< Colossians 2 >

1 But Y wole that ye wite, what bisynesse Y haue for you, and for hem that ben at Laodice, and whiche euere saien not my face in fleisch,
Nataka mjue jinsi ninavyojitaabisha kwa ajili yenu na kwa ajili ya wale walioko Laodikia, na pia kwa ajili ya wote ambao hawajapata kuniona mimi binafsi.
2 that her hertis ben coumfortid, and thei ben tauyt in charite, in to alle the richessis of the plente of the vndurstondyng, in to the knowyng of mysterie of God, the fadir of Jhesu Crist,
Kusudi langu ni watiwe moyo na kuunganishwa katika upendo, ili wapate ule utajiri wa ufahamu mkamilifu, ili waijue siri ya Mungu, yaani, Kristo mwenyewe,
3 in whom alle the tresouris of wisdom and of science ben hid.
ambaye ndani yake kumefichwa hazina zote za hekima na maarifa.
4 For this thing Y seie, that no man disseyue you in heiythe of wordis.
Nawaambia mambo haya ili mtu yeyote asiwadanganye kwa maneno ya kuwashawishi.
5 For thouy Y be absent in bodi, bi spirit Y am with you, ioiynge and seynge youre ordre and the sadnesse of youre bileue that is in Crist.
Kwa kuwa ingawa mimi siko pamoja nanyi kimwili, lakini niko pamoja nanyi kiroho, nami nafurahi kuuona utaratibu wenu na jinsi uthabiti wa imani yenu katika Kristo ulivyo.
6 Therfor as ye han takun Jhesu Crist oure Lord,
Hivyo basi, kama vile mlivyompokea Kristo Yesu kuwa Bwana, endeleeni kukaa ndani yake,
7 walke ye in hym, and be ye rootid and bieldid aboue in hym, and confermyd in the bileue, as ye han lerud, aboundinge in hym in doynge of thankyngis.
mkiwa na mizizi, na mmejengwa ndani yake, mkiimarishwa katika imani kama mlivyofundishwa, na kufurika kwa wingi wa shukrani.
8 Se ye that no man disseyue you bi filosofie and veyn fallace, aftir the tradicioun of men, aftir the elementis of the world, and not aftir Crist.
Angalieni mtu yeyote asiwafanye ninyi mateka kwa elimu batili na madanganyo matupu yanayotegemea mapokeo ya wanadamu na mafundisho ya ulimwengu badala ya Kristo.
9 For in hym dwellith bodilich al the fulnesse of the Godhed.
Maana ukamilifu wote wa Uungu umo ndani ya Kristo katika umbile la mwili wa kibinadamu,
10 And ye ben fillid in hym, that is heed of al principat and power.
nanyi mmepewa ukamilifu ndani ya Kristo, ambaye ndiye mkuu juu ya kila enzi na kila mamlaka.
11 In whom also ye ben circumcidid in circumcisioun not maad with hoond, in dispoyling of the bodi of fleisch, but in circumcisioun of Crist;
Katika Kristo pia mlitahiriwa kwa kutengwa mbali na asili ya dhambi, si kwa tohara inayofanywa kwa mikono ya wanadamu, bali kwa ile tohara iliyofanywa na Kristo,
12 and ye ben biried togidere with hym in baptim, in whom also ye han rise ayen bi feith of the worching of God, that reiside hym fro deth.
mkiwa mmezikwa pamoja naye katika ubatizo, na kufufuliwa pamoja naye kwa njia ya imani yenu katika uweza wa Mungu, aliyemfufua kutoka kwa wafu.
13 And whanne ye weren deed in giltis, and in the prepucie of youre fleisch, he quikenyde togidere you with hym;
Mlipokuwa wafu katika dhambi zenu na kutokutahiriwa katika asili yenu ya dhambi, Mungu aliwafanya mwe hai pamoja na Kristo. Alitusamehe dhambi zetu zote,
14 foryyuynge to you alle giltis, doynge awei that writing of decre that was ayens vs, that was contrarie to vs; and he took awei that fro the myddil, pitchinge it on the cros;
akiisha kuifuta ile hati yenye mashtaka yaliyokuwa yanatukabili, pamoja na maagizo yake. Aliiondoa isiwepo tena, akiigongomea kwenye msalaba wake.
15 and he spuylide principatis and poweris, and ledde out tristili, opynli ouercomynge hem in hym silf.
Mungu akiisha kuzivua enzi na mamlaka, alizifanya kuwa kitu cha fedheha hadharani kwa kuziburura kwa ujasiri, akizishinda katika msalaba wa Kristo.
16 Therfor no man iuge you in mete, or in drink, or in part of feeste dai, or of neomenye,
Kwa hiyo mtu asiwahukumu ninyi kuhusu vyakula au vinywaji, au kuhusu kuadhimisha sikukuu za dini, au Sikukuu za Mwezi Mwandamo au siku ya Sabato.
17 or of sabatis, whiche ben schadewe of thingis to comynge; for the bodi is of Crist.
Hizi zilikuwa kivuli cha mambo ambayo yangekuja, lakini ile iliyo halisi imo ndani ya Kristo.
18 No man disseyue you, willynge to teche in mekenesse, and religioun of aungelis, tho thingis whiche he hath not seyn, walkinge veynli, bolnyd with wit of his fleisch,
Mtu yeyote asiwaondolee thawabu yenu kwa kusisitiza kunyenyekea kwake na kuabudu malaika. Mtu kama huyo hudumu katika maono yake, akijivuna bila sababu katika mawazo ya kibinadamu.
19 and not holdynge the heed, of which al the bodi, bi boondis and ioynyngis togidere vndur mynystrid and maad, wexith in to encreessing of God.
Yeye amepoteza ushirikiano na Kichwa, ambaye kutoka kwake mwili wote unalishwa na kushikamanishwa pamoja kwa viungo na mishipa, nao hukua kwa ukuaji utokao kwa Mungu.
20 For if ye ben deed with Crist fro the elementis of this world, what yit as men lyuynge to the world demen ye?
Kwa kuwa mlikufa pamoja na Kristo, mkayaacha yale mafundisho ya msingi ya ulimwengu huu, kwa nini bado mnaishi kama ninyi ni wa ulimwengu? Kwa nini mnajitia chini ya amri:
21 That ye touche not, nether taaste,
“Msishike! Msionje! Msiguse!”?
22 nether trete with hoondis tho thingis, whiche alle ben in to deth bi the ilke vss, aftir the comaundementis and the techingis of men;
Haya yote mwisho wake ni kuharibika yanapotumiwa, kwa sababu msingi wake ni katika maagizo na mafundisho ya wanadamu.
23 whiche han a resoun of wisdom in veyn religioun and mekenesse, and not to spare the bodi, not in ony onour to the fulfillyng of the fleisch.
Kwa kweli amri kama hizo huonekana kama zina hekima, katika namna za ibada walizojitungia wenyewe, na unyenyekevu wa uongo na kuutawala mwili kwa ukali, lakini hayafai kitu katika kuzuia tamaa za mwili.

< Colossians 2 >