< Exodus 7 >

1 And the Lord seide to Moises, Lo! Y haue maad thee the god of Farao; and Aaron, thi brother, schal be thi prophete.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Tazama, nimekufanya kuwa kama Mungu kwa Farao, naye Aroni, huyo ndugu yako, atakuwa nabii wako.
2 Thou schalt speke to Aaron alle thingis whiche Y comaunde to thee, and he schal speke to Farao, that he delyuere the sones of Israel fro his hond.
Utasema kila kitu nitakachokuagiza, naye Aroni ndugu yako atamwambia Farao awaachie Waisraeli watoke katika nchi yake.
3 But Y schal make hard his herte, and Y schal multiplie my signes and merueils in the lond of Egipt, and he schal not here you;
Lakini nitaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu. Ingawa nitazidisha ishara na maajabu katika Misri,
4 and Y schal sende myn hond on Egipt, and Y schal lede out myn oost, and my puple, the sones of Israel, fro the lond of Egipt bi mooste domes;
hatawasikiliza. Kisha nitaupeleka mkono wangu juu ya Misri, na kwa matendo makuu ya hukumu nitavitoa vikundi vyangu, watu wangu Waisraeli.
5 and Egipcians schulen wite, that Y am the Lord, which haue holde forth myn hond on Egipt, and haue led out of the myddis of hem the sones of Israel.
Nao Wamisri watajua kuwa Mimi ndimi Bwana nitakapounyoosha mkono wangu dhidi ya Misri na kuwatoa Waisraeli watoke humo.”
6 And so Moises dide and Aaron; as the Lord comaundide, so thei diden.
Mose na Aroni wakafanya sawasawa kama vile Bwana alivyowaagiza.
7 Forsothe Moyses was of fourescoor yeer, and Aaron was of fourescoor yeer and thre, whanne thei spaken to Farao.
Mose alikuwa na umri wa miaka themanini na Aroni alikuwa na umri wa miaka themanini na mitatu walipozungumza na Farao.
8 And the Lord seide to Moises and to Aaron,
Bwana akamwambia Mose na Aroni,
9 Whanne Farao schal seie to you, Schewe ye signes to vs, thou schalt seie to Aaron, Take thi yerde, and caste forth it before Farao, and be it turned into a serpent.
“Farao atakapowaambia, ‘Fanyeni muujiza,’ basi mwambie Aroni, ‘Chukua fimbo yako na uitupe chini mbele ya Farao,’ nayo fimbo itakuwa nyoka.”
10 And so Moises and Aaron entriden to Farao, and diden as the Lord comaundide; and Aaron took the yeerde, and castide forth bifore Farao and hise seruauntis, which yerde was turned in to a serpent.
Ndipo Mose na Aroni wakaenda kwa Farao wakafanya sawasawa kama vile Bwana alivyoagiza. Aroni akaitupa ile fimbo yake chini mbele ya Farao na maafisa wake, nayo ikawa nyoka.
11 Forsothe Farao clepide wise men, and witchis, and thei also diden bi enchauntementis of Egipt, and bi summe priuy thingis in lijk maner;
Farao naye akawaita watu wenye maarifa na wachawi na waganga wa Kimisri, nao wakafanya vivyo hivyo kwa siri ya uganga wao.
12 and alle castiden forth her yerdis, whiche weren turned in to dragouns; but the yerde of Aaron deuouride `the yerdis of hem.
Kila mmoja alitupa fimbo yake chini, nayo ikawa nyoka. Lakini fimbo ya Aroni ikazimeza zile fimbo zao.
13 And the herte of Farao was maad hard, and he herde not hem, as the Lord comaundide.
Hata hivyo moyo wa Farao ukawa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
14 Forsothe the Lord seide to Moyses, The herte of Farao is maad greuouse, he nyle delyuere the puple;
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Moyo wa Farao ni mgumu, anakataa kuwaachia watu kuondoka.
15 go thou to hym eerli; lo! he schal go out to the watris, and thou schalt stonde in the comyng of hym on the brynke of the flood; and thou schalt take in thin honde the yerde, that was turned into a dragoun,
Nenda kwa Farao asubuhi wakati anapokwenda mtoni. Ngoja ukingoni mwa Naili ili uonane naye, na uchukue mkononi mwako fimbo ile iliyobadilishwa kuwa nyoka.
16 and thou schalt seie to hym, The Lord God of Ebrews sente me to thee, and seide, Delyuere thou my puple, that it make sacrifice to me in desert; til to present time thou noldist here.
Kisha umwambie, ‘Bwana, Mungu wa Waebrania, amenituma nikuambie: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu jangwani. Lakini hadi sasa hujasikiliza.
17 Therfor the Lord seith these thingis, In this thou schalt wite, that Y am the Lord; lo! Y schal smyte with the yerde, which is in myn hond, the watir of the flood, and it schal be turned in to blood;
Hili ndilo Bwana asemalo: Kwa hili utajua kuwa Mimi ndimi Bwana: Fimbo iliyo mkononi mwangu nitapiga nayo maji ya Naili nayo yatabadilika kuwa damu.
18 and the fischis that ben in the flood schulen die; and the watris schulen wexe rotun, and Egipcians drynkynge the watir of the flood schulen be turmentid.
Samaki waliomo katika Mto Naili watakufa, nao mto utanuka vibaya, Wamisri hawataweza kunywa hayo maji yake.’”
19 Also the Lord seide to Moises, Seie thou to Aaron, Take thi yerde, and holde forth thin hond on the watris of Egipt, and on the flodis of hem, and on the stremys `of hem, and on the mareis, and alle lakis of watris, that tho be turned in to blood; and blood be in al the lond of Egipt, as wel in vessils of tree as of stoon.
Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Chukua ile fimbo yako unyooshe mkono wako juu ya maji ya Misri, juu ya chemchemi na mifereji, juu ya madimbwi na mabwawa yote,’ navyo vitabadilika kuwa damu. Damu itakuwa kila mahali katika Misri, hata kwenye vyombo vya miti na vya mawe.”
20 And Moises and Aaron diden so, as the Lord comaundide; and Aaron reiside the yerde, and smoot the watir of the flood bifore Farao and hise seruauntis, which watir was turned in to blood;
Mose na Aroni wakafanya kama vile Bwana alivyokuwa amewaagiza. Akainua fimbo yake machoni pa Farao na maafisa wake na kuyapiga maji ya Mto Naili, na maji yote yakabadilika kuwa damu.
21 and fischis, that weren in the flood, dieden; and the flood was rotun, and Egipcians myyten not drynke the water of the flood; and blood was in al the lond of Egipt.
Samaki katika Mto Naili wakafa, nao mto ukanuka vibaya sana kiasi kwamba Wamisri hawakuweza kunywa maji yake. Damu ilikuwa kila mahali katika nchi ya Misri.
22 And the witchis of Egipcians diden in lijk maner by her enchauntementis; and the herte of Farao was maad hard, and he herde not hem, as the Lord comaundide.
Lakini waganga wa Misri kwa kutumia siri ya uganga wao wakafanya vivyo hivyo, nao moyo wa Farao ukawa mgumu, hakuwasikiliza Mose na Aroni, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
23 And he turnede awei hym silf, and entride in to his hows, nethir he took it to herte, yhe, in this tyme.
Badala yake, Farao akageuka, akaenda kwenye jumba lake la kifalme, wala hakulitia hili moyoni.
24 Forsothe alle Egipcians diggiden watir `bi the cumpas of the flood, to drinke; for thei myyten not drynke of the `watir of the flood.
Nao Wamisri wote wakachimba kandokando ya Mto Naili kupata maji ya kunywa, kwa sababu hawakuweza kunywa maji ya mto.
25 And seuene daies weren fillid, aftir that the Lord smoot the flood.
Zilipita siku saba baada ya Bwana kuyapiga maji ya Mto Naili.

< Exodus 7 >