< 2 Samuel 8 >

1 Forsothe it was doon aftir these thingis, Dauid smoot Filisteis, and made low hem; and Dauid took awei the bridil of tribute fro the hond of Filisteis.
Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Metheg-Amma kutoka mikononi mwa Wafilisti.
2 And Dauid smoot Moab, and mat hem with a coorde, and made euene to the erthe; forsothe `he mat twey cordis, oon to sle, and oon to quikene. And Moab seruyde Dauid vndur tribute.
Pia Daudi akawashinda Wamoabu. Akawafanya walale chini kwa mstari akawapima kwa urefu wa kamba. Kila alipopima urefu wa hiyo kamba mara mbili hilo kundi waliuawa na alipopima mara ya tatu aliwaacha hai. Kwa hiyo Wamoabu wakawa chini ya Daudi nao wakamletea kodi.
3 And Dauid smoot Adadezer, sone of Roob, kyng of Soba, whanne he yede forth to be lord ouer the flood Eufrates.
Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba, alipokwenda kurudisha tena utawala wake kwenye eneo la Mto Frati.
4 And whanne a thousynde and seuene hundrid kniytis of his part weren takun, and twenti thousynde of foot men, Dauid hoxide alle `drawynge beestis in charis; but Dauid lefte of tho an hundrid charis, that is, the horsis of an hundrid charis.
Daudi akateka magari yake ya vita 1,000, askari wapanda farasi 7,000 na askari 20,000 watembeao kwa miguu. Daudi akawakata wale farasi wote wakokotao magari mishipa ya miguu, isipokuwa farasi 100 hakuwakata.
5 Also Sirie of Damask cam, that it schulde bere help to Adadezer, kyng of Soba; and Dauid smoot of Sirie two and twenti thousynde of men.
Waaramu wa Dameski walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao.
6 And Dauid settide strengthe in Sirie of Damask, and Sirie was maad seruynge Dauid vndur tribute. And the Lord kepte Dauid in alle thingis, to what euer thingis he yede forth.
Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski, nao Waaramu wakawa watumwa wake na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.
7 And Dauid took goldun armeris and bies, whiche the seruauntis of Adadezer hadden, and he brouyte tho in to Jerusalem.
Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.
8 And of Bethe, and of Beroth, citees of Adadezer, Dauith the kyng took ful myche metal; `of the whiche Salomon made alle the brasen vessels in the temple, and the brasen see, and the pilers, and the auter.
Kutoka miji ya Beta na Berothai, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Mfalme Daudi akatwaa shaba nyingi sana.
9 Forsothe Thou, kyng of Emath, herde that Dauid hadde smyte al the strengthe of Adadezer.
Tou, mfalme wa Hamathi, aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri,
10 And Thou sente Joram, his sone, to `kyng Dauid, that he schulde grete hym, and thanke, and do thankyngis, for he hadde ouercome Adadezer, and hadde smyte hym; for Thou was enemy to Adadeser; and vessels of silver, and vessels of gold, and vessels of bras weren in his hond.
akamtuma mwanawe Yoramu kwa Mfalme Daudi kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Hadadezeri, kwa kuwa Hadadezeri alikuwa amepigana vita na Tou. Yoramu akamletea Daudi vyombo vya fedha, dhahabu na shaba.
11 And the same vessels kyng Dauid halewid `to the Lord, with the siluer and gold, whiche he hadde halewid of alle hethene men, whiche `hethene men he made suget of Sirye,
Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana, kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu kutoka kwa mataifa yote aliyokuwa ameyashinda:
12 and Moab, and the sones of Amon, and Filisteis, and Amalech, and of the spuylis of Adadezer, sone of Roob, kyng of Soba.
yaani Edomu, Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki. Pia akaweka wakfu nyara alizoteka kutoka kwa Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba.
13 Also Dauid made to hym a name, whanne he turnede ayen, whanne Sirie was takun, for eiytene thousynde weren slayn in the valey, where salt is maad, and in Gebelem, to thre and twenti thousynde.
Naye Daudi akapata sifa baada ya kurudi kutoka kuwaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.
14 And he settide keperis in Ydumee, and ordeinede strong hold, and al Ydumee was maad seruynge to Dauid; and the Lord kepte Dauid in alle thingis, to whateuer thingis he yede forth.
Akaweka kambi za askari walinzi katika Edomu yote, nao Waedomu wakawa chini ya Daudi. Bwana alimpatia Daudi ushindi kila alipokwenda.
15 And Dauid regnede on al Israel, and Dauid dide doom, and riytfulnesse to al his puple.
Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.
16 Forsothe Joab, the sone of Saruy, was ouer the oost; sotheli Josaphat, sone of Achilud, was chaunceler; and Sadoch,
Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
17 sone of Achitob, and Achymelech, sone of Abiathar, weren preestis; and Saraye was scryuyn.
Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Seraya alikuwa mwandishi;
18 Forsothe Bananye, sone of Joiada, was ouer Cerethi and Pherethi, that is, ouer archeris and arblasteris; sotheli the sones of Dauid weren prestis.
Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa washauri wa mfalme.

< 2 Samuel 8 >