< Jeremiah 25 >

1 The word of the Lord, that was maad to Jeremye, of al the puple of Juda, in the fourthe yeer of Joachym, the sone of Josie, the king of Juda, aftir that Jeconye was translatid in to Babiloyne; thilke is the firste yeer of Nabugodonosor, kyng of Babiloyne; which word Jeremy,
Neno likamjia Yeremia kuhusu watu wote wa Yuda, katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, ambao ulikuwa mwaka wa kwanza wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli.
2 the prophete, spak to al the puple of Juda, and to alle the dwelleris of Jerusalem, and seide,
Hivyo nabii Yeremia akawaambia watu wote wa Yuda na wale wote waishio Yerusalemu:
3 Fro the threttenthe yeer of the rewme of Josie, the sone of Amon, the kyng of Juda, `til to this dai, this is the three and twentithe yeer, the word of the Lord was maad to me; and Y spak to you, and Y roos bi niyt and spak, and ye herden not.
Kwa miaka ishirini na mitatu, kuanzia mwaka wa kumi na tatu wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda, hadi siku hii ya leo, neno la Bwana limekuwa likinijia, nami nimesema nanyi mara kwa mara, lakini hamkusikiliza.
4 And the Lord sente to you alle hise seruauntis profetis, and roos ful eerli, and sente, and ye herden not, nether ye bowiden youre eeris, for to here;
Ingawa Bwana amewatuma watumishi wake wote hao manabii kwenu mara kwa mara, hamkusikiliza wala hamkujali.
5 whanne he seide, Turne ye ayen, ech man fro his yuel weie, and fro youre worste thouytis, and ye schulen dwelle in the lond whiche the Lord yaf to you, and to youre fadris, fro the world and til in to the world.
Walisema, “Geukeni sasa, kila mmoja wenu kutoka njia yake mbaya na matendo yake maovu, ndipo mtaweza kukaa katika nchi ambayo Bwana aliwapa ninyi na baba zenu milele.
6 And nyle ye go aftir alien goddis, that ye serue hem, and worschipe hem, nether terre ye me to wrathfulnesse, in the werkis of youre hondis, and Y schal not turmente you.
Msiifuate miungu mingine ili kuitumikia na kuiabudu. Msinikasirishe kwa vitu ambavyo mmevitengeneza kwa mikono yenu.”
7 And ye herden not me, seith the Lord, that ye terreden me to wrathfulnesse in the werkis of youre hondis, in to youre yuel.
“Lakini ninyi hamkunisikiliza mimi, tena mkanikasirisha kwa vitu mlivyovitengeneza kwa mikono yenu, nanyi mmejiletea madhara juu yenu wenyewe,” asema Bwana.
8 Therfor the Lord of oostis seith these thingis, For that that ye herden not my wordis, lo!
Kwa hiyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asema hivi: “Kwa sababu hamkuyasikiliza maneno yangu,
9 Y schal sende, and take alle the kynredis of the north, seith the Lord, and Nabugodonosor, my seruaunt, the kyng of Babiloyne; and Y schal bringe hem on this lond, and on the dwelleris therof, and on alle naciouns, that ben in the cumpas therof; and Y schal sle hem, and Y schal sette hem in to wondryng, and in to hissyng, and in to euerlastynge wildirnessis.
nitayaita mataifa yote ya kaskazini na mtumishi wangu Nebukadneza mfalme wa Babeli,” asema Bwana. “Nitawaleta waishambulie nchi hii na wakazi wake wote, na dhidi ya mataifa yote yanayowazunguka. Nitawaangamiza kabisa na kuwafanya kitu cha kuchukiwa na kudharauliwa, na kuwa magofu daima.
10 And Y schal leese of hem the vois of ioye, and the vois of gladnesse, the vois of spouse, and the vois of spousesse, the vois of queerne, and the liyt of the lanterne.
Nitawaondolea sauti ya shangwe na furaha, sauti ya bibi na bwana arusi, sauti ya mawe ya kusagia, na mwanga wa taa.
11 And al the lond therof schal be in to wildirnesse, and in to wondring; and alle these folkis schulen serue the king of Babiloyne seuenti yeer.
Nchi hii yote itakuwa ukiwa na isiyofaa kitu, nayo mataifa haya yatamtumikia mfalme wa Babeli kwa miaka sabini.”
12 And whanne seuenti yeer ben fillid, Y schal visite on the kyng of Babiloyne, and on that folc the wickidnesse of hem, seith the Lord, and on the lond of Caldeis, and Y schal set it in to euerlastynge wildirnesses.
“Lakini miaka sabini itakapotimia, nitamwadhibu mfalme wa Babeli na taifa lake na nchi ya Wakaldayo kwa ajili ya hatia yao,” asema Bwana. “Nitaifanya kuwa ukiwa milele.
13 And Y schal brynge on that lond alle my wordis whiche Y spak ayens it, al thing that is writun in this book; what euer thingis Jeremye profeside ayens alle folkis;
Nitaleta juu ya nchi hiyo mambo yote niliyosema dhidi yake, yote yaliyoandikwa katika kitabu hiki, na kutolewa unabii na Yeremia dhidi ya mataifa yote.
14 for thei serueden to hem, whanne thei weren many folkis, and grete kingis; and Y schal yelde to hem aftir the werkis of hem, and aftir the dedis of her hondis.
Wao wenyewe watakuwa watumwa wa mataifa mengi na wafalme wakuu. Nitawalipizia sawasawa na matendo yao na kazi ya mikono yao.”
15 For the Lord of oostis, God of Israel, seith thus, Take thou the cuppe of wyn of this woodnesse fro myn hond, and thou schal birle therof to alle hethene men, to whiche Y schal sende thee.
Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, aliloniambia: “Chukua kutoka mkononi mwangu kikombe hiki kilichojaa divai ya ghadhabu yangu, na kuyanywesha mataifa yote ambayo ninakutuma kwao.
16 And thei schulen drynke, and schulen be disturblid, and schulen be woode of the face of swerd, which Y schal sende among hem.
Watakapoinywa, watapepesuka na kukasirika sana kwa sababu ya upanga nitakaoupeleka katikati yao.”
17 And Y took the cuppe fro the hond of the Lord, and Y birlide to alle folkis, to whiche the Lord sente me;
Hivyo nikakichukua kikombe kutoka mkononi mwa Bwana, na kuyafanya mataifa yote aliyonituma kwao kukinywa:
18 to Jerusalem, and to alle the citees of Juda, and to the kyngis therof, and to the princes therof; that Y schulde yyue hem in to wildirnesse, and in to wondring, and in to hissyng, and in to cursing, as this dai is; to Farao,
Yaani Yerusalemu na miji ya Yuda, wafalme wake na maafisa wake, kuwafanya magofu na kuwa kitu cha kuchukiza, cha dhihaka na laana, kama walivyo leo;
19 the king of Egipt, and to hise seruauntis, and to hise princes, and to al hise puple;
pia Farao mfalme wa Misri, watumishi wake, maafisa wake na watu wake wote,
20 and to alle men generali, to alle the kyngis of the lond Ansitidis, and to alle the kyngis of the lond of Filistiym, and to Ascalon, and to Gaza, and to Acoron, and to the residues of Azotus;
pia wageni wote walioko huko; wafalme wote wa nchi ya Usi; wafalme wote wa Wafilisti (wale wa Ashkeloni, Gaza, Ekroni na watu walioachwa huko Ashdodi);
21 to Idumee, and to Moab, and to the sones of Amon;
Edomu, Moabu na Amoni;
22 and to alle the kyngis of Tirus, and to alle the kingis of Sidon, and to the kingis of the lond of ilis that ben biyendis the see;
wafalme wote wa Tiro na Sidoni; wafalme wa nchi za pwani ngʼambo ya bahari;
23 and to Dedan, and Theman, and Buz, and to alle men that ben clippid on the long heer;
Dedani, Tema, Buzi na wote walio maeneo ya mbali;
24 and to alle the kingis of Arabie, and to alle the kingis of the west, that dwellen in desert;
wafalme wote wa Arabuni na wafalme wote wa watu wageni wanaoishi katika jangwa;
25 and to alle the kingis of Zambri, and to alle the kingis of Elam, and to alle the kyngis of Medeis; and to alle the kingis of the north,
wafalme wote wa Zimri, Elamu na Umedi;
26 of niy and of fer, to ech man ayens his brothir; and to alle the rewmes of erthe, that ben on the face therof; and kyng Sesac schal drynke after hem.
na wafalme wote wa pande za kaskazini, wa karibu na wa mbali, mmoja baada ya mwingine; yaani falme zote juu ya uso wa dunia. Baada ya hao wote, mfalme wa Sheshaki atakunywa pia.
27 And thou schalt seie to hem, The Lord of oostis, God of Israel, seith these thingis, Drynke ye, and be ye drunkun, and spue ye, and falle ye doun, and nyle ye rise fro the face of swerd which Y schal sende among you.
“Kisha uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Kunyweni, mlewe na mtapike; angukeni, wala msiinuke tena kwa sababu ya upanga nitakaotuma miongoni mwenu.’
28 And whanne thei nylen take the cuppe fro thin hond, that thei drynke, thou schalt seie to hem, The Lord of oostis seith these thingis, Ye drynkynge schulen drynke;
Lakini kama wakikataa kupokea kikombe kutoka mikononi mwako na kunywa, waambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: Ni lazima mnywe!
29 for lo! in the citee in which my name is clepid to help, Y bigynne to turmente, and schulen ye as innocentis be with out peyne? ye schulen not be with out peyne, for Y clepe swerd on alle the dwelleris of erthe, seith the Lord of oostis.
Tazama, nimeanza kuleta maafa juu ya mji ulio na Jina langu, na je, kweli ninyi mtaepuka kuadhibiwa? Hamwezi kuepuka kuadhibiwa, kwa maana nitaleta vita juu ya wote waishio duniani, asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.’
30 And thou schalt profesie to hem alle these wordis, and thou schalt seie to hem, The Lord schal rore fro an hiy, and fro his hooli dwellyng place he schal yyue his vois; he rorynge schal rore on his fairnesse; a myry song, as of men tredynge in pressouris, schal be sungun ayens alle dwelleris of erthe.
“Basi sasa toa unabii kwa maneno haya yote dhidi yao, uwaambie: “‘Bwana atanguruma kutoka juu; atatoa sauti ya ngurumo kutoka makao yake matakatifu na kunguruma kwa nguvu sana dhidi ya nchi yake. Atapiga kelele kama wao wakanyagao zabibu, atapiga kelele dhidi ya wote waishio duniani.
31 Sown is comun til to the laste partis of erthe, for whi doom is to the Lord with folkis, he is demed with ech fleisch; the Lord seith, Y haue youe wickid men to the swerd.
Ghasia zitasikika hadi miisho ya dunia, kwa maana Bwana ataleta mashtaka dhidi ya mataifa; ataleta hukumu juu ya wanadamu wote na kuwaua waovu wote,’” asema Bwana.
32 The Lord of oostis seith these thingis, Lo! turment schal go out fro folk in to folk, and a greet whirlwynd schal go out fro the endis of erthe.
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Tazama! Maafa yanaenea kutoka taifa moja hadi jingine; tufani kubwa inainuka kutoka miisho ya dunia.”
33 And the slayn men of the Lord schulen be in that dai fro the ende of the erthe `til to the ende therof; thei schulen not be biweilid, nether schulen be gaderid togidere, nether schulen be biried; thei schulen ligge in to a dunghil on the face of erthe.
Wakati huo, hao waliouawa na Bwana watatapakaa kila mahali, kuanzia mwisho mmoja wa dunia hadi mwisho mwingine. Hawataombolezewa wala kukusanywa au kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyoenea juu ya ardhi.
34 Yelle, ye scheepherdis, and crye, and, ye princypals of the floc, bispreynge you with aische; for youre daies ben fillid, that ye be slayn, and youre scateryngis ben fillid, and ye schulen falle as precious vessels.
Lieni na kuomboleza, enyi wachungaji, mgaagae mavumbini, ninyi viongozi wa kundi. Kwa maana wakati wenu wa kuchinjwa umewadia; mtaanguka na kuvunjavunjwa kama vyombo vizuri vya udongo.
35 And fleyng schal perische fro scheepherdis, and sauyng schal perische fro the principals of the floc.
Wachungaji hawatakuwa na mahali pa kukimbilia, viongozi wa kundi hawatapata mahali pa kutorokea.
36 The vois of the crye of scheepherdis, and the yellyng of the principals of the floc, for the Lord hath wastid the lesewis of hem.
Sikia kilio cha wachungaji, maombolezo ya viongozi wa kundi, kwa maana Bwana anayaharibu malisho yao.
37 And the feeldis of pees weren stille, for the face of wraththe of the strong veniaunce of the Lord.
Makao yao ya amani yataharibiwa kwa sababu ya hasira kali ya Bwana.
38 He as a lion hath forsake his tabernacle, for the lond of hem is maad in to desolacioun, of the face of wraththe of the culuer, and of the face of wraththe of the strong veniaunce of the Lord.
Kama simba ataacha pango lake, nchi yao itakuwa ukiwa kwa sababu ya upanga wa mdhalimu, na kwa sababu ya hasira kali ya Bwana Mungu.

< Jeremiah 25 >