< Isaiah 13 >

1 The birthun of Babiloyne, which birthun Ysaie, the sone of Amos, siy.
Neno kuhusu Babeli ambalo Isaya mwana wa Amozi aliliona:
2 Reise ye a signe on a myisti hil, and enhaunse ye vois; reise ye the hond, and duykis entre bi the yatis.
Twekeni bendera juu ya mlima usio na kitu, wapazieni sauti, wapungieni mkono waingie katika malango ya wenye heshima.
3 Y haue comaundid to myn halewid men, and Y clepid my stronge men in my wraththe, that maken ful out ioie in my glorie.
Nimewaamuru watakatifu wangu; nimewaita mashujaa wangu waitimize hasira yangu: wale wanaoshangilia ushindi wangu.
4 The vois of multitude in hillis, as of many puplis; the vois of sown of kyngis, of hethene men gaderit togidere. The Lord of oostis comaundide to the chyualry of batel,
Sikilizeni kelele juu ya milima, kama ile ya umati mkubwa wa watu! Sikilizeni, makelele katikati ya falme, kama mataifa yanayokusanyika pamoja! Bwana Mwenye Nguvu Zote anakusanya jeshi kwa ajili ya vita.
5 to men comynge fro a fer lond. The Lord cometh fro the hiynesse of heuene, and the vessels of his strong veniaunce, that he distrie al the lond.
Wanakuja kutoka nchi za mbali sana, kutoka miisho ya mbingu, Bwana na silaha za ghadhabu yake, kuangamiza nchi yote.
6 Yelle ye, for the dai of the Lord is niy; as wastyng it schal come of the Lord.
Ombolezeni, kwa maana siku ya Bwana i karibu, itakuja kama uharibifu kutoka kwa Mwenyezi.
7 For this thing alle hondis schulen be vnmyyti, and eche herte of man schal faile,
Kwa sababu ya hili, mikono yote italegea, moyo wa kila mtu utayeyuka.
8 and schal be al to-brokun. Gnawyngis and sorewis schulen holde Babiloyns; thei schulen haue sorewe, as they that trauelen of child. Ech man schal wondre at his neiybore; her cheris schulen be brent faces.
Hofu itawakamata, uchungu na maumivu makali yatawashika, watagaagaa kama mwanamke aliye na utungu wa kuzaa. Watatazamana kwa hofu kila mtu na mwenzake, nyuso zao zikiwaka kama moto.
9 Lo! the dai of the Lord schal come, cruel, and ful of indignacioun, and of wraththe, and of woodnesse; to sette the lond into wildirnesse, and to al to-breke the synneris therof fro that lond.
Tazameni, siku ya Bwana inakuja, siku katili, yenye ghadhabu na hasira kali, kuifanya nchi kuwa ukiwa na kuwaangamiza wenye dhambi waliomo ndani yake.
10 For whi the sterris of heuene and the schynyng of tho schulen not sprede abrood her liyt; the sunne is maade derk in his risyng, and the moone schal not schine in hir liyt.
Nyota za mbinguni na makundi ya nyota havitatoa mwanga wake. Jua linalochomoza litatiwa giza na mwezi hautatoa nuru yake.
11 And Y schal visite on the yuels of the world, and Y schal visite ayens wickid men the wickidnesse of hem; and Y schal make the pride of vnfeithful men for to reste, and Y schal make low the boost of stronge men.
Nitauadhibu ulimwengu kwa ajili ya uovu wake, waovu kwa ajili ya dhambi zao. Nitakomesha majivuno ya wenye kiburi, na nitakishusha kiburi cha watu wakatili.
12 A man of ful age schal be preciousere than gold, and a man schal be preciousere than pure gold and schynyng.
Nitawafanya wanadamu kuwa adimu kuliko dhahabu safi, watakuwa wachache sana kuliko dhahabu ya Ofiri.
13 On this thing I schal disturble heuene, and the erthe schal be moued fro his place; for the indignacioun of the Lord of oostis, and for the dai of wraththe of his strong veniaunce.
Kwa hiyo nitazifanya mbingu zitetemeke, nayo dunia itatikisika kutoka mahali pake katika ghadhabu ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika siku ya hasira yake iwakayo.
14 And it schal be as a doo fleynge, and as a scheep, and noon schal be that schal gadere togidere; ech man schal turne to his puple, and alle bi hem silf schulen fle to her lond.
Kama swala awindwaye, kama kondoo wasio na mchungaji, kila mmoja atarudi kwa watu wake mwenyewe, kila mmoja atakimbilia nchi yake ya kuzaliwa.
15 Ech man that is foundun, schal be slayn; and ech man that cometh aboue, schal falle doun bi swerd.
Yeyote atakayetekwa atapasuliwa tumbo, wote watakaokamatwa watauawa kwa upanga.
16 The yonge children of them schulen be hurtlid doun bifore the iyen of them; her housis schulen be rauischid, and her wyues schulen be defoulid.
Watoto wao wachanga watavunjwa vipande vipande mbele ya macho yao; nyumba zao zitatekwa na wake zao watatendwa jeuri.
17 Lo! Y schal reise on them Medeis, that seken not siluer, nethir wolen gold;
Tazama, nitawachochea Wamedi dhidi yao, ambao hawajali fedha wala hawafurahii dhahabu.
18 but thei shulen sle litle children bi arowis, and thei schulen not haue merci on wombis yyuynge mylk, and the iye of them schal not spare on sones.
Mishale yao itawaangusha vijana, hawatakuwa na huruma kwa watoto wachanga wala hawataangalia watoto kwa huruma.
19 And Babiloyne, thilke gloriouse citee in rewmes, noble in the pride of Caldeis, schal be destried, as God destried Sodom and Gomore.
Babeli, johari ya falme, utukufu wa kiburi cha Wababeli, itaangushwa na Mungu kama Sodoma na Gomora.
20 It shall not be enhabitid til in to the ende, and it schal not be foundid til to generacioun and generacioun; a man of Arabie schal not sette tentis there, and scheepherdis schulen not reste there.
Hautakaliwa na watu kamwe wala watu hawataishi humo kwa vizazi vyote. Hakuna Mwarabu atakayepiga hema lake huko, hakuna mchungaji atakayepumzisha makundi yake huko.
21 But wielde beestis schulen reste there, and the housis of hem schulen be fillid with dragouns; and ostrichis schulen dwelle there, and heeri beestis schulen skippe there.
Lakini viumbe wa jangwani watalala huko, mbweha watajaza nyumba zake, bundi wataishi humo nao mbuzi-mwitu watarukaruka humo.
22 And bitouris schulen answere there in the housis therof, and fliynge serpentis in the templis of lust.
Fisi watalia ndani ya ngome zake, mbweha ndani ya majumba yake ya kifahari. Wakati wake umewadia, na siku zake hazitaongezwa.

< Isaiah 13 >