< Daniel 8 >

1 In the thridde yeer of the rewme of Balthasar, the king, a visioun apperide to me. Y, Danyel, after that thing that Y hadde seyn in the bigynnyng,
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mfalme Belshaza, mimi Danieli niliona maono (baada ya maono ya awali yaliyonipata).
2 siy in my visioun, whanne Y was in the castel of Susis, which is in the cuntrei of Helam; sotheli Y siy in the visioun that Y was on the yate Vlay.
Nilipokuwa nikiangalia katika ndoto, niliona kwamba nilikuwa katika mji wa Shushani wenye ngome katika jimbo la Elamu. Niliona katika ndoto kuwa nilikuwa karibu na mfereji wa Ulai.
3 And Y reiside myn iyen, and Y siy; and lo! o ram stood bifor the mareis, and hadde hiy hornes, and oon hiyere than the tother, and vndurwexynge.
Nilitazama juu na nikaona mbele yangu kondoo dume lenye mapembe mawili, limesimama pembeni mwa mfereji. Pembe moja lilikuwa refu kuliko jingine, lakini pembe ndefu ilikuwa inakua pole pole kuliko ile fupi na pembe fupi ilirefuka na kuizidi nyingine.
4 Aftirward Y siy the ram wyndewynge with hornes ayens the eest, and ayens the west, and ayens the north, and ayens the south; and alle beestis myyten not ayenstonde it, nether be delyuered fro the hondis of it. And it dide bi his wille, and was magnefied.
Niliona kondoo mme akiishambulia magharibi, kisha kaskazini, na baadaye kusini; hakuna mnyama mwingine aliyeweza kusimama mbele yake. Hakuna yeyote aliyeweza kumwokoa yeyote katika mkono wake. Alifanya chochote kile alichokitaka, na alikuwa mtu mkubwa sana.
5 And Y vndurstood. Lo! forsothe a buk of geet cam fro the west on the face of al erthe, and touchide not the erthe; forsothe the buk of geet hadde a noble horn bitwixe hise iyen;
Na nilipokuwa natafakari juu ya haya, niliona beberu akitoka magharibi, na kuvuka katika uso wa dunia yote, akikimbia kwa kasi kana kwamba hakuonekana kama aligusa ardhini. Mbuzi huyo alikuwa na pembe kubwa katikati ya macho yake.
6 and he cam til to that horned ram, which Y hadde seyn stondynge bifore the yate, and he ran in the fersnesse of his strengthe to that ram.
Alienda mpaka kwa kondoo aliyekuwa na pembe mbili, nilikuwa nimemwona kondoo dume amesimama katika ukingo wa mfereji na mbuzi alikimbia kumwelekea kondoo dume kwa hasira kali.
7 And whanne he hadde neiyid niy the ram, he hurlide fersly on hym, and he smoot the ram, and al to-brak tweyne hornes of hym, and the ram miyte not ayenstonde hym. And whanne he hadde sent that ram in to erthe, he defoulide; and no man miyte delyuere the ram fro his hond.
Niliiona mbuzi ikija karibu na kondoo. Mbuzi alikuwa na hasira na kondoo, alimpiga kondoo na alizivunja pembe zake mbili. Kondoo hakuwa na nguvu za kusimama mbele zake. Mbuzi alimgonga kondoo akaanguka chini na akamkanyaga. Hapakuwa na yeyote wa kumwokoa kutoka katika nguvu zake.
8 Forsothe the buk of geet was maad ful greet; and whanne he hadde encreessid, the greet horn was brokun, and foure hornes risiden vndur it, bi foure wyndis of heuene.
Ndipo mbuzi alikua akawa mkubwa, lakini alipokuwa na nguvu, pembe kubwa ilivunjwa, na katika sehemu yake zilichipuka na kukua pembe nne kubwa zilizochomoza kuelekea pepo nne za mbingu.
9 Forsothe of oon of hem yede out o litil horn, and it was maad greet ayens the south, and ayens the eest, and ayens the strengthe.
Kutoka katika pembe moja ilichipuka pembe nyingine, ilikuwa ndogo hapo awali, lakini baadaye ilikuwa pembe kubwa upande wa kusini, na mashariki, na katika nchi ya uzuri.
10 And it was magnefied til to the strengthe of heuene, and it castide doun of the strengthe and of sterris, and defoulide tho.
Pembe ilikuwa kubwa na matokeo yake iliinua vita dhidi ya jeshi la mbinguni. Baadhi ya jeshi na nyota kadhaa zilitupwa chini duniani, na zilikanyagwa.
11 And he was magnefied til to the prince of strengthe, and he took awei fro hym the contynuel sacrifice, and castide doun the place of his halewyng.
Alizidi kuwa mkubwa, mkubwa kama kamanda wa jeshi la kimungu. Sadaka za kuteketezwa za kila siku ziliondolewa mbali na yeye, na sehemu yake takatifu zilitiwa unajisi.
12 Forsothe strengthe was youun to hym ayens the contynuel sacrifice for synnes, and treuthe schal be cast doun in erthe; and he schal haue prosperite, and schal do.
Kwasababu ya uasi, pembe ya mbuzi ilipewa jeshi, na sadaka za kuteketezwa zitasitishwa. Pembe itautupa ukweli chini ardhini, na itafanikiwa katika kila jambo ilifanyalo.
13 And Y herde oon of hooli aungels spekynge; and oon hooli aungel seide to another, Y noot to whom spekinge, Hou long the visioun, and the contynuel sacrifice, and the synne of desolacioun, which is maad, and the seyntuarie, and the strengthe schal be defoulid?
Kisha nilimsikia mtakatifu mmoja akiongea na mtakatifu mwingine akamjibu, “Mambo haya yatadumu kwa muda gani, maono haya ya sadaka ya kuteketezwa, dhambi ile iletayo uharibifu, ukabidhiajia wa sehemu takatifu, na jeshi la mbinguni kukanyagwa?
14 And he seide to hym, Til to the euentid and morewtid, two thousynde daies and thre hundrid; and the seyntuarie schal be clensid.
Aliniambia, “Itadumu kwa jioni na asubuhi zipatazo 2, 300. Baada ya hapo, mahali patakatifu patawekwa sawa.”
15 Forsothe it was doon, whanne Y, Danyel, siy the visioun, and axide the vndurstondyng, lo! as the licnesse of a man stood in my siyt.
Wakati mimi Danieli, nilipoona maono, nilijaribu kuyaelewa. na hapo mbele yangu alisimama yule aliyeoneakana kama mtu.
16 And Y herde the voys of a man bitwixe Vlai, and he criede, and seide, Gabriel, make thou Danyel to vndurstonde this visioun.
Niliisikia sauti ya mtu ikiita katikati ya kingo za mfereji wa Ulai. Alisema, “Gabrieli, msaidie mtu huyu kuelewa maono.”
17 And he cam, and stood bisidis where Y stood; and whanne he was comun, Y dredde, and felle on my face. And he seide to me, Thou, sone of man, vndurstonde, for the visioun schal be fillid in the tyme of ende.
Basi alikuja karibu na mahali niliposimama. Na alipokuja, niliogopa na nilisujudia hadi chini. Aliniambia,”Fahamu, mwana wa mtu, kwamba maono ni kwa ajili ya wakati wa mwisho.”
18 And whanne he spak to me, Y slood doun `plat to the erthe. And he touchide me, and settide me in my degree.
Alipokuwa anaongea na mimi, nilipata usiingizi mzito nikiwa nimelala kifudifudi. Kisha alinishika na kunisimamisha.
19 And he seide to me, Y schal schewe to thee what thingis schulen come in the laste of cursing, for the tyme hath his ende.
Akaniambia, “Tazama, nitakuonyesha kile kitachotokea baadaye katika kipindi cha ghadhabu, kwasababu maono haya yanahusu wakati wa mwisho uliopangwa.
20 The ram, whom thou siyest haue hornes, is the kyng of Medeis and of Perseis.
Na kuhusu kondoo mme uliyemwona, yule mwenye pembe mbili - ni wafalme wawili wa Umedi na Uajemi.
21 Forsothe the buc of geet is the kyng of Grekis; and the greet horn that was bitwixe hise iyen, he is the firste kyng.
Mbuzi dume ni mfalme wa Ugiriki. Pembe kubwa katikati ya macho yake ni mfalme wa kwanza.
22 Forsothe that whanne that horn was brokun, foure hornes risiden for it, foure kyngis schulen rise of the folc of hym, but not in the strengthe of hym.
Na kuhusu pembe iliyovunjika, ambayo katika nafasi yake pembe zingine nne zilichipuka - hizi ni falme nne zitakazoinuka kutoka katika taifa lake, lakini hazitakuwa na nguvu kubwa.
23 And after the rewme of hem, whanne `wickidnessis han encreessid, a kyng schal rise vnschamefast in face, and vndurstondyng proposisiouns, ether resouns set forth; and his strengthe schal be maad stalworthe,
Katika siku zijazo za falme hizo, wakati ambapo wahalifu watakuwa wamefikia kikomo chao, mfalme mwenye uso katili, na yeye mwenye akili sana, atainuka.
24 but not in hise strengthis. And more than it mai be bileuyd he schal waste alle thingis, and he schal haue prosperite, and schal do. And he schal sle stronge men, and the puple of seyntis,
Nguvu zake zitakuwa kubwa, lakini si kwa nguvu zake mwenyewe. Atakuwa wa kustaajabisha kwa kile atakachokuwa anakiharibu; atafanya na kufanikiwa. Atawaangamiza watu wenye nguvu, watu miongoni wa watakatifu.
25 bi his wille, and gile schal be dressid in his hond. And he schal magnefie his herte, and in abundaunce of alle thingis he schal sle ful many men. And he schal rise ayens the prince of princes, and withouten hond he schal be al to-brokun.
Ataufanya udanganyifu usitawi chini ya mkono wake kwasababu ya ujanja wake. Atawaangamiza watu wengi bila kutegemea. Atainuka pia hata kinyume cha Mfalme wa wafalme, na atavunjwa, lakini si kwa mkono wowote wa binadamu.
26 And the visioun, which is seid in the morewtid and euentid, is trewe. Therfor seele thou the visioun, for it schal be after many daies.
Maono kuhusu jioni na asubuhi ulizoambiwa ni ya kweli. Lakini uyafunge maono haya, kwa kuwa yanahusu siku nyingi za wakati ujao.
27 And Y, Danyel, was astonyed, and was sijk bi ful many daies; and whanne Y hadde rise, Y dide the werkis of the kyng; and Y was astonyed at the visioun, and `noon was that interpretide.
Ndipo mimi, Danieli nilichoka sana na nikalala nikiwa dhaifu kwa siku kadhaa. Kisha nikainuka na nikaenda kufanya kazi za mfalme. Lakini nilikuwa nimetishwa sana na maono, na hapakuwa na mtu yeyote aliyeweza kuyaelewa.

< Daniel 8 >