< Ezekiel 43 >
1 And he ledde me out to the yate, that bihelde to the eest weie.
Yule mtu kisha akanileta hata kwenye lango lililokuwa linaelekea mashariki.
2 And lo! the glorie of God of Israel entride bi the eest weie; and a vois was to it, as the vois of many watris, and the erthe schynede of the mageste of hym.
Tazama! Utukufu wa Mungu wa Israeli ukaja kutoka mashariki; sauti yake ilikuwa kama sauti ya maji mengi, na nchi iling'aa kwa utukufu wake.
3 And Y siy a visioun, bi the licnesse whiche Y hadde seyn, whanne he cam to distrie the citee; and the licnesse was lijc the biholdyng whiche Y hadde seyn bisidis the flood Chobar.
Yalikuwa yanalingana na sura ya ono nililolona, kulingana na ono nililokuwa nimeliona wakati alipokuja kuuteketeza mji, na maono yalikuwa kama maono ambayo niliyokuwa nimeyaona Keberi Kanali nikaanguka kifudi fudi.
4 And Y felle doun on my face, and the mageste of the Lord entride in to the temple, bi the weie of the yate that biheeld to the eest.
Hivyo utukufu wa Yahwe ukaja kwenye nyumba ya karibu na njia ya lango lililokuwa wazi kwa upande wa magharibi.
5 And the Spirit reiside me, and ledde me in to the ynnere halle; and lo! the hous was fillid of the glorie of the Lord.
Kisha Roho akanichukua na kunileta kwenye ua wa ndanni. Tazama! Utukufu wa Yahwe ulikuwa umeijaza nyumba.
6 And Y herde oon spekynge to me of the hous. And the man that stood bisidis me,
Mtu alisimama karibu na mimi, na nikamsikia mtu mwingine akizungumza na mimi kutoka kwenye nyumba.
7 seide to me, Thou, son of man, this is the place of my seete, and the place of the steppis of my feet, where Y dwelle in the myddis of the sones of Israel withouten ende; and the hous of Israel schulen no more defoule myn hooli name, thei, and the kyngis of hem in her fornicaciouns, and in the fallyngis of her kyngis, and in hiy places.
Akanambia, “Mwanadamu, hapa ndipo mahali pangu pa enzi na mahali kwa ajili ya ya miguu yangu, ambapo nitaishi kati ya watu wa Israeli milele. Nyumba ya Israeli haitalikufuru tena jina langu takatifu-wao au wafalme wao katika mahali patakatifu pao.
8 Whiche maden her threisfold bisidis my threisfold, and her postis bisidis my postis, and a wal was bitwixe me and hem; and thei defouliden myn hooli name in abhomynaciouns whiche thei diden; wherfor Y wastide hem in my wraththe.
Hawatalikufuru tena jina langu takatifu kwa kuweka kizingiti chao karibu na kizingiti changu, na nguzo yao ya lango karibu na nguzo yangu ya lango, bila kitu lakini ukuta kati yangu na wao. Wamelikufuru jina langu kwa matendo yao machafu, hivyo nimewala kwa hasira yangu.
9 Now therfor putte thei awei fer her fornicacioun, and the fallyng of her kyngis fro me; and Y schal dwelle euere in the myddis of hem.
Sasa waache waondoe udanganyifu wao na maiti za wafalme wao kutoka kwangu, na nitaishi katikati yao milele.
10 But thou, sone of man, schewe the temple to the hous of Israel, and be thei schent of her wickidnessis; and mete thei the bilding,
Mwanadamu, wewe mwenyewe utaiambia nyumba ya Israeli kuhusu nyumba hii hivyo watajiskia aibu ya uovu wao. Wanaweza kutafakari kuhusu haya maelezo.
11 and be thei aschamed of alle thingis whiche thei diden. Thou schalt schewe to hem, and thou schalt write bifore the iyen of hem the figure of the hous, and of the bildyng therof; the outgoyngis, and the entryngis, and al the discryuyng therof, and alle the comaundementis therof, and al the ordre therof, `and alle the lawis therof; that thei kepe alle the discryuyngis therof, and comaundementis therof, and do tho.
Kwa kuwa wameaibika kwa yote waliyoyafanya, kisha waonyeshe mchoro wa nyumba, maelezo yake, matokeo yake, maingio yake, na mchoro wake, sheria zake zote na kanuni. Kisha andika hivi chini mbele ya macho yao ili waweze kutunza michoro yote na kanuni zake zote, hivyo kama wazitiivo.
12 This is the lawe of the hous, in the hiynesse of the hil; alle the coostis therof in cumpas is the hooli of hooli thingis; therfor this is the lawe of the hous.
Hii ndiyo sheria kwa ajili ya nyumba: Kutoka kwenye kilele cha mlima hata mpaka wote unaoizunguka, patakuwa patakatifu sana. Tazama! Hii ndiyo sheria kwa ajili ya nyumba.
13 Forsothe these ben the mesuris of the auter, in a verieste cubit, that hadde a cubit and a spanne; in the bosum therof was a cubit in lengthe, and a cubit in breede; and the ende therof til to the brenke, and o spanne in cumpas; also this was the diche of the auter.
Hivi vitakuwa vipimo vya madhabahu katika dhiraa-hiyo dhiraa kuwa dhiraa ya kawaida na urefu wa kiganja. Hivyo mfereji ulio uzunguka madhabahu utakuwa dhiraa moja chini, na upana wake pia utakuwa dhiraa moja. Mpaka wa karibu uizungukayo machinjio shubiri moja. Hii itakuwa kitako cha madhabahu.
14 And fro the bosum of the erthe til to the laste heiythe weren twei cubitis, and the breede of o cubit; and fro the lesse heiythe til to the grettere heiythe were foure cubitis, and the breede was of o cubit;
Usawa wa kutoka kwenye mferji hadi kwenye machinijo ya chini ya madhabahu itakuwa dhiraa mbili, na hiyo machinjio yenyewe itakuwa dhiraa moja upana. Kisha kutoka machinjio madogo hadi kwenye machinjio makubwa ya madhabahu, itakuwa dhiraa nne, na machinjio makubwa yatakuwa dhraa moja upana.
15 forsothe thilke ariel, that is, the hiyere part of the auter, was of foure cubitis; and fro the auter `til to aboue weren foure hornes.
Meko juu ya madhabahu kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa ni dhiraa nne juu, na kuna pembe nne zilizoelekea juu kwenye meku.
16 And the auter of twelue cubitis in lengthe was foure cornerid with euene sidis, bi twelue cubitis of breede.
Meku ina dhiraa kumi na moja urefu na dhiraa kumi na mbili upana, za mraba.
17 And the heiythe of fourtene cubitis of lengthe was bi fourtene cubitis of breede, in foure corneris therof. And a coroun of half a cubit was in the cumpas therof, and the bosum therof was of o cubit bi cumpas; forsothe the degrees therof weren turned to the eest.
Mpaka wake ni dhiraa kumi na nne urefu na dhiraa kumi na nne upana pande zake zote nne, na ukingo wake ni nusu dhiraa upana. Mfereji ni dhiraa moja upana kuzuka kote pamoja na ngazi zielekeazo mashariki.”
18 And he seide to me, Thou, sone of man, the Lord God seith these thingis, These ben the customs of the auter, in what euer dai it is maad, that me offre on it brent sacrifice, and blood be sched out.
Kisha akanambia, “Mwanadamu, Bwana Yahwe asema hivi: Hizi ndizo sheria kwa ajili ya madhabahu katika siku watakayoitengeza, kwa ajili kutoa sadaka ya kuteketezwa kwenye hiyo, na kwa jili ya kunyunyiza damu juu yake.
19 And thou schalt yyue to preestis and dekenes, that ben of the seed of Sadoch, that neiyen to me, seith the Lord God, that thei offre to me a calf of the drooue for synne.
Utatoa ng'ombe kutoka kwenye kundi kama sadaka ya dhambi kwa ajili ya Walawi makuhani ambao ni uzao wa Zadoki, wale wajao karibu nami kunitumikia-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
20 And thou schalt take of the blood therof, and schalt putte on foure hornes therof, and on foure corneris of heiythe, and on the coroun in cumpas; and thou schalt clense it, and make clene.
Kisha utachukua baadhi ya damu yake na kuiweka juu pembe nne za madhabahu na pande nne za machinjio na kuuzunguka ukingo; utaitakasa na kufanya upatanisho kwa ajili yake.
21 And thou schalt take the calf which is offrid for synne, and thou schalt brenne it in a departid place of the hous, with out the seyntuarie.
Kisha chukua ng'ombe kama sadaka ya dhambi na iteketezwe katika eneneo lililotengwa la nje ya patakatifu.
22 And in the secounde dai thou schalt offre a buk of geet, which is with out wem, for synne; and thei schulen clense the auter, as thei clensiden in the calf.
Kisha katika siku ya pili utatoa mbuzi dume asiyekuwa na dosari kutoka kundini kama sadaka ya dhambi; makuhani wataisafisha madhabahu kama walivyoisafisha kwa ng'ombe.
23 And whanne thou hast fillid that clensyng, thou schalt offre a calf of the drooue, which calf is without wem, and a wether with out wem of the floc.
Utakapomaliza kusafisha, toa ng'ombe asiyekuwa na dosari kutoka kwenye mifugo na kondoo dume asiyekuwa na dosari kutoka kundini.
24 And thou schalt offre tho in the siyt of the Lord; and prestis schulen putte salt on tho, and schulen offre tho in to brent sacrifice to the Lord.
Watoe mbele ya Yahwe; makuhani watanyunyiza chumvi juu yao na kuwainua juu kama sadaka ya kutekezwa kwa Yahwe.
25 Bi seuene daies thou schalt make a buk of geet for synne, ech dai; and thei schulen offre a calf of the drooue, and a wether vnwemmed of scheep.
Utaandaa mbuzi dume kama sadaka ya dhambi kila siku kwa mda wa siku saba, na makuhani pia wataandaa ng'ombe asiye na dosari kutoka kwenye kundi na kondoo dume kutoka kwenye kundi.
26 Bi seuene daies thei schulen clense the auter, and schulen make it cleene, and thei schulen fille the hond therof.
Wataipatanisha madhabahu kwa siku saba na kuitakasa, wataitakasa kwa njia hii.
27 Forsothe whanne seuene daies ben fillid, in the eiythe dai and ferther prestis schulen make on the auter youre brent sacrifices, and tho thingis whiche thei offren for pees; and Y schal be plesid to you, seith the Lord God.
Watamaliza hizi siku saba, na katika siku ya nane na kuendelea itakuwa kwamba makuhani wataandaa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani kwenye madhabahu, ndipo nitakapowakubali-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”