< Isaiah 58 >

1 Crye thou, ceesse thou not; as a trumpe enhaunse thi vois, and schewe thou to my puple her grete trespassis, and to the hous of Jacob her synnes.
“Piga kelele, usizuie. Paza sauti yako kama tarumbeta. Watangazieni watu wangu uasi wao, na kwa nyumba ya Yakobo dhambi zao.
2 For thei seken me fro dai in to dai, and thei wolen knowe my weies; as a folk, that hath do riytfulnesse, and that hath not forsake the doom of her God; thei preien me domes of riytfulnesse, and wolen neiy to God.
Kwa maana kila siku hunitafuta, wanaonekana kutaka kujua njia zangu, kana kwamba walikuwa taifa linalotenda lililo sawa, na ambalo halijaziacha amri za Mungu wake. Hutaka kwangu maamuzi ya haki, nao hutamani Mungu awakaribie.
3 Whi fastiden we, and thou biheldist not; we mekiden oure soulis, and thou knewist not? Lo! youre wille is foundun in the dai of youre fastyng, and ye axen alle youre dettouris.
Wao husema, ‘Mbona tumefunga, nawe hujaona? Mbona tumejinyenyekeza, nawe huangalii?’ “Lakini katika siku ya kufunga kwenu, mnafanya mnavyotaka na kuwadhulumu wafanyakazi wenu wote.
4 Lo! ye fasten to chidyngis and stryuyngis, and smyten with the fist wickidli. Nyl ye fast, as `til to this dai, that youre cry be herd an hiy.
Kufunga kwenu huishia kwenye magomvi na mapigano, na kupigana ninyi kwa ninyi kwa ngumi za uovu. Hamwezi kufunga kama mnavyofanya leo na kutazamia sauti zenu kusikiwa huko juu.
5 Whether sich is the fastyng which Y chees, a man to turmente his soule bi dai? whether to bynde his heed as a sercle, and to make redi a sak and aische? Whethir thou schalt clepe this a fastyng, and a dai acceptable to the Lord?
Je, hii ndiyo aina ya mfungo niliouchagua, siku moja tu ya mtu kujinyenyekeza? Je, ni kwa kuinamisha kichwa chini kama tete, na kwa kujilaza juu ya nguo ya gunia na majivu? Je, huo ndio mnaouita mfungo, siku iliyokubalika kwa Bwana?
6 Whether not this is more the fastyng, which Y chees? Vnbynde thou the byndingis togidere of vnpitee, releesse thou birthuns pressynge doun; delyuere thou hem free, that ben brokun, and breke thou ech birthun.
“Je, hii si ndiyo aina ya mfungo niliyoichagua: kufungua minyororo ya udhalimu, na kufungua kamba za nira, kuwaweka huru walioonewa, na kuvunja kila nira?
7 Breke thi breed to an hungri man, and brynge in to thin hous nedi men and herborles; whanne thou seest a nakid man, hile thou hym, and dispise not thi fleisch.
Je, sio kushirikiana chakula chako na wenye njaa na kuwapatia maskini wasiokuwa na makao hifadhi, unapomwona aliye uchi, umvike, wala si kumkimbia mtu wa nyama na damu yako mwenyewe?
8 Thanne thi liyt schal breke out as the morewtid, and thin helthe schal rise ful soone; and thi riytfulnesse schal go bifore thi face, and the glorie of the Lord schal gadere thee.
Ndipo nuru yako itajitokeza kama mapambazuko na uponyaji wako utatokea upesi; ndipo haki yako itakapokutangulia mbele yako, na utukufu wa Bwana utakuwa mlinzi nyuma yako.
9 Thanne thou schalt clepe to help, and the Lord schal here; thou schalt crie, and he schal seie, Lo! Y am present, for Y am merciful, thi Lord God. If thou takist awei a chayne fro the myddis of thee, and ceessist to holde forth the fyngur, and to speke that profitith not;
Ndipo utaita, naye Bwana atajibu, utalia kuomba msaada, naye atasema: Mimi hapa. “Kama ukiiondoa nira ya udhalimu, na kunyoosha kidole na kuzungumza maovu,
10 whanne thou schedist out thi soule to an hungri man, and fillist a soule, `that is turmentid, thi liyt schal rise in derknessis, and thi derknessis schulen be as myddai.
nanyi kama mkimkunjulia mtu mwenye njaa nafsi zenu na kutosheleza mahitaji ya walioonewa, ndipo nuru yenu itakapongʼaa gizani, nao usiku wenu utakuwa kama adhuhuri.
11 And the Lord thi God schal yyue euere reste to thee, and schal fille thi soule with schynyngis, and schal delyuere thi boonys; and thou schalt be as a watri gardyn, and as a welle of watris, whose waters schulen not faile.
Bwana atakuongoza siku zote, atayatosheleza mahitaji yako katika nchi kame, naye ataitia nguvu mifupa yako. Utakuwa kama bustani iliyonyweshwa vizuri, kama chemchemi ambayo maji yake hayakauki kamwe.
12 And the forsakun thingis of worldis schulen be bildid in thee, and thou schalt reise the foundementis of generacioun and generacioun; and thou schalt be clepid a bildere of heggis, turnynge awei the pathis of wickidnessis.
Watu wako watajenga tena magofu ya zamani na kuinua misingi ya kale; utaitwa Mwenye Kukarabati Kuta Zilizobomoka, Mwenye Kurejeza Barabara za Makao.
13 If thou turnest awei thi foot fro the sabat, to do thi wille in myn hooli dai, and clepist the sabat delicat, and hooli, the gloriouse of the Lord, and glorifiest him, while thou doist not thi weies, and thi wille is not foundun, that thou speke a word;
“Kama ukitunza miguu yako isivunje Sabato, na kutokufanya kama vile upendavyo katika siku yangu takatifu, kama ukiita Sabato siku ya furaha na siku takatifu ya Bwana ya kuheshimiwa, kama utaiheshimu kwa kutoenenda katika njia zako mwenyewe, na kutokufanya yakupendezayo au kusema maneno ya upuzi,
14 thanne thou schalt delite on the Lord, and Y schal reise thee on the hiynesse of erthe, and Y schal fede thee with the eritage of Jacob, thi fadir; for whi the mouth of the Lord spak.
ndipo utakapojipatia furaha yako katika Bwana, nami nitakufanya upande juu ya miinuko ya nchi na kusherehekea urithi wa Yakobo baba yako.” Kinywa cha Bwana kimenena haya.

< Isaiah 58 >