< Ezra 4 >

1 Forsothe the enemyes of Juda and of Beniamyn herden, that the sones of caitifte bildiden a temple to the Lord God of Israel;
Adui za Yuda na Benyamini waliposikia kwamba watu waliorudi kutoka uhamishoni wanajenga Hekalu kwa ajili ya Bwana, Mungu wa Israeli,
2 and thei neiyeden to Zorobabel, and to the princes of fadris, and seiden to hem, Bilde we with you, for so as ye, we seken youre God; lo! we han offrid sacrificis fro the daies of Assoraddon, kyng of Assur, that brouyte vs hidur.
wakamjia Zerubabeli na viongozi wa jamaa, nao wakasema, “Turuhusuni tuwasaidie kujenga, kwa sababu sisi tunamtafuta Mungu wenu kama ninyi na tumekuwa tukimtolea dhabihu tangu wakati wa Esar-Hadoni mfalme wa Ashuru, aliyetuleta hapa.”
3 And Zorobabel, and Josue, and the othere princes of the fadris of Israel, seiden to hem, It is not to vs and to you, that we bilde an hows to oure God; but we vs silf aloone schulen bilde to `oure Lord God, as Cirus, the kyng of Persis, comaundide to vs.
Lakini Zerubabeli, Yeshua na viongozi wengine wa jamaa ya Israeli wakawajibu, “Ninyi hamna sehemu nasi katika kujenga Hekalu la Mungu wetu. Sisi peke yetu tutajenga Hekalu kwa ajili ya Bwana, Mungu wa Israeli, kama Mfalme Koreshi, mfalme wa Uajemi alivyotuagiza.”
4 Forsothe it was doon, that the puple of the lond lettide the hondis of the puple of Juda, and trobliden hem in bildyng.
Ndipo watu waliowazunguka wakajipanga kuwakatisha tamaa watu wa Yuda na kuwafanya waogope walipokuwa wakiendelea na ujenzi.
5 And thei hiriden counselouris ayens the Jewis, that thei schulden destrie the counseil of the Jewis, in alle the daies of Cirus, king of Persis, and `til to the rewme of Darius, king of Persis.
Wakaajiri washauri kuwapinga katika kazi yao, nao wakaipinga mipango yao wakati wote wa utawala wa Koreshi mfalme wa Uajemi hadi wakati wa utawala wa Dario mfalme wa Uajemi.
6 Forsothe in the rewme of Assueris, he is Artaxersis, in the bigynnyng of his rewme, thei writiden accusing ayens the dwellers of Juda and of Jerusalem;
Mnamo mwanzo wa utawala wa Ahasuero, hao adui waliandika mashtaka dhidi ya watu wa Yuda na Yerusalemu.
7 and in the daies of Artaxarses, Besellam wroot, Mytridates, and Thabel, and othere, that weren in the counsel of hem, to Artaxarses, kyng of Persis. For the pistle of accusyng was writun in langage of Sirie, and was red in word of Sirie.
Pia katika siku za utawala wa Artashasta mfalme wa Uajemi, Bishlamu, Mithredathi, Tabeeli pamoja na wenzao waliandika barua kwa Artashasta. Barua hiyo iliandikwa kwa mwandiko wa Kiaramu na katika lugha ya Kiaramu.
8 Reum, Beel, Theem, and Samsai, the scryuen, writen sich oon epistle fro Jerusalem to the kyng Artaxerses; Reum,
Rehumu afisa msimamizi na mwandishi Shimshai waliandika barua kwa Mfalme Artashasta dhidi ya watu wa Yerusalemu kama ifuatavyo:
9 Beel, Theem, and Samsai, the writere, and othere counselouris of hem, Dyney, Pharsathei, and Therphalei, Arphasei, Harthuei, men of Babiloyne, Susanne, Thanei, Dacei, men of Helam,
Rehumu afisa msimamizi na mwandishi Shimshai, pamoja na wenzao, yaani mahakimu na maafisa walio juu ya watu kuanzia Tripoli, Uajemi, Ereki na Babeli, Waelami wa Shushani,
10 and othere of hethene men, whiche the grete and gloriouse Asennaphar translatide, and made hem to dwelle in the citees of Samarie, and in othere cuntrees biyonde the flood, `in pees.
na watu wengine ambao mheshimiwa Asur-Banipali aliwahamisha na kuwakalisha katika mji wa Samaria na mahali pengine Ngʼambo ya Mto Frati.
11 This is the saumplere of the pistle, which thei senten to the kyng. `To Artaxerses, king, thi seruauntis, men `that ben biyende the flood, seyn helthe.
(Hii ndiyo nakala ya barua waliyompelekea.) Kwa Mfalme Artashasta, Kutoka kwa watumishi wako, watu wa Ngʼambo ya Mto Frati:
12 Be it knowun to the kyng, that the Jewis, that stieden fro thee, ben comun to vs `in to Jerusalem, the rebel and worste citee, which thei bilden, and thei maken the ground wallis therof, and arayen the wallis aboue.
Yapasa Mfalme ajue kuwa Wayahudi waliopanda kuja kwetu kutoka kwenu, wamekwenda Yerusalemu nao wanaujenga upya ule mji wa uasi na uovu. Wanajenga kuta upya na kukarabati misingi yake.
13 Nou therfor be it knowun to the kyng, that if thilke citee be bildid, and the wallis therof be restorid, thei schulen not yyue tribut, and tol, and annuel rentis, and this trespas schal come `til to the kyng.
Zaidi ya hayo, mfalme yampasa ajue kwamba kama mji huu ukijengwa na kuta zake zikafanywa upya, hakutakuwa na ulipaji wa kodi wala ada au ushuru, hivyo hazina za mfalme zitaathirika.
14 Therfor we ben myndeful of the salt, which we eeten in the paleis, and for we holden it vnleueful to se the harmes of the kyng, therfor we han sent and teld to the kyng;
Sisi sasa kwa kuwa tunawajibika kwa jumba la kifalme na kwamba siyo sawasawa kwetu kuona mfalme akidharauliwa, basi tunatuma ujumbe huu kumtaarifu mfalme,
15 that thou acounte in the bokis of stories of thi fadris, and thou schalt fynde writun in cronyclis, and thou schalt wite, that thilke citee is a rebel citee, and that it anoieth kyngis and prouynces, and batels ben reisid therynne of elde daies; wherfor also thilke citee was distried.
ili kwamba ufanyike uchunguzi kwenye kumbukumbu ya maandishi ya waliokutangulia. Katika kumbukumbu hizi utagundua kwamba mji huu ni wa maasi, unaowataabisha wafalme na majimbo, ni mahali pa maasi tangu zamani. Ndiyo maana mji huu uliharibiwa.
16 We tellen to the kyng, that if thilke citee be bildid, and the wallis therof be restorid, thou schalt not haue possessioun biyende the flood.
Tunamjulisha mfalme kwamba kama mji huu ukijengwa na kuta zake zikifanywa upya, hutabakiwa na chochote Ngʼambo ya Mto Frati.
17 The kyng sente word to Reum, Beel, Theem, and to Samsai, the scryuen, and to othere that weren in the counsel of hem, to the dwelleris of Samarie, and to othere biyendis the flood, and seide, Helthe and pees.
Mfalme alirudisha jibu hili: Kwa Rehumu, afisa msimamizi, mwandishi Shimshai na wenzenu wote wanaoishi katika Samaria na penginepo Ngʼambo ya Mto Frati: Salamu.
18 The accusyng, which ye senten to vs, was red opynli bifor me;
Barua mliyotutumia imesomwa na kutafsiriwa mbele yangu.
19 and it was comaundid of me, and thei rekenyden, and thei foundun, that thilke citee rebellith of elde daies ayens kyngis, and dissenciouns and batels ben reisid therynne;
Nilitoa amri na uchunguzi ukafanyika na imegundulika kwamba mji huu una historia ndefu ya maasi dhidi ya wafalme na pamekuwa mahali pa maasi na uchochezi.
20 for whi `and ful stronge kyngis weren in Jerusalem, which also weren lordis of al the cuntrei which is biyende the flood; also thei token tribut, and tol, and rentis.
Yerusalemu umepata kuwa na wafalme wenye nguvu wakitawala nchi yote iliyo Ngʼambo ya Mto Frati, wakitoza kodi, ada na ushuru huko.
21 Now therfor here ye the sentence, that ye forbede tho men, and that thilke citee be not bildid, til if perauenture it be comaundid of me.
Kwa hiyo toeni amri kwa watu hawa wasimamishe ujenzi, ili kwamba mji huu usiendelee kujengwa hadi nitakapoagiza.
22 Se ye, that this be not fillid necgligentli, and yuel encreesse litil `and litil ayens kyngis.
Mwe waangalifu msipuuze jambo hili. Kwa nini kuruhusu tishio hili kuendelea na kusababisha hasara kwa ufalme?
23 Therfor the saumple of the comaundement of kyng Artaxarses was red bifor Reum, Beel, Theem, and Samsai, the scryueyn, and her counseleris; and thei yeden hastili in to Jerusalem to the Jewis, and forbediden hem with arm and myyt.
Mara waliposomewa nakala ya barua ya Mfalme Artashasta, Rehumu na Shimshai aliyekuwa mwandishi na wenzao, walikwenda mara moja kwa Wayahudi huko Yerusalemu na kuwalazimisha kwa nguvu kusimamisha ujenzi.
24 Thanne the werk of Goddis hows in Jerusalem was left, and it was not maad til to the secounde yeer of Darius, king of Persis.
Hivyo kazi ya ujenzi wa nyumba ya Mungu huko Yerusalemu ikasimamishwa kabisa hadi mwaka wa pili wa utawala wa Dario mfalme wa Uajemi.

< Ezra 4 >