< Ezekiel 38 >

1 And the word of the Lord was maad to me,
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 and he seide, Thou, sone of man, Sette thi face ayens Gog, and ayens the lond of Magog, the prince of the heed of Mosoch and of Tubal; and profesie thou of hym.
“Mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya Gogu, katika nchi ya Magogu, mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali, tabiri dhidi yake
3 And thou schalt seie to hym, The Lord God seith these thingis, A! Gog, lo! Y to thee, prince of the heed of Mosoch and of Tubal;
na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ee Gogu, mimi ni kinyume nawe, mtawala mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali.
4 and Y schal lede thee aboute, and Y schal sette a bridil in thi chekis, and Y schal leede out thee, and al thin oost, horsis, and horsmen, alle clothid with haburiouns, a greet multitude of men, takynge spere, and scheeld, and swerd.
Nitakugeuza kuelekea ulikotoka na kukutia ndoana kwenye mataya yako na kukutoa nje wewe pamoja na jeshi lako lote, yaani, farasi wako, wapanda farasi wako waliojiandaa tayari kwa vita, pamoja na kundi kubwa la wajeuri wakiwa na ngao na vigao, wote wakipunga panga zao.
5 Perseis, Ethiopiens, and Libiens with hem, alle ben araied with scheeldis and helmes.
Uajemi, Kushi na Putu watakuwa pamoja nao, wote wakiwa na ngao na kofia za chuma,
6 Gomer, and alle the cumpenyes of hym, the hous of Togorma, the sidis of the north, and al the strengthe therof, and many puplis ben with thee.
pia Gomeri pamoja na vikosi vyake vyote, na Beth-Togarma kutoka kaskazini ya mbali pamoja na vikosi vyake vyote, mataifa mengi wakiwa pamoja nawe.
7 Make redi, and araye thee, and al thi multitude which is gaderid to thee, and be thou in to comaundement to hem.
“‘Jiandae, uwe tayari, wewe na makundi yako yote ya wajeuri yaliyokusanyika pamoja nawe, nawe waamrishe.
8 Aftir many daies thou schalt be visitid, in the laste of yeeris thou schalt come to the lond, that turnede ayen fro swerd, and was gaderid of many puplis, to the hillis of Israel that weren desert ful ofte; this was led out of puplis, and alle men dwellide tristili ther ynne.
Baada ya siku nyingi utaitwa vitani. Katika miaka ijayo, utaivamia nchi ile ambayo imepona kutoka vita, ambayo watu wake walikusanywa kutoka mataifa mengi kuja katika milima ya Israeli, ambayo kwa muda mrefu ilikuwa imeachwa ukiwa. Wameletwa kutoka mataifa na sasa wote wanaishi katika hali ya salama.
9 Forsothe thou schalt stie, and schalt come as a tempest, and as a cloude, for to hile the lond, thou, and alle thi cumpanyes, and many puplis with thee.
Wewe na vikosi vyako vyote na mataifa mengi yaliyo pamoja nawe mtapanda juu, mtawazoa kama tufani na kuifunika nchi kama wingu.
10 The Lord God seith these thingis, In that dai wordis schulen stie on thin herte, and thou schalt thenke the worste thouyt;
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile mawazo yataingia moyoni mwako nawe utapanga mipango mibaya.
11 and schalt seie, Y schal stie to the lond with out wal, and Y schal come to hem that resten and dwellen sikirli; alle these dwellen with out wal, barris and yatis ben not to hem;
Utasema, “Nitapigana vita na nchi ambayo vijiji vyake havina maboma. Nitawashambulia watu wanaoishi kwa amani na wasiotarajia vita: wote wanaishi bila maboma na bila malango na makomeo.
12 that thou rauysche spuylis, and asaile prei; that thou brynge in thin hond on hem that weren forsakun, and afterward restorid, and on the puple which is gaderid of hethene men, that bigan to welde, and to be enhabitere of the nawle of erthe.
Nitateka mateka na kuchukua nyara mali za wale waliorudi kuishi katika mahame na wale watu waliokusanywa kutoka kwa mataifa, ambao sasa wana mifugo na mali nyingi, wanaoishi katikati ya nchi.”
13 Saba, and Dedan, and the marchauntis of Tharsis, and alle the liouns therof schulen seie to thee, Whether thou comest to take spuylis? Lo! to rauysche prey thou hast gaderid thi multitude, that thou take awei gold and siluer, and do awei purtenaunce of houshold and catel, and that thou rauysche preyes with out noumbre.
Sheba na Dedani pamoja na wafanyabiashara wa Tarshishi na vijiji vyake vyote watakuambia, “Je, umekuja kuteka mateka? Je, umekusanya makundi yako ya wajeuri ili kuchukua nyara mali, kutwaa fedha na dhahabu, kutunyangʼanya mifugo na mali na kuteka nyara nyingi zaidi?”’
14 Therfor profesie thou, sone of man; and thou schalt seie to Gog, The Lord God seith these thingis, Whether not in that dai, whanne my puple Israel schal dwelle tristili, thou schalt wite;
“Kwa hiyo, mwanadamu, tabiri na umwambie Gogu: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile, watu wangu Israeli watakapokuwa wanaishi salama, Je, wewe mwenyewe hutalijua hilo?
15 and schalt come fro thi place, fro the sidis of the north, thou, and many puplis with thee, alle stieris of horsis, a greet cumpany, and an huge oost;
Utakuja kutoka kwako huko kaskazini ya mbali, ukiwa pamoja na mataifa mengi, wote wakiwa wamepanda farasi, kundi kubwa, jeshi kuu.
16 and thou as a cloude schalt stie on my puple Israel, that thou hile the erthe? Thou schalt be in the laste daies, and Y schal brynge thee on my lond, that my folkis wite, whanne Y schal be halewid in thee, thou Gog, bifor the iyen of them.
Utakuja dhidi ya watu wangu Israeli kama wingu lifunikavyo nchi. Siku zijazo, ee Gogu, nitakuleta wewe dhidi ya nchi yangu, ili kwamba mataifa wapate kunijua Mimi nitakapojionyesha mtakatifu kwa kukupitia wewe mbele ya macho yao.
17 The Lord God seith these thingis, Therfor thou art he of whom Y spak in elde daies, in the hond of my seruauntis, profetis of Israel, that profesieden in the daies of tho tymes, that Y schulde bringe thee on hem.
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Je, wewe si yule niliyenena juu yako katika siku za zamani kwa kupitia kwa watumishi wangu manabii wa Israeli? Wakati ule walitabiri kwa miaka mingi kwamba ningekuleta upigane nao.
18 And it schal be, in that dai, in the dai of the comyng of Gog on the lond of Israel, seith the Lord God, myn indignacioun schal stie in my strong veniaunce, and in my feruour;
Hili ndilo litakalotokea katika siku ile: Gogu atakaposhambulia nchi ya Israeli, hasira yangu kali itaamka, asema Bwana Mwenyezi.
19 Y spak in the fier of my wraththe.
Katika wivu wangu na ghadhabu yangu kali ninasema kuwa wakati ule patakuwepo tetemeko kuu katika nchi ya Israeli.
20 For in that dai schal be grete mouyng on the lond of Israel; and fischis of the see, and beestis of erthe, and briddis of the eir, and ech crepynge beeste which is mouyd on erthe, and alle men that ben on the face of erthe, schulen be mouyd fro my face; and hillis schulen be vndurturned, and heggis schulen falle doun, and ech wal schal falle doun in to erthe.
Samaki wa baharini, ndege wa angani, wanyama wa kondeni, kila kiumbe kitambaacho ardhini, na watu wote walio juu ya uso wa nchi watatetemeka mbele zangu. Milima itapinduka, majabali yatapasuka na kila ukuta utaanguka chini.
21 And Y schal clepe togidere a swerd ayens hym in alle myn hillis, seith the Lord God; the swerd of ech man schal be dressid ayens his brother.
Nitaita upanga vita dhidi ya Gogu juu ya milima yangu yote, asema Bwana Mwenyezi. Upanga wa kila mtu utakuwa dhidi ya ndugu yake.
22 And thanne Y schal deme hym bi pestilence, and blood, and greet reyn, and bi greet stoonys; Y schal reyn fier and brymstoon on hym, and on his oost, and on many puplis that ben with hym.
Nitatekeleza hukumu juu yake kwa tauni na kwa umwagaji wa damu. Nitaifanya mvua ya mafuriko kunyesha, mvua ya mawe na moto wa kiberiti juu yake na juu ya vikosi vyake na juu ya mataifa mengi walio pamoja naye.
23 And Y schal be magnefied, and Y shal be halewid, and Y shal be knowun bifore the iyen of many folkis; and thei schulen wite, that Y am the Lord.
Nami hivyo ndivyo nitakavyoonyesha ukuu wangu na utakatifu wangu, nami nitajijulisha mbele ya macho ya mataifa mengi. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’

< Ezekiel 38 >