< Deuteronomy 2 >
1 And we yeden forth fro thennus, and camen in to the wildirnesse that ledith to the Reed See, as the Lord seide to me; and we cumpassiden the hil of Seir in long tyme.
Kisha tukageuka nyuma na kusafiri kuelekea jangwani kwa njia inayoelekea Bahari ya Shamu, kama Bwana alivyonielekeza. Kwa muda mrefu tulitembea kuzunguka vilima katika nchi ya Seiri.
2 And the Lord seide to me, It sufficith to you to cumpasse this hil;
Kisha Bwana akaniambia,
“Umetembea kuzunguka hii nchi ya vilima kwa muda wa kutosha; sasa geukia kaskazini.
4 And comaunde thou to the puple, and seie, Ye schulen passe bi the termes of youre britheren, the sones of Esau, that dwellen in Seir, and thei schulen drede you.
Wape watu maagizo haya: ‘Mko karibu kupita katikati ya nchi ya ndugu zako ambao ni wazao wa Esau, ambao wanaishi Seiri. Watawaogopa, lakini mwe waangalifu.
5 Therfor se ye diligentli, that ye be not moued ayens hem; for Y schal not yyue to you of the land `of hem as myche as the steppe of o foot may trede, for Y yaf the hil of Seir in to the possessioun of Esau.
Msiwachokoze kwa vita kwa maana sitawapa ninyi sehemu yoyote ya nchi yao, hata sehemu ya kutosha kuweka wayo wenu juu yake. Nimempa Esau nchi ya vilima ya Seiri kama yake mwenyewe.
6 Ye schulden bie of hem metis for money, and ye schulen ete; ye schulden drawe, and drynke watir bouyt.
Mtawalipa fedha kwa chakula mtakachokula na maji mtakayokunywa.’”
7 Thi Lord God blesside thee in al the werk of thin hondis; he knewe thi weye, hou thou passidist this moste wildirnesse, bi fourti yeer; and thi Lord God dwellide with thee, and no thing failide to thee.
Bwana Mungu wenu amewabariki kwa kazi yote ya mikono yenu. Amewalinda katika safari yenu katikati ya jangwa hili kubwa. Kwa miaka hii arobaini Bwana Mungu wenu amekuwa pamoja nanyi, na hamkupungukiwa na kitu chochote.
8 And whanne we hadden passid bi oure britheren, the sones of Esau, that dwelliden in Seir, bi the weie of the feeld of Elath, and of Asiongaber, we camen to the weie that ledith in to deseert of Moab.
Basi tulipita kwa ndugu zetu wazao wa Esau ambao wanaishi Seiri. Tuligeuka kutoka njia ya Araba ambayo inatokea Elathi na Esion-Geberi, tukasafiri kufuata njia ya jangwa la Moabu.
9 And the Lord seide to me, Fiyte thou not ayens Moabitis, nether bigyn thou batel ayens hem, for Y schal not yyue to thee ony thing of the lond `of hem, for Y yaf Ar in to possessioun to `the sones of Loth.
Kisha Bwana akaniambia, “Usiwasumbue Wamoabu kwa vita, kwa kuwa sitawapa sehemu yoyote ya nchi yao. Nimetoa nchi ya Ari kwa wazao wa Loti kama milki yao.”
10 Emyn, `that is, griseful men, weren first dwelleris therof, a greet puple, and strong, and so hiy, that thei weren bileued as giantis,
(Waemi walikuwa wakiishi huko hapo zamani, watu wenye nguvu na wengi, warefu kama Waanaki.
11 of the generacioun of Enachym, and thei weren lijk the sones of Enachym; forsothe Moabitis clepen hem Emyn.
Kama walivyokuwa Waanaki, hao pia walikuwa kama Warefai, lakini Wamoabu waliwaita Waemi.
12 Forsothe Horreis dwelliden bifore in Seir, and whanne thei weren put out, and weren doon awey, `the sones of Esau dwelliden there, as Israel dide in the lond of his possessioun, which the Lord yaf to hym.
Wahori waliishi Seiri, lakini wazao wa Esau waliwafukuza. Waliwaangamiza Wahori na kukaa mahali pao, kama Waisraeli walivyofanya katika nchi ambayo Bwana aliwapa kama milki yao.)
13 Therfor we riseden, that we schulden passe the stronde of Zared, and camen to it.
Bwana akasema, “Sasa ondokeni mvuke Bonde la Zeredi.” Hivyo tukavuka bonde.
14 Sotheli the tyme in whiche we yeden fro Cades Barne `til to the passynge of the stronde of Zared, was of eiyte and thretti yeer, til al the generacioun of `men fiyteris was wastid fro `the castels, as the Lord hadde swore; whos hond was ayens hem,
Miaka thelathini na minane ilipita tangu wakati tulipoondoka Kadesh-Barnea mpaka tulipovuka Bonde la Zeredi. Kwa wakati huo kile kizazi chote cha wanaume kuanzia wale wawezao kwenda vitani kilikuwa kimekufa, kama Bwana alivyokuwa amewaapia.
15 that thei schulden perische fro the myddis of `the castels.
Mkono wa Bwana uliwakabili hadi alipowaangamiza wote huko kambini.
16 Forsothe after that alle the fiyteris felden doun,
Ikawa baada ya mtu wa mwisho kuanzia wale wawezao kwenda vitani kufa,
17 the Lord spak to me, and seide,
Bwana akaniambia,
18 Thou schalt passe to dai the termes of Moab,
“Leo utapita katika nchi ya Moabu huko Ari.
19 the cytee, Ar bi name, and thou schalt neiy in the nyy coost of the sones of Amon; be thou war that thou fiyte not ayens hem, nether be moued to batel; for Y schal not yyue to thee of the lond of the sones of Amon, for Y yaf it to the `sones of Loth in to possessioun.
Utakapokuja kwa Waamoni, msiwasumbue wala kuwachokoza kwa vita, kwa kuwa sitawapa ardhi yoyote iliyo ya Waamoni kuwa milki yenu. Nimeitoa kama milki ya wazao wa Loti.”
20 It is arettid the lond of giauntis, and giauntis enhabitiden therynne sumtyme, whiche giauntis Amonytis clepen Zonym;
(Hiyo pia ilidhaniwa kuwa nchi ya Warefai waliokuwa wakiishi huko, lakini Waamoni waliwaita Wazamzumi.
21 a myche puple and greet, and of noble lengthe, as Enachym, whiche the Lord dide awey fro the face of hem,
Walikuwa watu wenye nguvu na wengi, warefu kama Waanaki. Bwana akawaangamiza kutoka mbele ya Waamoni, ambao waliwafukuza na kukaa mahali pao.
22 and made hem to dwelle for `tho giauntis, as he dide to the sones of Esau, that dwellen in Seire, `and dide awai Horreis, and yaf to hem the lond `of Horreis, which `the sones of Esau welden `til in to present tyme.
Bwana alikuwa amefanya vivyo hivyo kwa wazao wa Esau, ambao waliishi Seiri, wakati alipowaangamiza Wahori watoke mbele yao. Waliwafukuza na wao wakaishi mahali pao mpaka leo.
23 Also men of Capadocie puttiden out Eueys, that dwelliden in Asseryn, `til to Gaza; which yeden out fro Capadocie, and diden awey Eueis, and dwelliden for hem.
Nao Waavi ambao waliishi katika vijiji mpaka Gaza, Wakaftori waliokuja kutoka Kaftori waliwaangamiza na kukaa mahali pao.)
24 Rise ye, and `passe ye the stronde of Arnon; lo! Y haue bitake in `thin hond Seon, king of Esebon, of Amorreis; and his lond bigynne thou `to welde, and smyte thou batel ayens him.
“Ondoka sasa na uvuke Bonde la Arnoni. Tazama, nimemweka mikononi mwako Sihoni Mwamori, mfalme wa Heshboni na nchi yake. Anza kuimiliki nchi hiyo na umwingize katika vita.
25 To dai Y schal bigynne to sende thi drede and strengthe in to puplis that dwellen vndir al heuene, that whanne thi name is herd, thei drede, and tremble bi the maner of wymmen trauelynge of child, and `be holdun with sorewe.
Siku hii ya leo nitaanza kuwatia hofu na woga mataifa yote chini ya mbingu wawaogope ninyi. Watakaposikia taarifa zenu, watatetemeka na kufadhaika kwa sababu yenu.”
26 Therfor Y sente messangeris fro the wildirnesse of Cademoch to Seon, kyng of Esebon; and Y seide with pesible wordis,
Kutoka jangwa la Kedemothi nilituma wajumbe wenye maneno ya amani kwa Sihoni mfalme wa Heshboni kusema,
27 We schulen passe thorou thi lond, we schulen go in the comyn weie; we schulen not bowe nether to the riyt side, nether to the left side.
“Turuhusu tupite katika nchi yako. Tutapita katika barabara kuu, hatutageuka kuume wala kushoto.
28 Sille thow metis `to vs for prijs, that we ete; yif thow watir for money, and so we schulen drynke. Oneli it is that thou graunte passage to vs,
Tuuzie chakula tule na maji tunywe kwa thamani yake katika fedha. Turuhusu tu tupite kwa miguu,
29 as the sones of Esau diden, that dwellen in Seir, and as Moabitis diden, that dwellen in Ar, til we comen to Jordan, and passen to the lond which oure Lord God schal yyue to vs.
kama wazao wa Esau ambao wanaishi Seiri na Wamoabu ambao wanaishi Ari walivyotufanyia, mpaka tuvuke Yordani kuingia nchi ambayo Bwana Mungu wetu anatupatia.”
30 And Seon, kyng of Esebon, nolde yyue passage `to vs; for thi Lord God made hard his spirit, and made sad in yuel `the herte of hym, that he schulde be bitakun in to thin hondis, as thou seest now.
Lakini Sihoni mfalme wa Heshboni alikataa kuturuhusu kupita. Kwa kuwa Bwana Mungu wako alikuwa ameifanya roho yake kuwa ngumu na moyo wake kuwa mkaidi ili amweke kwenye mikono yenu, kama alivyofanya sasa.
31 And the Lord seide to me, Lo, Y bigan to bitake to thee Seon, and his lond; bigynne thou to welde it.
Bwana akaniambia, “Tazama, nimeanza kuwapa Mfalme Sihoni na nchi yake kwako. Sasa anzeni kuishinda na kuimiliki nchi yake.”
32 And Seon yede out ayens vs with al his puple to batel in Jasa.
Wakati Sihoni pamoja na jeshi lake lote walipokuja kukutana nasi katika vita huko Yahazi,
33 And oure Lord God bitook hym to vs, and we han smyte hym with hise sones, and al his puple.
Bwana Mungu wetu alimweka mikononi mwetu, nasi tukamwangamiza pamoja na wanawe na jeshi lake lote.
34 And we token in that tyme alle the citees, whanne the dwelleris of tho citees, men, and wymmen, and children weren slayn; we leften not in hem ony thing,
Kwa wakati ule tuliteka miji yake yote na kuiangamiza kabisa: wanaume, wanawake na watoto. Hatukumwacha yeyote.
35 outakun beestis that camen in to the part of men takynge prey, and outakun spuylis of the cytees whiche we tokun.
Lakini mifugo na nyara tulizoziteka kutoka ile miji tulijichukulia wenyewe.
36 Fro Aroer, which is on the brenke of the stronde of Arnon, fro the toun which is set in the valey, `til to Galaad, no town was ether citee, that ascapide oure hondis.
Kutoka Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kutoka mji ulio ndani ya bonde, hata mpaka Gileadi, hapakuwa na mji hata mmoja uliokuwa na nguvu kutushinda. Bwana Mungu wetu alitupa yote.
37 Oure Lord God bitook alle to vs; outakun the lond of the sones of Amon, to which lond we neiyiden not, and outakun alle thingis that liggen to the stronde of Jeboth, and outakun the citees of the munteyns, and alle places fro whiche oure Lord God forbeed vs.
Lakini kulingana na amri ya Bwana Mungu wetu, hamkujiingiza katika nchi yoyote ya Waamoni, wala katika sehemu yoyote iliyo kandokando ya Mto Yaboki, wala katika miji iliyoko katika vilima.