< Genesis 37 >
1 Forsothe Jacob dwellide in the lond of Canaan, in which his fadir was a pilgrym; and these weren the generaciouns of hym.
Yakobo akaishi Kanaani katika nchi ambayo baba yake alikuwa ameishi.
2 Joseph whanne he was of sixtene yeer, yit a child, kepte a flok with hise britheren, and was with the sones of Bala and Zelfa, wyues of his fadir; and he accuside his britheren at the fadir of `the worste synne.
Zifuatazo ni habari za Yakobo. Yosefu, kijana wa miaka kumi na saba, alikuwa akichunga makundi ya kondoo na mbuzi pamoja na ndugu zake wa mama wengine, yaani wana wa Bilha na wana wa Zilpa wake za baba yake, naye akawa akimletea baba yake taarifa mbaya kuhusu hao ndugu zake.
3 Forsothe Israel louyde Joseph ouer alle hise sones, for he hadde gendrid hym in eelde; and he made to Joseph a cote of many colours.
Basi, Israeli akampenda Yosefu kuliko yeyote miongoni mwa kaka zake, kwani ni mwanawe wa uzeeni, akamshonea joho lililorembwa vizuri sana.
4 Forsothe hise britheren sien that he was loued of the fader more than alle, and thei hatiden hym, and myyten not speke ony thing pesibli to hym.
Ndugu zake walipoona kwamba baba yao anampenda Yosefu kuliko yeyote mwingine miongoni mwao, walimchukia na hawakusema naye neno lolote jema.
5 And it bifelde that he telde to hise britheren a sweuene seyn, which cause was `the seed of more hatrede.
Yosefu akaota ndoto, naye alipowaeleza ndugu zake, wakamchukia zaidi.
6 And Joseph seide to his britheren, Here ye the sweuene which Y seiy,
Akawaambia, “Sikilizeni ndoto niliyoota:
7 Y gesside that we bounden to gidere handfuls, and that as myn handful roos, and stood, and that youre handfuls stoden aboute and worschipiden myn handful.
Tulikuwa tukifunga miganda ya nafaka shambani, ghafula mganda wangu ukasimama wima, wakati miganda yenu ikiuzunguka na kuuinamia.”
8 Hise britheren answerden, Whether thou shalt be oure kyng, ethir we shulen be maad suget to thi lordschip? Therfor this cause of sweuenys and wordis mynystride the nurschyng of enuye, and of hatrede.
Ndugu zake wakamwambia, “Wewe unakusudia kututawala? Hivi kweli wewe utatutawala sisi?” Wakaongeza kumchukia zaidi kwa sababu ya ndoto yake pamoja na yale aliyowaambia.
9 Also Joseph seiy another sweuene, which he telde to the britheren, and seide, Y seiy bi a sweuene that as the sunne, and moone, and enleuen sterris worschipiden me.
Kisha akaota ndoto nyingine, akawaambia ndugu zake akisema, “Sikilizeni, nimeota ndoto nyingine, wakati huu jua, mwezi na nyota kumi na moja zilikuwa zinanisujudia.”
10 And whanne he hadde teld this sweuene to his fadir, and britheren, his fadir blamyde him, and seide, What wole this sweuene to it silf which thou hast seyn? Whether Y and thi modir, and thi britheren, schulen worschipe thee on erthe?
Alipomwambia baba yake pamoja na ndugu zake, baba yake akamkemea akisema, “Ni ndoto gani hii uliyoota? Hivi kweli mama yako na mimi na ndugu zako tutakuja kukusujudia wewe hadi nchi?”
11 Therfor hise britheren hadden enuye to hym. Forsothe the fadir bihelde pryuely the thing,
Ndugu zake wakamwonea wivu, lakini baba yake akaliweka jambo hilo moyoni.
12 and whanne his britheren dwelliden in Sichem, aboute flockis of the fadir `to be kept,
Basi, ndugu zake walikuwa wamekwenda kuchunga makundi ya baba yao karibu na Shekemu,
13 Israel seide to Joseph, Thi britheren kepen scheep in Sichymys; come thou, Y schal sende thee to hem.
naye Israeli akamwambia Yosefu, “Kama ujuavyo, ndugu zako wanachunga makundi huko karibu na Shekemu. Njoo, nitakutuma kwao.” Yosefu akajibu, “Vema sana, niko tayari.”
14 And whanne Joseph answerde, Y am redi, Israel seide, Go thou, and se whether alle thingis ben esi anentis thi britheren, and scheep; and telle thou to me what is doon. He was sent fro the valey of Ebron, and cam into Sichem;
Kwa hiyo akamwambia, “Nenda uone kama mambo yote ni salama kwa ndugu zako na makundi, kisha uniletee habari.” Ndipo akamtuma Yosefu kutoka Bonde la Hebroni. Yosefu alipofika Shekemu,
15 and a man foond hym errynge in the feeld, and `the man axide, what he souyte.
mtu mmoja akamkuta akizungukazunguka mashambani na akamuuliza, “Unatafuta nini?”
16 And he answerde, Y seke my britheren, schewe thou to me where thei kepten flockis.
Akajibu, “Ninawatafuta ndugu zangu. Unaweza kuniambia wanachunga wapi makundi yao?”
17 And the man seide to hym, Thei yeden awei fro this place; forsothe Y herde hem seiynge, Go we into Dothaym. And Joseph yede aftir his britheren, and foond hem in Dothaym.
Yule mtu akajibu, “Wamehama hapa. Nilisikia wakisema, ‘Twende Dothani.’” Kwa hiyo Yosefu akawafuatilia ndugu zake na kuwakuta karibu na Dothani.
18 And whanne thei hadden seyn hym afer, bifor that he neiyede to hem,
Ndugu zake walipomwona akiwa mbali, kabla hajawafikia, wakapanga shauri baya la kumuua.
19 thei thouyten to sle hym, and spaken to gidere, Lo! the dremere cometh, come ye,
Wakaambiana, “Yule mwota ndoto anakuja!
20 sle we hym, and sende we into an eld sisterne, and we schulen seie, A wielde beeste ful wickid hath deuourid hym; and thanne it schal appere what hise dremes profiten to hym.
Njooni sasa, tumuue na kumtupa katika shimo mojawapo na tuseme kwamba mnyama mkali amemrarua. Kisha tutaona matokeo ya ndoto zake.”
21 Sotheli Ruben herde this, and enforside to delyuere hym fro her hondis,
Reubeni aliposikia jambo hili, akajaribu kumwokoa kutoka mikononi mwao akasema, “Tusiutoe uhai wake.
22 and seide, Sle we not the lijf of hym, nether schede we out his blood, but caste ye hym into an eeld cisterne, which is in the wildirnesse, and kepe ye youre hondis gilteles. Forsothe he seide this, willynge to delyuere hym fro her hondis, and to yelde to his fadir.
Tusimwage damu yoyote. Mtupeni katika shimo lililoko hapa jangwani, lakini msimguse.” Reubeni alisema hivyo ili amwokoe kutoka mikononi mwao, kisha amrudishe nyumbani kwa baba yake.
23 Therfor anoon as Joseph cam to hise britheren, thei dispuyliden hym of the coote, doun to the heele, and of many colours, and senten into the eeld cisterne,
Kwa hiyo Yosefu alipowafikia ndugu zake, walimvua lile joho lake, lile joho lililorembwa vizuri alilokuwa amevaa.
Kisha wakamchukua wakamtupa katika shimo. Wakati huo shimo lilikuwa tupu, halikuwa na maji ndani yake.
25 And thei saten `to ete breed; and thei sien that Ismaelitis weigoers camen fro Galaad, and that her camels baren swete smellynge spiceries, and `rosyn, and stacten, into Egipt.
Walipokaa ili wale chakula chao, wakainua macho wakaona msafara wa Waishmaeli ukija kutoka Gileadi. Ngamia wao walikuwa wamepakizwa mizigo ya vikolezo, uvumba na manemane, nao walikuwa njiani kuvipeleka Misri.
26 Therfor Judas seide to hise britheren, What schal it profite to vs, if we schulen sle oure brother, and schulen hide his blood?
Yuda akawaambia ndugu zake, “Tutafaidi nini ikiwa tutamuua ndugu yetu na kuificha damu yake?
27 It is betere that he be seeld to Ismalitis, and oure hondis be not defoulid, for he is oure brother and fleisch. The britheren assentiden to these wordis;
Njooni, tumuuze kwa hawa Waishmaeli. Tusimguse, kwa kuwa hata hivyo yeye ni ndugu yetu, nyama yetu na damu yetu wenyewe.” Ndugu zake wakakubali.
28 and whanne marchauntis of Madian passiden forth, thei drowen hym out of the cisterne, and seelden hym to Ismaelitis, for thriytti platis of siluer; whiche ledden hym in to Egipt.
Kwa hiyo wale wafanyabiashara Wamidiani walipofika pale, ndugu zake wakamtoa Yosefu kutoka kwenye lile shimo, na kumuuza kwa shekeli ishirini za fedha kwa wale Waishmaeli, ambao walimpeleka Misri.
29 And Ruben turnede ayen to the cisterne, and foond not the child;
Reubeni aliporudi kutazama kwenye lile shimo na kuona kwamba Yosefu hayupo, alirarua nguo zake.
30 and he to-rente his closis, and he yede to hise britheren, and seide, The child apperith not, and whidir schal Y go?
Akawarudia ndugu zake na kusema, “Kijana hayuko mle! Nielekee wapi sasa?”
31 Forsothe thei token his coote, and dippiden in the blood of a kide, which thei hadden slayn; and senten men that baren to the fadir,
Kisha wakalichukua lile joho la Yosefu, wakachinja mbuzi na kulichovya katika damu.
32 and seiden, We han founde this coote, se, whether it is the coote of thi sone, ether nai.
Wakalichukua lile joho lililorembwa vizuri na kulipeleka kwa baba yao na kusema, “Tumeliokota hili joho. Uchunguze uone kama ni la mwanao.”
33 And whanne the fader hadde knowe it, he seide, It is the coote of my sone, a wielde beeste ful wickid hath ete hym, a beeste hath deuourid Joseph.
Baba yao akalitambua akasema, “Hili ni joho la mwanangu! Mnyama mkali amemrarua. Hakika Yosefu ameraruliwa vipande vipande.”
34 And he to-rente his clothis, and he was clothid with an heire, and biweilide his sone in myche tyme.
Kisha Yakobo akararua nguo zake, akavaa nguo ya gunia na kumwombolezea mwanawe kwa siku nyingi.
35 Sothely whanne hise fre children weren gaderid to gidere, that thei schulden peese the sorewe of the fadir, he nolde take counfort, but seide, Y schal go doun in to helle, and schal biweile my sone. And the while Jacob contynude in wepyng, (Sheol )
Wanawe wote na binti zake wakaja kumfariji, lakini hakukubali kufarijiwa. Akasema, “Hapana, nitamwombolezea mwanangu mpaka nimfikie kaburini.” Kwa hiyo baba yake akaendelea kumlilia. (Sheol )
36 Madianytis seelden Joseph into Egipt to Putifar, chast `and onest seruaunt of Farao, maistir of the chyualrie.
Wakati ule ule, Wamidiani wakamuuza Yosefu huko Misri kwa Potifa, mmojawapo wa maafisa wa Farao, aliyekuwa mkuu wa ulinzi.