< Deuteronomy 5 >

1 And Moises clepide al Israel, and seide to hym, Here, thou Israel, the cerymonyes and domes, whiche Y speke to dai in youre eeris; lerne ye tho, and `fille ye in werk.
Mose akawaita Israeli wote, akawaambia: Ee Israeli, sikilizeni amri na sheria ninazowatangazia leo. Jifunzeni, na mwe na hakika kuzifuata.
2 Oure Lord God made a boond of pees with vs in Oreb;
Bwana Mungu wetu alifanya Agano nasi katika mlima wa Horebu.
3 he made not couenaunt, `that is, of lawe writun, with oure fadris, but with vs that ben present, and lyuen.
Si kwamba Bwana alifanya Agano na baba zetu, bali alifanya nasi, nasi sote ambao tuko hai hapa leo.
4 Face to face he spak to vs in the hil, fro the myddis of the fier.
Bwana alisema nanyi uso kwa uso kutoka moto juu ya mlima.
5 Y was recouncelere and mediatour bitwixe God and you in that tyme, that Y schulde telle to you the wordis `of hym, for ye dredden the fier, and `stieden not in to the hil. And `the Lord seide,
(Wakati huo nilisimama kati ya Bwana na ninyi kuwatangazia neno la Bwana, kwa sababu mliogopa ule moto, nanyi hamkupanda mlimani.) Naye Mungu alisema:
6 Y am thi Lord God, that ladde thee out of the lond of Egipt, fro the hows of seruage.
“Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
7 Thou schalt not haue alien Goddis in my siyt.
Usiwe na miungu mingine ila mimi.
8 Thou schalt not make to thee a grauun ymage, nether a licnesse of alle thingis that ben in heuene aboue, and that ben in erthe bynethe, and that lyuen in watris vndur erthe;
Usijitengenezee sanamu katika umbo la kitu chochote kilicho juu mbinguni au duniani chini au ndani ya maji.
9 thou schalt not herie tho, `and thou schalt not worschipe tho; for Y am thi Lord God, `God a feruent louyer; and Y yelde the wickidnesse of fadris, in to sones in to the thridde and the fourthe generacioun to hem that haten me,
Usivisujudie wala kuviabudu; kwa kuwa Mimi, Bwana Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, ninayewaadhibu watoto kwa ajili ya dhambi za baba zao hadi kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
10 and Y do mersy in to many thousyndis to hem that louen me, and kepen myn heestis.
lakini ninaonyesha upendo kwa maelfu ya vizazi vya wale wanipendao na kuzishika amri zangu.
11 Thou schalt not mystake the name of thi Lord God in veyn, for he schal not be vnpunyschid, that takith the name of God on a veyn thing.
Usilitaje bure jina la Bwana Mungu wako, kwa kuwa Bwana hataacha kumhesabia hatia yeye alitajaye jina lake bure.
12 Kepe thou the `day of sabat that thou halewe it, as thi Lord God comaundide to thee.
Adhimisha siku ya Sabato na kuiweka takatifu, kama Bwana Mungu wako alivyokuagiza.
13 In sixe daies thou schalt worche, and thou schalt do alle thi werkis;
Kwa siku sita utafanya kazi na kutenda shughuli zako zote.
14 the seventhe day is `of sabat, that is the reste of thi Lord God. Thou schalt not do therynne ony thing of werk; thou, and thi sone, and douyter, seruaunt, and handmaide, and oxe, and asse, and `al thi werk beeste, and the pilgrym which is with ynne thi yatis; that thi seruaunt reste and thin handmaide, as also thou.
Lakini siku ya Saba ni Sabato kwa Bwana, Mungu wako. Siku hiyo hutafanya kazi yoyote, wewe, wala mwanao au binti yako, wala mtumishi wa kiume au mtumishi wa kike, wala ngʼombe wako, punda wako au mnyama wako yeyote, wala mgeni aliyeko malangoni mwako, ili kwamba mtumishi wako wa kiume na wa kike wapate kupumzika kama wewe.
15 Bithenke thou, that also thou seruedist in Egipt, and thi Lord God ledde thee out fro thennus, in a strong hond, and arm holdun forth; therfor he comaundide to thee, that thou schuldist kepe the `dai of sabat.
Kumbuka mlikuwa watumwa huko Misri, na Bwana Mungu wenu aliwatoa huko kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa. Kwa hiyo Bwana Mungu wako amekuagiza kuiadhimisha siku ya Sabato.
16 Onoure thi fadir and thi modir, as thi Lord God comaundide to thee, that thou lyue in long tyme, and that it be wel to thee, in the lond which thi Lord God schal yyue to thee.
Waheshimu baba yako na mama yako, kama Bwana Mungu wako alivyokuagiza, ili siku zako zipate kuwa nyingi na kufanikiwa katika nchi Bwana Mungu wako anayokupa.
17 Thou schalt not sle.
Usiue.
18 Thou schalt not do letcherie.
Usizini.
19 And thou schalt not do thefte.
Usiibe.
20 Thou schalt not speke fals witnessyng ayens thi neiybore.
Usimshuhudie jirani yako uongo.
21 Thou schalt not coueite `the wijf of thi neiybore, not hows, not feeld, not seruaunt, not handmayde, not oxe, not asse, and alle thingis that ben hise.
Usitamani mke wa jirani yako. Usitamani nyumba ya jirani yako au shamba lake, mtumishi wake wa kiume au wa kike, ngʼombe au punda wake, wala kitu chochote cha jirani yako.”
22 The Lord spak these wordis to al youre multitude, in the hil, fro the myddis of fier and of cloude and of myist, with greet vois, and addide no thing more; and he wroot tho wordis in two tablis of stoon, whiche he yaf to me.
Hizi ndizo amri alizozitangaza Bwana kwa sauti kubwa kwa kusanyiko lenu lote huko mlimani kutoka kwenye moto, wingu na giza nene, wala hakuongeza chochote zaidi. Kisha akaziandika juu ya vibao viwili vya mawe, naye akanipa mimi.
23 Forsothe after that ye herden the vois fro the myddis of the derknessis, and sien the hil brenne, alle ye princis of lynagis, and the grettere men in birthe, neiyiden to me, and seiden, Lo!
Mliposikia sauti kutoka kwenye giza, mlima ulipokuwa ukiwaka moto, viongozi wenu wote wa makabila yenu na wazee wenu walinijia mimi.
24 oure Lord God schewide to vs his maieste and greetnesse; we herden his vois fro the myddis of fier, and we preueden to day that a man lyuede, `while God spak with man.
Nanyi mkasema, “Bwana Mungu wetu ametuonyesha utukufu na enzi yake, nasi tumesikia sauti yake kutoka kwenye moto. Leo tumeona kwamba mwanadamu anaweza kuishi hata kama Mungu akizungumza naye.
25 Whi therfor schulen we die, and schal this gretteste fier deuoure vs? For if we heren more the vois of oure Lord God, we schulen die.
Lakini sasa, kwa nini tufe? Moto huu mkubwa utatuteketeza sisi na tutakufa kama tukiendelea kusikia sauti ya Bwana Mungu wetu zaidi.
26 What is ech man, that he here the vois of God lyuynge, that spekith fro the myddis of fier, as we herden, and that he may lyue?
Ni mtu yupi mwenye mwili ambaye amewahi kuisikia sauti ya Mungu aliye hai akizungumza kutoka kwenye moto, kama sisi tulivyoisikia, naye akaishi?
27 Rathere neiye thou, and here thou alle thingis whiche oure Lord God schal seie to thee; and thou schalt speke to vs, and we schulen here, and schulen do tho wordis.
Sogea karibu usikie yale yote asemayo Bwana Mungu wetu. Kisha utuambie chochote kile ambacho Bwana Mungu wetu anakuambia. Tutasikiliza na kutii.”
28 And whanne the Lord hadde herd this, he seide to me, Y herde the vois of the wordis of this puple, whiche thei spaken to thee; thei spaken wel alle thingis.
Bwana aliwasikia wakati mlipozungumza nami, na Bwana akaniambia, “Nimesikia kile hawa watu walichokuambia. Kila kitu walichokisema ni kizuri.
29 Who schal yyue `that thei haue siche soule, that thei drede me, and kepe alle my comaundementis in al tyme, that it be wel to hem and to the sones `of hem, with outen ende?
Laiti kama mioyo yao ingekuwa na mwelekeo wa kuniogopa na kuzishika amri zangu zote daima, ili kwamba wafanikiwe wao pamoja na watoto wao milele!
30 Go thou, and seye to hem, Turne ye ayen in to youre tentis.
“Nenda uwaambie warudi kwenye mahema yao.
31 Sotheli stonde thou here with me, and Y schal speke to thee alle comaundementis, and cerymonyes, and domes, whiche thou schalt teche hem, that thei do tho in the lond which Y schal yyue to hem in to possessioun.
Lakini wewe baki hapa pamoja nami ili niweze kukupa maagizo yote, amri na sheria ambazo utawafundisha wazifuate katika nchi ninayokwenda kuwapa waimiliki.”
32 Therfor kepe ye, and `do ye tho thingis, whiche the Lord God comaundide to you; ye schulen not bowe awey, nether to the riyt side nether to the left side,
Hivyo kuweni waangalifu kuyafanya yale Bwana Mungu wenu aliyowaagiza; msigeuke upande wa kuume wala wa kushoto.
33 but ye schulen go bi the weie whiche youre Lord God comaundide, that ye lyue, and that it be wel to you, and that youre daies be lengthid in the lond of youre possessioun.
Fuateni yale yote ambayo Bwana Mungu wenu aliwaagiza, ili mpate kuishi, kustawi na kuziongeza siku zenu katika nchi mtakayoimiliki.

< Deuteronomy 5 >