden aboute the kyng.
Mfalme akamtuma Yehudi akachukue kile kitabu. Yehudi akakileta hicho kitabu kutoka kwenye chumba cha Elishama mwandishi, na akakisoma mbele ya mfalme na maafisa wakiwa wamesimama kando ya mfalme.
22 Forsothe the kyng sat in the wyntir hous, in the nynthe monethe; and a panne ful of coolis was set bifore hym.
Ulikuwa mwezi wa tisa, na mfalme alikuwa ameketi chumba cha wakati wa baridi akiota moto.
23 And whanne Judi hadde red thre pagyns, ethir foure, he kittide it with the knyf of a scryueyn, and castide in to the fier, `that was in the panne, til al the book was wastid bi the fier, that was on the panne.
Hata ikawa kila wakati Yehudi alipomaliza kusoma kurasa tatu au nne za hicho kitabu, mfalme alizikata kwa kisu cha mwandishi na kuzitupia motoni, hadi kitabu chote kikateketea.
24 And the kyng and alle hise seruauntis, that herden alle these wordis, dredden not, nethir to-renten her clothis.
Mfalme na watumishi wake wote waliosikia yote yaliyosomwa hawakuonyesha hofu yoyote, wala hawakuyararua mavazi yao.
25 Netheles Elnathan, and Dalaie, and Gamarie ayenseiden the kyng, that he schulde not brenne the book; and he herde not hem.
Hata ingawa Elnathani, Delaya na Gemaria walimsihi mfalme asikichome kile kitabu, yeye hakuwasikiliza.
26 And the kyng comaundide to Jeremyel, sone of Amalech, and to Saraie, sone of Esreel, and to Selemye, sone of Abdehel, that thei schulden take Baruc, the writer, and Jeremye, the profete; forsothe the Lord hidde hem.
Badala yake, mfalme akamwamuru Yerameeli, mwana wa mfalme, Seraya mwana wa Azrieli, na Shelemia mwana wa Abdeeli kuwakamata mwandishi Baruku na nabii Yeremia. Lakini Bwana alikuwa amewaficha.
27 And the word of the Lord was maad to Jeremye, the profete, aftir that the kyng hadde brent the book and wordis, whiche Baruc hadde write of Jeremyes mouth;
Baada ya mfalme kuchoma kile kitabu kilichokuwa na yale maneno Baruku aliyokuwa ameyaandika kutoka kinywani mwa Yeremia, neno la Bwana lilimjia Yeremia likisema:
28 and he seid, Eft take thou another book, and write therynne alle the former wordis, that weren in the firste book, which Joachym, the kyng of Juda, brente.
“Chukua kitabu kingine na uandike juu yake maneno yote yaliyokuwa katika kile kitabu cha kwanza, ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda amekiteketeza kwa moto.
29 And thou schalt seie to Joachym, kyng of Juda, The Lord seith these thingis, Thou brentist that book, and seidist, What hast thou write therynne, tellynge, The kyng of Babiloyne schal come hastynge, and schal distrie this lond, and schal make man and beeste to ceesse therof?
Mwambie pia Yehoyakimu mfalme wa Yuda, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ulikiteketeza kile kitabu ukasema, “Kwa nini uliandika kwenye kitabu kwamba kwa hakika mfalme wa Babeli angekuja na kuangamiza nchi hii, na kuwakatilia mbali watu na wanyama kutoka humo?”
30 Therfor the Lord seith these thingis ayens Joachym, king of Juda, Noon schal be of hym, that schal sitte on the seete of Dauid; and his careyn schal be cast forth to the heete bi dai, and to the forst bi niyt.
Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana kuhusu Yehoyakimu mfalme wa Yuda: Hatakuwa na mtu yeyote atakayekalia kiti cha enzi cha Daudi; maiti yake itatupwa nje kwenye joto wakati wa mchana na kupigwa na baridi wakati wa usiku.
31 And Y schal visite ayens hym, and ayens his seed, and ayens hise seruauntis, her wickidnessis. And Y schal bryng on hem, and on the dwelleris of Jerusalem, and on the men of Juda, al the yuel which Y spak to hem, and thei herden not.
Nitamwadhibu yeye, watoto wake na watumishi wake kwa ajili ya uovu wao. Nitaleta juu yao na wote waishio Yerusalemu na watu wa Yuda kila maafa niliyoyasema dhidi yao, kwa sababu hawajasikiliza.’”
32 Forsothe Jeremye took an other book, and yaf it to Baruc, the writer, the sone of Nerie, which wroot therynne of Jeremyes mouth alle the wordis of the book, which book Joachym, the kyng of Juda, hadde brent bi fier; and ferthermore many mo wordis weren addid than weren bifore.
Kisha Yeremia akachukua kitabu kingine na kumpa mwandishi Baruku mwana wa Neria, naye kama Yeremia alivyosema, Baruku akaandika juu yake maneno yote ya kile kitabu ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda alikuwa amekichoma moto, na maneno mengine mengi yaliyofanana na hayo yaliyoongezewa humo.

< Jeremiah 36 >