< Ezekiel 1 >

1 And it was don, in the thrittithe yeer, in the fourthe monethe, in the fyuethe dai of the moneth, whanne Y was in the myddis of caitifs, bisidis the flood Chobar, heuenes weren openyd, and Y siy the reuelaciouns of God.
Katika mwaka wa thelathini, mwezi wa nne, siku ya tano ya mwezi, wakati nilipokuwa miongoni mwa hao waliokuwa uhamishoni kando ya Mto Kebari, mbingu zilifunguka nami nikaona maono ya Mungu.
2 In the fyueth dai of the monethe; thilke is the fyuethe yeer of passing ouer of Joachym, kyng of Juda;
Katika siku ya tano ya mwezi, ilikuwa mwaka wa tano wa kuhamishwa kwa Mfalme Yehayakini,
3 the word of the Lord was maad to Ezechiel, preest, the sone of Busi, in the lond of Caldeis, bisidis the flood Chobar; and the hond of the Lord was maad there on hym.
neno la Bwana lilimjia Ezekieli kuhani, mwana wa Buzi, kando ya Mto Kebari, katika nchi ya Wakaldayo. Huko mkono wa Bwana ulikuwa juu yake.
4 And Y siy, and lo! a whirlewynd cam fro the north, and a greet cloude, and fier wlappynge in, and briytnesse in the cumpas therof; and as the licnesse of electre fro the myddis therof, that is, fro the myddis of the fier.
Nilitazama, nikaona dhoruba kubwa ikitoka kaskazini, wingu kubwa sana pamoja likiwa na umeme wa radi likiwa limezungukwa na mwanga mkali. Katikati ya huo moto kulikuwa kama rangi ya manjano ya chuma kinapokuwa ndani ya moto.
5 And of myddis therof was a licnesse of foure beestis. And this was the biholdyng of tho, the licnesse of a man in tho.
Katika ule moto kulikuwa na kitu kinachofanana na viumbe vinne vyenye uhai. Katika kuonekana kwake vilikuwa na umbo mfano wa mwanadamu,
6 And foure faces weren to oon, and foure wyngis weren to oon.
lakini kila kimoja kilikuwa na nyuso nne na mabawa manne.
7 And the feet of tho weren streiyt feet, and the soole of the foote of tho was as the soole of a foot of a calf, and sparclis, as the biholdynge of buylynge bras.
Miguu yao ilikuwa imenyooka, nyayo za miguu yao zilikuwa kama kwato za miguu ya ndama, nazo zilimetameta kama shaba iliyosuguliwa.
8 And the hondis of a man weren vndur the wyngis of tho, in foure partis. And tho hadden faces and wyngis bi foure partis;
Chini ya mabawa yao katika pande zao nne walikuwa na mikono ya mwanadamu. Wote wanne walikuwa na nyuso na mabawa,
9 and the wyngis of tho weren ioyned togidir of oon to another. Tho turneden not ayen, whanne tho yeden, but eche yede bifore his face.
nayo mabawa yao yaligusana. Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja, hawakugeuka walipokuwa wanatembea.
10 Forsothe the licnesse `of the face of tho was the face of a man and the face of a lioun at the riythalf of tho foure. Forsothe the face of an oxe was at the left half of tho foure; and the face of an egle was aboue tho foure.
Kuonekana kwa nyuso zao kulikuwa hivi: Kila mmoja wa wale wanne alikuwa na uso wa mwanadamu na kwa upande wa kulia kila mmoja alikuwa na uso wa simba, upande wa kushoto alikuwa na uso wa ngʼombe pia kila mmoja alikuwa na uso wa tai.
11 And the faces of tho and the wengis of tho weren stretchid forth aboue. Twei wyngis of eche weren ioyned togidere, and tweyne hiliden the bodies of tho.
Hivyo ndivyo zilivyokuwa nyuso zao. Mabawa yao yalikunjuliwa kuelekea juu, kila mmoja alikuwa na mabawa mawili ambayo kila moja liligusa bawa la mwenzake kila upande na mabawa mengine mawili yakifunika mwili wake.
12 And ech of tho yede bifore his face. Where the fersnesse of the wynd was, thidur tho yeden, and turneden not ayen, whanne tho yeden.
Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja. Popote roho alipotaka kwenda, ndipo walipokwenda pasipo kugeuka.
13 And the licnesse of the beestis, and the biholdyng of tho, was as of brennynge coolis of fier, and as the biholdyng of laumpis. This was the siyt rennynge aboute in the myddis of beestis, the schynyng of fier, and leit goynge out of the fier.
Kuonekana kwa vile viumbe hai katikati kulikuwa kama makaa ya mawe yanayowaka au kama mienge. Moto ule ulikuwa ukienda mbele na nyuma katikati ya vile viumbe, ulikuwa na mwangaza mkali na katikati ya ule moto kulitoka kimulimuli kama umeme wa radi.
14 And the beestis yeden, and turneden ayen at the licnesse of leit schynynge.
Vile viumbe vilipiga mbio kwenda na kurudi, kama vimulimuli vya umeme wa radi.
15 And whanne Y bihelde the beestis, o wheel, hauuynge foure faces, apperide on the erthe, bisidis the beestis.
Nilipokuwa nikitazama vile viumbe hai, niliona gurudumu moja juu ya ardhi kando ya kila kiumbe kikiwa na nyuso zake nne.
16 And the biholdyng of the wheelis and the werk of tho was as the siyt of the see; and o licnesse was of tho foure; and the biholdyng and the werkis of tho, as if a wheel be in the myddis of a wheel.
Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa hayo magurudumu na muundo wake: yalingʼaa kama zabarajadi, nayo yote manne yalifanana. Kila gurudumu lilikuwa na gurudumu jingine ndani yake.
17 Tho goynge yeden bi foure partis of tho, and turneden not ayen, whanne tho yeden.
Yalipokwenda yalielekea upande wowote wa pande nne walipoelekea wale viumbe, magurudumu hayakuzunguka wakati viumbe vile vilipokwenda.
18 Also stature, and hiynesse, and orible biholdyng was to the wheelis; and al the bodi was ful of iyen in the cumpas of tho foure.
Kingo zake zilikuwa ndefu kwenda juu na za kutisha, nazo zote nne zilijawa na macho pande zote.
19 And whanne the beestis yeden, the wheelis also yeden togidere bisidis tho. And whanne the beestis weren reisid fro the erthe, the wheelis also weren reisid togidere.
Vile viumbe hai vilipokwenda, magurudumu yaliyokuwa kando yao yalisogea na wakati hivyo viumbe hai vilipoinuka kutoka ardhini magurudumu nayo yaliinuka.
20 Whidur euere the spirit yede, whanne the spirit yede thedur, also the wheelis suynge it weren reisid togidere; for whi the spirit of lijf was in the wheelis.
Mahali popote roho alipokwenda wale viumbe nao walikwenda, nayo magurudumu yaliinuka pamoja navyo, kwa sababu roho ya vile viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
21 Tho yeden with the beestis goynge, and tho stoden with the beestis stondynge. And with the beestis reisid fro erthe, also the wheelis suynge tho beestis weren reisid togidere; for the spirit of lijf was in the wheelis.
Wakati viumbe vile viliposogea, nayo magurudumu yalisogea, viumbe viliposimama kimya, nayo pia yalisimama kimya, viumbe vilipoinuka juu ya nchi magurudumu yaliinuliwa pamoja navyo kwa kuwa roho ya hivyo viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
22 And the licnesse of the firmament was aboue the heed of the beestis, and as the biholdyng of orible cristal, and stretchid abrood on the heed of tho beestis aboue.
Juu ya vichwa vya hao viumbe hai palikuwa na kitu mfano wa eneo lililokuwa wazi, lililokuwa angavu kabisa na lenye kutisha.
23 Forsothe vndur the firmament the wyngis of tho beestis weren streiyt, of oon to anothir; ech beeste hilide his bodi with twei wyngis, and an other was hilid in lijk maner.
Chini ya hiyo nafasi mabawa yao yalitanda moja kuelekea jingine, kila mmoja alikuwa na mabawa mengine mawili yaliyofunika mwili wake.
24 And Y herde the sown of wyngis, as the sown of many watris, as the sown of hiy God. Whanne tho yeden, ther was as a sown of multitude, as the sown of oostis of batel; and whanne tho stoden, the wyngis of tho weren late doun.
Viumbe wale waliposogea nilisikia sauti ya mabawa yao, kama ngurumo ya maji yaendayo kasi, kama sauti ya Mwenyezi, kama makelele ya jeshi. Waliposimama kimya walishusha mabawa yao.
25 For whi whanne a vois was maad on the firmament, that was on the heed of tho, tho stoden, and leten doun her wyngis.
Ndipo ikaja sauti toka juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao, waliposimama mabawa yao yakiwa yameshushwa.
26 And on the firmament, that was aboue the heed of tho, was as the biholdyng of a saphire stoon, the licnesse of a trone; and on the licnesse of the trone was a licnesse, as the biholdyng of a man aboue.
Juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi. Na juu ya kile kiti cha enzi kulikuwa na umbo mfano wa mwanadamu.
27 And Y siy as a licnesse of electre, as the biholding of fier with ynne, bi the cumpas therof; fro the lendis of hym and aboue, and fro the lendis of him til to bynethe, Y siy as the licnesse of fier schynynge in cumpas,
Nikaona kwamba kutokana na kile nilichoona kama kiuno chake kuelekea juu alionekana kama chuma inayowaka kana kwamba imejaa moto na kuanzia kiuno kwenda chini alionekana kama moto na mwanga mkali ulimzunguka.
28 as the biholdynge of the reynbowe, whanne it is in the cloude in the dai of reyn. This was the biholdyng of schynyng bi cumpas. This was a siyt of the licnesse of the glorie of the Lord. And Y siy, and felle doun on my face; and Y herde the vois of a spekere.
Kama vile kuonekana kwa upinde wa mvua mawinguni siku ya mvua, ndivyo ulivyokuwa ule mngʼao uliomzunguka. Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa utukufu wa Bwana. Nilipouona, nikaanguka kifudifudi, nikasikia sauti ya mtu anaongea.

< Ezekiel 1 >