< Hosea 6 >

1 In her tribulacioun thei schulen rise eerli to me. Come ye, and turne we ayen to the Lord;
“Njooni, tumrudie Bwana. Ameturarua vipande vipande lakini atatuponya; ametujeruhi lakini atatufunga majeraha yetu.
2 for he took, and schal heele vs; he schal smyte, and schal make vs hool.
Baada ya siku mbili atatufufua; katika siku ya tatu atatuinua, ili tuweze kuishi mbele zake.
3 He schal quykene vs after twei daies, and in the thridde dai he schal reise vs, and we schulen lyue in his siyt. We schulen wite, and sue, that we knowe the Lord. His goyng out is maad redi at the morewtid, and he schal come as a reyn to vs, which is timeful and lateful to the erthe.
Tumkubali Bwana, tukaze kumkubali yeye. Kutokea kwake ni hakika kama vile kuchomoza kwa jua; atatujia kama mvua za masika, kama vile mvua za vuli ziinyweshavyo nchi.”
4 Effraym, what schal Y do to thee? Juda, what schal Y do to thee? Youre merci is as a cloude of the morewtid, and as deew passynge forth eerli.
“Nifanye nini nawe, Efraimu? Nifanye nini nawe, Yuda? Upendo wako ni kama ukungu wa asubuhi, kama umande wa alfajiri utowekao.
5 For this thing Y hewide in profetis, Y killide hem in the wordis of my mouth;
Kwa hiyo ninawakata ninyi vipande vipande kwa kutumia manabii wangu; nimewaua ninyi kwa maneno ya kinywa changu, hukumu zangu zinawaka kama umeme juu yenu.
6 and thi domes schulen go out as liyt. For Y wolde merci, and not sacrifice, and Y wolde the kunnyng of God, more than brent sacrificis.
Kwa maana nataka rehema, wala si dhabihu, kumkubali Mungu zaidi kuliko sadaka za kuteketezwa.
7 But thei as Adam braken the couenaunt; there thei trespassiden ayens me.
Wamevunja Agano kama Adamu: huko hawakuwa waaminifu kwangu.
8 Galaad the citee of hem that worchen idol, is supplauntid with blood; and
Gileadi ni mji wenye watu waovu, umetiwa madoa kwa nyayo za damu.
9 as the chekis of men `that ben theues. Partener of prestis sleynge in the weie men goynge fro Sichem, for thei wrouyten greet trespasse.
Kama wanyangʼanyi wamviziavyo mtu, ndivyo magenge ya makuhani wafanyavyo; wanaulia watu kwenye njia iendayo Shekemu, wakifanya uhalifu wa aibu.
10 In the hous of Israel Y siy an orible thing; there the fornicaciouns of Effraym.
Nimeona jambo la kutisha katika nyumba ya Israeli. Huko Efraimu amejitolea kwa ukahaba na Israeli amenajisika.
11 Israel is defoulid; but also thou, Juda, sette heruest to thee, whanne Y schal turne the caitiftee of my puple.
“Pia kwa ajili yako, Yuda, mavuno yameamriwa. “Wakati wowote ningerejesha neema ya watu wangu,

< Hosea 6 >