< Ecclesiastes 3 >
1 Alle thingis han tyme, and alle thingis vndur sunne passen bi her spaces.
Kuna wakati kwa ajili ya kila jambo, nayo majira kwa kila tendo chini ya mbingu:
2 Tyme of birthe, and time of diyng; tyme to plaunte, and tyme to drawe vp that that is plauntid.
wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa, wakati wa kupanda na wakati wa kungʼoa yaliyopandwa,
3 Tyme to sle, and tyme to make hool; tyme to distrie, and tyme to bilde.
wakati wa kuua na wakati wa kuponya, wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga,
4 Tyme to wepe, and tyme to leiye; tyme to biweile, and tyme to daunse.
wakati wa kulia na wakati wa kucheka, wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza,
5 Tyme to scatere stoonys, and tyme to gadere togidere; tyme to colle, and tyme to be fer fro collyngis.
wakati wa kutawanya mawe na wakati wa kukusanya mawe, wakati wa kukumbatia na wakati wa kutokumbatia,
6 Tyme to wynne, and tyme to leese; tyme to kepe, and tyme to caste awei.
wakati wa kutafuta na wakati wa kupoteza, wakati wa kuweka na wakati wa kutupa,
7 Tyme to kitte, and tyme to sewe togidere; tyme to be stille, and tyme to speke.
wakati wa kurarua na wakati wa kushona, wakati wa kunyamaza na wakati wa kuzungumza,
8 Tyme of loue, and tyme of hatrede; tyme of batel, and tyme of pees.
wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia, wakati wa vita na wakati wa amani.
9 What hath a man more of his trauel?
Mfanyakazi anapata faida gani kutokana na taabu yake?
10 I siy the turment, which God yaf to the sones of men, that thei be occupied therynne.
Nimeona mzigo Mungu alioweka juu ya wanadamu.
11 God made alle thingis good in her tyme, and yaf the world to disputyng of hem, that a man fynde not the werk which God hath wrouyt fro the bigynnyng `til in to the ende.
Amefanya kila kitu kiwe kizuri kwa wakati wake. Pia ameiweka hiyo milele katika mioyo ya wanadamu, wala hawawezi kutambua kwa kina yale ambayo Mungu amefanya tangu mwanzo hadi mwisho.
12 And Y knew that no thing was betere `to a man, `no but to be glad, and to do good werkis in his lijf.
Ninajua kwamba hakuna kitu bora kwa wanadamu kuliko kuwa na furaha na kutenda mema wakati wanapoishi.
13 For whi ech man that etith and drinkith, and seeth good of his trauel; this is the yifte of God.
Tena ni karama ya Mungu kila mtu apate kula na kunywa na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote.
14 I haue lerned that alle werkis, whiche God made, lasten stidfastli `til in to with outen ende; we moun not adde ony thing to tho, nether take awei fro tho thingis, whiche God made, that he be dred.
Ninajua kwamba kila kitu anachokifanya Mungu kitadumu milele, hakuna kinachoweza kuongezwa au kupunguzwa. Mungu hufanya hivyo ili watu wamche yeye.
15 That thing that is maad, dwellith perfitli; tho thingis that schulen come, weren bifore; and God restorith that, that is goon.
Chochote kilichopo kilishakuwepo, na kitakachokuwepo kimekwishakuwepo kabla; naye Mungu huyaita yale yaliyopita yarudi tena.
16 I siy vndur sunne vnfeithfulnesse in the place of doom; and wickidnesse in the place of riytfulnesse.
Pia nikaona kitu kingine tena chini ya jua: Mahali pa kutolea hukumu, uovu ulikuwepo, mahali pa kupatia haki, uovu ulikuwepo.
17 And Y seide in myn herte, The Lord schal deme a iust man, and an vnfeithful man; and the tyme of ech thing schal be thanne.
Nikafikiri moyoni mwangu, “Mungu atawaleta hukumuni wote wawili wenye haki na waovu, kwa maana kutakuwako na wakati kwa ajili ya kila jambo, wakati kwa ajili ya kila tendo.”
18 I seide in myn herte of the sones of men, that God schulde preue hem, and schewe that thei ben lijk vnresonable beestis.
Pia nikafikiri, “Kuhusu wanadamu, Mungu huwajaribu ili wajione kwamba wao ni kama wanyama.
19 Therfor oon is the perisching of man and of beestis, and euene condicioun is of euer eithir; as a man dieth, `so and tho beestis dien; alle beestis brethen in lijk maner, and a man hath no thing more than a beeste.
Hatima ya mwanadamu ni kama ile ya wanyama; wote wana mwisho unaofanana: Jinsi anavyokufa mnyama, ndivyo anavyokufa mwanadamu. Wote wana pumzi inayofanana; mwanadamu hana cha zaidi kuliko mnyama. Kila kitu ni ubatili.
20 Alle thingis ben suget to vanyte, and alle thingis goen to o place; tho ben maad of erthe, and tho turnen ayen togidere in to erthe.
Wote huenda mahali panapofanana; wote hutoka mavumbini, mavumbini wote hurudi.
21 Who knowith, if the spirit of the sones of Adam stieth vpward, and if the spirit of beestis goith dounward?
Ni nani ajuaye kama roho ya mtu huenda juu na roho ya mnyama hushuka chini ardhini?”
22 And Y perseyuede that no thing is betere, than that a man be glad in his werk, and that this be his part; for who schal brynge hym, that he knowe thingis that schulen come after hym?
Kwa hiyo nikaona kwamba hakuna kitu kilicho bora zaidi kwa mwanadamu kuliko kuifurahia kazi yake, kwa sababu hilo ndilo fungu lake. Kwa maana ni nani awezaye kumrudisha ili aje kuona kile kitakachotendeka baada yake?