< Hebrews 1 >

1 God, that spak sum tyme bi prophetis in many maneres to oure fadris, at the
Zamani Mungu alisema na baba zetu kwa njia ya manabii mara nyingi na kwa njia mbalimbali,
2 laste in these daies he hath spoke to vs bi the sone; whom he hath ordeyned eir of alle thingis, and bi whom he made the worldis. (aiōn g165)
lakini katika siku hizi za mwisho anasema nasi kwa njia ya Mwanawe, ambaye amemweka kuwa mrithi wa vitu vyote, na ambaye kupitia kwake aliuumba ulimwengu. (aiōn g165)
3 Which whanne also he is the briytnesse of glorie, and figure of his substaunce, and berith alle thingis bi word of his vertu, he makith purgacioun of synnes, and syttith on the riythalf of the maieste in heuenes;
Mwana ni mngʼao wa utukufu wa Mungu na mfano halisi wa nafsi yake, akivihifadhi vitu vyote kwa neno lake lenye uweza. Akiisha kufanya utakaso kwa ajili ya dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Aliye Mkuu huko mbinguni.
4 and so myche is maad betere than aungels, bi hou myche he hath eneritid a more dyuerse name bifor hem.
Kwa hiyo alifanyika bora kuliko malaika, kama jina alilorithi lilivyo bora kuliko lao.
5 For to whiche of the aungels seide God ony tyme, Thou art my sone, Y haue gendrid thee to dai? And eftsoone, Y schal be to hym in to a fadir, and he schal be to me in to a sone?
Kwa maana ni malaika yupi ambaye wakati wowote Mungu alipata kumwambia, “Wewe ni Mwanangu; leo mimi nimekuzaa?” Au tena, “Mimi nitakuwa Baba yake, naye atakuwa Mwanangu?”
6 And whanne eftsoone he bryngith in the firste bigetun sone in to the world, he seith, And alle the aungels of God worschipe hym.
Tena, Mungu amletapo mzaliwa wake wa kwanza ulimwenguni, anasema, “Malaika wote wa Mungu na wamsujudu.”
7 But he seith to aungels, He that makith hise aungels spiritis, and hise mynystris flawme of fier.
Anenapo kuhusu malaika asema, “Huwafanya malaika wake kuwa pepo, watumishi wake kuwa miali ya moto.”
8 But to the sone he seith, God, thi trone is in to the world of world; a yerde of equite is the yerde of thi rewme; (aiōn g165)
Lakini kwa habari za Mwana asema, “Kiti chako cha enzi, Ee Mungu, kitadumu milele na milele, nayo haki itakuwa fimbo ya utawala ya ufalme wako. (aiōn g165)
9 thou hast louyd riytwisnesse, and hatidist wickidnesse; therfor the God, thi God, anoyntide thee with oile of ioye, more than thi felowis.
Umependa haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako kwa kukupaka mafuta ya furaha.”
10 And, Thou, Lord, in the bigynnyng foundidist the erthe, and heuenes ben werkis of thin hondis; thei schulen perische,
Pia asema, “Hapo mwanzo, Ee Bwana, uliweka misingi ya dunia, nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.
11 but thou schalt perfitli dwelle; and alle schulen wexe elde as a cloth, and thou schalt chaunge hem as a cloth,
Hizo zitatoweka, lakini wewe utadumu; zote zitachakaa kama vazi.
12 and thei schulen be chaungid. But thou art the same thi silf, and thi yeeris schulen not faile.
Utazikungʼutakungʼuta kama joho, nazo zitachakaa kama vazi. Lakini wewe hubadiliki, nayo miaka yako haikomi kamwe.”
13 But to whiche of the aungels seide God at ony tyme, Sitte thou on my riythalf, till Y putte thin enemyes a stool of thi feet?
Je, ni kwa malaika yupi ambaye Mungu amepata kumwambia wakati wowote, “Keti mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako”?
14 Whether thei alle ben not seruynge spiritis, sente to seruen for hem that taken the eritage of heelthe?
Je, malaika wote si roho watumikao, waliotumwa kuwahudumia wale watakaourithi wokovu?

< Hebrews 1 >