< 3 John 1 >
1 The eldere man to Gayus, most dere brother, whom Y loue in treuthe.
Mzee: Kwa Gayo rafiki yangu, nimpendaye katika kweli.
2 Most dere brothir, of alle thingis Y make preyer, that thou entre, and fare welefuly, as thi soule doith welefuli.
Mpendwa, naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya njema kama vile roho yako ifanikiwavyo.
3 Y ioyede greetli, for britheren camen, and baren witnessing to thi treuthe, `as thou walkist in treuthe.
Ilinifurahisha sana baadhi ya ndugu walipokuja na kutueleza juu ya uaminifu wako katika kweli na jinsi unavyoendelea kuenenda katika hiyo kweli.
4 Y haue not more grace of these thingis, than that Y here that my sones walke in treuthe.
Sina furaha kubwa kuliko hii, kusikia kwamba watoto wangu wanaenenda katika kweli.
5 Most dere brother, thou doist feithfuli, what euer thou worchist in britheren, and that in to pilgrymys,
Rafiki mpendwa, wewe ni mwaminifu kwa yale unayowatendea ndugu, ingawa wao ni wageni kwako.
6 which yeldiden witnessing to thi charite, in the siyt of the chirche; which thou leddist forth, and doist wel worthili to God.
Wameshuhudia kuhusu upendo wako mbele ya kanisa. Utafanya vyema ukiwasafirisha kama inavyostahili kwa Mungu.
7 For thei wenten forth for his name, and token no thing of hethene men.
Ilikuwa ni kwa ajili ya hilo Jina waliondoka, bila kukubali kupokea msaada wowote kutoka kwa watu wasioamini.
8 Therfor we owen to resseyue siche, that we be euen worcheris of treuthe.
Kwa hiyo imetupasa sisi kuonyesha ukarimu kwa watu kama hao ili tuweze kutenda kazi pamoja kwa ajili ya kweli.
9 I hadde write perauenture to the chirche, but this Diotrepes, that loueth to bere primacie in hem, resseyueth not vs.
Nililiandikia kanisa, lakini Deotrefe, yeye apendaye kujifanya wa kwanza, hakubali mamlaka yetu.
10 For this thing, if Y schal come, Y schal moneste hise werkis, whiche he doith, chidinge ayens vs with yuel wordis. And as if these thingis suffisen not to hym, nether he resseyueth britheren, and forbedith hem that resseyuen, and puttith out of the chirche.
Hivyo kama nikija, nitakumbuka matendo yake atendayo, akitusingizia kwa maneno ya hila. Wala hatosheki na hayo anayotusingizia, bali pia hukataa kuwakaribisha ndugu, na hata huwazuia wale walio tayari kufanya hivyo na kuwafukuza watoke kanisani.
11 Moost dere brothir, nyle thou sue yuel thing, but that that is good thing. He that doith wel, is of God; he that doith yuel, seeth not God.
Rafiki mpendwa, usiige lile lililo baya bali lile lililo jema. Yeyote atendaye mema atoka kwa Mungu, bali atendaye mabaya hajamwona Mungu.
12 Witnessing is yoldun to Demetrie of alle men, and of treuthe it silf; but also we beren witnessing, and thou knowist, that oure witnessing is trewe.
Kila mtu ameshuhudia mema kuhusu Demetrio, vivyo hivyo hata na hiyo kweli yenyewe. Sisi pia twashuhudia mema juu yake, nanyi mwajua kwamba ushuhuda wetu ni kweli.
13 Y hadde many thingis to wryte to thee, but Y wolde not write to thee bi enke and penne.
Ninayo mambo mengi ya kukuandikia, lakini sipendi kuandika kwa kalamu na wino.
14 For Y hope soone to se thee, and we schulen speke mouth to mouth. Pees be to thee. Frendis greten thee wel. Greete thou wel frendis bi name.
Badala yake, nataraji kukuona upesi, nasi tutaongea pamoja ana kwa ana. Amani iwe kwako. Rafiki zetu walioko hapa wanakusalimu. Wasalimu hao rafiki zetu walioko huko, kila mmoja kwa jina lake.