< Genesis 22 >
1 And aftir that these thingis weren don, God assaiede Abraham, and seide to hym, Abraham! Abraham! He answerde, Y am present.
Baadaye Mungu akamjaribu Abrahamu. Akamwambia, “Abrahamu!” Abrahamu akajibu, “Mimi hapa.”
2 God seide to him, Take thi `sone oon gendrid, whom thou louest, Ysaac; and go into the lond of visioun, and offre thou hym there in to brent sacrifice, on oon of the hillis whiche Y schal schewe to thee.
Kisha Mungu akamwambia, “Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, Isaki umpendaye, uende katika nchi ya Moria. Mtoe huko kama sadaka ya kuteketezwa juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia.”
3 Therfor Abraham roos bi niyt, and sadlide his asse, and ledde with hym twey yonge men, and Ysaac his sone; and whanne he hadde hewe trees in to brent sacrifice, he yede to the place which God hadde comaundid to him.
Abrahamu akaamka asubuhi na mapema siku iliyofuata, akamtayarisha punda wake. Akawachukua watumishi wake wawili pamoja na Isaki mwanawe. Baada ya kuchanja kuni za kutosha kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa, akaondoka kuelekea mahali Mungu alipokuwa amemwambia.
4 Forsothe in the thridde dai he reiside hise iyen, and seiy a place afer;
Siku ya tatu Abrahamu akainua macho, akapaona mahali pale kwa mbali.
5 and he seide to hise children, Abide ye here with the asse, Y and the child schulen go thidur; and aftir that we han worschipid, we schulen turne ayen to you.
Akawaambia watumishi wake, “Kaeni hapa pamoja na punda, wakati mimi na kijana tunakwenda kule. Tutakwenda kuabudu na kisha tutawarudia.”
6 And he took the trees of brent sacrifice, and puttide on Ysaac his sone; forsothe he bar fier, and a swerd in hise hondis. And whanne thei tweyne yeden togidere, Isaac seide to his fadir, My fadir!
Abrahamu akachukua kuni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, akamtwika Isaki mwanawe, yeye mwenyewe akachukua moto na kisu. Walipokuwa wakienda pamoja,
7 And he answerde, What wolt thou, sone? He seide, Lo! fier and trees, where is the beeste of brent sacrifice?
Isaki akanena akamwambia Abrahamu baba yake, “Baba yangu!” Abrahamu akaitika, “Mimi hapa, mwanangu.” Isaki akasema, “Moto na kuni zipo, Je, yuko wapi mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa?”
8 Abraham seide, My sone, God schal puruey to hym the beeste of brent sacrifice.
Abrahamu akajibu, “Mwanangu, Mungu mwenyewe atajipatia mwana-kondoo kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa.” Nao hawa wawili wakaendelea mbele pamoja.
9 Therfor thei yeden to gidere, and camen to the place whiche God hadde schewid to hym, in which place Abraham bildide an auter, and dresside trees a boue; and whanne he hadde bounde to gidere Ysaac, his sone, he puttide Ysaac in the auter, on the heep of trees.
Walipofika mahali pale alipokuwa ameambiwa na Mungu, Abrahamu akajenga madhabahu hapo, akaziweka kuni juu yake. Akamfunga Isaki mwanawe na akamlaza kwenye madhabahu, juu ya zile kuni.
10 And he helde forth his hond, and took the swerd to sacrifice his sone.
Kisha akanyoosha mkono wake na akachukua kisu ili amchinje mwanawe.
11 And lo! an aungel of the Lord criede fro heuene, and seide, Abraham! Abraham!
Lakini malaika wa Bwana akamwita kutoka mbinguni, akamwambia, “Abrahamu! Abrahamu!” Akajibu, “Mimi hapa.”
12 Which answerde, I am present. And the aungel seide to hym, Holde thou not forth thin honde on the child, nether do thou ony thing to him; now Y haue knowe that thou dredist God, and sparidist not thin oon gendrid sone for me.
Akamwambia, “Usimdhuru kijana, wala usimtendee jambo lolote. Sasa ninajua kwamba unamcha Mungu, kwa sababu hukunizuilia mwanao, mwana wako wa pekee.”
13 Abraham reiside hise iyen, and he seiy `bihynde his bak a ram cleuynge bi hornes among breris, which he took, and offride brent sacrifice for the sone.
Abrahamu akainua macho yake, akaona kondoo dume amenaswa pembe zake nyuma yake katika kichaka. Akaenda akamchukua huyo kondoo dume, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.
14 And he clepide the name of that place, The Lord seeth; wherfore it is seyd, til to dai, The Lord schal see in the hil.
Abrahamu akapaita mahali pale Yehova-Yire. Mpaka siku ya leo inasemekana, “Katika mlima wa Bwana itapatikana.”
15 Forsothe the aungel of the Lord clepide Abraham the secounde tyme fro heuene,
Basi malaika wa Bwana akamwita Abrahamu kutoka mbinguni mara ya pili,
16 and seide, The Lord seith, Y haue swore bi my silf, for thou hast do this thing, and hast not sparid thin oon gendrid for me,
akasema, “Ninaapa kwa nafsi yangu, asema Bwana, kwamba kwa sababu umefanya jambo hili na hukunizuilia mwanao, mwana wako wa pekee,
17 Y schal blesse thee, and Y schal multiplie thi seed as the sterris of heuene, and as grauel which is in the brynk of the see; thi seed schal gete the yatis of hise enemyes;
hakika nitakubariki, na nitauzidisha uzao wako kama nyota za angani na kama mchanga ulioko pwani. Wazao wako watamiliki miji ya adui zao,
18 and alle the folkis of erthe schulen be blessid in thi seed, for thou obeiedist to my vois.
na kupitia uzao wako mataifa yote duniani yatabarikiwa, kwa sababu umenitii.”
19 Abraham turnede ayen to hise children, and thei yeden to Bersabee to gidere, and he dwellide there.
Ndipo Abrahamu akawarudia watumishi wake, wakaondoka wakaenda wote pamoja mpaka Beer-Sheba. Abrahamu akaishi huko Beer-Sheba.
20 And so whanne these thingis weren don, it was teld to Abraham that also Melcha hadde bore sones to Nachor his brother;
Baada ya muda, Abrahamu akaambiwa, “Milka pia amepata watoto, amemzalia ndugu yako Nahori wana:
21 Hus the firste gendrid, and Buz his brothir, and Chamuhel the fadir of Sireis,
Usi mzaliwa wake wa kwanza, Buzi nduguye, Kemueli (baba wa Aramu),
22 and Cased, and Asan, and Feldas,
Kesedi, Hazo, Pildashi, Yidlafu na Bethueli.”
23 and Jedlaf, and Batuhel, of whom Rebecca was borun; Melcha childide these eiyte to Nachor brother of Abraham.
Bethueli akamzaa Rebeka. Milka alimzalia Nahori nduguye Abrahamu hao wana wanane.
24 Forsothe his concubyn, Roma bi name, childide Thabee, and Gaon, and Thaas, and Maacha.
Suria wake Nahori aliyeitwa Reuma pia alikuwa na wana: Teba, Gahamu, Tahashi na Maaka.