< Amos 1 >

1 The wordis of Amos ben these, that was in the schepherdis thingis of Thecue, whiche he siy on Israel, in the daies of Osie, king of Juda, and in the daies of Jeroboam, sone of Joas, kyng of Israel, bifor twei yeeris of the erthe mouynge.
Maneno ya Amosi, mmoja wa wachunga wanyama wa Tekoa: yale aliyoyaona kuhusu Israeli miaka miwili kabla ya tetemeko la ardhi, wakati Uzia alikuwa mfalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yehoashi alikuwa mfalme wa Israeli.
2 And he seide, The Lord schal rore fro Sion, and schal yyue his vois fro Jerusalem; and the faire thingis of schepherdis mourenyden, and the cop of Carmele was maad drie.
Alisema: “Bwana ananguruma toka Sayuni, pia ananguruma kutoka Yerusalemu; malisho ya wachunga wanyama yanakauka, kilele cha Karmeli kinanyauka.”
3 The Lord seith these thingis, On thre grete trespassis of Damask, and on foure, I shal not conuerte it, for it threischide Galaad in irun waynes.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Dameski, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu aliipura Gileadi kwa vyombo vya chuma vyenye meno.
4 And Y schal sende fier in to the hous of Asael, and it schal deuoure the housis of Benadab.
Nitatuma moto juu ya nyumba ya Hazaeli ambao utateketeza ngome za Ben-Hadadi.
5 And Y schal al to-breke the barre of Damask, and Y schal leese a dwellere fro the feeld of idol, and hym that holdith the ceptre fro the hous of lust and of letcherie; and the puple of Sirie schal be translatid to Sirenen, seith the Lord.
Nitalivunja lango la Dameski; nitamwangamiza mfalme aliyeko katika Bonde la Aveni, na yeye ambaye anaishika fimbo ya utawala katika Beth-Edeni. Watu wote wa Aramu watakwenda uhamishoni huko Kiri,” asema Bwana.
6 The Lord seith these thingis, On thre grete trespassis of Gasa, and on foure, Y schal not conuerte it, for it translatide perfit caitifte, to close that togidere in Idumee.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Gaza, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu walichukua mateka jumuiya nzima na kuwauza kwa Edomu,
7 And Y schal sende fier in to the wal of Gasa, and it schal deuoure the housis therof.
nitatuma moto juu ya kuta za Gaza ambao utateketeza ngome zake.
8 And Y schal leese the dwelleris of Azotus, and hym that holdith the ceptre of Ascalon; and Y schal turne myn hond on Accaron, and the remenauntis of Filisteis schulen perische, seith the Lord God.
Nitamwangamiza mfalme wa Ashdodi na yeye aishikaye fimbo ya utawala katika Ashkeloni. Nitaugeuza mkono wangu dhidi ya Ekroni, hadi Mfilisti wa mwisho atakapokufa,” asema Bwana Mwenyezi.
9 The Lord God seith these thingis, On thre grete trespassis of Tire, and on foure, Y schal not conuerte it, for thei closiden togidere perfit caitifte in Idumee, and hadde not mynde on the boond of pees of britheren.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Tiro, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu ameuza jumuiya nzima ya mateka kwa Edomu, na kutokujali mapatano ya undugu,
10 And Y schal sende fier in to the wal of Tire, and it schal deuoure the housis therof.
Nitatuma moto kwenye kuta za Tiro ambao utateketeza ngome zake.”
11 The Lord seith these thingis, On thre grete trespassis of Edom, and on foure, Y schal not conuerte it, for it pursuede bi swerd his brother, and defoulide the merci of hym, and helde ferthere his woodnesse, and kepte his indignacioun `til in to the ende.
Hili ndilo Bwana asemalo: “Kwa dhambi tatu za Edomu, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu alimfuatia ndugu yake kwa upanga, alikataa kuonyesha huruma yoyote, kwa sababu hasira yake kali iliendelea kupanda wakati wote na ghadhabu iliwaka bila kuzuiliwa.
12 Y schal sende fier in to Theman, and it schal deuoure the housis of Bosra.
Nitatuma moto juu ya Temani ambao utateketeza ngome za Bosra.”
13 The Lord seith these thingis, On thre grete trespassis of the sones of Amon, and on foure, Y schal not conuerte hym, for he karf the wymmen with childe of Galaad, for to alarge his terme.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Amoni, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu aliwatumbua wanawake wajawazito wa Gileadi ili kuongeza mipaka yake.
14 And Y schal kyndle fier in the wal of Rabbe, and it schal deuoure the housis therof, in yellyng in the dai of batel, and in whirlwynd in the dai of mouyng togidere.
Nitatuma moto kwenye kuta za Raba ambao utateketeza ngome zake katikati ya vilio vya vita katika siku ya mapigano, katikati ya upepo mkali katika siku ya dhoruba.
15 And Melchon schal go in to caitifte, he and hise princes togidere, seith the Lord.
Mfalme wake atakwenda uhamishoni, yeye pamoja na maafisa wake,” asema Bwana.

< Amos 1 >