< Daniel 2 >
1 In the secounde yeer of the rewme of Nabugodonosor, Nabugodonosor siy a dreem; and his spirit was aferd, and his dreem fledde awei fro hym.
Katika mwaka wa pili wa utawala wake, Nebukadneza aliota ndoto. Mawazo yake yakasumbuka na hakuweza kulala.
2 Therfor the kyng comaundide, that the dyuynours, and astronomyens, and witchis, and Caldeis schulden be clepid togidere, that thei schulden telle to the kyng hise dremys; and whanne thei weren comun, thei stoden bifor the king.
Hivyo mfalme akawaita waganga, wasihiri, wachawi na wanajimu ili wamwambie ndoto yake aliyokuwa ameota. Walipoingia ndani na kusimama mbele ya mfalme,
3 And the king seide to hem, Y siy a dreem, and Y am schent in mynde, and Y knowe not what Y siy.
akawaambia, “Niliota ndoto inayonisumbua, nami nataka nijue maana yake.”
4 And Caldeis answeriden the kyng bi Sirik langage, Kyng, liue thou with outen ende; seie thi dreem to thi seruauntis, and we schulen schewe to thee the expownyng therof.
Ndipo wanajimu wakamjibu mfalme kwa lugha ya Kiaramu, “Ee mfalme, uishi milele! Waambie watumishi wako hiyo ndoto, nasi tutaifasiri.”
5 And the kyng answeride, and seide to Caldeis, The word is goen awei fro me; if ye schewen not to me the dreem, and expownyng therof, ye schulen perische, and youre housis schulen be forfetid.
Mfalme akawajibu wanajimu, “Nimeamua hivi kwa uthabiti: Ikiwa hamtaniambia ndoto yangu ilikuwa ipi na kuifasiri, mtakatwa vipande vipande na nyumba zenu zitafanywa kuwa vifusi.
6 Forsothe if ye tellen the dreem, and the expownyng therof, ye schulen take of me meedis and yiftis, and myche onour; therfor schewe ye to me the dreem, and the interpretyng therof.
Lakini mkiniambia ndoto yangu na kuielezea, mtapokea kwangu zawadi, tuzo na heshima kubwa. Basi niambieni ndoto yangu na mnifasirie.”
7 Thei answeriden the secounde tyme, and seiden, The kyng seie the dreem to hise seruauntis, and we schulen schewe the interpretyng therof.
Wakajibu kwa mara nyingine, “Mfalme na awaambie watumishi wake ndoto yake, nasi tutaifasiri.”
8 The kyng answeride, and seide, Certis Y woot, that ye ayenbien the tyme, and witen that the word is goen awei fro me.
Ndipo mfalme akajibu, “Nina hakika kuwa mnajaribu kupata muda zaidi, kwa sababu mnatambua kuwa nimeamua hivi kwa uthabiti:
9 Therfor if ye schewen not to me the dreem, o sentence is of you, for ye maken an interpretyng bothe fals and ful of disseit, that ye speke to me til the tyme passe; therfor seie ye the dreem to me, that Y wite, that ye speke also the veri interpretyng therof.
Ikiwa hamtaniambia ndoto yangu, ipo adhabu moja tu kwenu. Mmefanya shauri kuniambia habari za kunipotosha na mambo maovu, mkitumaini kwamba hali itabadilika. Hivyo basi, niambieni hiyo ndoto, nami nitajua kuwa mwaweza kunifasiria.”
10 Therfor Caldeis answeriden bifor the kyng, and seiden, Kyng, no man is on erthe, that mai fille thi word; but nether ony greet man and myyti of kyngis axith siche a word of ony dyuynour, and astronomyen, and of a man of Caldee.
Wanajimu wakamjibu mfalme, “Hakuna mtu duniani ambaye anaweza kufanya analotaka mfalme! Vilevile hakuna mfalme hata awe mkuu na mwenye uweza namna gani, aliyeuliza kitu kama hicho kwa mganga au kwa msihiri, wala kwa mnajimu yeyote.
11 For the word which thou, kyng, axist, is greuouse, nether ony schal be foundun, that schal schewe it in the siyt of the king, outakun goddis, whos lyuyng is not with men.
Anachouliza mfalme ni kigumu mno. Hakuna yeyote awezaye kumfunulia mfalme isipokuwa miungu, nao hawaishi miongoni mwa wanadamu.”
12 And whanne this word was herd, the kyng comaundide, in woodnesse and in greet ire, that alle the wise men of Babiloyne schulden perische.
Jambo hili lilimkasirisha na kumghadhibisha mfalme mno hata kuagiza kuuawa kwa wenye hekima wote wa Babeli.
13 And bi the sentence goon out, the wise men weren slayn; and Danyel and hise felows weren souyt, that thei schulden perische.
Hivyo amri ikatolewa ya kuwaua wenye hekima, nao watu wakatumwa kuwatafuta Danieli na rafiki zake ili wawaue.
14 Thanne Danyel axide of the lawe and sentence, of Ariok, prynce of chyualrie of the kyng, that was gon out to sle the wise men of Babiloyne.
Wakati Arioko, mkuu wa askari wa walinzi wa mfalme, alikuwa amekwenda kuwaua watu wenye hekima wa Babeli, Danieli akazungumza naye kwa hekima na busara.
15 And he axide hym, that hadde take power of the kyng, for what cause so cruel a sentence yede out fro the face of the kyng. Therfor whanne Ariok hadde schewid the thing to Danyel,
Akamuuliza huyo afisa wa mfalme, “Kwa nini mfalme ametoa amri kali hivyo?” Ndipo Arioko akamweleza Danieli jambo hilo.
16 Danyel entride, and preyede the kyng, that he schulde yyue tyme to hym to schewe the soilyng to the kyng.
Aliposikia jambo hili, Danieli akamwendea mfalme, akamwomba ampe muda ili aweze kumfasiria ile ndoto.
17 And he entride in to his hous, and schewide the nede to Ananye, and to Misael, and Asarie,
Ndipo Danieli akarudi nyumbani kwake na kuwaeleza rafiki zake Hanania, Mishaeli na Azaria jambo hilo.
18 hise felowis, that thei schulden axe merci of the face of God of heuene on this sacrament; and that Danyel and hise felowis schulden not perische with othere wise men of Babiloyne.
Aliwasihi waombe rehema kutoka kwa Mungu wa mbinguni kuhusu siri hii, ili yeye na rafiki zake wasije wakauawa pamoja na wenye hekima wengine wa Babeli.
19 Thanne the priuyte was schewid to Danyel bi a visioun in nyyt. And Danyel blesside God of heuene, and seide,
Wakati wa usiku lile fumbo lilifunuliwa kwa Danieli katika maono. Ndipo Danieli akamhimidi Mungu wa mbinguni,
20 The name of the Lord be blessid fro the world, and til in to the world, for wisdom and strengthe ben hise;
na akasema: “Lihimidiwe jina la Mungu milele na milele; hekima na uweza ni vyake.
21 and he chaungith tymes and ages, he translatith rewmes and ordeyneth; he yyueth wisdom to wise men, and kunnyng to hem that vndurstonden techyng, ether chastisyng;
Yeye hubadili nyakati na majira; huwaweka wafalme na kuwaondoa. Huwapa hekima wenye hekima, na maarifa wenye ufahamu.
22 he schewith deepe thingis and hid, and he knowith thingis set in derknessis, and liyt is with hym.
Hufunua siri na mambo yaliyofichika; anajua yale yaliyo gizani, nayo nuru hukaa kwake.
23 God of oure fadris, Y knowleche to thee, and Y herie thee, for thou hast youe wisdom and strengthe to me; and now thou hast schewid to me tho thingis, whiche we preieden thee, for thou hast openyd to vs the word of the kyng.
Ninakushukuru na kukuhimidi, Ee Mungu wa baba zangu: Umenipa hekima na uwezo, umenijulisha kile tulichokuomba, umetujulisha ndoto ya mfalme.”
24 Aftir these thingis Danyel entride to Ariok, whom the kyng hadde ordeyned, that he schulde leese the wise men of Babiloyne, and thus he spak to hym, Leese thou not the wise men of Babiloyne; leede thou me in bifor the siyt of the kyng, and Y schal telle the soilyng to the kyng.
Ndipo Danieli akamwendea Arioko, ambaye mfalme alikuwa amemteua kuwaua wenye hekima wa Babeli, akamwambia, “Usiwaue wenye hekima wa Babeli. Nipeleke kwa mfalme, nami nitamfasiria ndoto yake.”
25 Thanne Ariok hastynge ledde in Danyel to the kyng, and seide to him, Y haue foundun a man of the sones of passyng ouer of Juda, that schal telle the soilyng to the kyng.
Arioko akampeleka Danieli kwa mfalme mara moja na kumwambia, “Nimempata mtu miongoni mwa watu wa uhamisho kutoka Yuda ambaye anaweza kumwambia mfalme maana ya ndoto yake.”
26 The kyng answeride, and seide to Danyel, to whom the name was Balthasar, Whethir gessist thou, that thou maist verili schewe to me the dreem which Y siy, and the interpretyng therof?
Mfalme akamuuliza Danieli (aliyeitwa pia Belteshaza), “Je, unaweza kuniambia nilichoona katika ndoto yangu na kuifasiri?”
27 And Danyel answeride bifore the king, and seide, The priuytee which the kyng axith, wise men, and astronomyens, and dyuynours, and lokeris of auteris, moun not schewe to the kyng.
Danieli akajibu, “Hakuna mwenye hekima, msihiri, mganga au mwaguzi anayeweza kumweleza mfalme siri aliyouliza,
28 But God is in heuene, that schewith priuytees, which hath schewid to thee, thou king Nabugodonosor, what thingis schulen come in the laste tymes. Thi dreem and visiouns of thin heed, in thi bed, ben sich.
lakini yuko Mungu mbinguni afunuaye siri. Amemwonyesha Mfalme Nebukadneza kitakachotokea siku zijazo. Ndoto yako na maono yaliyopita mawazoni mwako ulipokuwa umelala kitandani mwako ni haya:
29 Thou, kyng, bigunnest to thenke in thi bed, what was to comynge aftir these thingis; and he that schewith priuetees, schewide to thee what thingis schulen come.
“Ee mfalme, ulipokuwa umelala kitandani, yalikujia mawazo kuhusu mambo yatakayotokea baadaye, naye mfunuaji wa siri akakuonyesha ni kitu gani kitakachotokea.
30 And this sacrament is schewid to me, not bi wisdom which is in me more than in alle lyuynge men, but that the interpretyng schulde be maad opyn to the kyng, and thou schuldist knowe the thouytis of thi soule.
Kwangu mimi, nimefunuliwa siri hii, si kwa sababu nina hekima kubwa kuliko watu wengine wanaoishi, bali ni ili wewe, ee mfalme, upate kujua tafsiri, na ili uweze kuelewa kile kilichopita mawazoni mwako.
31 Thou, kyng, siyest, and lo! as o greet ymage; thilke ymage was greet, and hiy in stature, and stood bifore thee, and the loking therof was ferdful.
“Ee mfalme, ulitazama, na mbele yako ilisimama sanamu kubwa, kubwa mno kupita kiasi, sanamu iliyongʼaa na kutisha kwa kuonekana kwake.
32 The heed of this ymage was of best gold, but the brest and armes weren of siluer; certis the wombe and thies weren of bras,
Kichwa cha ile sanamu kilikuwa kimetengenezwa kwa dhahabu safi, kifua chake na mikono yake vilikuwa vya fedha, tumbo lake na mapaja yake vilikuwa vya shaba,
33 but the leggis weren of irun; forsothe sum part of the feet was of irun, sum was of erthe.
miguu yake ilikuwa ya chuma, na nyayo zake zilikuwa chuma nazo sehemu nyingine zilikuwa udongo wa mfinyanzi uliochomwa.
34 Thou siyest thus, til a stoon was kit doun of the hil, with outen hondis, and smoot the ymage in the irun feet therof and erthene feet, and al to-brak tho.
Ulipokuwa unaangalia, jiwe lilikatwa, lakini si kwa mikono ya mwanadamu. Lile jiwe liliipiga ile sanamu kwenye nyayo zake za chuma na udongo wa mfinyanzi, na kuivunja.
35 Thanne the irun, tijl stoon, ether erthene vessel, bras, siluer, and gold, weren al to-brokun togidere, and dryuun as in to a deed sparcle of a large somer halle, that ben rauyschid of wynd, and no place is foundun to tho; forsothe the stoon, that smoot the ymage, was maad a greet hil, and fillide al erthe.
Ndipo ile chuma, ule udongo wa mfinyanzi, ile shaba, ile fedha na ile dhahabu vikavunjika vipande vipande kwa wakati mmoja, na vikawa kama makapi katika sakafu ya kupuria nafaka wakati wa kiangazi. Upepo ukavipeperusha bila kuacha hata alama. Lakini lile jiwe lililoipiga ile sanamu likawa mlima mkubwa mno na kuijaza dunia yote.
36 This is the dreem. Also, thou kyng, we schulen seie bifor thee the interpretyng therof.
“Hii ndiyo iliyokuwa ndoto, nasi sasa tutamfasiria mfalme.
37 Thou art kyng of kyngis, and God of heuene yaf to thee rewme, strengthe, and empire, and glorie;
Ee mfalme, wewe ni mfalme wa wafalme. Mungu wa mbinguni amekupa wewe utawala, uweza, nguvu na utukufu.
38 and he yaf in thin hond alle thingis, in whiche the sones of men, and the beestis of the feeld, and the briddis of the eir dwellen, and ordeynede alle thingis vndur thi lordschip; therfor thou art the goldun heed.
Mikononi mwako amewaweka wanadamu, wanyama wa kondeni, na ndege wa angani. Popote waishipo amekufanya wewe kuwa mtawala juu yao wote. Wewe ndiye kile kichwa cha dhahabu.
39 And another rewme lesse than thou schal rise aftir thee; and the thridde rewme, an other of bras, that schal haue the empire of al erthe.
“Baada yako, ufalme mwingine utainuka, ulio dhaifu kuliko wako. Baadaye utafuata ufalme wa tatu, ule wa shaba, nao utatawala juu ya dunia yote.
40 And the fourthe rewme schal be as irun, as irun makith lesse, and makith tame alle thingis, so it schal make lesse, and schal al to-breke alle these rewmes.
Hatimaye, kutakuwako na ufalme wa nne, wenye nguvu kama chuma, kwa maana chuma huvunja na kupondaponda kila kitu; kama vile chuma ivunjavyo vitu vipande vipande, ndivyo ufalme huo utakavyopondaponda na kuvunjavunja nyingine zote.
41 Forsothe that thou siest a part of the feet and fyngris of erthe of a pottere, and a part of irun, the rewme shal be departid; which netheles schal rise of the plauntyng of irun, `bi that that thou siest irun meynd with a tijl stoon of clei,
Kama vile ulivyoona kuwa kwa sehemu nyayo na vidole vilikuwa vya udongo wa mfinyanzi uliochomwa na kwa sehemu nyingine chuma, hivyo huu utakuwa ufalme uliogawanyika; hata hivyo utakuwa na sehemu zenye nguvu za chuma ndani yake, kama vile ulivyoona chuma imechanganywa na udongo wa mfinyanzi.
42 and the toos of the feet in parti of irun, and in parti of erthe, in parti the rewme schal be sad, and in parti to-brokun.
Kama vile vidole vyake vya miguu vilikuwa kwa sehemu chuma na sehemu udongo wa mfinyanzi, hivyo ufalme huo kwa sehemu utakuwa na nguvu na kwa sehemu udhaifu.
43 Forsothe that thou siest irun meynd with a tiel stoon of clei, sotheli tho schulen be meynd togidere with mannus seed; but tho schulen not cleue to hem silf, as irun mai not be meddlid with tyel stoon.
Kama vile ulivyoona chuma kikiwa kimechanganyikana na udongo wa mfinyanzi uliochomwa, ndivyo watu watakavyokuwa mchanganyiko, wala hawatabaki wameungana tena, kama vile chuma kisivyoweza kuchanganyikana na udongo wa mfinyanzi.
44 Forsothe in the daies of tho rewmes, God of heuene shal reise a rewme, that schal not be distried with outen ende, and his rewme schal not be youun to another puple; it schal make lesse, and schal waste alle these rewmes, and it schal stonde with outen ende,
“Katika siku za wafalme hao, Mungu wa mbinguni atauweka ufalme ambao kamwe hautaangamizwa, wala hautaachiwa taifa jingine. Utaziponda zile falme zote na kuzikomesha, bali wenyewe utadumu milele.
45 bi this that thou siest, that a stoon was kit doun of the hil with outen hondis, and maad lesse the tiel stoon, and irun, and bras, and siluer, and gold. Greet God hath schewid to the kyng, what thingis schulen come aftirward; and the dreem is trewe, and the interpretyng therof is feithful.
Hii ndiyo maana ya maono ya jiwe lililochongwa kutoka mlimani, lakini si kwa mikono ya mwanadamu, lile jiwe ambalo lilivunja chuma, shaba, udongo wa mfinyanzi, fedha na dhahabu vipande vipande. “Mungu Mkuu amemwonyesha mfalme kile kitakachotokea wakati ujao. Ndoto hii ni ya kweli na tafsiri yake ni ya kuaminika.”
46 Thanne king Nabugodonosor felle doun on his face, and worschipide Danyel, and comaundide sacrifices and encense to be brouyt, that tho schulden be sacrifised to hym.
Ndipo Mfalme Nebukadneza akaanguka kifudifudi mbele ya Danieli kumpa heshima, akaagiza wamtolee Danieli sadaka na uvumba.
47 Therfor the kyng spak, and seide to Danyel, Verili youre God is God of goddis, and Lord of kyngis, that schewith mysteries, for thou miytist opene this sacrament.
Mfalme akamwambia Danieli, “Hakika Mungu wako ni Mungu wa miungu, na Bwana wa wafalme, na mfunuaji wa siri zote, kwa maana umeweza kufunua siri hii.”
48 Thanne the kyng reiside Danyel an hiy, and yaf many yiftis and grete to hym; and ordeynede hym prince and prefect, ether cheef iustise, ouer alle the prouynces of Babiloyne, and maister ouer alle the wise men of Babiloyne.
Ndipo mfalme akamweka Danieli nafasi ya juu, na kumpa zawadi nyingi tele. Akamfanya kuwa mtawala wa jimbo lote la Babeli, na kumweka kuwa mkuu wa wenye hekima wote.
49 Forsothe Danyel axide of the kyng, and ordeynede Sidrac, Misaac, and Abdenago ouer alle the werkis of the prouynce of Babiloyne; but Danyel hym silf was in the yatis of the kyng.
Zaidi ya hayo, kwa ombi la Danieli, mfalme akawateua Shadraki, Meshaki na Abednego kuwa wasimamizi wa jimbo la Babeli, huku Danieli akibaki katika ukumbi wa mfalme.