< Ephesians 3 >
1 For the grace of this thing I Poul, the boundun of Crist Jhesu, for you hethene men,
Kwa sababu hii, mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu ninyi watu wa Mataifa:
2 if netheles ye han herd the dispensacioun of Goddis grace, that is youun to me in you.
Kwa hakika mmekwisha kusikia kuhusu ile huduma ya neema ya Mungu niliyopewa kwa ajili yenu,
3 For bi reuelacioun the sacrament is maad knowun to me, as Y aboue wroot in schort thing,
yaani, ile siri iliodhihirishwa kwangu kwa njia ya ufunuo, kama nilivyotangulia kuandika kwa kifupi.
4 as ye moun rede, and vndurstonde my prudence in the mysterie of Crist.
Kwa kusoma haya, basi mtaweza kuelewa ufahamu wangu katika siri ya Kristo.
5 Which was not knowun to othere generaciouns to the sones of men, as it is now schewid to his hooli apostlis and prophetis in the spirit,
Siri hii haikudhihirishwa kwa wanadamu katika vizazi vingine kama vile sasa ilivyodhihirishwa na Roho kwa mitume na manabii watakatifu wa Mungu.
6 that hethene men ben euen eiris, and of oo bodi, and parteneris togidere of his biheest in Crist Jhesu bi the euangelie;
Siri hii ni kwamba, kwa njia ya Injili, watu wa Mataifa ni warithi pamoja na Israeli, viungo vya mwili mmoja na washiriki pamoja wa ahadi katika Kristo Yesu.
7 whos mynystre Y am maad, bi the yifte of Goddis grace, which is youun to me bi the worchyng of his vertu.
Nimekuwa mtumishi wa Injili hii kwa kipawa cha neema ya Mungu niliyopewa kwa nguvu yake itendayo kazi.
8 To me, leeste of alle seyntis, this grace is youun to preche among hethene men the vnserchable richessis of Crist,
Ingawa mimi ni mdogo kuliko aliye mdogo kabisa miongoni mwa watakatifu wote, nilipewa neema hii: ili niwahubirie watu wa Mataifa kuhusu utajiri usiopimika ulio ndani ya Kristo,
9 and to liytne alle men, which is the dispensacioun of sacrament hid fro worldis in God, that made alle thingis of nouyt; (aiōn )
na kuweka wazi kwa kila mtu siri hii iliyokuwa imefichwa tangu zamani katika Mungu, aliyeumba vitu vyote. (aiōn )
10 that the myche fold wisdom of God be knowun to princis and potestatis in heuenli thingis bi the chirche,
Ili sasa kwa njia ya Kanisa, hekima yote ya Mungu ipate kujulikana kwa watawala na wenye mamlaka katika ulimwengu wa roho,
11 bi the bifore ordinaunce of worldis, which he made in Crist Jhesu oure Lord. (aiōn )
sawasawa na kusudi lake la milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōn )
12 In whom we han trist and nyy comyng, in tristenyng bi the feith of hym.
Ndani yake na kwa njia ya imani katika yeye twaweza kumkaribia Mungu kwa uhuru na kwa ujasiri.
13 For which thing Y axe, that ye faile not in my tribulaciouns for you, which is youre glorie.
Kwa hiyo, nawaomba msikate tamaa kwa sababu ya mateso yangu kwa ajili yenu, hayo ni utukufu wenu.
14 For grace of this thing Y bowe my knees to the fadir of oure Lord Jhesu Crist,
Kwa sababu hii nampigia Baba magoti,
15 of whom ech fadirhod in heuenes and in erthe is named,
ambaye ubaba wote wa kila jamaa za mbinguni na za duniani unatokana naye.
16 that he yyue to you, aftir the richessis of his glorie, vertu to be strengthid bi his spirit in the ynnere man,
Namwomba Mungu awaimarishe kwa kuwatia nguvu mioyo yenu kwa njia ya Roho wake kwa kadiri ya utajiri wa utukufu wake,
17 that Crist dwelle bi feith in youre hertis; that ye rootid and groundid in charite,
ili kwamba, Kristo apate kukaa mioyoni mwenu kwa njia ya imani. Nami ninaomba kwamba ninyi mkiwa wenye mizizi tena imara katika msingi wa upendo,
18 moun comprehende with alle seyntis, which is the breede, and the lengthe, and the hiynesse, and the depnesse;
mwe na uwezo wa kufahamu pamoja na watakatifu wote jinsi ulivyo upana, urefu, kimo na kina upendo wa Kristo,
19 also to wite the charite of Crist more excellent than science, that ye be fillid in al the plentee of God.
na kujua upendo huu unaopita fahamu, ili mpate kujazwa na kufikia kipimo cha ukamilifu wote wa Mungu.
20 And to hym that is myyti to do alle thingis more plenteuousli than we axen or vndurstondun, bi the vertu that worchith in vs,
Basi kwa yeye awezaye kutenda mambo ya ajabu yasiyopimika kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya uweza wake ule utendao kazi ndani yetu,
21 to hym be glorie in the chirche, and in Crist Jhesu, in to alle the generaciouns of the world of worldis. Amen. (aiōn )
yeye atukuzwe katika kanisa na katika Kristo Yesu kwa vizazi vyote, milele na milele. Amen. (aiōn )