< Galatians 1 >

1 Poul the apostle, not of men, ne bi man, but bi Jhesu Crist, and God the fadir,
Mimi ni Paulo mtume. Mimi sio mtume kutoka kwa wanadamu wala kupitia kwa mwanadamu, lakini kupitia kwa Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua kutoka kwa wafu.
2 that reiside hym fro deth, and alle the britheren that ben with me, to the chirchis of Galathie,
Pamoja na ndugu wote na mimi, ninayaandikia makanisa ya Galatia.
3 grace to you and pees of God the fadir, and of the Lord Jhesu Crist,
Neema iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo,
4 that yaf hym silf for oure synnes, to delyuere vs fro the present wickid world, bi the wille of God and of oure fadir, (aiōn g165)
aliyejitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu ili kwamba atukomboe na nyakati hizi za uovu, kutokana na mapenzi ya Mungu wetu na Baba. (aiōn g165)
5 to whom is worschip and glorie in to worldis of worldis. Amen. (aiōn g165)
Kwake uwe utukufu milele na milele. (aiōn g165)
6 I wondur, that so soone ye be thus moued fro hym that clepid you in to the grace of Crist, in to another euangelie; which is not anothir,
Ninashangaa kwamba mnageukia haraka kwenye injili nyingine. Ninashangaa kwamba mnageukia mbali kutoka kwake yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo.
7 but that ther ben summe that troublen you, and wolen mysturne the euangelie of Crist.
Hakuna injili nyingine, lakini kuna baadhi ya watu wanao wasababishieni nyinyi matatizo na kutaka kubadilisha injili ya Kristo.
8 But thouy we, or an aungel of heuene, prechide to you, bisidis that that we han prechid to you, be he acursid.
Lakini hata kama ni sisi au malaika kutoka mbinguni atatangaza kwenu injili tofauti na ile tuliyoitangaza kwenu, na alaaniwe.
9 As Y haue seid bifore, and now eftsoones Y seie, if ony preche to you bisidis that that ye han vndurfongun, be he cursid.
Kama tulivyo sema mwanzoni, na sasa nasema tena, “Kama kuna mtu atawatangazia kwenu injili tofauti na mliyoipokea, na alaaniwe.”
10 For now whether counsele Y men, or God? or whether Y seche to plese men? If Y pleside yit men, Y were not Cristis seruaunt.
Kwani sasa hivi ninatafuta uthibitisho wa watu au Mungu? Ninatafuta kuwafurahisha wanadamu? Kama ninaendelea kujaribu kuwafurahisha wanadamu, mimi sio mtumishi wa Kristo.
11 For, britheren, Y make knowun to you the euangelie, that was prechid of me, for it is not bi man;
Ndugu, ninataka ninyi mjue kwamba injili niliyoitangaza haitokani na wanadamu.
12 ne Y took it of man, ne lernyde, but bi reuelacioun of Jhesu Crist.
Sikuipokea kutoka kwa mtu, wala sikufundishwa. Badala yake, ilikuwa ni kwa ufunuo wa Yesu Kristo kwangu.
13 For ye han herd my conuersacioun sumtyme in the Jurie, and that Y pursuede passyngli the chirche of God, and fauyt ayen it.
Mmekwisha sikia juu ya maisha yangu ya nyuma katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyokuwa nikilitesa kwa ukali kanisa la Mungu zaidi ya kipimo na kuliteketeza.
14 And Y profitide in the Jurie aboue many of myn eueneldis in my kynrede, and was more aboundauntli a folewere of my fadris tradiciouns.
Nilikuwa nimeendelea katika Dini ya Kiyahudi zaidi ya ndugu zangu wengi Wayahudi. Nilikuwa na bidii sana katika tamaduni za baba zangu.
15 But whanne it pleside hym, that departide me fro my modir wombe,
Lakini Mungu alipendezwa kunichagua mimi kutoka tumboni mwa mama. Aliniita mimi kupitia neema yake
16 and clepide bi his grace, to schewe his sone in me, that Y schulde preche hym among the hethene, anoon Y drowy me not to fleisch and blood; ne Y cam to Jerusalem to the apostlis,
kumdhihirisha Mwanawe ndani yangu, ili kwamba nimtangaze yeye miongoni mwa watu wa mataifa. Wala sikutafuta ushauri wa mwili na damu
17 that weren tofor me, but Y wente in to Arabie, and eftsoones Y turnede ayen in to Damask.
na sikupanda kwenda Yerusalem kwa wale waliokuwa mitume kabla yangu. Badala yake nilienda Uarabuni na baadae kurudi Damesiki.
18 And sith thre yeer aftir Y cam to Jerusalem, to se Petre, and Y dwellide with hym fiftene daies;
Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kumtembelea Kefa, nikakaa naye kwa siku kumi na tano.
19 but Y sawy noon othere of the apostlis, but James, oure Lordis brother.
Lakini sikuona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndungu yake na Bwana.
20 And these thingis which Y write to you, lo! tofor God Y lie not.
Tazama, mbele za Mungu, sidanganyi kwa kile niandikacho kwenu.
21 Afterward Y cam in to the coostis of Syrie and Cilicie.
Kisha nilikwenda mikoa ya Shamu na Kilikia.
22 But Y was vnknowun bi face to the chirchis of Judee, that weren in Crist; and thei hadden oonli an heryng,
Sikuwa najulikana kwa macho kwa makanisa ya Uyahudi yale yaliyokuwa katika Kristo,
23 that he that pursuede vs sum tyme, prechide now the feith, ayens which he fauyte sum tyme;
lakini walikuwa wakisikia tu, “Yeye aliyekuwa akitutesa sasa anatangaza imani aliyokuwa akiiharibu.”
24 and in me thei glorifieden God.
Walikuwa wakimtukuza Mungu kwa ajili yangu.

< Galatians 1 >