< Exodus 34 >

1 And aftirward God seide, Hewe to thee twey tablis of stoon at the licnesse of the formere, and Y schal write on tho tablis thilke wordis, whiche the tablis, that thou `hast broke, hadden.
Bwana akamwambia Mose, “Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, nami nitaandika juu yake maneno yale yaliyokuwa kwenye vile vibao vya kwanza, ulivyovivunja.
2 Be thou redi in the morewtid, that thou stie anoon in to the hil of Synai; and thou schalt stonde with me on the cop of the hil;
Uwe tayari asubuhi, kisha upande juu ya Mlima Sinai. Uje mbele zangu kukutana nami huko juu ya mlima.
3 no man stie with thee, nether ony man be seyn bi al the hil, and oxun and scheep be not fed ayens `the hil.
Mtu yeyote asije pamoja nawe, wala asionekane mtu popote juu ya mlima, wala kondoo na mbuzi au ngʼombe wasilishe karibu mbele ya huo mlima.”
4 Therfor Moises hewide twey tablis of stoon, whiche manere tablis weren bifore, and he roos bi nyyt, and stiede in to the hil of Synay, as the Lord comaundide to hym; and he bar with hym the tablis.
Kwa hiyo Mose akachonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, naye akapanda juu ya Mlima Sinai asubuhi na mapema, kama Bwana alivyokuwa amemwagiza, akachukua vile vibao viwili vya mawe mikononi mwake.
5 And whanne the Lord hadde come doun bi a cloude, Moises stood with hym, and clepide inwardli `the name of the Lord;
Kisha Bwana akashuka katika wingu akasimama pamoja naye huko, akalitangaza jina lake, Bwana.
6 and whanne the Lord passide bifore hym, he seide, Lordschipere, Lord God, mercyful, and pitouse, pacient, and of myche mersiful doyng, and sothefast,
Bwana akapita mbele ya Mose, akitangaza, “Bwana, Bwana, Mungu mwenye huruma na neema, asiye mwepesi wa hasira, mwingi wa upendo na uaminifu,
7 which kepist couenaunt and mercy in to `a thousande, which doist awey wickidnesse, and trespassis, and synnes, and noon bi hym silf is innocent anentis thee, which yeldist the wickidnesse of fadris to sones and to sones of sones, into the thridde and fourthe generacioun.
akidumisha upendo kwa maelfu, pia akisamehe uovu, uasi na dhambi. Lakini haachi kuadhibu mwenye hatia; huwaadhibu watoto na watoto wao kwa ajili ya dhambi ya baba zao hata katika kizazi cha tatu na cha nne.”
8 And hastili Moises was bowid low `in to erthe, and worschipide,
Mara Mose akasujudu na kuabudu.
9 and seide, Lord, if Y haue founde grace in thi siyt, Y biseche that thou go with vs, for the puple is of hard nol, and that thou do awey oure wickidnesses and synnes, and welde vs.
Mose akasema, “Ee Bwana, kama nimepata kibali mbele zako, basi Bwana uende pamoja nasi. Ingawa watu hawa ni wenye shingo ngumu, samehe uovu wetu na dhambi yetu, tuchukue kuwa urithi wako.”
10 The Lord answeride, Y schal make couenaunt, and in siyt of alle men Y schal make signes, that weren neuer seyn on erthe, nether in ony folkis, that this puple, in whos myddis thou art, se the ferdful werk of the Lord, which Y schal make.
Kisha Bwana akasema: “Tazama ninafanya Agano mbele ya watu wako wote. Mbele ya watu wako wote nitafanya maajabu ambayo hayajafanyika katika taifa lolote katika ulimwengu wote. Watu wale mnaoishi miongoni mwao wataona jinsi ilivyo ya kushangaza ile kazi nitakayowafanyia mimi Bwana wenu.
11 Kepe thou alle thingis, whiche Y comaundide to thee to dai; I my silf schal caste out bifor thi face Amorrey, and Cananey, and Ethei, and Ferezei, and Euey, and Jebusei.
Tii yale ninayokuamuru leo. Tazama nawafukuza mbele yako Waamori, Wakanaani, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
12 Be war, lest ony tyme thou ioyne frendschipis with the dwelleris of that lond, whiche frenschipis be in to fallyng to thee.
Uwe mwangalifu, usifanye agano na wale wanaokaa katika nchi ile unayoiendea, la sivyo watakuwa mtego katikati yako.
13 But also distrie thou `the auteris of hem, breke the ymagis, and kitte doun the woodis;
Bomoa madhabahu yao, vunja mawe yao ya kuabudia na ukatekate nguzo zao za Ashera.
14 `nyl thou worschipe an alien God; `the Lord a gelous louyere is his name, God is a feruent louyere;
Usiabudu mungu mwingine, kwa kuwa Bwana, ambaye jina lake ni Wivu, ni Mungu mwenye wivu.
15 make thou not couenaunt with the men of tho cuntreis, lest whanne thei han do fornycacioun with her goddis, and han worschipid the symylacris of hem, ony man clepe thee, that thou ete of thingis offrid to an ydol.
“Uwe mwangalifu usifanye agano na wale watu wanaoishi katika nchi, kwa maana wakati wanapojifanyia ukahaba kwa miungu yao na kuwatolea kafara, watakualika wewe nawe utakula sadaka za matambiko yao.
16 Nether thou schalt take a wyif of her douytris to thi sones, lest aftir that tho douytris han do fornycacioun, thei make also thi sones to do fornicacioun in to her goddis.
Unapowachagua baadhi ya binti zao kuwa wake wa wana wenu na binti hao wakajifanyia ukahaba kwa miungu yao, watawaongoza wana wenu kufanya vivyo hivyo.
17 Thou schalt not make to thee yotun goddis.
“Usijifanyie sanamu za kusubu.
18 Thou schalt kepe the solempynyte of therf looues; seuene daies thou schalt ete therf looues, as Y comaundide to thee, in the time of the monethe of newe fruytis; for in the monethe of veer tyme thou yedist out of Egipt.
“Utaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu, kama nilivyokuamuru. Fanya hivi kwa wakati ulioamriwa, katika mwezi wa Abibu, ndio mwezi wa nne, kwa kuwa katika mwezi huo ndipo wewe ulipotoka Misri.
19 Al thing of male kynde that openeth the wombe schal be myn, of alle lyuynge beestis, as wel of oxun, as of scheep, it schal be myn.
“Mzaliwa wa kwanza wa kila tumbo ni mali yangu, pamoja na wazaliwa wa kwanza wote wa kiume wa mifugo yako, ikiwa ni wa ngʼombe au wa kondoo au mbuzi.
20 Thou schalt ayenbie with a scheep the firste gendrid of an asse, ellis if thou yyuest not prijs therfor, it schal be slayn. Thou schalt ayenbie the firste gendrid of thi sones; nether thou schalt appere voide in my siyt.
Utakomboa mzaliwa wa kwanza wa punda kwa mwana-kondoo, lakini kama humkomboi, utavunja shingo yake. Utakomboa wazaliwa wako wa kwanza wote wa kiume. “Mtu yeyote asije mbele zangu mikono mitupu.
21 Sixe daies thou schalt worche, the seuenthe day thou schalt ceesse to ere and repe.
“Kwa siku sita utafanya kazi, lakini siku ya saba utapumzika, hata ikiwa ni majira ya kulima au ya kuvuna lazima upumzike.
22 Thou schalt make to thee the solempnyte of woukis in the firste thingis of fruytis of thi ripe corn of wheete, and the solempnyte, whanne alle thingis ben gadrid in to bernes, whanne the tyme `of yeer cometh ayen.
“Utaadhimisha Sikukuu ya Majuma kwa malimbuko ya mavuno ya ngano, na Sikukuu ya Mavuno mwishoni mwa mwaka.
23 Ech male kynde of thee schal appere in thre tymes of the yeer in the siyt of the Lord Almyyti, thi God of Israel.
Mara tatu kwa mwaka wanaume wako wote watakuja mbele za Bwana Mwenyezi, Mungu wa Israeli.
24 For whanne Y schal take awei folkis fro thi face, and Y schal alarge thi termes, noon schal sette tresouns to thi lond, while thou stiest and apperist in the siyt of thi Lord God, thries in the yeer.
Nitawafukuza mataifa mbele yako na kupanua mipaka ya nchi yako, wala hakuna mtu yeyote atakayeitamani nchi yako wakati unapokwenda mara tatu kila mwaka kuonana na Bwana Mungu wako.
25 Thou schalt not offre on sour dow the blood of my sacrifice, nethir ony thing of the slayn sacrifice of the solempnyte of fase schal abide in the morewtid.
“Usinitolee damu ya dhabihu pamoja na kitu chochote chenye chachu, wala usibakize dhabihu yoyote ya Sikukuu ya Pasaka mpaka asubuhi.
26 Thou schalt offre in the hows of thi Lord God the firste of the fruytis of thi lond. Thou schalt not sethe a kide in the mylk of his modir.
“Leta matunda ya kwanza yaliyo bora zaidi ya ardhi yako katika nyumba ya Bwana Mungu wako. “Usimchemshe mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.”
27 And the Lord seide to Moises, Write thou these wordis, bi whiche Y smoot a boond of pees, bothe with thee and with Israel.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Andika maneno haya, kwa maana kulingana na maneno haya, nimefanya Agano na wewe pamoja na Israeli.”
28 Therfor Moises was there with the Lord bi fourti daies and bi fourti nyytis, he eet not breed, and drank not watir; and he wroot in tablys ten wordis of the boond of pees.
Mose alikuwa huko pamoja na Bwana kwa siku arobaini usiku na mchana bila kula chakula wala kunywa maji. Naye akaandika juu ya vibao maneno ya Agano, yaani zile Amri Kumi.
29 And whanne Moises cam doun fro the hil of Synai, he helde twei tablis of witnessyng, and he wiste not that his face was horned of the felouschipe of Goddis word.
Mose alipoteremka kutoka Mlima Sinai akiwa na vile vibao viwili vya Ushuhuda mikononi mwake, hakujua kuwa uso wake ulikuwa ukingʼaa, kwa sababu alikuwa amezungumza na Bwana.
30 Forsothe Aaron and the sones of Israel sien Moises face horned,
Aroni na Waisraeli wote walipomwona Mose, kuwa uso wake unangʼaa, waliogopa kumkaribia.
31 and thei dredden to neiye niy, and thei weren clepid of hym, `and thei turneden ayen, as wel Aaron as the princis of the synagoge; and after that Moises spak, thei camen to hym,
Lakini Mose akawaita, kwa hiyo Aroni na viongozi wote wa jumuiya wakarudi, naye akazungumza nao.
32 yhe alle the sones of Israel; to whiche Moises comaundide alle thingis, whiche he hadde herd of the Lord in the hil of Synai.
Baadaye Waisraeli wote wakamkaribia, naye akawapa amri zote Bwana alizompa katika Mlima wa Sinai.
33 And whanne the wordis weren fillid, he puttide a veil on his face;
Mose alipomaliza kuzungumza nao, akaweka utaji kwenye uso wake.
34 and he entride to the Lord, and spak with hym, and dide awey that veil, til he yede out; and thanne he spak to the sones of Israel alle thingis, that weren comaundid to hym;
Lakini kila wakati Mose alipoingia mbele za Bwana kuzungumza naye, aliondoa ule utaji mpaka alipotoka nje. Naye alipotoka nje na kuwaambia Waisraeli lile ambalo ameagizwa,
35 whiche sien that the face of Moyses goynge out was horned, but eft he hilide his face, if ony tyme he spak to hem.
waliona kuwa uso wake unangʼaa. Kisha Mose angeliweka tena utaji juu ya uso wake mpaka alipokwenda kuzungumza na Bwana.

< Exodus 34 >