< Genesis 20 >
1 Abraham yede forth fro thennus in to the lond of the south, and dwellide bitwixe Cades and Sur, and was a pilgrym in Geraris;
Basi Abrahamu akaendelea mbele kutoka huko hadi nchi ya Negebu na akaishi kati ya Kadeshi na Shuri. Kwa muda mfupi alikaa Gerari kama mgeni,
2 and he seide of Sare, his wijf, Sche is my sistir. Therfor Abymalec, kyng of Gerare, sente, and took hir.
huko Abrahamu akasema kuhusu Sara mkewe, “Huyu ni dada yangu.” Kisha Abimeleki mfalme wa Gerari akatuma Sara aletwe, naye akamchukua.
3 Sotheli God cam to Abymalec bi a sweuene in the nyyt, and seide to hym, Lo! thou schalt die, for the wooman which thou hast take, for sche hath an hosebond.
Lakini Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto wakati wa usiku na kumwambia, “Wewe ni kama mfu kwa sababu ya huyu mwanamke uliyemchukua; yeye ni mke wa mtu.”
4 Forsothe Abymalech touchide not hir; and he seide, Lord, whether thou schalt sle folc vnkunnynge and iust?
Wakati huo Abimeleki alikuwa bado hajamsogelea, kwa hiyo akasema, “Je, Bwana utaliharibu taifa lisilo na hatia?
5 Whether he seide not to me, Sche is my sistir, and sche seide, He is my brother? In the symplenesse of myn herte, and in the clennesse of myn hondis Y dide this.
Hakusema kwangu, ‘Huyu ni dada yangu,’ naye Sara pia hakusema, ‘Huyu ni kaka yangu’? Nimefanya haya kwa dhamiri njema na mikono safi.”
6 And the Lord seide to hym, And Y woot that thou didist bi symple herte, and therfor Y kepte thee, lest thou didist synne ayens me, and I suffride not that thou touchidist hir;
Kisha Mungu akamwambia katika ndoto, “Ndiyo, najua ya kwamba umefanya haya kwa dhamiri safi, kwa hiyo nimekuzuia usinitende dhambi. Ndiyo sababu sikukuacha umguse.
7 now therfor yelde thou the wijf to hir hosebonde, for he is a profete; and he schal preye for thee, and thou schalt lyue; sotheli if thou nylte yelde, wite thou that thou schalt die bi deeth, thou and alle thingis that ben thine.
Sasa umrudishe huyo mke wa mtu, kwa maana ni nabii, naye atakuombea nawe utaishi. Lakini kama hutamrudisha, ujue kwa hakika kuwa wewe na watu wako wote mtakufa.”
8 And anoon Abynalech roos bi nyyt, and clepide alle his seruauntis, and spak alle these wordis in the eeris of hem; and alle men dredden greetli.
Kesho yake asubuhi na mapema Abimeleki akawaita maafisa wake wote, na baada ya kuwaambia yote yaliyotokea, waliogopa sana.
9 Sotheli Abymalec clepide also Abraham, and seide to hym, What hast thou do to vs? what synneden we ayens thee, for thou hast brouyt in on me and on my rewme a greuouse synne? thou hast do to vs whiche thingis thou ouytist not do.
Kisha Abimeleki akamwita Abrahamu na kumwambia, “Wewe umetufanyia nini? Nimekukosea nini hata ukaleta hatia kubwa namna hii juu yangu na ufalme wangu? Umenifanyia mambo ambayo hayakupasa kufanyika.”
10 And eft Abimalech axide, and seide, What thing seiyist thou, that thou woldist do this?
Abimeleki akamuuliza Abrahamu, “Ulikuwa na kusudi gani kufanya hivi?”
11 Abraham answerde, Y thouyte with me, and seide, in hap the drede of God is not in this place; and thei schulen sle me for my wijf;
Abrahamu akajibu, “Niliwaza kwamba, ‘Hakika hakuna hofu ya Mungu mahali hapa, nao wataniua kwa sababu ya mke wangu.’
12 in other maner forsothe and sche is my sister verili, the douyter of my fadir, and not the douyter of my moder; and Y weddide hir in to wijf;
Pamoja na hayo, ni kweli kwamba yeye ni dada yangu, binti wa baba yangu ingawa si mtoto wa mama yangu; basi akawa mke wangu.
13 sotheli aftir that God ladde me out of the hous of my fadir, Y seide to hir, Thou schalt do this mercy with me in ech place to which we schulen entre; thou schalt seie, that Y am thi brother.
Wakati Bwana aliponifanya nisafiri mbali na nyumbani mwa baba yangu, nilimwambia, ‘Hivi ndivyo utakavyoonyesha pendo lako kwangu: Kila mahali tutakapokwenda, kuhusu mimi sema, “Huyu ni kaka yangu.”’”
14 Therfore Abymelech took scheep, and oxun, and seruauntis, and handmaydenes, and yaf to Abraham; and he yeldide to him Sare, `his wijf, and seide, The lond is bifor you;
Kisha Abimeleki akatwaa kondoo na ngʼombe, na watumwa wa kiume na wa kike akampa Abrahamu, akamrudisha Sara kwa mumewe.
15 dwelle thou, where euere it plesith thee. Forsothe Abymelech seide to Sare, Lo!
Abimeleki akasema, “Nchi yangu iko mbele yako, ishi popote unapotaka.”
16 Y yaf a thousand platis of siluer to thi brother; this schal be to thee in to hiling of iyen to al men that ben with thee; and whider euere thou goist, haue thou mynde that thou art takun.
Akamwambia Sara, “Ninampa kaka yako shekeli elfu moja za fedha. Hii ni kufidia kosa lililofanyika dhidi yako mbele ya wote walio pamoja nawe; haki yako imethibitishwa kabisa.”
17 Sotheli for Abraham preiede, God curide Abymelech, and his wijf, and handmaydens, and thei childiden;
Kisha Abrahamu akamwomba Mungu, naye Mungu akamponya Abimeleki, mke wake, na watumwa wake wa kike kwamba waweze kupata watoto tena,
18 for God hadde closid ech wombe of the hows of Abymelech, for Sare, the wijf of Abraham.
kwa kuwa Bwana alikuwa ameyafunga matumbo ya wote katika nyumba ya Abimeleki kwa sababu ya Sara, mke wa Abrahamu.