< Acts 28 >

1 And whanne we hadden ascapid, thanne we knewen that the ile was clepid Militene. And the hethene men diden to vs not litil curtesie.
Tulipokwisha fika salama kwenye nchi kavu, tuligundua kwamba kile kisiwa kinaitwa Malta.
2 And whanne a fier was kyndelid, thei refreschiden vs alle, for the reyn that cam, and the coold.
Wenyeji wa hapo walikuwa wema sana kwetu. Mvua ilikuwa inaanza kunyesha na kulikuwa na baridi, hivyo waliwasha moto, wakatukaribisha.
3 But whanne Poul hadde gederid `a quantite of kittingis of vines, and leide on the fier, an edder sche cam forth fro the heete, and took hym bi the hoond.
Paulo aliokota mzigo mdogo wa kuni akawa anazitia motoni. Hapo, kwa sababu ya lile joto la moto, nyoka akatoka katika kuni akamnasa Paulo mkononi na kujishikilia hapo.
4 And whanne the hethene men of the ile siyen the beest hangynge in his hoond, thei seiden togidir, For this man is a manquellere; and whanne he scapide fro the see, Goddis veniaunce suffrith hym not to lyue in erthe.
Wenyeji wa pale walipokiona kile kiumbe kinaning'inia kwenye mkono wake waliambiana, “Bila shaka mtu huyu amekwisha ua mtu, na ingawa ameokoka kuangamia baharini, Haki haitamwacha aendelee kuishi!”
5 But he schoke awei the beest in to the fier, and hadde noon harm.
Lakini Paulo alikikung'utia kile kiumbe motoni na hakuumizwa hata kidogo.
6 And thei gessiden that he schulde be turned `in to swellyng, and falle doun sudenli, and die. But whanne thei abiden longe, and sien that no thing of yuel was don in him, thei turneden hem togider, and seiden, that he was God.
Wale watu walikuwa wakitazamia kwamba angevimba au hapohapo angeanguka chini na kufa. Baada ya kungojea kwa muda mrefu bila kuona kwamba Paulo amepatwa na jambo lolote lisilo la kawaida, walibadilisha fikira zao juu yake, wakasema kuwa ni mungu.
7 And in tho placis weren maners of the prince of the ile, Puplius bi name, which resseyuede vs bi thre daies benygnli, and foond vs.
Karibu na mahali pale palikuwa na mashamba ya Publio, mkuu wa kile kisiwa. Publio alitukaribisha kirafiki, tukawa wageni wake kwa siku tatu.
8 And it bifel, that the fader of Pupplius lai trauelid with fyueris and blodi flux. To whom Poul entride, and whanne he hadde preied, and leid his hondis on hym, he helide hym.
Basi, ikawa kwamba baba yake Publio alikuwa amelala kitandani, mgonjwa, ana homa na kuhara. Paulo alikwenda kumwona na baada ya kusali, akaweka mikono yake juu ya mgonjwa, akamponya.
9 And whanne this thing was don, alle that in the ile hadden sijknesses, camen, and weren heelid.
Kutokana na tukio hilo, wagonjwa wote katika kile kisiwa walikuja wakaponywa.
10 Which also onouriden vs in many worschipis, and puttiden what thingis weren necessarie to vs, whanne we schippiden.
Watu walitupatia zawadi mbalimbali na wakati tulipoanza tena safari, walitia ndani ya meli masurufu tuliyohitaji.
11 And after thre monethis we schippiden in a schip of Alisaundre, that hadde wyntrid in the ile, to which was an excellent singne of Castours.
Baada ya miezi mitatu tulianza tena safari yetu kwa meli moja ya Aleksandria iitwayo “Miungu Pacha”. Meli hiyo ilikuwa imetia nanga kisiwani wakati wote wa baridi.
12 And whanne we camen to Siracusan, we dwelliden there thre daies.
Tulifika katika mji wa Sirakusa, tukakaa hapo kwa siku tatu.
13 Fro thennus we seiliden aboute, and camen to Regyum; and aftir oo dai, while the south blew, in the secounde dai we camen to Puteolos.
Toka huko tuling'oa nanga, tukazunguka na kufika Regio. Baada ya siku moja, upepo ulianza kuvuma kutoka kusini, na baada ya siku mbili tulifika bandari ya Potioli.
14 Where whanne we founden britheren, we weren preied to dwelle there anentis hem seuene daies. And so we camen to Rome.
Huko tuliwakuta ndugu kadhaa ambao walituomba tukae nao kwa juma moja. Hivi ndivyo tulivyopata kufika Roma.
15 And fro thennus whanne britheren hadden herd, thei camen to vs to the cheping of Appius, and to the Thre tauernes.
Ndugu wa kule Roma walipopata habari zetu, wakaja kutulaki kwenye soko la Apio na Mikahawa Mitatu. Paulo alipowaona alimshukuru Mungu, akapata moyo.
16 And whanne Poul hadde seyn hem, he dide thankyngis to God, and took trist. And whanne `we camen to Rome, it was suffrid to Poul to dwelle bi hym silf, with a kniyt kepinge him.
Tulipofika Roma, Paulo aliruhusiwa kukaa peke yake pamoja na askari mmoja wa kumlinda.
17 And after the thridde dai, he clepide togidir the worthieste of the Jewis. And whanne thei camen, he seide to hem, Britheren, Y dide no thing ayens the puple ether custom of fadris, and Y was boundun at Jerusalem, and was bitakun in to the hondis of Romayns.
Baada ya siku tatu, Paulo aliwaita pamoja viongozi wa Kiyahudi wa mahali hapo. Walipokusanyika, Paulo aliwaambia, “Wananchi wenzangu, mimi, ingawa sikufanya chochote kibaya wala kupinga desturi za wazee wetu, nilitiwa nguvuni kule Yerusalemu na kutiwa mikononi mwa Waroma.
18 And whanne thei hadden axid of me, wolden haue delyuerid me, for that no cause of deth was in me.
Waliponihoji na kuona kwamba sikuwa na hatia yeyote, walitaka kuniacha.
19 But for Jewis ayenseiden, Y was constreyned to appele to the emperour; not as hauynge ony thing to accuse my puple.
Lakini Wayahudi wengine walipinga jambo hilo, nami nikalazimika kukata rufani kwa Kaisari, ingawa sikuwa na chochote cha kuwashtaki wananchi wenzangu.
20 Therfor for this cause Y preiede to se you, and speke to you; for for the hope of Israel Y am gird aboute with this chayne.
Ni kwa sababu hiyo nimeomba kuonana na kuongea nanyi, maana nimefungwa minyororo hii kwa sababu ya tumaini lile la Israeli.”
21 And thei seiden to hym, Nether we han resseyued lettris of thee fro Judee, nether ony of britheren comynge schewide, ether spak ony yuel thing of thee.
Wao wakamwambia, “Sisi hatujapokea barua yoyote kutoka Yudea, wala hakuna ndugu yeyote aliyefika hapa na kutoa habari rasmi au kusema chochote kibaya juu yako.
22 But we preyen to here of thee, what thingis thou felist; for of this sect it is knowun to vs, that euerywhere me ayenseith it.
Lakini tunafikiri inafaa tusikie kutoka kwako mwenyewe mambo yaliyo kichwani mwako. Kwa maana tujualo sisi kuhusu hicho kikundi ni kwamba kinapingwa kila mahali.”
23 And whanne thei hadden ordeined a dai to hym, many men camen to hym in to the in. To whiche he expownede, witnessinge the kyngdom `of God, and counseilide hem of Jhesu, of the lawe of Moyses, and profetis, for the morewe til to euentid.
Basi, walipanga naye siku kamili ya kukutana, na wengi wakafika huko alikokuwa anakaa. Tangu asubuhi mpaka jioni Paulo aliwaeleza na kuwafafanulia juu ya Ufalme wa Mungu akijaribu kuwafanya wakubali habari juu ya Yesu kwa kutumia Sheria ya Mose na maandiko ya manabii.
24 And summe bileueden to these thingis that weren seid of Poul, summe bileueden not.
Baadhi yao walikubali maneno yake, lakini wengine hawakuamini.
25 And whanne thei weren not consentinge togidir, thei departiden. And Poul seide o word, For the Hooli Goost spak wel bi Ysaye, the profete, to oure fadris,
Basi, kukawa na mtengano wa fikira kati yao. Walipokuwa wanakwenda zao, Paulo alisema jambo hili, “Kweli ni sawa yale aliyoyanena Roho Mtakatifu kwa wazee wenu kwa njia ya nabii Isaya
26 and seide, Go thou to this puple, and seie to hem, With eere ye schulen here, and ye schulen not vndirstonde; and ye seynge schulen se, and ye schulen not biholde.
akisema: Nenda kwa watu hawa ukawaambie: kusikia mtasikia, lakini hamtaelewa; kutazama mtatazama, lakini hamtaona.
27 For the herte of this puple is greetli fattid, and with eeris thei herden heuyli, and thei closiden togider her iyen, lest perauenture thei se with iyen, and with eeris here, and bi herte vndurstonde, and be conuertid, and Y hele hem.
Maana akili za watu hawa zimepumbaa, wameziba masikio yao, wamefumba macho yao. La sivyo, wangeona kwa macho yao, wangesikia kwa masikio yao. Wangeelewa kwa akili zao, na kunigeukia, asema Bwana, nami ningewaponya.”
28 Therfor be it knowun to you, that this helthe of God is sent to hethen men, and thei schulen here.
Halafu Paulo akamaliza na kusema, “Jueni basi, kwamba ujumbe wa Mungu juu ya wokovu umepelekwa kwa watu wa mataifa. Wao watasikiliza!”
29 And whanne he hadde seid these thingis, Jewis wenten out fro hym, and hadden myche questioun, ethir musyng, among hem silf.
Paulo alipokwisha sema hayo, Wayahudi walijiondokea huku wakiwa wanabishana vikali wao kwa wao.
30 And he dwellide ful twei yeer in his hirid place; and he resseyuede alle that entryden to hym,
Kwa muda wa miaka miwili mizima Paulo aliishi katika nyumba aliyoipanga yeye mwenyewe; akawa anawakaribisha wote waliofika kumsalimu.
31 and prechide the kingdom of God, and tauyte tho thingis that ben of the Lord Jhesu Crist, with al trist, with out forbedyng. Amen.
Alikuwa akihubiri Ufalme wa Mungu na kufundisha juu ya Bwana Yesu Kristo kwa uhodari, bila kizuizi.

< Acts 28 >