< 2 Thessalonians 2 >

1 But, britheren, we preien you bi the comyng of oure Lord Jhesu Crist, and of oure congregacioun in to the same comyng,
Ndugu, kuhusu kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo na kukusanyika kwetu pamoja mbele zake, tunawasihi,
2 that ye be not mouyd soone fro youre witt, nether be aferd, nether bi spirit, nether bi word, nether bi epistle as sent bi vs, as if the dai of the Lord be nyy.
msiyumbishwe kwa urahisi wala msitiwe wasiwasi na roho wala neno au barua inayosemekana kuwa imetoka kwetu, isemayo kwamba siku ya Bwana imekwisha kuwako.
3 No man disseyue you in ony manere. For but dissencioun come first, and the man of synne be schewid, the sonne of perdicioun,
Mtu yeyote na asiwadanganye kwa namna yoyote kwa maana siku ile haitakuja mpaka uasi utokee kwanza, na yule mtu wa kuasi adhihirishwe, yule ambaye amehukumiwa kuangamizwa kabisa.
4 that is aduersarie, and is enhaunsid ouer `al thing that is seid God, or that is worschipid, so that he sitte in the temple of God, and schewe hym silf as if he were God.
Yeye atapingana na kujitukuza juu ya kila kitu kiitwacho Mungu au kinachoabudiwa, ili kujiweka juu katika Hekalu la Mungu, akijitangaza mwenyewe kuwa ndiye Mungu.
5 Whether ye holden not, that yit whanne Y was at you, Y seide these thingis to you?
Je, hamkumbuki ya kwamba nilipokuwa pamoja nanyi niliwaambia mambo haya?
6 And now what withholdith, ye witen, that he be schewid in his tyme.
Nanyi sasa mnajua kinachomzuia, ili apate kudhihirishwa wakati wake utakapowadia.
7 For the priuete of wickidnesse worchith now; oneli that he that holdith now, holde, til he be do awei.
Maana ile nguvu ya siri ya uasi tayari inatenda kazi, lakini yule anayeizuia ataendelea kufanya hivyo mpaka atakapoondolewa.
8 And thanne thilke wickid man schal be schewid, whom the Lord Jhesu schal sle with the spirit of his mouth, and schal distrie with liytnyng of his comyng;
Hapo ndipo yule mwasi atafunuliwa, ambaye Bwana Yesu atamteketeza kwa pumzi ya kinywa chake na kumwangamiza kabisa kwa utukufu wa kuja kwake.
9 hym, whos comyng is bi the worching of Sathanas, in al vertu, and signes,
Kuja kwa yule mwasi kutaonekana kana kwamba ni kutenda kazi kwake Shetani ambaye hutumia nguvu zote, ishara, maajabu ya uongo,
10 and grete wondris, false, and in al disseit of wickidnesse, to hem that perischen. For that thei resseyueden not the charite of treuthe, that thei schulden be maad saaf.
na kila aina ya uovu kwa wale wanaoangamia kwa sababu walikataa kuipenda kweli wapate kuokolewa.
11 And therfor God schal sende to hem a worching of errour, that thei bileue to leesing,
Kwa sababu hii, Mungu ameruhusu watawaliwe na nguvu ya udanganyifu, ili waendelee kuamini uongo,
12 that alle be demed, whiche bileueden not to treuthe, but consentiden to wickidnesse.
na wahukumiwe wote ambao hawakuiamini ile kweli, bali wamefurahia uovu.
13 But, britheren louyd of God, we owen to do thankyngis euermore to God for you, that God chees vs the firste fruytis in to heelthe, in halewing of spirit and in feith of treuthe;
Lakini imetupasa sisi kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu, ndugu mpendwao na Bwana, kwa sababu Mungu aliwachagua ninyi tangu mwanzo ili mwokolewe kwa kutakaswa na Roho kwa kuiamini kweli.
14 in which also he clepide you bi oure gospel, in to geting of the glorie of oure Lord Jhesu Crist.
Kwa kusudi hili Mungu aliwaita kwa njia ya kuhubiri kwetu Injili, ili mpate kushiriki katika utukufu wa Bwana Yesu Kristo.
15 Therfor, britheren, stonde ye, and holde ye the tradiciouns, that ye han lerud, ethir bi word, ethir bi oure pistle.
Hivyo basi, ndugu wapendwa, simameni imara na myashike sana yale mafundisho tuliyowapa ikiwa ni kwa maneno ya kinywa au kwa barua.
16 And oure Lord Jhesu Crist him silf, and God oure fadir, which louyde vs, and yaf euerlastinge coumfort and good hope in grace, (aiōnios g166)
Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu, aliyetupenda na kwa neema yake akatupatia faraja ya milele na tumaini jema, (aiōnios g166)
17 stire youre hertis, and conferme in al good werk and word.
awafariji mioyo yenu na kuwaimarisha katika kila neno na tendo jema.

< 2 Thessalonians 2 >