< Genesis 5 >

1 This is the book of generacioun of Adam, in the dai wher ynne God made man of nouyt. God made man to the ymage and licnesse of God;
Hii ni orodha ya vizazi vya Adamu. Katika siku ambayo Mungu alimuumba mtu, aliwaumba katika mfano wake mwenyewe.
2 God formede hem male and female, and blesside hem, and clepide the name of hem Adam, in the day in which thei weren formed.
Mwanaume na mwanamke aliwaumba. Akawabariki na akawaita Adam wakati walipoumbwa.
3 Forsothe Adam lyuede an hundrid yeer and thretti, and gendride a sone to his ymage and liknesse, and clepide his name Seth.
Wakati Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, akamzaa mwana katika sura yake mwenyewe, kwa mfano wake, na akamuita jina lake Sethi.
4 And the daies of Adam after that he gendride Seth weren maad eiyte hundrid yeer, and he gendride sones and douytris.
Baada ya Adamu kumzaa Sethi, aliishi miaka mia nane. Akawazaa wana wengi waume na wake.
5 And al the tyme in which Adam lyuede was maad nyne hundrid yeer and thretti, and he was deed.
Adamu akaishi miaka 930 kisha akafariki.
6 Also Seth lyuede an hundrid and fyue yeer, and gendride Enos.
Wakati Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
7 And Seth lyuede aftir that he gendride Enos eiyte hundrid and seuen yeer, and gendride sones and douytris.
Baada ya kumzaa Enoshi, akaishi miaka 807 na akawazaa wana wengi waume na wake.
8 And alle the daies of Seth weren maad nyne hundrid and twelue yeer, and he was deed.
Sethi akaishi miaka 912 kisha akafariki.
9 Forsothe Enos lyuede nynti yeer, and gendride Caynan;
Wakati Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
10 aftir whos birthe Enos lyuede eiyte hundrid and fiftene yeer, and gendride sones and douytris.
Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
11 And alle the daies of Enos weren maad nyne hundrid and fyue yeer, and he was deed.
Enoshi aliishi miaka 905 na kisha akafariki.
12 Also Caynan lyuyde seuenti yeer, and gendride Malalehel.
Wakati Kanani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
13 And Caynan lyuede after that he gendride Malalehel eiyte hundrid and fourti yeer, and gendride sones and douytris.
Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
14 And alle the dayes of Caynan weren maad nyn hundrid and ten yeer, and he was deed.
Kenani aliishi miaka 910, na kisha akafariki.
15 Forsothe Malalehel lyuede sixti yeer and fyue, and gendride Jared.
Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, alimzaa Yaredi.
16 And Malalehel lyuede aftir that he gendride Jared eiyte hundrid and thretti yeer, and gendride sones and douytris.
Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
17 And alle the daies of Malalehel weren maad eiyte hundrid nynti and fyue yeer, and he was deed.
Mahalaleli aliishi miaka 895 na kisha akafariki.
18 And Jared lyuede an hundrid and two and sixti yeer, and gendride Enoth.
Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, alimzaa Henoko.
19 And Jared lyuede aftir that he gendride Enoth eiyte hundrid yeer, and gendride sones and douytris.
Baada ya kumzaa Henoko, Yaredi aliishi miaka mianane. Akazaa wana wengi waume na wake.
20 And alle the dayes of Jared weren maad nyn hundrid and twei and sexti yeer, and he was deed.
Yaredi aliishi miaka 962 na kisha akafariki.
21 Forsothe Enoth lyuede fyue and sixti yeer, and gendride Matusalem.
Henoko alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, akamzaa Methusela.
22 And Enoth yede with God; and Enoth lyuede after that he gendride Matusalem thre hundrid yeer, and gendride sones and douytris.
Henoko akaenenda na Mungu miaka miatatu baada ya kumzaa Methusela. Aliwazaa wana wengi wa ume na wake.
23 And alle the daies of Enoth weren maad thre hundride and fyue and sexti yeer.
Henoko aliishi miaka 365.
24 And Enoth yeed with God, and apperide not afterward, for God took hym awei.
Henoko alienenda na Mungu, na kisha alitoweka, kwa kuwa Mungu alimtwaa.
25 Also Matusalem lyuede an hundrid and `fourscoor yeer and seuene, and gendride Lameth.
Wakati Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, alimzaa Lameki.
26 And Matusalem lyuede after that he gendride Lameth seuene hundrid and `fourscoor yeer and twei, and gendride sones and douytris.
Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
27 And alle the daies of Matusale weren maad nyn hundrid and nyn and sixti yeer, and he was deed.
Methusela aliishi miaka 969. Kisha akafariki.
28 Forsothe Lameth lyuede an hundrid and `fourscoor yeer and two, and gendride a sone;
Wakati Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
29 and clepide his name Noe, and seide, This man schal comforte vs of the werkis and traueilis of oure hondis, in the loond which the Lord curside.
Akamuita jina lake Nuhu, akisema, “Huyu ndiye atatupatia pumziko kutoka katika kazi yetu na kutoka katika kazi ya taabu ya mikono yetu, ambayo lazima tuifanye kwa sababu ya ardhi ambayo Yahwe ameilaani.”
30 And Lameth lyuede after that he gendride Noe fyue hundrid `nynti and fyue yeer, and gendride sones and douytris.
Lameki aliishi miaka 595 baada ya kumzaa baba wa Nuhu. Akazaa wanawengi wa ume na wake.
31 And alle the daies of Lameth weren maad seuene hundrid `thre scoor and seuentene yeer, and he was deed.
Lameki aliishi miaka 777. Kisha akafariki.
32 Forsothe Noe whanne he was of fyue hundrid yeer gendride Sem, Cham, and Jafeth.
Baada ya Nuhu kuishi miaka miatano, akamzaa Shemu, Hamu, na Yafethi.

< Genesis 5 >