< Acts 2 >
1 And whanne the daies of Pentecost weren fillid, alle the disciplis weren togidre in the same place.
Siku ya Pentekoste ilipowadia, waamini wote walikuwa mahali pamoja.
2 And sodeynli ther was maad a sown fro heuene, as of a greet wynde comynge, and it fillide al the hous where thei saten.
Ghafula sauti kama mvumo mkubwa wa upepo mkali uliotoka mbinguni ukaijaza nyumba yote walimokuwa wameketi.
3 And diuerse tungis as fier apperiden to hem, and it sat on ech of hem.
Zikatokea ndimi kama za moto zilizogawanyika na kukaa juu ya kila mmoja wao.
4 And alle weren fillid with the Hooli Goost, and thei bigunnen to speke diuerse langagis, as the Hooli Goost yaf to hem for to speke.
Wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, wakaanza kunena kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia.
5 And ther weren in Jerusalem dwellinge Jewis, religiouse men, of ech nacioun that is vndur heuene.
Basi walikuwepo Yerusalemu Wayahudi wanaomcha Mungu kutoka kila taifa chini ya mbingu.
6 And whanne this vois was maad, the multitude cam togidere, and thei weren astonyed in thouyt, for ech man herde hem spekinge in his langage.
Waliposikia sauti hii, umati wa watu ulikusanyika pamoja wakistaajabu, kwa sababu kila mmoja wao aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe.
7 And alle weren astonyed, and wondriden, and seiden togidere, Whether not alle these that speken ben men of Galyle,
Wakiwa wameshangaa na kustaajabu wakauliza, “Je, hawa wote wanaozungumza si Wagalilaya?
8 and hou herden we ech man his langage in which we ben borun?
Imekuwaje basi kila mmoja wetu anawasikia wakinena kwa lugha yake ya kuzaliwa?
9 Parthi, and Medi, and Elamyte, and thei that dwellen at Mesopotami, Judee, and Capodosie, and Ponte,
Wapathi, Wamedi, Waelami, wakazi wa Mesopotamia, Uyahudi, Kapadokia, Ponto na Asia,
10 and Asie, Frigie, and Pamfilie, Egipt, and the parties of Libie, that is aboue Sirenen, and `comelingis Romayns, and Jewis,
Frigia, Pamfilia, Misri na pande za Libya karibu na Kirene na wageni kutoka Rumi,
11 and proselitis, men of Crete, and of Arabie, we han herd hem spekynge in oure langagis the grete thingis of God.
Wayahudi na waongofu, Wakrete na Waarabu, sote tunawasikia watu hawa wakisema mambo makuu ya ajabu ya Mungu katika lugha zetu wenyewe.”
12 And alle weren astonyed, and wondriden, `and seiden togidere, What wole this thing be?
Wakiwa wameshangaa na kufadhaika wakaulizana, “Ni nini maana ya mambo haya?”
13 And othere scorneden, and seiden, For these men ben ful of must.
Lakini wengine wakawadhihaki wakasema, “Hawa wamelewa divai!”
14 But Petre stood with the enleuene, and reiside vp his vois, and spak to hem, Ye Jewis, and alle that dwellen at Jerusalem, be this knowun to you, and with eris perseyue ye my wordis.
Ndipo Petro akasimama pamoja na wale mitume kumi na mmoja, akainua sauti yake na kuhutubia ule umati wa watu, akasema: “Wayahudi wenzangu na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, jueni jambo hili mkanisikilize.
15 For not as ye wenen, these ben dronkun, whanne it is the thridde our of the dai;
Hakika watu hawa hawakulewa kama mnavyodhania, kwa kuwa sasa ni saa tatu asubuhi!
16 but this it is, that was seid bi the prophete Johel,
La, hili ni jambo lililotabiriwa na nabii Yoeli, akisema:
17 And it schal be in the laste daies, the Lord seith, Y schal helde out my spirit on ech fleisch; and youre sones and youre douytris schulen prophesie, and youre yonge men schulen se visiouns, and youre eldris schulen dreme sweuenes.
“‘Katika siku za mwisho, asema Mungu, nitamimina Roho wangu juu ya wote wenye mwili. Wana wenu na binti zenu watatabiri, vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota ndoto.
18 And on my seruauntis and myn handmaidens in tho daies Y schal schede out of my spirit, and thei schulen prophecie.
Hata juu ya watumishi wangu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile nitamimina Roho wangu, nao watatabiri.
19 And Y schal yyue grete wondris in heuene aboue, and signes in erthe bynethe, blood, and fier, and heete of smoke.
Nami nitaonyesha maajabu juu mbinguni, na ishara chini duniani: damu, moto, na mawimbi ya moshi.
20 The sunne schal be turned in to derknessis, and the moone in to blood, bifor that the greet and the opyn dai of the Lord come.
Jua litakuwa giza na mwezi utakuwa mwekundu kama damu, kabla ya kuja siku ile kuu ya Bwana iliyo tukufu.
21 And it schal be, ech man which euere schal clepe to help the name of the Lord, schal be saaf.
Na kila mtu atakayeliitia jina la Bwana, ataokolewa.’
22 Ye men of Israel, here ye these wordis. Jhesu of Nazareth, a man preued of God bifor you bi vertues, and wondris, and tokenes, which God dide bi hym in the myddil of you,
“Enyi Waisraeli, sikilizeni maneno haya nisemayo: Yesu wa Nazareti alikuwa mtu aliyethibitishwa kwenu na Mungu kwa miujiza, maajabu na ishara, ambayo Mungu alitenda miongoni mwenu kupitia kwake, kama ninyi wenyewe mjuavyo.
23 as ye witen, ye turmentiden, and killiden hym bi the hoondis of wyckid men, bi counseil determyned and bitakun bi the forknouwyng of God.
Huyu mtu akiisha kutolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa kwa kujua kwake Mungu tangu zamani, ninyi, kwa mikono ya watu wabaya, mlimuua kwa kumgongomea msalabani.
24 Whom God reiside, whanne sorewis of helle weren vnboundun, bi that that it was impossible that he were holdun of it.
Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu akamwondolea uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana yeye kushikiliwa na nguvu za mauti.
25 For Dauid seith of hym, Y saiy afer the Lord bifore me euermore, for he is on my riythalf, that Y be not mouyd.
Kwa maana Daudi asema kumhusu yeye: “‘Nalimwona Bwana mbele yangu daima. Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume, sitatikisika.
26 For this thing myn herte ioiede, and my tunge made ful out ioye, and more ouere my fleisch schal reste in hope.
Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao utapumzika kwa tumaini.
27 For thou schalt not leeue my soule in helle, nethir thou schalt yiue thin hooli to se corrupcioun. (Hadēs )
Kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Aliye Mtakatifu wako kuona uharibifu. (Hadēs )
28 Thou hast maad knowun to me the weies of lijf, thou schalt fille me in myrthe with thi face.
Umenionyesha njia za uzima, utanijaza na furaha mbele zako.’
29 Britheren, be it leueful boldli to seie to you of the patriark Dauid, for he is deed and biried, and his sepulcre is among vs in to this dai.
“Ndugu zangu Waisraeli, nataka niwaambie kwa uhakika kwamba baba yetu Daudi alikufa na kuzikwa, nalo kaburi lake lipo hapa mpaka leo.
30 Therfore whanne he was a prophete, and wiste, that with a greet ooth God hadde sworn to hym, that of the fruyt of his leende schulde oon sitte on his seete,
Lakini alikuwa nabii na alijua ya kuwa Mungu alikuwa amemwahidi kwa kiapo kwamba angemweka mmoja wa wazao wake penye kiti chake cha enzi.
31 he seynge afer spak of the resurreccioun of Crist, for nether he was left in helle, nether his fleisch saiy corrupcioun. (Hadēs )
Daudi, akiona mambo yaliyoko mbele, akanena juu ya kufufuka kwa Kristo, kwamba hakuachwa kaburini, wala mwili wake haukuona uharibifu. (Hadēs )
32 God reiside this Jhesu, to whom we alle ben witnessis.
Mungu alimfufua huyu Yesu na sisi sote ni mashahidi wa jambo hilo.
33 Therfor he was enhaunsid bi the riythoond of God, and thorouy the biheest of the Hooli Goost that he took of the fadir, he schedde out this spirit, that ye seen and heren.
Basi ikiwa yeye ametukuzwa kwa mkono wa kuume wa Mungu, amepokea kutoka kwa Baba ahadi ya Roho Mtakatifu, naye amemimina kile mnachoona sasa na kusikia.
34 For Dauid stiede not in to heuene; but he seith, The Lord seide to my Lord,
Kwa kuwa Daudi hakupaa kwenda mbinguni, lakini anasema, “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume,
35 Sitte thou on my riyt half, til Y putte thin enemyes a stool of thi feet.
hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
36 Therfor moost certeynli wite al the hous of Israel, that God made hym bothe Lord and Crist, this Jhesu, whom ye crucefieden.
“Kwa hiyo Israeli wote na wajue jambo hili kwa uhakika kwamba: Mungu amemfanya huyu Yesu, ambaye ninyi mlimsulubisha, kuwa Bwana na Kristo.”
37 Whanne thei herden these thingis, thei weren compunct in herte; and thei seiden to Petre and othere apostlis, Britheren, what schulen we do?
Watu waliposikia maneno haya yakawachoma mioyo yao, wakawauliza Petro na wale mitume wengine, “Ndugu zetu tufanye nini?”
38 And Petre seide to hem, Do ye penaunce, and eche of you be baptisid in the name of Jhesu Crist, in to remissioun of youre synnes; and ye schulen take the yifte of the Hooli Goost.
Petro akawajibu, “Tubuni, mkabatizwe kila mmoja wenu kwa jina la Yesu Kristo, ili mpate kusamehewa dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
39 For the biheest is to you, and to youre sones, and to alle that ben fer, which euer oure Lord God hath clepid.
Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu na watoto wenu, na kwa wote walio mbali, na kila mtu ambaye Bwana Mungu wetu atamwita amjie.”
40 Also with othere wordis ful many he witnesside to hem, and monestide hem, and seide, Be ye sauyd fro this schrewid generacioun.
Petro akawaonya kwa maneno mengine mengi na kuwasihi akisema, “Jiepusheni na kizazi hiki kilichopotoka.”
41 Thanne thei that resseyueden his word weren baptisid, and in that dai soulis weren encreesid, aboute thre thousinde;
Wale wote waliopokea ujumbe wa Petro kwa furaha wakabatizwa na siku ile waliongezeka watu wapatao 3,000.
42 and weren lastynge stabli in the teching of the apostlis, and in comynyng of the breking of breed, in preieris.
Nao wakawa wanadumu katika mafundisho ya mitume, katika ushirika, katika kumega mkate na katika kusali.
43 And drede was maad to ech man. And many wondris and signes weren don bi the apostlis in Jerusalem, and greet drede was in alle.
Kila mtu akaingiwa na hofu ya Mungu, nayo miujiza mingi na ishara zikafanywa na mitume.
44 And alle that bileueden weren togidre, and hadden alle thingis comyn.
Walioamini wote walikuwa mahali pamoja, nao walikuwa na kila kitu shirika.
45 Thei selden possessiouns and catel, and departiden tho thingis to alle men, as it was nede to ech.
Waliuza mali zao na vitu walivyokuwa navyo, kila mtu akagawiwa kadiri ya mahitaji yake.
46 And ech dai thei dwelliden stabli with o wille in the temple, and braken breed aboute housis, and token mete with ful out ioye and symplenesse of herte,
Siku zote kwa moyo mmoja walikutana ndani ya ukumbi wa Hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, wakila chakula chao kwa furaha na moyo mweupe,
47 and herieden togidere God, and hadden grace to al the folk. And the Lord encreside hem that weren maad saaf, ech dai in to the same thing.
wakimsifu Mungu na kuwapendeza watu wote. Kila siku Bwana akaliongeza kanisa wale waliokuwa wakiokolewa.