< Acts 10 >

1 A man was in Cesarie, Cornelie bi name, a centurien of the cumpanye of knyytis, that is seid of Italie;
Katika mji wa Kaisaria palikuwa na mtu jina lake Kornelio, ambaye alikuwa jemadari wa kile kilichojulikana kama kikosi cha Kiitalia.
2 a religious man, and dredinge the Lord, with al his meyne; doynge many almessis to the puple, and preynge the Lord euere more.
Yeye alikuwa mcha Mungu pamoja na wote wa nyumbani mwake. Aliwapa watu sadaka nyingi na kumwomba Mungu daima.
3 This say in a visioun opinli, as in the nynthe oure of the dai, an aungel of God entringe in to hym, and seiynge to hym, Cornelie.
Siku moja alasiri, yapata saa tisa, aliona maono waziwazi, malaika wa Mungu akimjia na kumwambia, “Kornelio!”
4 And he bihelde hym, and was a dred, and seide, Who art thou, Lord? And he seide to hym, Thi preieris and thin almesdedis han stied vp in to mynde, in the siyt of the Lord.
Kornelio akamkazia macho kwa hofu akasema, “Kuna nini, Bwana?” Malaika akamwambia, “Sala zako na sadaka zako kwa maskini zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za Mungu.
5 And now sende thou men in to Joppe, and clepe oon Symount, that is named Petre.
Sasa tuma watu waende Yafa wakamwite mtu mmoja jina lake Simoni aitwaye Petro.
6 This is herborid at a man Symount, curiour, whos hous is bisidis the see. This schal seie to thee, what it bihoueth thee to do.
Yeye anaishi na Simoni mtengenezaji ngozi ambaye nyumba yake iko kando ya bahari.”
7 And whanne the aungel that spak to hym, was gon awei, he clepide twei men of his hous, and a knyyt that dredde the Lord, whiche weren at his bidding.
Yule malaika aliyekuwa akizungumza naye alipoondoka, Kornelio akawaita watumishi wake wawili pamoja na askari mmoja mcha Mungu aliyekuwa miongoni mwa wale waliomtumikia.
8 And whanne he hadde told hem alle these thingis, he sente hem in to Joppe.
Akawaambia mambo yote yaliyotukia, kisha akawatuma waende Yafa.
9 And on the dai suynge, while thei maden iournei, and neiyeden to the citee, Petre wente vp in to the hiest place of the hous to preie, aboute the sixte our.
Siku ya pili yake, walipokuwa wameukaribia mji, wakati wa adhuhuri, Petro alipanda juu ya nyumba kuomba.
10 And whanne he was hungrid, he wolde haue ete. But while thei maden redi, a rauysching of spirit felde on hym;
Alipokuwa akiomba akahisi njaa, akatamani kupata chakula. Lakini wakati walikuwa wakiandaa chakula, akalala usingizi mzito sana.
11 and he say heuene openyd, and a vessel comynge doun, as a greet scheet with foure corneris, to be lette doun fro heuene in to erthe,
Akaona mbingu zimefunguka na kitu kama nguo kubwa kikishushwa duniani kwa ncha zake nne.
12 in which weren alle foure footid beestis, and crepinge of the erthe, and volatilis of heuene.
Ndani yake walikuwepo aina zote za wanyama wenye miguu minne, nao watambaao nchini, na ndege wa angani.
13 And a vois was maad to hym, Rise thou, Petre, and sle, and ete.
Ndipo sauti ikamwambia “Petro, ondoka, uchinje na ule.”
14 And Petre seide, Lord, forbede, for Y neuer ete ony comun thing and vnclene.
Petro akajibu, “La hasha Bwana! Sijawahi kamwe kula kitu chochote kilicho najisi.”
15 And eft the secounde tyme the vois was maad to him, That thing that God hath clensid, seye thou not vnclene.
Ile sauti ikasema naye mara ya pili, “Usikiite najisi kitu chochote Mungu alichokitakasa.”
16 And this thing was don bi thries; and anoon the vessel was resseyued ayen.
Jambo hili lilitokea mara tatu na ghafula ile nguo ikarudishwa mbinguni.
17 And while that Petre doutide with ynne hym silf, what the visioun was that he say, lo! the men, that weren sent fro Corneli, souyten the hous of Symount, and stoden at the yate.
Wakati Petro akiwa bado anajiuliza kuhusu maana ya maono haya, wale watu waliokuwa wametumwa na Kornelio wakaipata nyumba ya Simoni mtengenezaji wa ngozi wakawa wamesimama mbele ya lango.
18 And whanne thei hadden clepid, thei axiden if Symount, that is named Petre, hadde there herbore.
Wakabisha hodi na kuuliza kama Simoni aliyeitwa Petro alikuwa anaishi hapo.
19 And while Petre thouyte on the visioun, the spirit seide to hym, Lo! thre men seken thee.
Wakati Petro akiwa anafikiria juu ya yale maono, Roho Mtakatifu akamwambia, “Simoni, wako watu watatu wanaokutafuta.
20 Therfor ryse thou, and go doun, and go with hem, and doute thou no thing, for Y sente hem.
Inuka na ushuke, usisite kwenda nao kwa kuwa mimi nimewatuma.”
21 And Petre cam doun to the men, and seide, Lo! Y am, whom ye seken; what is the cause, for which ye ben come?
Petro akashuka na kuwaambia wale watu waliokuwa wametumwa kutoka kwa Kornelio, “Mimi ndiye mnayenitafuta. Mmekuja kwa sababu gani?”
22 And thei seiden, Cornelie, the centurien, a iust man, and dredinge God, and hath good witnessyng of alle the folc of Jewis, took aunswere of an hooli aungel, to clepe thee in to his hous, and to here wordis of thee.
Wale watu wakamjibu, “Tumetumwa na Kornelio yule jemadari. Yeye ni mtu mwema anayemcha Mungu, na anaheshimiwa na Wayahudi wote. Yeye ameagizwa na malaika mtakatifu akukaribishe nyumbani kwake, ili asikilize maneno utakayomwambia.”
23 Therfor he ledde hem inne, and resseyuede in herbore; and that nyyt thei dwelliden with hym. And in the dai suynge he roos, and wente forth with hem; and sum of the britheren folewiden hym fro Joppe, that thei be witnessis to Petre.
Basi Petro akawakaribisha wakafuatana naye ndani, akawapa pa kulala. Kesho yake akaondoka pamoja nao, na baadhi ya ndugu kutoka Yafa wakafuatana naye.
24 And the other dai he entride in to Cesarie. And Cornelie abood hem, with hise cousyns, and necessarie freendis, that weren clepid togidere.
Siku iliyofuata wakawasili Kaisaria. Kornelio alikuwa akiwangoja pamoja na jamaa yake na marafiki zake wa karibu.
25 And it was don, whanne Petre was come ynne, Corneli cam metynge hym, and felle doun at hise feet, and worschipide him.
Petro alipokuwa akiingia ndani, Kornelio alikuja kumlaki, akaanguka miguuni pake kwa heshima.
26 But Petre reiside hym, and seide, Aryse thou, also Y my silf am a man, as thou.
Lakini Petro akamwinua akamwambia, “Simama, mimi ni mwanadamu tu.”
27 And he spak with hym, and wente in, and foonde many that weren come togidere.
Petro alipokuwa akizungumza naye akaingia ndani na kukuta watu wengi wamekusanyika.
28 And he seide to hem, Ye witen, how abhomynable it is to a Jewe, to be ioyned ether to come to an alien; but God schewide to me, that no man seye a man comyn, ethir vnclene.
Akawaambia, “Mnajua kabisa kwamba ni kinyume cha sheria yetu Myahudi kuchangamana na mtu wa Mataifa au kumtembelea. Lakini Mungu amenionyesha kwamba nisimwite mtu yeyote kuwa najisi au asiye safi.
29 For which thing Y cam, whanne Y was clepid, with out douting. Therfor Y axe you, for what cause han ye clepid me?
Ndiyo sababu ulipotuma niitwe nilikuja bila kupinga lolote. Basi sasa naomba unieleze kwa nini umeniita?”
30 And Cornelie seide, To dai foure daies in to this our, Y was preiynge and fastynge in the nynthe our in myn hous. And lo! a man stood bifore me in a whijt cloth, and seide,
Kornelio akajibu, “Siku nne zilizopita, nilikuwa nyumbani nikisali saa kama hii, saa tisa alasiri. Ghafula mtu aliyevaa nguo zilizongʼaa akasimama mbele yangu,
31 Cornelie, thi preier is herd, and thin almesdedis ben in mynde in the siyt of God.
akasema, ‘Kornelio, maombi yako yamesikiwa na sadaka zako kwa maskini zimekumbukwa mbele za Mungu.
32 Therfor sende thou in to Joppe, and clepe Symount, that is named Petre; this is herborid in the hous of Symount coriour, bisidis the see. This, whanne he schal come, schal speke to thee.
Basi tuma watu waende Yafa wakaulize mtu mmoja Simoni aitwaye Petro, yeye ni mgeni katika nyumba ya Simoni mtengenezaji ngozi, ambaye nyumba yake iko kando ya bahari.’
33 Therfor anoon Y sente to thee, and thou didist wel in comynge to vs. `Now therfor we alle ben present in thi siyt, to here the wordis, what euer ben comaundid to thee of the Lord.
Nilituma watu kwako mara moja, nawe umefanya vyema kuja. Basi sasa sisi sote tuko hapa mbele za Mungu kuyasikiliza yote ambayo Bwana amekuamuru kutuambia.”
34 And Petre openyde his mouth, and seide, In trewthe Y haue foundun, that God is no acceptor of persoones;
Ndipo Petro akafungua kinywa chake akasema, “Mungu hana upendeleo,
35 but in eche folk he that dredith God, and worchith riytwisnesse, is accept to hym.
Lakini katika kila taifa, kila mtu amchaye na kutenda yaliyo haki hukubaliwa naye.
36 God sente a word to the children of Israel, schewinge pees bi Jhesu Crist; this is Lord of alle thingis.
Ninyi mnajua ule ujumbe uliotumwa kwa Israeli, ukitangaza habari njema za amani kwa Yesu Kristo. Yeye ni Bwana wa wote.
37 Ye witen the word that is maad thorou al Judee, and bigan at Galile, aftir the baptym that Joon prechide, Jhesu of Nazareth;
Mnajua yale yaliyotukia katika Uyahudi wote kuanzia Galilaya baada ya mahubiri ya Yohana Mbatizaji:
38 hou God anoyntide hym with the Hooli Goost, and vertu; which passide forth in doynge wel, and heelynge alle men oppressid of the deuel, for God was with hym.
Jinsi Mungu alivyomtia Yesu wa Nazareti mafuta katika Roho Mtakatifu na jinsi alivyokwenda huku na huko akitenda mema na kuponya wote waliokuwa wameonewa na nguvu za ibilisi, kwa sababu Mungu alikuwa pamoja naye.
39 And we ben witnessis of alle thingis, whiche he dide in the cuntrei of Jewis, and of Jerusalem; whom thei slowen, hangynge in a tre.
“Sisi ni mashahidi wa mambo yote aliyoyafanya katika Uyahudi na Yerusalemu. Wakamuua kwa kumtundika msalabani.
40 And God reiside this in the thridde dai, and yaf hym to be maad knowun,
Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu siku ya tatu na akamwezesha kuonekana na watu.
41 not to al puple, but to witnessis bifor ordeyned of God; to vs that eeten and drunken with hym, after that he roos ayen fro deth.
Hakuonekana kwa watu wote, lakini kwetu sisi tuliochaguliwa na Mungu kuwa mashahidi, ambao tulikula na kunywa naye baada ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu.
42 And he comaundide to vs to preche to the puple, and to witnesse, that he it is, that is ordeyned of God domesman of the quyk and of deede.
Naye alituamuru kuhubiri kwa watu wote na kushuhudia kwamba ndiye alitiwa mafuta na Mungu kuwa hakimu wa walio hai na wafu.
43 To this alle prophetis beren witnessing, that alle men that bileuen in hym, schulen resseyue remyssioun of synnes bi his name.
Manabii wote walishuhudia juu yake kwamba kila mtu amwaminiye hupokea msamaha wa dhambi katika Jina lake.”
44 And yit while that Petre spak these wordis, the Hooli Goost felde on alle that herden the word.
Wakati Petro alikuwa akisema maneno haya, Roho Mtakatifu aliwashukia wote waliokuwa wakisikiliza ule ujumbe.
45 And the feithful men of circumcisioun, that camen with Petre, wondriden, that also in to naciouns the grace of the Hooli Goost is sched out.
Wale wa tohara walioamini waliokuja na Petro walishangaa kwa kuona kuwa kipawa cha Roho Mtakatifu kimemwagwa juu ya watu wa Mataifa.
46 For thei herden hem spekynge in langagis, and magnyfiynge God.
Kwa kuwa waliwasikia wakinena kwa lugha mpya na kumwadhimisha Mungu. Ndipo Petro akasema,
47 Thanne Petre answeride, Whether ony man may forbede watir, that these ben not baptisid, that han also resseyued the Hooli Goost as we?
“Je, kuna mtu yeyote anayeweza kuzuia watu hawa wasibatizwe kwa maji? Wamempokea Roho Mtakatifu kama sisi tulivyompokea.”
48 And he comaundide hem to be baptisid in the name of the Lord Jhesu Crist. Thanne thei preieden hym, that he schulde dwelle with hem sum daies.
Kwa hiyo akaamuru wabatizwe kwa jina la Yesu Kristo. Wakamsihi Petro akae nao kwa siku chache.

< Acts 10 >