< Isaiah 65 >
1 Thei souyten me, that axiden not bifore; thei that souyten not me, founden me. Y seide, Lo! Y, lo! Y, to hethene men that knewen not me, and that clepiden not mi name to help.
“Nilijifunua kwa watu wale ambao hawakuniulizia. Nimeonekana na watu wale ambao hawakunitafuta. Kwa taifa lile ambalo halikuliita Jina langu, nilisema, ‘Niko hapa, niko hapa.’
2 I stretchide forth myn hondis al dai to a puple vnbileueful, that goith in a weie not good, aftir her thouytis.
Mchana kutwa nimeinyoosha mikono yangu kwa watu wakaidi, wanaokwenda katika njia ambazo si nzuri, wafuatao mawazo yao wenyewe:
3 It is a puple that stirith me to wrathfulnesse, euere bifore my face; whiche offren in gardyns, and maken sacrifice on tiel stoonys;
taifa ambalo daima hunikasirisha machoni pangu, wakitoa dhabihu katika bustani na kufukiza uvumba juu ya madhabahu za matofali;
4 whiche dwellen in sepulcris, and slepen in the templis of idols; whiche eten swynes fleisch, and vnhooli iwisch is in the vessels of hem;
watu waketio katikati ya makaburi na kukesha mahali pa siri, walao nyama za nguruwe, nazo sufuria zao zina mchuzi wa nyama zilizo najisi,
5 whiche seien to an hethene man, Go thou awei fro me, neiy thou not to me, for thou art vncleene; these schulen be smoke in my stronge veniaunce, fier brennynge al dai.
wasemao, ‘Kaa mbali; usinikaribie, kwa maana mimi ni mtakatifu mno kwako!’ Watu wa aina hiyo ni moshi katika pua zangu, ni moto uwakao mchana kutwa.
6 Lo! it is writun bifore me; Y schal not be stille, but Y schal yelde, and Y schal quyte in to the bosum of hem youre wickidnessis,
“Tazama, jambo hili hubakia limeandikwa mbele zangu: sitanyamaza, bali nitalipiza kwa ukamilifu; nitalipiza mapajani mwao:
7 and the wickidnessis of youre fadris togidere, seith the Lord, whiche maden sacrifice on mounteyns, and diden schenschipe to me on litle hillis; and Y schal mete ayen the firste werk of hem in her bosum.
dhambi zenu na dhambi za baba zenu,” asema Bwana. “Kwa sababu walitoa dhabihu za kuteketezwa juu ya milima na kunichokoza mimi juu ya vilima, nitawapimia mapajani mwao malipo makamilifu kwa matendo yao ya zamani.”
8 The Lord seith thes thingis, As if a grape be foundun in a clustre, and it be seid, Distrie thou not it, for it is blessyng; so Y schal do for my seruantis, that Y leese not al.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama vile divai mpya ingali bado inapatikana katika kishada cha zabibu, nao watu husema, ‘Usikiharibu, kwa kuwa bado kuna kitu kizuri ndani yake,’ hivyo ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu; sitawaangamiza wote.
9 And Y schal lede out of Jacob seed, and of Juda a man hauynge in possessioun myn hooli hillis; and my chosun men schulen enherite it, and my seruauntis schulen dwelle there.
Nitawaleta wazao kutoka kwa Yakobo, na kutoka kwa Yuda wale watakaomiliki milima yangu, nao watu wangu wateule watairithi, nako huko wataishi watumishi wangu.
10 And the feeldi places schulen be into floodis of flockis, and the valei of Achar in to a restyng place of droues of neet, to my puple that souyten me.
Sharoni itakuwa malisho kwa ajili ya makundi ya kondoo, na Bonde la Akori mahali pa kupumzikia kwa makundi ya ngʼombe, kwa ajili ya watu wangu wanaonitafuta.
11 And Y schal noumbre you in swerd, that forsoken the Lord, that foryaten myn hooli hil, whiche setten a boord to fortune, and maken sacrifice theronne,
“Bali kwenu ninyi mnaomwacha Bwana na kuusahau mlima wangu mtakatifu, ninyi mnaoandaa meza kwa ajili ya Bahati, na kujaza mabakuli ya mvinyo uliochanganywa kwa ajili ya Ajali,
12 and alle ye schulen falle bi sleyng; for that that Y clepide, and ye answeriden not; Y spak, and ye herden not; and ye diden yuel bifor myn iyen, and ye chesiden tho thingis whiche Y nolde.
nitawaagiza mfe kwa upanga, nanyi nyote mtainama chini ili kuchinjwa; kwa kuwa niliwaita lakini hamkuitika, nilisema lakini hamkusikiliza. Mlitenda maovu machoni pangu, nanyi mkachagua mambo yale yanayonichukiza.”
13 For these thingis, the Lord God seith these thingis, Lo! my seruauntis schulen ete, and ye schulen haue hungur; lo! my seruauntis schulen drynke, and ye schulen be thirsti;
Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Watumishi wangu watakula, lakini ninyi mtaona njaa; watumishi wangu watakunywa lakini ninyi mtaona kiu; watumishi wangu watafurahi, lakini ninyi mtaona haya.
14 lo! my seruauntis schulen be glad, and ye schulen be aschamed; lo! my seruauntis schulen herie, for the ful ioie of herte, and ye schulen crie, for the sorewe of herte, and ye schulen yelle, for desolacioun of spirit.
Watumishi wangu wataimba kwa furaha ya mioyo yao, lakini ninyi mtalia kutokana na uchungu wa moyoni, na kupiga yowe kwa sababu ya uchungu wa roho zenu.
15 And ye schulen leeue youre name in to an ooth to my chosun men; and the Lord God schal sle thee, and he schal clepe hise seruauntis bi another name.
Mtaliacha jina lenu kuwa laana kwa watu wangu waliochaguliwa; Bwana Mwenyezi atawaua ninyi, lakini watumishi wake atawapa jina jingine.
16 In which he that is blessid on erthe, schal be blessid in God amen; and he that swerith in erthe, shal swere in God feithfuli; for the formere angwischis ben youun to foryetyng, and for tho ben hid fro youre iyen.
Yeye aombaye baraka katika nchi atafanya hivyo kwa Mungu wa kweli; yeye aapaye katika nchi ataapa kwa Mungu wa kweli. Kwa kuwa taabu za zamani zitasahaulika na kufichwa kutoka machoni pangu.
17 For lo! Y make newe heuenes and a newe erthe, and the formere thingis schulen not be in mynde, and schulen not stie on the herte.
“Tazama, nitaumba mbingu mpya na dunia mpya. Mambo ya zamani hayatakumbukwa, wala hayatakuja akilini.
18 But ye schulen haue ioie, and make ful out ioiyng til in to with outen ende, in these thingis whiche Y make; for lo! Y make Jerusalem ful out ioiynge, and the puple therof ioie.
Lakini furahini na kushangilia daima katika hivi nitakavyoumba, kwa kuwa nitaumba Yerusalemu uwe wa kupendeza, nao watu wake wawe furaha.
19 And Y schal make ful out ioiyng in Jerusalem, and Y schal haue ioie in my puple; and the vois of weping and the vois of cry schal no more be herd ther ynne.
Nami nitaifurahia Yerusalemu na kuwafurahia watu wangu; sauti ya maombolezo na ya kilio haitasikika humo tena.
20 A yong child of daies schal no more be there, and an eld man that fillith not hise daies; for whi a child of an hundrid yeer schal die, and a synnere of an hundrid yeer schal be cursid.
“Kamwe hatakuwepo tena ndani yake mtoto mchanga atakayeishi siku chache tu, au mzee ambaye hataishi akatimiza miaka yake. Yeye atakayekufa akiwa na umri wa miaka mia moja atahesabiwa kwamba ni kijana tu, yeye ambaye hatafika miaka mia moja, atahesabiwa kuwa amelaaniwa.
21 And thei schulen bilde housis, and schulen enhabite hem, and thei schulen plaunte vynes, and schulen ete the fruytis of tho.
Watajenga nyumba na kuishi ndani yake; watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.
22 Thei schulen not bilde housis, and an othir schal enhabite hem, thei schulen not plaunte, and an othir schal ete; for whi the daies of my puple schulen be after the daies of the tree, and the werkis of
Hawatajenga nyumba, nao watu wengine waishi ndani yake, au kupanda mazao na wengine wale. Kwa kuwa kama zilivyo siku za mti, ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, wateule wangu watafurahia kwa siku nyingi kazi za mikono yao.
23 her hondis schulen be elde to my chosun men. Thei schulen not trauele in veyn, nether thei schulen gendre in disturblyng; for it is the seed of hem that ben blessid of the Lord, and the cosyns of hem ben with hem.
Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa watoto ili wapatwe na majanga, kwa kuwa watakuwa taifa lililobarikiwa na Bwana, wao na wazao wao pamoja nao.
24 And it schal be, bifor that thei crien, Y schal here; yit while thei speken, Y schal here.
Kabla hawajaita, nitajibu, nao wakiwa katika kunena, nitasikia.
25 A wolf and a lomb schulen be fed togidere, and a lioun and an oxe schulen ete stree, and to a serpent dust schal be his breed; thei schulen not anoie, nether schulen sle, in al myn hooli hil, seith the Lord.
Mbwa mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja, naye simba atakula nyasi kama maksai, lakini mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka. Hawatadhuru wala kuharibu katika mlima wangu mtakatifu wote,” asema Bwana.