< Acts 18 >
1 Aftir these thingis Poul yede out of Atenes, and cam to Corinthie.
Baada ya haya, Paulo akaondoka Athene akaenda Korintho.
2 And he fonde a man, a Jewe, Aquila bi name, of Ponte bi kynde, that late cam from Ytalie, and Priscille, his wijf, for that Claudius comaundide alle Jewis to departe fro Rome; and he cam to hem.
Huko akakutana na Myahudi mmoja jina lake Akila, mwenyeji wa Ponto, ambaye alikuwa amewasili karibuni kutoka Italia pamoja na mkewe Prisila, kwa sababu Klaudio alikuwa ameamuru Wayahudi wote waondoke Rumi. Paulo akaenda kuwaona,
3 And for he was of the same craft, he dwellide with hem, and wrouyte; and thei weren of roopmakeris craft.
naye kwa kuwa alikuwa mtengeneza mahema kama wao, akakaa na kufanya kazi pamoja nao.
4 And he disputide in the synagoge bi ech sabat, puttynge among the name of the Lord Jhesu; and he counselide Jewis and Grekis.
Kila Sabato Paulo alikuwa akihojiana nao katika sinagogi, akijitahidi kuwashawishi Wayahudi na Wayunani.
5 And whanne Silas and Tymothe camen fro Macedonye, Poul yaf bisynesse to the word, and witnesside to the Jewis, that Jhesu is Crist.
Sila na Timotheo walipowasili kutoka Makedonia, walimkuta Paulo akiwa amejitolea muda wake wote katika kuhubiri, akiwashuhudia Wayahudi kwamba Yesu ndiye Kristo
6 But whanne thei ayenseiden and blasfemyden, he schoke awei hise clothis, and seide to hem, Youre blood be on youre heed; Y schal be clene from hennus forth, and schal go to hethene men.
Wayahudi walipompinga Paulo na kukufuru, yeye aliyakungʼuta mavazi yake, akawaambia, “Damu yenu na iwe juu ya vichwa vyenu! Mimi sina hatia, nimetimiza wajibu wangu. Kuanzia sasa nitawaendea watu wa Mataifa.”
7 And he passide fro thennus, and entride in to the hous of a iust man, Tite bi name, that worschipide God, whos hous was ioyned to the synagoge.
Kisha akaondoka mle kwenye sinagogi, akaenda nyumbani kwa mtu mmoja jina lake Tito Yusto, aliyekuwa mcha Mungu. Nyumba yake ilikuwa karibu na sinagogi.
8 And Crispe, prince of the synagoge, bileuede to the Lord, with al his hous. And many of the Corinthies herden, and bileueden, and weren cristened.
Kiongozi wa hilo sinagogi, aliyeitwa Krispo, akamwamini Bwana, yeye pamoja na watu wote wa nyumbani mwake. Nao Wakorintho wengi waliomsikia Paulo pia wakaamini na kubatizwa.
9 And the Lord seide bi nyyt to Poul bi a visioun, Nyle thou drede, but speke, and be not stille;
Usiku mmoja Bwana akamwambia Paulo katika maono, “Usiogope, lakini endelea kusema wala usinyamaze,
10 for Y am with thee, and no man schal be put to thee to noye thee, for myche puple is to me in this citee.
kwa maana mimi niko pamoja nawe, wala hakuna mtu atakayeweza kukushambulia ili kukudhuru, kwa kuwa ninao watu wengi katika mji huu ambao ni watu wangu.”
11 And he dwellide there a yeer and sixe monethis, techinge among hem the word of God.
Hivyo Paulo akakaa huko kwa muda wa mwaka mmoja na nusu, akiwafundisha neno la Mungu.
12 But whanne Gallion was proconsul of Acaye, Jewis risen vp with oo wille ayens Poul, and ledden hym to the doom,
Lakini wakati Galio alipokuwa msaidizi wa mwakilishi wa mtawala huko Akaya, Wayahudi waliungana kumshambulia Paulo, wakamkamata na kumpeleka mahakamani.
13 and seiden, Ayens the lawe this counselith men to worschipe God.
Wakamshtaki wakisema, “Mtu huyu anawashawishi watu wamwabudu Mungu kinyume cha sheria.”
14 And whanne Poul bigan to opene his mouth, Gallion seide to the Jewis, If there were ony wickid thing, ether yuel trespas, ye Jewis, riytli Y schulde suffre you;
Paulo alipotaka kujitetea, Galio akawaambia Wayahudi, “Kama ninyi Wayahudi mlikuwa mkilalamika kuhusu makosa makubwa ya uhalifu ingekuwa haki kwangu kuwasikiliza.
15 but if questiouns ben of the word, and of names of youre lawe, bisee you silf; Y wole not be domesman of these thingis.
Lakini kwa kuwa linahusu maneno, majina na sheria yenu, amueni ninyi wenyewe. Mimi sitakuwa mwamuzi wa mambo haya.”
16 And he droof hem fro the doom place.
Akawafukuza kutoka mahakamani.
17 And alle token Sostenes, prince of the synagoge, and smoten him bifor the doom place; and no thing of these was to charge to Gallion.
Ndipo wote wakamkamata Sosthene kiongozi wa sinagogi, wakampiga mbele ya mahakama, lakini Galio hakujali kitendo chao hata kidogo.
18 And whanne Poul hadde abidun many daies, he seide fare wel to britheren, and bi boot cam to Syrie. And Priscille and Aquila camen with hym, whiche hadden clippid his heed in Tencris; for he had a vow.
Baada ya kukaa Korintho kwa muda, Paulo akaagana na wale ndugu walioamini, akasafiri kwa njia ya bahari kwenda Shamu akiwa amefuatana na Prisila na Akila. Walipofika Kenkrea, Paulo alinyoa nywele zake kwa kuwa alikuwa ameweka nadhiri.
19 And he cam to Effesie, and there he lefte hem; and he yede in to the synagoge, and disputide with Jewis.
Walipofika Efeso, Paulo aliwaacha Prisila na Akila huko, lakini yeye akaingia kwenye sinagogi akawa anajadiliana na Wayahudi.
20 And whanne thei preieden, that he schulde dwelle more time,
Walipomwomba akae nao kwa muda mrefu zaidi hakukubali.
21 he consentide not, but he made `fare wel, and seide, Eft Y schal turne ayen to you, if God wole; and he wente forth fro Effesi.
Lakini alipokuwa akiondoka, akaahidi, “Nitarudi kama Mungu akipenda.” Kisha akasafiri kwa njia ya bahari kutoka Efeso.
22 And he cam doun to Cesarie, and he yede vp, and grette the chirche, and cam doun to Antiochie.
Alitia nanga Kaisaria, akaenda Yerusalemu na kulisalimu kanisa, kisha akaenda Antiokia.
23 And whanne he hadde dwellide there sumwhat of time, he wente forth, walkinge bi rewe thorou the cuntrei of Galathie, and Frigie, and confermyde alle the disciplis.
Baada ya kukaa huko kwa muda, akaondoka na kwenda sehemu moja hadi nyingine huko Galatia na Frigia, akiwaimarisha wanafunzi wote.
24 But a Jewe, Apollo bi name, a man of Alisaundre of kinde, a man eloquent, cam to Effesie; and he was myyti in scripturis.
Basi akaja Efeso Myahudi mmoja, jina lake Apolo, mwenyeji wa Iskanderia. Yeye alikuwa na elimu kubwa, pia alikuwa hodari katika Maandiko.
25 This man was tauyt the weie of the Lord, and was feruent in spirit, and spak, and tauyte diligentli tho thingis that weren of Jhesu, and knew oonli the baptym of Joon.
Alikuwa amefundishwa katika njia ya Bwana, naye alikuwa na bidii katika roho, akafundisha kwa usahihi juu ya Yesu, ingawa alijua tu ubatizo wa Yohana.
26 And this man bigan to do tristili in the synagoge. Whom whanne Priscille and Aquila herden, thei token hym, and more diligentli expowneden to hym the weie of the Lord.
Apolo alianza kunena kwa ujasiri mkubwa katika sinagogi. Lakini Prisila na Akila walipomsikia, walimchukua kando na kumweleza njia ya Mungu kwa ufasaha zaidi.
27 And whanne he wolde go to Acaie, britheren excitiden, and wroten to the disciplis, that thei schulden resseyue hym; which whanne he cam, yaf myche to hem that bileueden.
Naye Apolo alipotaka kwenda Akaya, ndugu wa Efeso walimtia moyo, wakawaandikia wanafunzi huko ili wamkaribishe. Alipofika huko, aliwasaidia sana wale ambao, kwa neema ya Mungu, walikuwa wameamini.
28 For he greetli ouercam Jewis, and schewide opynli bi scripturis, that Jhesu is Crist.
Kwa uwezo mkubwa aliwakanusha hadharani Wayahudi waliokuwa wakipinga, akionyesha kwa njia ya Maandiko kwamba Yesu ndiye Kristo.