< Deuteronomy 27 >

1 Forsothe Moyses comaundide, and the eldre men, to the puple of Israel, and seiden, Kepe ye ech `comaundement which Y comaunde to you to dai.
Mose na wazee wa Israeli wakawaagiza watu: “Yashikeni maagizo haya yote ninayowaagiza leo.
2 And whanne ye han passid Jordan, in to the lond which thi Lord God schal yyue to thee, thou schalt reyse grete stoonus, and thou schalt make tho pleyn with chalk,
Mtakapokuwa mmevuka Mto Yordani na kuingia katika nchi awapayo Bwana Mungu wenu, msimamishe mawe makubwa na mkayatie lipu.
3 that thou mow write in tho alle the wordis of this lawe, whanne Jordan is passid, that thou entre in to the lond which thi Lord God schal yyue to thee, the lond flowynge with mylke and hony, as he swoor to thi fadris.
Andikeni juu yake maneno yote ya sheria hii wakati mtakapokuwa mmevuka na kuingia katika nchi awapayo Bwana Mungu wenu, nchi itiririkayo maziwa na asali, kama vile Bwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaahidi.
4 Therfor whanne thou hast passid Jordan, reise thou the stonus whiche Y comaunde to dai to thee, in the hil of Hebal; and thou schalt make tho pleyn with chalk.
Mtakapokuwa mmevuka Yordani, simamisheni mawe haya juu ya Mlima Ebali, kama ninavyowaagiza leo, mkayatie lipu.
5 And there thou schalt bilde an auter to thi Lord God, of stoonys whiche yrun touchide not,
Huko mjengeeni Bwana Mungu wenu madhabahu, madhabahu ya mawe. Msitumie kifaa chochote cha chuma juu yake.
6 and of stonys vnformed and vnpolischid; and thou schalt offre theron brent sacrifices to thi Lord God; and thou schalt offre pesible sacrifices,
Jengeni madhabahu ya Bwana Mungu wenu kwa mawe ya shambani, na mtoe sadaka za kuteketezwa juu yake kwa Bwana Mungu wenu.
7 and thou schalt ete there, and thou schalt make feeste bifor thi Lord God.
Toeni sadaka za amani juu yake, mkizila na kufurahia mbele za Bwana Mungu wenu.
8 And thou schalt write pleynli and clereli on the stoonys alle the wordis of this lawe.
Nanyi mtaandika maneno yote ya sheria hii kwa wazi sana juu ya mawe haya ambayo mmesimamisha.”
9 And Moises and the preestis of the kynde of Leuy seiden to al Israel, Israel, perseyue thou, and here; to day thou art maad the puple of thi Lord God;
Kisha Mose na makuhani, ambao ni Walawi, wakawaambia Israeli wote, “Nyamaza ee Israeli, sikiliza! Sasa umekuwa taifa la Bwana Mungu wako.
10 thou schalt here his vois, and thou schalt do `the comaundementis, and riytfulnessis, whiche Y comaunde to thee to dai.
Mtii Bwana Mungu wako, na kufuata amri zake na maagizo ninayokupa leo.”
11 And Moises comaundide to the puple in that day,
Siku ile ile Mose akawaagiza watu:
12 and seide, These men schulen stonde on the hil of Garizym to blesse the Lord, whanne Jordan `is passid; Symeon, Leuy, Judas, Isachar, Joseph, and Benjamyn.
Mtakapovuka Mto Yordani, makabila haya yatasimama juu ya Mlima Gerizimu kubariki watu: Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Yosefu na Benyamini.
13 And euene ayens these men schulen stonde in the hil of Hebal to curse, Ruben, Gad, and Aser, Zabulon, Dan, and Neptalym.
Makabila haya yatasimama juu ya Mlima Ebali kwa kutamka laana: Reubeni, Gadi, Asheri, Zabuloni, Dani na Naftali.
14 And the dekenes schulen pronounce, and schulen seie `with hiy vois to alle the men of Israel,
Nao Walawi watawasomea watu wote wa Israeli kwa sauti kubwa:
15 Cursid is the man that makith a grauun ymage and yotun togidere, abhomynacioun of the Lord, the werk of `hondis of crafti men, and schal sette it in priuey place; and al the puple schal answere, and schal seie, Amen!
“Alaaniwe mtu afanyaye sanamu ya kuchonga au mwenye kusubu sanamu, kitu ambacho ni chukizo kwa Bwana, kazi ya mikono ya fundi stadi, na kuisimamisha kwa siri.”
16 He is cursid that onoureth not his fadir and modir; and al the puple schal seie, Amen!
“Alaaniwe mtu amdharauye baba yake na mama yake.”
17 Cursid is he that `berith ouer the termes of his neiybore; and al the puple schal seie, Amen!
“Alaaniwe mtu asogezaye jiwe la mpaka wa jirani yake.”
18 Cursid is he that makith a blynde man to erre in the weie; and al the puple schal seie, Amen!
“Alaaniwe mtu ampotoshaye kipofu njiani.”
19 He is cursid that peruertith the doom of a comelyng, of a fadirles, ethir modirles child, and of a widewe; and al the puple schal seie, Amen!
“Alaaniwe mtu apotoshaye haki ya mgeni, yatima au mjane.”
20 Cursid is he that slepith with `the wijf of his fadir, and schewith the hiling of his bed; and al the puple schal seie, Amen!
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mke wa baba yake, kwa maana anadharau malazi ya baba yake.”
21 Cursid is he that slepith with ony beeste; and al the puple schal seie, Amen!
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mnyama yeyote.”
22 Cursid is he that slepith with his sistir, the douytir of his fadir, ethir of his modir; and al the puple schal seie, Amen!
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na dada yake, binti wa baba yake au binti wa mama yake.”
23 Cursid is he that slepith with his wyues modir; and al the puple schal seye, Amen!
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mama mkwe wake.”
24 Cursid is he that sleeth pryueli his neiybore; and al the puple schal seie, Amen!
“Alaaniwe mtu amuuaye jirani yake kwa siri.”
25 Cursid is he that slepith with `the wijf of his neiybore; and al the puple schal seie, Amen!
“Alaaniwe mtu apokeaye rushwa ili kumuua mtu asiye na hatia.”
26 Cursid is he that takith yiftis, that he smyte the lijf of innocent blood; and al the puple schal seie, Amen! Cursid is he that dwellith not in the wordis of this lawe, nethir `parfourmeth tho in werk; and al the puple schal seie, Amen!
“Alaaniwe mtu yule ambaye hatashikilia maneno ya sheria hii kwa kuyatekeleza.”

< Deuteronomy 27 >