< Jeremiah 18 >
1 The word that was maad of the Lord to Jeremye,
Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
2 and seide, Rise thou, and go doun in to the hous of a pottere, and there thou schalt here my wordis.
“Shuka uende mpaka nyumba ya mfinyanzi, nami huko nitakupa ujumbe wangu.”
3 And Y yede doun in to the hous of a pottere, and lo! he made a werk on a wheel.
Kwa hiyo nikashuka mpaka kwenye nyumba ya mfinyanzi, nikamkuta akifinyanga kwa gurudumu lake.
4 And the vessel was distried, which he made of clei with hise hondis; and he turnede it, and made it another vessel, as it pleside in hise iyen to make.
Lakini chombo alichokuwa akikifinyanga kutokana na udongo kilivunjika mikononi mwake, hivyo mfinyanzi akakifanya kuwa chombo kingine, umbo jingine kama vile ilivyoonekana vyema kwake yeye.
5 And the word of the Lord was maad to me,
Kisha neno la Bwana likanijia kusema:
6 and he seide, Whether as this pottere doith, Y mai not do to you, the hous of Israel? seith the Lord. Lo! as cley is in the hond of a pottere, so ye, the hous of Israel, ben in myn hond.
“Ee nyumba ya Israeli, je, siwezi kuwafanyia kama huyu mfinyanzi afanyavyo?” asema Bwana. “Kama vile udongo ulivyo katika mikono ya mfinyanzi, ndivyo mlivyo katika mkono wangu, ee nyumba ya Israeli.
7 Sudenli Y schal speke ayens a folk, and ayens a rewme, that Y drawe out, and distrie, and leese it.
Ikiwa wakati wowote nikitangaza kuwa taifa au ufalme utangʼolewa, utaangushwa na kuangamizwa,
8 If thilke folk doith penaunce of his yuel, which Y spak ayens it, also Y schal do penaunce on the yuel, which Y thouyte to do to it.
ikiwa lile taifa nililolionya litatubia uovu wake, ndipo nitakapokuwa na huruma, wala sitawapiga kwa maafa niliyokuwa nimewakusudia.
9 And Y schal speke sudenli of a folk, and of a rewme, that Y bilde, and plaunte it.
Ikiwa wakati mwingine nitatangaza kuwa taifa ama utawala ujengwe na kuwekwa wakfu,
10 If it doith yuel bifore myn iyen, that it here not my vois, Y schal do penaunce on the good which Y spak, that Y schulde do to it.
ikiwa utafanya maovu mbele zangu na hukunitii, ndipo nitakapoghairi makusudio yangu mema niliyokuwa nimeyakusudia.
11 Now therfor seie thou to a man of Juda, and to the dwellere of Jerusalem, and seie, The Lord seith these thingis, Lo! Y make yuel ayens you, and Y thenke a thouyte ayens you; ech man turne ayen fro his yuel weie, and dresse ye youre weies and youre studies.
“Basi kwa hiyo waambie watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Tazama! Ninaandaa maafa kwa ajili yenu, nami ninabuni mabaya dhidi yenu. Kwa hiyo geukeni kutoka njia zenu mbaya, kila mmoja wenu, tengenezeni njia zenu na matendo yenu.’
12 Whiche seiden, We han dispeirid, for we schulen go after oure thouytis, and we schulen do ech man the schrewidnesse of his yuel herte.
Lakini wao watajibu, ‘Hakuna faida. Tutaendelea na mipango yetu wenyewe, kila mmoja wetu atafuata ukaidi wa moyo wake mbaya.’”
13 Therfor the Lord seith these thingis, Axe ye hethene men, who herde siche orible thingis, whiche the virgyn of Israel hath do greetli?
Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana: “Ulizia miongoni mwa mataifa: Ni nani alishasikia jambo kama hili? Jambo la kutisha sana limefanywa na Bikira Israeli.
14 Whether snow of the Liban schal fail fro the stoon of the feeld? ether coolde watris brekynge out, and fletynge doun moun be takun awei?
Je, barafu ya Lebanoni iliwahi kutoweka kwenye miteremko yake ya mawe wakati wowote? Je, maji yake baridi yatokayo katika vyanzo vilivyo mbali yaliwahi kukoma kutiririka wakati wowote?
15 For my puple hath foryete me, and offriden sacrifices in veyn, and snaperiden in her weies, and in the pathis of the world, that thei yeden bi tho in a weie not trodun;
Lakini watu wangu wamenisahau mimi, wanafukizia uvumba sanamu zisizofaa kitu, zilizowafanya wajikwae katika njia zao na katika mapito ya zamani. Zimewafanya wapite kwenye vichochoro na kwenye barabara ambazo hazikujengwa.
16 that the lond of hem schulde be in to desolacioun, and in to an hissyng euerlastinge; for whi ech that passith bi it, schal be astonyed, and schal moue his heed.
Nchi yao itaharibiwa, itakuwa kitu cha kudharauliwa daima; wote wapitao karibu nayo watashangaa na kutikisa vichwa vyao.
17 As a brennynge wynd Y schal scatere hem bifor the enemy; Y schal schewe to hem the bak and not the face, in the dai of the perdicioun of hem.
Kama upepo utokao mashariki, nitawatawanya mbele ya adui zao; nitawapa kisogo wala sio uso, katika siku ya maafa yao.”
18 And thei seiden, Come ye, and thenke we thouytis ayens Jeremye; for whi the lawe schal not perische fro a preest, nether councel schal perische fro a wijs man, nether word schal perische fro a profete; come ye, and smyte we hym with tunge, and take we noon heede to alle the wordis of hym.
Wakasema, “Njooni, tutunge hila dhidi ya Yeremia; kwa kuwa kufundisha sheria kwa kuhani hakutapotea, wala shauri litokalo kwa mwenye hekima, wala neno la manabii. Hivyo njooni, tumshambulie kwa ndimi zetu na tusijali chochote asemacho.”
19 Lord, yyue thou tent to me, and here thou the vois of myn aduersaries.
Nisikilize, Ee Bwana, sikia wanayosema washtaki wangu!
20 Whether yuel is yoldun for good, for thei han diggid a pit to my soule; haue thou mynde, that Y stoode in thi siyt, to speke good for hem, and to turne awei thin indignacioun fro hem.
Je, mema yalipwe kwa mabaya? Lakini wao wamenichimbia shimo. Kumbuka kwamba nilisimama mbele yako na kunena mema kwa ajili yao, ili wewe ugeuze hasira yako kali mbali nao.
21 Therfor yyue thou the sones of hem in to hungur, and lede forth hem in to the hondis of swerd; the wyues of hem be maad with out children, and be maad widewis, and the hosebondis of hem be slayn bi deth; the yonge men of hem be persid togidere bi swerd in batel.
Kwa hiyo uwaache watoto wao waone njaa; uwaache wauawe kwa makali ya upanga. Wake zao wasiwe na watoto, na wawe wajane; waume wao wauawe, nao vijana wao waume wachinjwe kwa upanga vitani.
22 Cry be herd of the housis of hem, for thou schalt bringe sudenli a theef on hem; for thei diggiden a pit to take me, and hidden snaris to my feet.
Kilio na kisikike kutoka kwenye nyumba zao ghafula uwaletapo adui dhidi yao, kwa kuwa wamechimba shimo ili kunikamata na wameitegea miguu yangu mitego.
23 But thou, Lord, knowist al the councel of hem ayens me in to deth; do thou not merci to the wickidnesse of hem, and the synne of hem be not doon awei fro thi face; be thei maad fallynge doun in thi siyt, in the tyme of thi stronge veniaunce; vse thou hem to othir thing than thei weren ordeyned.
Lakini unajua, Ee Bwana, hila zao zote za kuniua. Usiyasamehe makosa yao wala usifute dhambi zao mbele za macho yako. Wao na waangamizwe mbele zako; uwashughulikie wakati wa hasira yako.