< Hosea 7 >

1 Whanne Y wolde heele Israel, the wickidnesse of Effraym was schewid, and the malice of Samarie was schewid, for thei wrouyten a leesyng. And a niyt theef entride, and robbid; a dai theef was withoutforth.
kila mara nilipotaka kumponya Israeli, dhambi za Efraimu zinafichuliwa na maovu ya Samaria yanafunuliwa. Wanafanya udanganyifu, wevi huvunja nyumba, maharamia hunyangʼanya barabarani,
2 And lest thei seien in her hertis, that Y haue mynde on al the malice of hem, now her fyndyngis han cumpassid hem, tho ben maad bifor my face.
lakini hawafahamu kwamba ninakumbuka matendo yao yote mabaya. Dhambi zao zimewameza, ziko mbele zangu siku zote.
3 In her malice thei gladiden the kyng, and in her leesyngys `thei gladiden the princes.
“Wanamfurahisha sana mfalme kwa maovu yao, wakuu wao kwa uongo wao.
4 Alle that doen auoutrie, ben as an ouene maad hoot of a bakere. The citee restide a litil fro the medlyng of sour douy, til al was maad sour `of sour douy.
Wote ni wazinzi, wanawaka kama tanuru ambayo moto wake mwokaji hana haja ya kuuchochea kuanzia kukanda unga hadi umekwisha kuumuka.
5 The dai of oure kyng; the princis bigunnen to be wood of wyn; he stretchide forth his hoond with scorneris.
Katika sikukuu ya mfalme wetu wakuu wanawaka kwa mvinyo, naye anawaunga mkono wenye mizaha.
6 For thei applieden her herte as an ouene, whanne he settide tresoun to hem. Al the niyt he slepte bakynge hem, in the morewtid he was maad hoot, as the fier of flawme.
Mioyo yao ni kama tanuru, wanamwendea kwa hila. Hasira yao inafoka moshi usiku kucha, wakati wa asubuhi inalipuka kama miali ya moto.
7 Alle weren maad hoot as an ouene, and thei deuouriden her iugis. Alle the kyngis of hem fellen doun, and noon is among hem that crieth to me.
Wote ni moto kama tanuru; wanawaangamiza watawala wao. Wafalme wake wote wanaanguka, wala hakuna yeyote kati yao aniitaye mimi.
8 Effraym hym silf was medlid among puplis; Effraym was maad a loof bakun vndur aischis, which is not turned ayen.
“Efraimu anajichanganya na mataifa; Efraimu ni mkate ambao haukuiva.
9 Aliens eeten the strengthe of hym, and he knew not; but also hoor heeris weren sched out in hym, and he knew not.
Wageni wananyonya nguvu zake, lakini hafahamu hilo. Nywele zake zina mvi hapa na pale, lakini hana habari.
10 And the pride of Israel schal be maad low in the face therof; thei turneden not ayen to her Lord God, and thei souyten not hym in alle these thingis.
Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yake, lakini pamoja na haya yote harudi kwa Bwana Mungu wake wala kumtafuta.
11 And Effraym was maad as a culuer disseyued, not hauynge herte. Thei clepiden Egipt to help, thei yeden to Assiriens.
“Efraimu ni kama hua, hudanganywa kwa urahisi na hana akili: mara anaita Misri, mara anageukia Ashuru.
12 And whanne thei ben goen forth, Y schal sprede abrood on hem my net, Y schal drawe hem doun as a brid of the eir. Y schal beete hem, bi the heryng of the cumpany of hem.
Wakati watakapokwenda, nitatupa wavu wangu juu yao; nitawavuta chini waanguke kama ndege wa angani. Nitakaposikia wakikusanyika pamoja, nitawanasa.
13 Wo to hem, for thei yeden awei fro me; thei schulen be distried, for thei trespassiden ayens me. And Y ayenbouyte hem, and thei spaken leesyngis ayenus me.
Ole wao, kwa sababu wamepotoka kutoka kwangu! Maangamizi ni yao kwa sababu wameniasi! Ninatamani kuwakomboa, lakini wanasema uongo dhidi yangu.
14 And thei crieden not to me in her herte, but yelliden in her beddis. Thei chewiden code on wheete, and wyn, and thei yeden awei fro me.
Hawanililii mimi kutoka mioyoni mwao, bali wanaomboleza vitandani mwao. Hukusanyika pamoja kwa ajili ya nafaka na divai mpya, lakini hugeukia mbali nami.
15 And Y tauyte, and coumfortide the armes of hem, and thei thouyten malice ayens me.
Niliwafundisha na kuwatia nguvu, lakini wanapanga mabaya dhidi yangu.
16 Thei turneden ayen, that thei schulden be with out yok; thei ben maad as a gileful bowe. The princis of hem schulen falle doun bi swerd, for the woodnesse of her tunge; this is the scornyng of hem in the lond of Egipt.
Hawamgeukii Yeye Aliye Juu Sana, wako kama upinde wenye kasoro. Viongozi wao wataanguka kwa upanga kwa sababu ya maneno yao ya jeuri. Kwa ajili ya hili watadhihakiwa katika nchi ya Misri.

< Hosea 7 >