< Genesis 6 >

1 And whanne men bigunnen to be multiplied on erthe, and hadden gendrid douytris,
Ikawa wakati watu walipoanza kuongezeka juu ya uso wa nchi na wana wa kike wakazaliwa kwao,
2 the sones of God seiyen the douytris of men that thei weren faire, and token wyues to hem of alle whiche thei hadden chose.
wana wa Mungu walipoona kuwa mabinti wa wanadamu ni wenye kuvutia. waliwachukua kuwa wake zao, kila waliye mchagua.
3 And God seide, My spirit schal not dwelle in man with outen ende, for he is fleisch; and the daies of hym schulen be an hundrid and twenti yeer.
Yahwe akaema, “roho yangu haitasalia kwa mwanadamu milele, kwa kuwa wao ni nyama. Wataishi miaka 120.”
4 Sotheli giauntis weren on erthe in tho daies, forsothe aftir that the sones of God entriden to the douytris of men, and tho douytris gendriden; these weren myyti of the world and famouse men.
Majitu makubwa yalikuwa juu ya uso wa nchi nyakati hizo, na hata baada ya hapo. Hii ilitokea wakati wana wa Mungu walipowaoa binti za wanadamu, na kupata watoto pamoja nao. Hawa walikuwa watu hodari zamani, watu wenye sifa.
5 Sotheli God seiy that myche malice of men was in erthe, and that al the thouyt of herte was ententif to yuel in al tyme,
Yahwe akaona kwamba uovu wa watu umezidi katika nchi, na kwamba mawazo ya mioyo yao daima inaelekea tu katika uovu.
6 and repentide him that he hadde maad man in erthe; and God was war bifore ayens tyme to comyng, and was touchid with sorewe of herte with ynne;
Yahwe akajuta kuwa amemuumba mwanadamu juu ya nchi, na ikamuhuzunisha moyo wake.
7 and seide, Y schal do awei man, whom Y made of nouyt, fro the face of the erthe, fro man til to lyuynge thingis, fro crepynge beeste til to the briddis of heuene; for it repentith me that Y made hem.
Kwa hiyo Yahwe akasema, “Nitamfutilia mbali mwanadamu ambaye nimemuumba katika uso wa nchi; mwanadamu na wanyama wakubwa, na vitambaavyo na ndege wa angani, kwa kuwa nimehuzunika kuwa nimeviumba.”
8 Forsothe Noe foond grace bifore the Lord.
Lakini Nuhu akapata neema ya upendeleo machoni pa Yahwe.
9 These ben the generaciouns of Noe. Noe was a iust man and perfit in hise generaciouns; Noe yede with God,
Kulikuwa na matukio kumuhusu Nuhu. Nuhu alikuwa mtu mwenye haki, na asiye na lawama miongoni mwa watu wa kipindi chake. Nuhu alitembea na Mungu.
10 and gendride thre sones, Sem, Cam, and Jafeth.
Nuhu akafanyika baba wa wana watatu wa kiume: Shem, Ham na Yafeti.
11 Forsothe the erthe was corrupt bifore God, and was fillid with wickidnes.
Nchi iliharibika mbele za Mungu, na ikajaa ghasia.
12 And whanne God seiy, that the erthe was corrupt, for ech fleisch ether man hadde corrupt his weie on erthe,
Mungu akaiona nchi; tazama, ilikuwa imeharibika, kwa kuwa wote wenye mwili walikuwa wameharibu njia zao juu ya nchi.
13 he seide to Noe, The ende of al fleisch is comen bifore me; the erthe is fillid with wickidnesse of the face of hem, and Y schal distrye hem with the erthe.
Mungu akamwambia Nuhu, “Nimeona kuwa sasa niwakati wa mwisho kwa wote wenye mwili, kwa kuwa inchi imejaa ghasia kutokana na wao. Hakika, nitawaharibu wao pamoja na nchi.
14 Make thou to thee a schip of trees hewun and planed; thou schalt make dwellynge placis in the schip, and thou schalt anoynte it with pitche with ynne and with outforth.
Tengeneza safina ya mti wa mvinje kwa ajili yako. Tengeneza vyumba katika safina, na vifunike kwa lami ndani na nje.
15 And so thou schalt make it. The lengthe of the schip schal be of thre hundrid cubitis, the brede schal be of fifti cubitis, and the hiynesse therof schal be of thretti cubitis.
Hivi ndivyo utakavyofanya: urefu wa safina dhiraa miatatu, upana wake dhiraa hamsini, kwenda juu kwake dhiraa thelathini.
16 Thou schalt make a wyndow in the schip, and thou schalt ende the hiynesse therof in a cubite; sotheli thou schalt sette the dore of the schip in the side binethe; thou shalt make soleris and placis of thre chaumbris in the schip.
Tengeneza paa la safina, na ulimalize kwa kipimo cha dhiraa kutoka juu ubavuni. Weka mlango katika ubavu wa safina na utengeneze dari ya chini, ya pili na ya tatu.
17 Lo! Y schal brynge `watris of diluuye ether greet flood on erthe, and Y schal sle ech fleisch in which is the spirit of lijf vndir heuene, and alle thingis that ben in erthe, schulen be wastid.
Sikiliza, nimekaribia kuleta gharika ya maji juu ya nchi, kuharibu wenye mwili wote wakaao ndani ya nchi wenye pumzi ya uhai chini ya mbingu. Kila kitu kilichopo juu ya nchi kitakufa.
18 And Y schal sette my couenaunt of pees with thee; and thou schalt entre in to the schip, and thy sones, and thi wijf, and the wiues of thi sones schulen entre with thee.
Lakini nitalifanya thabiti agano langu na wewe. Utaingia ndani ya safina, wewe, na wana wako wa kiume, na mke wako, pamoja na wake za wanao.
19 And of alle lyuynge beestis of al fleisch thou schalt brynge in to the schip tweyne and tweyne, of male kynde and female, that thei lyue with thee;
Kwa kila kiumbe hai chenye mwili, viwili vya kila aina utavileta ndani ya safina, ili visalie hai pamoja nawe, vya kike na vya kiume.
20 of briddis bi her kynde, and of werk beestis in her kynde, and of ech crepynge beeste of erthe, by her kynde; tweyne and tweyne of alle schulen entre with thee, that thei moun lyue.
Katika ndege kwa jinsi yake, na wanyama wakubwa kwa jinsi yake, kila kitambaacho ardhini kwa jinsi yake, viwili viwili vya kila aina vitakuja kwako ili viwe salama.
21 Therfore thou schalt take with thee of alle metis that moun be etun, and thou schalt bere to gidre at thee, and tho schulen be as well to thee as to the beestis in to mete.
Kusanya kila aina ya chakula kinacholiwa kwa ajili yako na ukitunze, ili kwamba viwe chakula chako na chao.”
22 Therfor Noe dide alle thingis whiche God comaundide to hym.
Kwa hiyo Nuhu akafanya hivi. kulingana na yote ambayo Mungu alimuagiza, ndivyo alifanya.

< Genesis 6 >

The World is Destroyed by Water
The World is Destroyed by Water