< Deuteronomy 10 >

1 In that tyme the Lord seide to me, Hewe thou twei tablis of stoon to thee, as the formere weren; and stie thou to me `in to the hil. And thou schalt make an arke,
Wakati ule Bwana aliniambia, “Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza uje kwangu juu mlimani. Pia utengeneze Sanduku la mbao.
2 `ether a cofere, of tree, and Y schal write in the tablis, the wordis that weren in these tablis whiche thou brakist bifore; and thou schalt putte tho tablis in to the arke.
Nitaandika juu ya vibao maneno yaliyokuwa katika vile vibao vya kwanza, ambavyo ulivivunja. Kisha utaviweka ndani ya Sanduku.”
3 Therfor Y made an ark of the trees of Sechim, and whanne Y hadde hewe twei tablis of stoon, at the licnesse of the formere tablis, Y stiede in to the hil, and hadde the tablis in the hondis.
Hivyo nikatengeneza Sanduku kwa mti wa mshita, nikachonga pia vibao vya mawe kama vile vya kwanza, kisha nikakwea mlimani nikiwa na vibao viwili mikononi mwangu.
4 And he wroot in the tablis, bi that that he `hadde writun bifore, ten wordis, whiche the Lord spak to you in the hil, fro the myddis of the fyer, whanne the puple was gaderid, and he yaf the tablis to me.
Bwana akaandika juu ya hivi vibao kile alichokuwa amekiandika kabla, Amri Kumi alizokuwa amewatangazia juu mlimani, kutoka kwenye moto siku ile ya kusanyiko. Bwana akanikabidhi.
5 And Y turnide ayen fro the hil, and cam doun, and puttide the tablis in to the arke which Y hadde maad, `whiche tablis ben there hidur to, as the Lord comaundide to me.
Kisha nikashuka kutoka mlimani na kuweka vibao ndani ya Sanduku nililokuwa nimelitengeneza, kama Bwana alivyoniagiza, navyo viko huko sasa.
6 Forsothe the sones of Israel moueden tentis fro Beroth of the sones of Jachan in to Mosera, where Aaron was deed, and biried, for whom his sone Eleazar was set in preesthod.
(Waisraeli walisafiri kutoka visima vya Yaakani hadi Mosera. Huko Aroni alifariki na kuzikwa, naye Eleazari mwanawe akachukua nafasi yake kama kuhani.
7 Fro thennus thei camen in to Galgad; fro which place thei yeden forth, and settiden tentis in Jehabatha, in the lond of watris and of strondis.
Kutoka pale, walisafiri hadi Gudgoda wakaendelea mpaka Yotbatha, nchi yenye vijito vya maji.
8 In that tyme Y departide the lynage of Leuy, that it schulde bere the arke of boond of pees of the Lord, and schulde stonde bifor hym in seruyce, and schulde blesse in his name til in to present dai.
Wakati huo Bwana aliteua kabila la Lawi kulibeba Sanduku la Agano la Bwana, kusimama mbele za Bwana ili kutoa huduma, na kutangaza baraka kwa Jina lake, kama wanavyofanya mpaka leo.
9 For which thing Leuy hadde not part, nether possession with hise brithren, for the Lord hym silf is his possessioun, as thi Lord God bihiyte to hym.
Hiyo ndiyo sababu ya Walawi kutokuwa na sehemu wala urithi miongoni mwa ndugu zao; Bwana ndiye urithi wao, kama Bwana Mungu wao alivyowaambia.)
10 Forsothe Y stood in the hil as bifore, fourti daies and fourti niytis, and the Lord herde me also in this tyme, and nolde leese thee.
Basi nilikaa mlimani kwa siku arobaini usiku na mchana, kama nilivyofanya mara ya kwanza, pia Bwana alinisikiliza hata wakati huu. Haikuwa nia yake kuwaangamiza.
11 And he seide to me, Go thou, and go bifor this puple, that it entre, and welde the lond which Y swoor to her fadris, that Y schulde yeue to hem.
Bwana akaniambia, “Nenda, ukawaongoze watu katika njia yao ili kwamba waweze kuingia na kuimiliki nchi ile niliyowaapia baba zao kuwapa.”
12 And now, Israel, what axith thi Lord God of thee, no but that thou drede thi Lord, and go in hise weies, and that thou loue hym, and serue thi Lord God in al thin herte, and in al thi soule;
Na sasa, ee Israeli, Bwana Mungu wako anataka nini kwako ila kumcha Bwana Mungu wako, kwenda katika njia zake, kumpenda na kumtumikia Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote,
13 and that thou kepe the comaundementis of thi Lord God, and the cerymonyes of hym, whiche Y comaunde to thee to dai, that it be wel to thee.
na kuyashika maagizo ya Bwana na amri zake ninazokupa leo kwa mafanikio yako mwenyewe?
14 Lo! heuene is of thi Lord God, and heuene of heuene; the erthe and alle thingis that ben ther ynne ben hise;
Mbingu, hata mbingu za juu sana, dunia na kila kitu kilichomo ndani yake, ni mali ya Bwana Mungu wako.
15 and netheles the Lord was glued to thi fadris, and louede hem, and he chees her seed after hem, and you of alle folkis, as it is preued to dai.
Hata hivyo Bwana alikuwa na shauku na baba zako, akawapenda na akawachagua ninyi, wazao wao, kuliko mataifa yote, kama ilivyo leo.
16 Therfor circumcide ye the prepucie, `ethir vnclennesse, of youre herte, and no more make ye harde youre nol.
Kwa hiyo tahirini mioyo yenu, na msiwe na shingo ngumu tena.
17 For youre Lord God hym silf is God of goddis, and Lord of lordis, `God greet, and miyti, and feerdful, which takith not persoone, nether yiftis.
Kwa kuwa Bwana Mungu wenu ni Mungu wa miungu na Bwana wa mabwana, Mungu mkuu, mwenye uweza na wa kutisha, ambaye hana upendeleo na hapokei rushwa.
18 He makith doom to the fadirles, and modirles, and to the widewe; he loueth a pilgrym, and yyueth to hym lyiflode and clothing.
Huwapigania yatima na wajane, humpenda mgeni, akimpa chakula na mavazi.
19 And therfor `loue ye pilgryms, for also ye weren comelyngis in the lond of Egipt.
Nanyi wapendeni wageni, kwa kuwa ninyi wenyewe mlikuwa wageni huko Misri.
20 Thou schalt drede thi Lord God, and thou schalt serue hym aloone, and thou schalt cleue to hym, and thou schalt swere in his name.
Mche Bwana Mungu wako na umtumikie yeye. Shikamana naye kwa uthabiti na kuapa kwa jina lake.
21 He is thi preisyng, and thi God, that made to thee these grete dedis, and ferdful, whiche thin iyen siyen.
Yeye ni sifa yako; yeye ni Mungu wako, ambaye alikutendea yale maajabu makubwa na ya kutisha uliyoyaona kwa macho yako mwenyewe.
22 In seuenti men thi fadris yeden doun in to Egipt, and lo! now thi Lord God hath multiplied thee as the sterris of heuene.
Baba zako walioshuka kwenda Misri jumla yao walikuwa sabini, na sasa Bwana Mungu wako amekufanya wengi kama nyota za angani.

< Deuteronomy 10 >